NG'OMBE ZAIDI YA 341,098 WAPIGWA CHAPA SIMANJIRO


Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti (wapili kulia) baada ya kupewa zawadi ya nguo ya jadi na wafugaji wa kata ya Naisinyai kwenye ziara yake Wilayani Simanjiro, kulia ni Mkuu wa wilaya hiyo mhandisi Zephania Chaula na kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Jackson Leskar Sipitieck na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa huo Arnold Msuya. 


Ng'ombe 341,098 wamepigwa chapa Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, ili kutekeleza agizo la Serikali la upigaji chapa mifugo kwa ajili ya utambuzi na kuepuka migogoro ya mara kwa mara. 

Katibu Tawala wa Wilaya ya Simanjiro Zuwena Omary, aliyasema hayo juzi wakati akisoma taarifa kwa mkuu wa mkoa huo Alexander Mnyeti. Omary alisema lengo la wilaya hiyo ni kupiga chapa ng'ombe 437,925 hivyo wamefikia asilimia 79 hadi kufikia Desemba 31 mwaka jana. 
Alisema zoezi hilo lilitarajiwa kukamilika mwezi Desemba mwaka jana ila baada ya serikali kuongeza muda hadi Januari 31 mwaka huu, watakuwa wamefanikiwa kukamilisha. Alisema wilaya hiyo ina mabwawa mawili ya Nyumba ya Mungu na Kidapash, ambayo shughuli za uvuvi zinafanyika na jitihada za kudhibiti uvuvi haramu zimefanyika. 
Kwenye sekta ya kilimo, umwagiliaji na ushirika alisema kuna ekari 346,000 zinazofaa kwa kilimo ambapo takribani ekari 144,00 hutumika kwa kilimo cha mazao ya chakula na biashara. "Mahitaji ya chakula kwa mwaka kwa wakazi wote ni tani 42,000 za nafaka na hali ya chakula ni ya kuridhisha kwenye maeneo mengi kwani wananchi wanatumia chakula kilichovunwa msimu wa Kilimo wa 2016/2017. 
Alisema kwa upande wa mradi wa maji kutoka mto Ruvu hadi mji mdogo wa Orkesumet, serikali itautekeleza kupitia sh40 bilioni, za fedha za ndani na ufadhili wa benki ya maendeleo ya watu wa uarabuni. Mkuu wa mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti aliagiza kila wilaya ya mkoa huo kuhakikisha inakuwa na viwanda 15 ili kutekeleza agizo la serikali la kila mkoa uwe na viwanda 100.

Mnyeti alisema wilaya ya Simanjiro iwe na viwanda 15 na nyingine zitekeleze hilo ili kuhakikisha uzalishaji wa ajira unafanyika na kufikia lengo la kuwa na uchumi wa kati.

WAKULIMA SKIMU YA UMWAGILIAJI MPUNGA NYAMAGOGO MANYONI WALALAMIKIA HALMASHAURI KUTELEKEZA KATAPILA

Na Jumbe Ismailly-Manyoni 
WAKULIMA wa skimu ya umwagiliaji mpunga ya Nyamagogo,iliyopo katika Kijiji cha Chikuyu,wilayani Manyoni,Mkoani Singida wameiomba serikali kuangalia uwezekano wa kuitengeneza katapila lililokuwa likisaidia kusafisha mifereji ya kuoitisha maji kwenye mashamba hayo ili waweze kuongeza uzalishaji wa zao hilo ambao kwa sasa umepungua.

Mwenyekiti wa skimu hiyo ya umwagiliaji Nyamagogo,Abdallah Rajabu Maganga alisema katapila hilo ambalo limetelekezwa tangu mwaka 2012 kutokana na kukosekana kwa vipuli vinavyohitajika kulifufua kwa sababu kifaa hicho ni aina ya kizamani na hivyo matengenezo yake siyo rahisi na badala yake lingefaa kuuzwa kwa njia yam nada.

“Tatizo wanavyosema sema ni greda la kizamani unaona bwana spea zake hazipatikani sasa tunajiuliza wanaproses kwamba wanataka kuliuza unaona bwana sasa huyo unayemuuzia atalifanyia nini kama kweli ni greda la zamani ambapo hakauna spea”alifafanua Maganga.

Alifafanua mwenyekiti huyo wa (WAUWA) kwamba ili kuwasaidia wakulima wa zao hilo na kwa sababu sasa hivi dunia ni ya utandawazi spea zinapatikana sehemu yeyote pale hata kama Marekani wanaweza kwenda au kuagiza ili liweze kutengenezwa kwa manufaa ya wakulima hao wa skimu ya umwagiliaji.

Mwenyekiti huyo hata hivyo aliyataja baadhi ya athari wanazopata wakulima hao kuwa ni pamoja na kujaa kwa maji ambayo hupeleka na mchanga na kusababisha mto kuwa juu na kuanza kukata mikato,lakini endapo wangelipata greda hilo lingeweza kuwasaidia kutoa michanga na maji kufuata mkondo wake unaokubalika badala ya hivi sasa ambapo maji mengi yanapotea bure huku kipato chao kikipotea.

Naye diwani wa kata ya Chikuyu,Benjameni Kamoga alisema kuwa kwa taarifa za awali kutoka Halmashauri zilisema kinachosumbua katapila hilo ni kukosekana kwa cheni ambayo inahitaji nguvu katika matengenezo ili wakulima waweze kunufaika na kuwepo kwa miundombinu hiyo ya kilimo.

“Kwa mfano kuna mikato ambayo imesababishwa na maji kujaa pamoja na ujenzi wa nguzo za umeme,Tanesco walikuja wakatuzibiazibia lakini hawakujua ukubwa, kwa maana hiyo kama lingekuwa zima hili lingetufanyiakazi nzuri”.alibainisha diwani Kamoga.
baadhi ya Skimu za umwagiliaji mashamba ya mpunga Nyamagogo,wilayani Manyoni,Mkoani Singida yaliyoathirika kutokana na kujaa kwa maji ambayo hupeleka na mchanga na kusababisha mto kuwa juu na kuanza kukata mikato,kwa sababu ya kukosekana kwa katapila litakalotoa michanga na maji kufuata mkondo wake unaokubalika badala ya hivi sasa ambapo maji mengi yanapotea bure huku kipato chao kikishuka. 
baadhi ya mitaro iliyojaa mchanga pamoja na takataka na hivyo kusababisha maji kukosa mwelekeo na hivyo kusambaa ovyo kwenye maeneo mengine.
Katapila lililokuwa likiwasaidia wakulima wa skimu ya umwagiliaji mpanga Nyamagogo,wilayani Manyoni,Mkoani Singida kutojaa kwa maji ambayo hupeleka mchanga na kusababisha mto kuwa juu na kuanza kukata mikato,kwa sababu ya kukosekana kwa katapila litakalotoa michanga na maji kufuata mkondo wake unaokubalika badala ya hivi sasa ambapo maji mengi yanapotea bure huku kipato chao kikishuka.(Picha zote Na Jumbe Ismailly)

KAMISHNA JENERALI MAGEREZA, DK. JUMA MALEWA ATETA NA MAHABUSU GEREZA KEKO MAADHIMISHO WIKI YA SHERIA NCHINI

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akiwasili katika Gereza la Mahabusu Keko jijini Dar es salaam katika ziara yake ya kikazi kukagua gereza hilo leo Januari 28, 2018 ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Sheria hapa nchini. Jeshi la Magereza ni moja ya wadau muhimu katika sekta ya Sheria hapa nchini.Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akisalimiana na Mkuu wa Gereza la Mahabusu Keko, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Kiangi Abdallah alipowasili katika ziara yake ya kikazi kukagua gereza hilo ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Sheria hapa nchini. Wengine ni Maafisa Waandamizi wa Jeshi hilo. Mkuu wa Gereza la Mahabusu Keko, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Kiangi Abdallah akitoa taarifa fupi mbele ya Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa kabla ya kumkaribisha kuongea na Mahabusu wa Gereza Keko(hawapo pichani).Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akiongea na Mahabusu wa Gereza Keko(awapo pichani) leo Januari 28, 2018 alipotembelea gereza hilo ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Sheria hapa nchini.Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akimsikiliza Mahabusu ambaye ni raia wa kigeni mara baada ya kuongea na Mahabusu wa Gereza Keko.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akikagua jiko la gesi katika Gereza la Mahabusu Keko. Jeshi la Magereza tayari limeanza kutekeleza maelekezo ya Serikali ya kuachana na matumizi ya kuni kwa kutumia nishati ya gesi katika baadhi ya magereza nchini hivyo kutunza mazingira.
Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakiwa katika chumba Maalum, Gereza Keko ambapo chumba hicho kitatumika katika Uendeshaji wa Mashauli mbalimbali kwa kutumia njia ya TEHAMA. Uwepo wa mfumo huu utalipunguzia gharama Jeshi la Magereza katika kuwasafirisha Mahabusu mahakamani na kuwarejesha magerezani.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa(katikati) akiwa katika Chumba Maalum ambacho kitatumika katika uendeshaji wa mashauli kwa kutumia njia ya TEHAMA(wa kwanza kushoto) ni Kaimu Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Noel James(wa kwanza kulia) ni Mkuu wa Gereza Keko, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Kiangi Abdallah (Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

Comments

Popular posts from this blog

AMANI YETU TUILINDE NAIBU WAZIRI CHANDE AZUNGUMZA KATIKA IJITIMAI JIJINI DODOMA

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.