Posts

Showing posts from July, 2025

WATANZANIA WAHAMASISHWA KUSHIRIKI KATIKA UCHAGUZI MKUU WA 2025

Image
    Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kikao cha Tume na wawakilishi wa watu wenye ulemavu kuhusu uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika jijini Dar es Salaam leo Julai 31,2025.  Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kikao cha Tume na wawakilishi wa watu wenye ulemavu kuhusu uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika jijini Dar es Salaam leo Julai 31,2025.  Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg Kailima Ramadhani akitoa mada wakati wa Kikao cha Tume na wawakilishi wa watu wenye ulemavu kuhusu uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika jijini Dar es Salaam leo Julai 31,2025.  Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg Kailima Ramadhani akitoa mada wakati wa Kikao cha Tu...

RAIS SAMIA AZINDUA USAFIRISHAJI WA MIZIGO KWA TRENI YA UMEME YA SGR

Image
  Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan akioepelusha bendera ikiwa ni ishara ya kuzindua usafirishaji wa mizigo kwa kutumia usafiri wa Treni ya umeme ya SGR kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma eneo la Kwala Marshalling Yard mkoani Pwani, leo. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi Kongani ya Viwanda ya Kwala (Kwala Industrial Park) iliyopo Kwala, Kibaha vijijini mkoani Pwani tarehe 31 Julai, 2025. Lengo kuu la Kongani ya viwanda ni kujenga viwanda 2000 na kwasasa kuna viwanda 12 katika eneo lenye ekari 2500.     Aliyosema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan #Uzinduzi wa safari za mizigo kwa kutumia reli ya kisasa ya SGR ni ushahidi kuwa Tanzania imeamua kwa dhati kuimarisha mfumo wa usafirishaji wa mizigo kuanzia kwenye barabara, usafiri wa anga, maji na reli. #Reli ya SGR kutoka bandari ya Dar es Salaam hadi Dodoma, ni sehemu ya mkakati wa kitaifa wa kup...

TADB YATOA MIKOPO YA RIBA NAFUU YA TRILIONI 1.129 KWA WAKULIMA KWA MIAKA KUMI

Image
  Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), Bw. Frank Nyabundege, akimkabidhi hundi ya shilingi milioni 400,000,000 kwa ajili ya kudhamini maadhimisho ya Siku ya Wakulima (Nanenane) Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli,yanayotarajia kuanza Agosti Mosi katika Viwanja vya Nanenane eneo Nzuguni jijini Dodoma. @@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@ KATIKA  kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wakulima (Nanenane),ambayo kitaifa yatafanyika mkoani Dodoma, Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imetoa mikopo ya riba nafuu yenye thamani ya jumla ya Shilingi Trilioni 1.129 katika kipindi cha miaka kumi kwa lengo la kuwawezesha wakulima kiuchumi. Akizungumza leo Julai 31,2025 jijini Dodoma na waandishi wa habari kuhusiana na maonyesho hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Frank Nyabundege, amesema benki hiyo imejikita kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuleta mageuzi ya kilimo kwa kumkomboa mkulima wa kawaida kupitia upatikanaji wa mikopo...