Posts

Showing posts from July, 2022

WAZIRI MKENDA ATANGAZA TUME YA MIKOPO KWA WANAFUNZI ELIMU YA JUU

Image
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda akitangaza tume ya kuchunguza utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu tarehe 29 Julai 2022 Jijini Dar es laam wakati akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari nchini juu ya mwelekeo wa Wizara, Vipaumbele na maeneo ya kimkakati katika utekelezaji kwa Mwaka wa fedha 2022/23. Na Mathias Canal, WEST Wakati dirisha la maombi ya mikopo kwa mwaka wa masomo 2022/2023 likiwa wazi kwa muda wa siku 70 kuanzia Julai 19 hadi Septemba 30 mwaka huu, Serikali imetangaza Tume ya watu watatu kuchunguza utoaji wa mikopo.   Tume hiyo itaongozwa na Prof Allan Mushi ambaye ni mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe Morogoro, Idd Makame kutoka Zanzibar na Dkt Martin Chegeni ambao wote kwa pamoja ni wataalamu wa mifumo waliobobea katika sayansi ya Kompyuta na Takwimu.   Tume hiyo itachunguza uhalali katika utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia mwaka 2017/2018 mpaka 2021/2022 ili kubaini kama kulikuw

WAZIRI MAKAMBA,AWATOA HOFU WAKAZI WA VIJIJI 20 VYA LUDEWA KUHUSU UMEME

Image
  Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba akizungumza na Wananchi katika Kijiji cha Lugarawa wilayani Ludewa baada ya kufika kijijini hapo kutatua changamoto ya upatikanaji umeme.  Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba akimsikiliza mmoja wa Wananchi katika Kijiji cha Lugarawa wilayani Ludewa baada ya kufika kijijini hapo kutatua changamoto ya upatikanaji umeme.  Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba akizungumza na  mmoja wa Wananchi katika Kijiji cha Lugarawa wilayani Ludewa baada ya kufika kijijini hapo kutatua changamoto ya upatikanaji umeme.  ************************** Waziri wa Nishati, Mhe Januari ametoa ufumbuzi wa changamoto ya miaka mingi ya  mgawo wa umeme wa masaa 12 kwa vijiji 20 katika Wilaya ya Ludewa ambavyo vimekuwa vikipata umeme kutoka kampuni ya Madope.  Kampuni hiyo ya Madope inayoendesha mradi huo mdogo wa umeme wa maji (MW 1.7  inaundwa na wadau mbalimbali wakiwemo Jumuiya ya Watumia Umeme Lugarawa na Halmashauri ya Wil

MWENGE WA UHURU WAZINDUA MRADI WA MAJI NGOGWA -KITWANA KAHAMA

Image
  Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahili Nyanzabara Geraruma akimtwisha Ndoo ya Maji Mwanamke, mara baada ya kumaliza kuzindua Mradi wa Majisafi na Salama kutoka Ziwa Victoria wa Ngogwa-Kitwana katika Manispaa ya Kahama. Na Marco Maduhu, KAHAMA KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahili Nyanzabara Geraruma, amezindua Mradi wa Majisafi na Salama kutoka Ziwa Victoria wa Ngogwa

RAIS DKT.HUSSEIN ALI MWINYI AJUMUIKA NA WANAFUNZI WA KIDATU CHA SITA NA CHA NNE KATIKA CHAKULA ALICHOWAANDALIA IKULU NDOGO PAGALI PEMBA

Image
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj.Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Viongozi wa Masjid Munawwara Mfikiwa Wilaya ya Chakechake Pemba,alipowasili kwa ajili ya kuhudhuria Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Masjid hiyo leo 29-7-2022.(Picha na Ikulu) RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na kuwasalimia Wananchi wa Mfikiwa baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa, iliyofanyika katika Masjid Munawwara Mfikiwa leo 29-7-2022.(Picha na Ikulu) RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akitikia dua ikisomwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh.Saleh Omar Kabi (kulia kwa Rais) baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Masjid Munawwara Mfikiwa Wilaya ya Chakechake Pemba leo 29-7-2022.(Picha na Ikulu  

KINANA ASHAURI BARABARA NNE DAR-TUNDUMA JIANDAE KUHESABIWA

Image
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana akivishwa Skafu Alipowasili katika ofisi za CCM Mkoa wa Mbeya. Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana akipokewa na viongozi na wanachana katika ofisi za CCM Mkoa wa Mbeya. Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana akipitia ripoti ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM na Uhai wa Chama katika Ofisi za CCM Mkoa wa Mbeya. akisamiana na Wanachama na Viongozi wa CCM  katika ukumbi wa mikutano wa Benjamin Mkapa kwa ajili ya mkutano wa ndani na wanachama na viongozi wa CCM na serikali. Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka, Akizungumza patoja na Viongozi na wanachama wa CCM  katika ukumbi wa mikutano wa Benjamin Mkapa mkoani Mbeya Wanachama Wa Chama Cha Mapinduzi wakifurahia Jambo wakati wa kakao Cha Makamu Mwenyekiti wa CCM Ndg Abdul Rahman kinana pamoja na Viongozi wa CCM Mko

WANANCHI SAME WAMUUA KIBOKO ALIYEKUWA AKIWASUMBUWA

Image
Kiboko dume ambaye kwa muda mrefu amekuwa akisumbua Wananchi wa Kata ya Mabilioni Wilayani Same Mkoa wa Kilimanjaro na kukwamisha shughuli za maendeleo kama  kilimo, ufugaji na uchotaji wa maji katika Mto Pangani ameuawa kwa kupigwa risasi katika msako ulioongozwa na vikosi kutoka TAWA  Kiboko huyo aliyepewa jina la Babu ambaye ameua jumla ya Watu  6, zaidi ya ng’ombe 8, punda na mbuzi tangu mwaka 2017  alikuwa akihusishwa na imani za kishirikina kwani jitihada mbalimbali za kumdhibiti hazikufanikiwa katika kipindi chote Tarehe 17 Juni 2022 kiboko huyo alimuua kwa kumshambulia Mwanaume mmoja aliyekuwa anakwenda shambani kumwagilia ndipo Mkuu wa Wilaya ya Same, Edward Mpogolo alipoagiza kuhakikisha kila mbinu zinatumika kumuua Kiboko huyo ili Wananchi warudi kufanya shughuli za maendeleo kwa amani Baada ya kuanza msako kiboko huyo aliuawa tarehe 28 Julai 2022 saa 11 alfajiri baada ya kuweka mtego na kupigwa risasi ya kichwa na Mzee Ally Miraji Sengela (Hunter) aliyesaidiwa na Mzee Fue O

TANZANIA, USWISI KUENDELEZA USHIRIKIANO

Image
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akitoa hotuba yake katika hafla ya kuadhimisha Siku ya Taifa ya Uswisi iliyofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 28 Julai 2022 Balozi wa Uswisi nchini Mhe. Didier Chassot akitoa hotuba yake katika hafla ya kuandimisha Siku ya Taifa ya Uswisi iliyofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 28 Julai 2022 Hafla ya kuadhimisha Siku ya Taifa ya Uswisi iliyofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 28 Julai 2022 ikiendelea. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula na alozi wa Uswisi nchini Mhe. Didier Chassot wakifurahia jambo kwenye hafla ya kuadhimisha Siku ya Taifa ya Uswisi iliyofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 28 Julai 2022 TANZANIA, USWISI KUENDELEZA USHIRIKIANO Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Uswisi zimeahidi kuendeleza zaidi ushirikiano katika nyanja mbalimbali ikiwemo teknolojia ya habari na mawasiliano, elimu, afya, ujenzi wa miund

TANZANIA, URUSI KUONGEZA MAENEO YA USHIRIKIANO

Image
  Serikali ya Tanzania na Urusi zimekubaliana kuongeza maeneo ya ushirikiano katika sekta za biashara na uwekezaji,utalii pamoja na utamaduni. Makubaliano hayo yamefikiwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk alipokutana kwa mazungumzo na Balozi wa Urusi nchini, Mhe. Andrey Levonovish Avetsyan katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam. Balozi Mbarouk amesema kuwa Tanzania na Urusi zimekuwa na ushirikiano wa muda mrefu wa kihistoria ambao uliasisiwa na Waasisi wa Mataifa hayo mawili…….“ kutokana na uhusiano mzuri tulionao umechangia kuimarisha sekta ya utalii, elimu pamoja na afya,” alisema Balozi Mbarouk Balozi Mbarouk aliongeza kuwa Tanzania na Urusi zitaendelea kujikita zaidi kufungua maeneo mapya ya ushirikiano katika sekta za biashara, uwekezaji, utalii na masuala mengine ya kiuchumi kwa maslahi mapana ya mataifa hayo. Kwa upande wake Balozi wa Urusi nchini, Mhe. Andrey Levonovish Avetsyan ameishukuru Tanzania kwa

WAZIRI MULAMULA AMUAGA BALOZI WA PAKISTAN NCHINI TANZANIA

Image
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akimsikiliza Balozi wa Pakistan anayemaliza kipindi chake cha kuhudumu nchini Mhe. Mohammad Saleem alipokuwa akimuaga katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam. Mazungumo baina Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula Balozi wa Pakistan anayemaliza kipindi chake cha kuhudumu nchini Mhe. Mohammad Saleem yakiendelea katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb)  na Balozi wa Misri nchini Tanzania Mhe. Mohamed Gaber wakiwa katika mazungumzo yaliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb)  na Balozi wa Misri nchini Tanzania Mhe. Mohamed Gaber wakiwa katika picha ya pamoja na Maafisa wa Ubalozi na Wizara Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano

NMB yazindua mikopo ya nyumba

Image
  Afisa Mkuu wa Ukaguzi wa Ndani wa Benki ya NMB, Benedicto Baragomwa, akiagana na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Kheri James, baada ya kuzindua kongamano la fursa za makazi lililoandaliwa na Benki ya NMB jijini Dar es Salaam leo Julai 29, 2022. Kulia ni Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam, Donatus Richard na wa pili kulia ni Mkuu wa Idara ya Wateja Binafsi NMB, Aikansia Muro. Benki ya NMB yatoa mikopo ya nyumba yenye thamani ya zaidi ya bilioni 35 nchini nzima Na Mwandishi Wetu Benki ya NMB kupitia bidhaa yake ya ‘Makazi Loan’ kwa mkipindi cha miaka mitatu imetoa Zaidi ya silingi bilioni 35 kuwezesha waTanzania mbalimbali kupata mikopo ikiwa ni utekelezaji wa dhamira ya benki hiyo katika kuendeleza ujenzi wa nyumba nchini . Akizungumza wakati wa semina iliyowakutanisha wadau mbalimbali wa mnyororo wa thamani ya sekta ya ujenzi iliyoandaliwa na benki hiyo jijini Dar es Salaam jana, Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Benki ya NMB, Benedicto Baragomwa alisema bidhaa hiyo ya 'Mak

TMDA YALONGA NA WANAHABARI KUHUSU MIKAKATI YAO

Image
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA),  Dkt. Adam Mitangu Fimbo,akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya habari Maelezo jijini Dodoma  ambapo alisema kuwa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba ni taasisi ya Serikali iliyopo chini ya wizara ya Afya yenye jukumu la kulinda afya ya jamii kwa kudhibiti ubora, Usalama na ufanisi wa dawa chanjo, vifaa tiba na vitendanishi pamoja na udhibiti wa bidhaa za Tumbaku. Mkurugenzi huyo aliendelea kusema kwamba Kwa kipindi cha  Julai 2021 hadi 2022 kwa jumla malengo mkakati wa TMDA yametekelezwa kwa ufanisi  na kwa mafanikio makubwa. TMDAemeendelea kushikilia cheti cha ithibati kwa  kiwango cha ISO 9001;2015 baada ya kukidhi vigezo kufuatia kaguzi zilizofanyika, Kaguzi hizo hufanyika kila baada ya miaka mitatu na wahakiki hutoka nje ya nchi. Mkurugenzi akiwaonyesha wanahabari vyeti amabavyo hutolewa kwa ubora wa dawa Wanahabari wakimsikiliza mkurugenzi alaipokuwa akizungumza Mkurugenzi Msaidizi idara ya habari Maelezo Za