Posts

KUMBUKUMBU YA MIAKA 40 YA KIFO CHA ALIYEKUWA WAZIRI MKUU MAREHEMU SOKOINE

Image
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari MAELEZO, Zamaradi Kawawa, akizungumza kabla ya kumkalibisha msemaji wa familia ya Sokoine kuzungumza na wanahabari katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO jijini Dodoma leo. Msemaji wa Familia ya Marehemu Edward Moringe Sokoine, Kipuyo Lembris, akizungumza na wanahabari ,kuhusu kumbukumbu ya miaka 40 ya kifo cha  aliyekuwa waziri mkuu kipenzi cha Watanzania  14.4.2024. hapo Luhindo Dakawa Morogoro mwaka 1984 ,akitokea bungeni Dodoma,  alibainisha  kwamba kutakuwa na misa  nyumbani kwake  Monduli Juu ya kumuombea , inatalajiwa kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa kidini na kiserikali akiwemo Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.   Edward Sokoine alizaliwa Jumatatu, Agosti mosi, 1938, katika mji wa "Monduli" mkoani "Arusha" alipata elimu ya kimsingi na ya kati katika shule ya "Monduli", kisha, mnamo  1956, akajiunga na shule ya "Omboy" ili akamilishe elimu yake ya sekondari.  Mnamo  1961, Edward Sokoine alijiunga

WANAKIJIJI WAANZA UJENZI WA "DAVID MASSAMBA MEMORIAL SECONDARY SCHOOL"

Image
Wakazi wa Kijiji cha Kurwaki, Kata ya Mugango wameanza ujenzi wa "David Massamba Memorial Secondary School." Sekondari hii ambayo itakuwa ya pili kwa Kata ya Mugango inajengwa ikiwa imepewa jina la Marehemu Prof David  Massamba, mzaliwa wa Kijiji cha Kurwaki, na aliyekuwa bingwa wa mabingwa wa lugha ya Kiswahili. Kazi kubwa za ustawishaji wa Lugha ya Kiswahili zilizofanywa na Marehemu Prof David Massamba, kwa kushirikiana na Wataalamu wenzake, ni pamoja na: *Kuandika vitabu vinavyotumika Vyuo Vikuu na Sekondari (Sarufi Maumbo ya Kiswahili Sanifu) *Uandishi wa Kamusi ya Kiswahili Michango ya awali ya ujenzi: (i) Wanakijiji: Tsh 1,870,000 (ii) Familia Massamba: Tsh 800,000 (iii) Wazaliwa 2 wa Kurwaki: Tsh 750,000       (Dr Rukonge Manoko & Ndg Kawawa Jackson) (iv) Diwani wa Kata: Tsh 200,000 (v) Wazazi wa Kijiji jirani, Kiriba: Tsh 80,000 (vi) Walimu Makada: Tsh 70,000 Michango ya Mbunge wa Jimbo: (i) Binafsi: Saruji Mifuko 250 (ii) Mfuko wa Jimbo: Saruji Mifuko 205 Akaunti

MAJI YA BOMBA MUSOMA VIJIJINI - MAKABIDHIANO YA UTEKELEZAJI WA MRADI WA USAMBAZAJI WA MAJI YA BOMBA YAFANYIKA KIJIJINI KWIKUBA

Image
  Kata za Busambara (vijiji: Kwikuba, Maneke na Mwiringo) na Kiriba (vijiji: Bwai Kumsoma, Bwai Kwitururu na Kiriba) zimeshuhudia Mkataba wa kusambaziwa maji ya bomba kutoka Ziwa Victoria ukitiwa saini katika Kijijini cha Kwikuba. Makabiadhiano hayo kati ya RUWASA na MKANDARASI (Otonde Construction & General Supplies Ltd) yalifanyika siku ya Jumatano asubuhi, 20.3.2024. Walioshuhudia utiaji wa saini za Mkataba huo ni: wananchi kutoka Kata hizo mbili, viongozi kadhaa wa Chama (CCM) na Serikali, DAS Wilaya ya Musoma, na Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini. RUWASA inasifiwa sana kwa kufanya kazi nzuri Musoma Vijijini - hongereni sana RUWASA! Gharama za Mradi huu: Jumla ni: Tsh bilioni 4.42 Kazi za awali zitatumia: Tsh bilioni 1.44 Tafadhali sikiliza CLIP/VIDEO iliyoambatanishwa hapa. Ofisi ya Mbunge Jimbo la Musoma Vijijini www.musomavijijini.or.tz Tarehe: Jumanne, 26.3.2024

TUTAHAKIKISHA TUNATOA HATI KUPITIA MRADI WA LTIP- MHANDISI SANGA

Image
Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga akizungumza wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kukagua hatua iliyofikiwa na thamani ya fedha iliyotumika katika Utekelezaji wa Mradi wa Uboreshaji Usalama wa Milki za Ardhi Katika Mji wa Nzega mkoa wa Tabora tarehe 27 Machi 2024. Wa pili kushoto ni Naibu Waziri wa Ardhi Mhe, Geophrey Pinda. Sehemu ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) wakimsikiliza Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Mhandisi Anthony Sanga (hayupo pichani) wakati Kamati hiyo ilipokwenda kukagua hatua iliyofikiwa na thamani ya fedha iliyotumika katika utekelezaji wa Mradi wa Uboreshaji Usalama wa Milki za Ardhi Katika Mji wa Nzega mkoa wa Tabora tarehe 27 Machi 2024. Naibu Waziri wa Ardhi Mhe, Geophrey Pinda akizungumza katika  ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kukagua hatua iliyofikiwa na thamani ya fedha iliyotumika k

LEO ILIKUWA ZAMU YA MIKOA YA LINDI, ARUSHA NA GEITA KUOMBA BAJETI ZA MIKOA YAO KWENYE KAMATI YA TAMISEMI

Image
Mwenyekiti wa kamati ya Kudumu ya Bunge TAMISEMI, Dennis Londo, akizungumza leo  katika mkutano wa kamati yake  kwa ajili ya kuanza kujadili bajeti za mikoa ya Lindi, Arusha na Geita katika ukumbi wa bunge wa Anne Makinda, jijini Dodoma Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Zainab Telack, akisoma bajeti ya mkoa wake  katika kikao cha kamati ya Kudumu ya bunge kilichofanyika leo jijini Dodoma. Baadhi ya Maofisa wa mkoa wa Lindi wakifuatilia hotuba hiyo. Mkuu wa mkoa wa Arusha John Mongela, akisoma bajeti ya mkoa wake mbele ya kamati ya Kudumu ya Bunge  ya TAMISEMI iliyokutana leo jijini Dodoma. Maofisa wa Mkoa wa Arusha wakifatilia hotuba ya mkuu wao Wajumbe wa kamati hiyo  wakipitia vitabu vya bajeti katika kikao hicho. Mwenyekiti Londo. akisisitiza jambo alipokuwa akizungumza na viongozi wa mkoa wa Geita ukiongozwa na Mkuu wao wa mkoa Martine Shigella Martine Shigella (wapili Kushoto), na maafisa wake wakimsikiliza kw amakini Mwenyekiti wa Kamati Lon do Mwenyekiti Londo akitanabaisha jambo Wabunge w

KUSUASUA UJENZI LAINI YA UMEME TABORA-URAMBO KWAMSIKITISHA DKT. BITEKO

Image
📌 Aagiza Meneja Mkuu ETDCO kuondolewa 📌 Azitaka Taasisi za Wizara ya Nishati wasifanye kazi kwa mazoea 📌 Asema Watendaji wasioweza kuishi Maono ya Rais Samia wajitafakari Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amekagua mradi wa ujenzi wa Kituo cha Kupoza umeme cha Uhuru kilichopo wilayani Urambo mkoani Tabora na kueleza kutoridhishwa kwake na kazi ya ujenzi wa laini ya msongo wa  kV 132 kutoka Tabora hadi Urambo ambayo inatekelezwa na kampuni tanzu ya TANESCO (ETDCO). Kazi ya ujenzi wa Kituo cha kupoza umeme cha Uhuru imegawanyika katika sehemu mbili ambapo ujenzi wa kituo cha kupoza umeme unafanywa na kampuni ya TBEA kutoka China ambao wamefikia asilimia 84 ya utekelezaji huku kazi ya ujenzi wa laini ya umeme kutoka Tabora hadi Urambo (km 115) ikifanywa na kampuni ya ETDCO ambao wamefikia asilimia 10 tu ya utekelezaji. Kufuatia hali ya kusuasua kwa ujenzi wa laini hiyo, Dkt. Biteko ameiagiza Bodi ya TANESCO kumwondoa Meneja Mkuu wa ETDCO Muhamed Abdallah amba

SIKU YA MISITU DUNIANI (THE INTERNATIONAL DAY OF FORESTS) - MUSOMA VIJIJINI WAISHEREHEKEA KWA KUPANDA MITI MASHULENI

Image
TAREHE hii ni  21.3.2024 ni siku ya Umoja wa Mataifa (UN) ya kukumbushana umuhimu wa misitu ya aina zote. UN ilipitisha azimio la siku hii (tarehe 21 Machi ya kila mwaka) kwenye Mkutano wake wa tarehe 28.11.2013 Kaulimbiu 2024: Misitu na Ubunifu                         (Forests and Innovations) Jimbo la Musoma Vijijini: Misitu na Ubunifu Kwa muda wa zaidi ya wiki mbili, Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo akishirikiana na Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Dkt Khalfany Haule, na Meneja wa Misitu (TFS) Wilaya, Ndugu Boniphace Kaberege wamekuwa wakigawa na kupanda mamia ya miche ya miti ya matunda, mbao na kivuli kwenye shule kadhaa za misingi na sekondari za Jimboni mwetu. Kampeni hii ni endelevu! Sherehe ya Uzinduzi wa Upandaji miti Jana, TFS Wilaya chini ya uongozi wa Ndugu Boniphace Kaberege ilitoa mafunzo ya umuhimu wa misitu kwa maisha na ustawi wa jamii zetu. Mafunzo hayo yalifanywa kwenye Sekondari ya Suguti. Wanafunzi na Walimu wote wa Sekondari hiyo, wakiongozwa na