Posts

Showing posts from May, 2025

BUNGE LAMKABIDHI TUZO MAALUM RAIS DKT. SAMIA

Image
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, akipokea Tuzo Maalumu ya Heshima kutoka kwa Bunge la Tanzania ikikabidhiwa na Spika wa Bunge Dkt, Tulia Ackson ikiwa ni Tuzo ya kuthamini kazi Kubwa na Nzuri aliyofanya katika kuleta Maendeleo Nchini. Hafla ya kukabidhi Tuzo hiyo imefanyika Viwanja vya Bunge la Tanzania Mkoani Dodoma leo.    

WAZIRI MKUU AKUTANA NA MAKAMU WA RAIS WA SHIRIKA LA MAENDELEO LA JAPAN (JICA) JICA

Image
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Makamu wa Rais wa Shirika la Kimataifa la  Maendeleo la Japan (JICA), Bi Miyazaki Katsura  (kulia)  katika mazungumzo yaliyofanyika kwenye hoteli ya New Otani, Tokyo nchini Japan, Mei 28, 2025. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) …. *JICA, Benki ya Dunia na AFDB watoa Dola za Marekani mil 516 miradi ya kilimo *Washauri elekezi wawili Mjapan na Mtanzaniia wawekwa TIC kurahisha uwekezaji   WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA) limeihakikishia Serikali ya Tanzania inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa itaendelea kushirikiana nayo katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ya wananchi. Hatua hiyo imetokana na namna ambavyo Serikali imekuwa ikisimamia kikamilifu matumizi ya fedha mbalimbali zinazotolewa na wadau wa maendeleo likiwemo shirika hilo. Waziri Mkuu amesema “Serikali itaendelea itaendelea kusimamia ...

MAAGIZO MAALUM KWA KATIBU MKUU CCM KUHUSU UTEUZI WA WAGONBEA

Image
  Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambaye pia ni Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Mei 30, 2025, ametoa maagizo mahsusi kwa Katibu Mkuu wa CCM kuhusu mchakato wa uteuzi wa wagombea kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025. Agizo hilo limetolewa wakati wa hotuba yake kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalum wa CCM uliofanyika jijini Dodoma, ambapo pia alizindua Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa kipindi cha 2025–2030. Katika hotuba yake, Rais Samia alielekeza wazi kuwa majina ya wanachama wanaotaka kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya CCM yawasilishwe kwake ifikapo tarehe 1 Juni 2025. Alisisitiza kuwa hakuna mwanachama anayepaswa kuwasilisha jina lake kwa madai ya kuungwa mkono na yeye binafsi au Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi. Alibainisha kuwa nafasi maalum kumi za uteuzi zitashughulikiwa na viongozi hao baada ya uchaguzi mkuu. “Ninamuagiza Katibu Mkuu kuhakikisha kuwa majina ya wanaotaka kugombea yamefika mezani kwangu kabla ya tarehe 1 Juni. Hakuna mgombea a...

MAENEO SITA YA VIPAUMBELE UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM 2020/2025. DKT. BITEKO

Image
Dkt. Doto Biteko akizungumza katika mkutano huo Wanahabari wakiwajibika katika mkutamno huo  * CCM yajivunia kuimarisha upatikanaji wa huduma bora kwa jamii *Rais Samia asema CCM kuzindua Ilani yake kesho * CCM yazalisha ajira 800,000 kwa vijana 2020/2025 Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita aliyowasilisha ni ya mwisho katika utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2020. Amesema hayo Mei 29, 2025 wakati akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Mkutano Mkuu Maalum wa CCM Taifa – 2025 jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa. Ametaja maeneo sita muhimu ya vipaumbele katika utekelezaji wa Ilani hiyo ya CCM kuwa ni pamoja na kulinda na kuimarisha misingi ya utu, usawa, haki na uongozi bora ili kudumisha amani, umoja na mshikamano wa Taifa. Dkt. ...