WANA CCM TUSIBWETEKE, UCHAGUZI HUU UNAUSHINDANI MKUBWA TUJIPANGE -KINANA.
Makamu
Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara Abdulrahman Kinana akizungumza na
Viongozi Wa CCM katika kikao maalumu cha Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya
Rorya mkoani Mara akiwa katika ziara ya kuimarisha Chama mkoani humo
Makamu
Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara Abdulrahman Kinana Akisalimiana na
Mtoto wa Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere Ndg. Madaraka
Nyerere, alipofika kuzuru kaburi hilo Mwitongo, wilayani Butiama Mkoa wa
Mara akiwa katika ziara ya kuimarisha mkoani humo.
Makamu
Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara Abdulrahman Kinana akiweka shada la
maua katika kaburi la Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere alipofika
kuzuru kaburi hilo Mwitongo, wilayani Butiama Mkoa wa Mara akiwa katika
ziara ya kuimarisha mkoani humo.
@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@
MAKAMU
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Abdulrahman
Kinana amewaeleza wanachama wa Chama hicho uchaguzi wa Serikali za mitaa
mwaka huu na uchaguzi mkuu mwakani utakuwa na ushindani hivyo
wasibwete.
Akizungumza
katika kikao kazi cha ndani na Wana CCM Wilaya ya Rorya mkoani Mara
ambako anaendelea na ziara ya kikazi, jana, Kinana amesema kuna kanuni
za uchaguzi za vyombo vya dola.
“Tunatakiwa
tufuate maadili ya uchaguzi na tufanye kila linalowezekana na nimepata
ahadi nyingi kwamba tutashinda kwenye uchaguzi unaokuja wa Serikali za
mitaa mwaka huu, niwambie utakuwa na ushindani.
“Kwa
sababu zile sheria za uchaguzi zilizotungwa bungeni zinatoa nafasi ya
ushindani, kwa hiyo tusibwete, badala yake tujipange vizuri. Tunatakiwa
tujipange wanachama ili tupate ushindi wa kishindo mwaka huu pamoja na
uchaguzi mkuu mwaka 2025,” amesema.
Kinana
amesisitiza kuwa kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa ni vema wana
CCM wakashikamana na kama kuna mtu mchana yuko upande wa CCM na usiku
upinzani anapaswa kuwekwa kando haraka.
“Hatuwezi
kukubali watu wavae nguo za kijani mchana halafu baadaye unabadilika,
hatuwezi kukubali,” amesema Kinana ambaye pia ni Mlezi wa CCM Mkoa wa
Mara.
Aidha,
amesisitiza umoja na mshikamano na kama kuna changamoto zozote
wanapaswa kuzizungumza kama Chama kupata ufumbuzi wake. “Tunatakiwa
tushikamane na tuzingatie kanuni na katiba yetu ya CCM.”
Kuhusu
viongozi ambao wamechaguliwa na sasa wako madarakani wakiwemo madiwani
na wabunge, Kinana amesema waachwe wafanye kazi na hakuna sababu ya
kuwavuruga.
“Kuna
watu wanaitwa madalali wa vyeo, kazi yao ni kuuza vyeo anakuja kwako
anakwambia mwaka ujao unatakiwa tukuchague wewe, ukisikia hivyo ujue
anatafuta riziki na akimaliza kuzungumza anaomba nauli, ujue huyo ni
dalali.
“Wakati mwingine anakupigia simu anakwambia hebu nirushie bando kuna habari nataka nikupe. Hao ni madali, ukija kuanguka anasema mimi nilikusaidia ila wajumbe wamekuangusha.” Ameeleza.
Amesema
kwa kuwa kipindi cha uchaguzi bado hakijafika na kuna watu wanatamaa ya
kuwa madiwani, ingawa jambo hilo si dhambi, lakini ni muhimu utaratibu
wa Chama na kanuni mbalimbali ziheshimiwe.
Katika
hatua nyingine Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Bara
Abdulrahman Kinana amewasisitiza wanachama wa chama hicho na wananchi
kwa ujumla kuachana na tabia za ukabila akieleza kuwa ni mambo ya
kizamani na yanawagawa.
Akizungumza
na wajumbe wa halmashauri kuu ya CCM Wilaya ya Roria, mkoani Mara,
alisema nchi kuwa na makabila ni jambo la kawaida ila ukabila ni jambo
baya, akieleza kuwa kumuhukumu mtu kwa jambo ambalo hana uwezo nalo sio
sahihi.
Kinana
alisema hayo baada ya baadhi ya wajumbe kuibua hoja kwamba kuna mambo
yanafanyika katika wilaya ya Roria ambayo yanaashiria kuwepo kwa
changamoto ya ukabila miongoni mwao.
Alisema
Baba wa taifa Julius Nyerere ametoka mkoa huo, na ni kabila dogo sana
na ameongoza nchi kwa miaka 24, na kwamba alipendwa, aliheshimiwa,
alithaminiwa na alitukuzwa sio kwa sababu ya ukabila bali ni kazi
aliyokuwa anafanya, utendaji na uadilifu wake uliomfanya aheshimika
Tanzania, Afrika na duniani.
“Sasa
usimpe mtu nafasi ya uongozi kwasababu ya kabila lake, dini au umbile
usimuhukumu, hayo ni mambo ya kizamani sana, tuangalie mtu anauwezo
atafanya kazi atajituma na kujitolea, mnampima kwa vigezo sio kwamba
huyu ni ndugu yangu.
“Mtu
mmoja kwenye kabila lako akipata cheo anakusaidia nini hasa wewe
mwenyewe? Uko kijijini kule mngekuwa mnagawana mshahara sawa, kila mmoja
anakuletea 300,000 kutoka kwenye mshahara wake kwasababu ni kabila lako
sawa… wekeni watu kwa uwezo,” alisisitiza Kinana.
Aidha,
alieleza kuwa jambo ambalo Baba wa taifa aliwaachia ni umoja wa
kitaifa, akitolea mfano kwamba kuna nchi jirani, hakuzibainisha kwa
majina, kwamba mtu hawezi kuwa gavana wa jimbo kama anatoka sehemu
nyingine, lakini Tanzania wanafanya kazi nchi nzima.
Comments
Post a Comment