URA SACCOS YAKABIDHI VIFAA TIBA KWA HOSPITALI ZA JESHI LA POLISI


 Kamishna wa Operesheni na Mafunzo kutoka Jeshi la Polisi nchini, NsatoMarijani   akizungumza kabla ya kupokea Vifaa Tiba kwa ajili ya Hospitali za jeshi la Polisi vilivyotolewa na Chama cha kuweka akiba na Kukopa cha URA Saccos  katika Hospitali ya Kilwa Road Jijini Dar es Salaam
 Kamanda wa kikosi cha Afya nchini, Paul Kasabago akizungumza juu ya hali ya Vituo vya Afya vya Jeshi la Polisi nchini.
 Kikosi cha Bendi cha Jeshila Polisi nchini kikitoa Burudani kwa watu waliofika katika hafla ya kupokea vifaa tiba kutoka URA Saccos
 Naibu Kamishna Azizi Mohamed ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Kuweka na kukopa cha URA Saccos  akizungumz akatika hafala hiyo yamakabidhiano ya vifaa Tiba iliyofanyiak Kilwa Road Jijini Dar es Salaam
  Kamishna wa Operesheni na Mafunzo kutoka Jeshi la Polisi nchini, NsatoMarijani, akikata utepe kuashiria uzinduzi na kupokea Vifaa Tiba kutoka URA Saccos
  Kamishna wa Operesheni na Mafunzo kutoka Jeshi la Polisi nchini, NsatoMarijani akifanyiwa kipimo cha Presha na Sukari kutoka kwa Afisa Muuguzi PC Stella Sizya kutoka Hospitali ya Rufaa ya Polisi Kilwa Road.
  Kamishna wa Operesheni na Mafunzo kutoka Jeshi la Polisi nchini, NsatoMarijani  akionyeshwa baadhi ya Vifaa  tiba vilivyotolewa na URA Saccos
  Kamishna wa Operesheni na Mafunzo kutoka Jeshi la Polisi nchini, NsatoMarijani akisaini karatasi za makabidhiano ya Vifaaa na  Naibu Kamishna Azizi Mohamed ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Kuweka na kukopa cha URA Saccos
 Kikundi cha Ngoma cha Jeshi la Polisi nchini kikitoa Burudani
Picha ya Pmoja ya viongozi wa meza kuu na wakuu mwa vikosi mbalimbali
 

KUBENEA ATOA MILIONI 14 ZA MFUKO WA JIMBO KUJENGA VIVUKO VIWILI MABIBO

   Mbunge wa Jimbo la  Ubungo, Saed Kubenea akikabidhi fedha kwa ajili ya kulipia kivuko kilichokuwa watu wakilipishwa 200 kwa kila wakipita.
 Mbunge wa Jimbo la  Ubungo, Saed Kubenea akizungumza na wakazi  wa Mabibo wakati alipokwa akifanya ziara ya kutembelea miradi na kusikiliza kero za wananchi, ambapo aliweza kutoa kiasi cha Shilingi Milioni 14 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja na kuamua kununua kivuko cha mtu Binafsi ili watu waweze kupita bure kuliko awali ambapo walikuwa wakilipishwa shilingi 200.
  Mbunge wa Jimbo la  Ubungo, Saed Kubenea akizungumza na wakazi  wa Mabibo wakati alipokwa akifanya ziara ya kutembelea miradi na kusikiliza kero za wananchi
  Mbunge wa Jimbo la  Ubungo, Saed Kubenea  akiwa katika mitaa ya  Mabibo wakati alipokwa akifanya ziara ya kutembelea miradi na kusikiliza kero za wananchi
  Mbunge wa Jimbo la  Ubungo, Saed Kubenea akitembea na wakazi  wa Mabibo wakati alipokwa akifanya ziara ya kutembelea miradi na kusikiliza kero za wananchi
 Mmoja ya wakazi wa mabibo akiwasilisha hoja yake kwa mbunge wa jimbo la Ubungo Saed Kubenea wakati alipofanya ziara ya kusikiliza kero za Wananchi
 Mmoja ya wakazi wa mabibo akiwasilisha hoja yake kwa mbunge wa jimbo la Ubungo Saed Kubenea wakati alipofanya ziara ya kusikiliza kero za Wananchi

SERIKALI YASIKIA KILIO CHA WADAU WA SEKTA YA UWINDAJI WA KITALII NCHINI, YAONGEZEA MIAKA MIWILI YA UMILIKI WA LESENI ZA VITALU

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wadau wa sekta ya uwindaji wa kitalii katika mkutano uliondaliwa na Wizara yake mjini Dodoma jana kwa ajili ya kujadili mikakati mbalimbali ya kuimarisha sekta hiyo ikiwemo utekelezaji wa azma ya Serikali ya kuanzisha utaratibu mpya wa utoaji wa leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii kwa njia ya mnada. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mej. Jen. Gaudence Milanzi na Naibu Katibu Mkuu, Dk. Aloyce Nzuki (kulia).  

Na Hamza Temba, Dodoma
...............................................................
Serikali imesikia kilio cha wadau wa sekta ya uwindaji wa kitalii nchini na kuamua kuongeza muda wa miaka miwili ya umiliki wa leseni za vitalu 95 vya uwindaji wa kitalii ambazo zilikuwa ziishe muda wake tarehe 31 Desemba mwaka huu (2017).

Uamuzi huo umefikiwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla wakati wa kikao cha majumuisho na watendaji wa Wizara hiyo muda mfupi baada ya kumalizika kwa mkuano wa wadau wa sekta hiyo ulioandaliwa na Wizara hiyo mjini Dodoma jana.

Akizungumzia uamuzi huo Dk. Kigwangalla alisema, lengo ni kuwapa muda wawekezaji hao ili waweze kujiandaa na mabadiliko ya mfumo mpya wa utowaji wa leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii kwa njia ya mnada ikiwemo kurudisha baadhi ya gharama za uwekezaji walizoweka katika vitalu hivyo.

Awali akizungumza katika mkutano huo wa wadau Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Kampuni za Uwindaji wa Kitalii nchini, Michael Mantheakis alimuomba Waziri Kigwangalla kuwaongezea muda wa umiliki wa leseni zao kuanzia miaka mitano au mitatu na nusu ili waweze kurudisha gharama za uwekezaji walizowekeza katika vitalu hivyo ikiwemo ujenzi wa miundombinu, makambi na vifaa vyake pamoja na maji.

Hata hivyo, Waziri Kigwangalla aliweka wazi msimamo wa Serikali wa kutimiza azma yake ya kuingia kwenye utaratibu mpya wa utoaji wa leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii kwa njia ya mnada na kusema kuwa kamwe haitorudi nyuma na kwamba utekelezaji wa zoezi hilo hauwezi kusubiri muda mrefu kiasi hicho.

Akizungumzia kuhusu hatua ya utekelezaji wa utaratibu huo, Waziri Kigwangalla alisema kwa sasa taratibu za kuandaa Sheria za usimamizi zinaendelea na zinatarajiwa kukamilika mwezi Februari 2018 pamoja na kanuni zake zinazotarajiwa kukamilika mwezi Aprili 2018.

Aidha, alisema mfumo maalumu wa kielektroniki unaandaliwa ambapo maombi yote ya leseni za umiliki wa vitalu vya uwindaji kwa njia ya mnada yatafanyika kwa uwazi kwa njia ya mtandao.

Alisema baada ya kukamilika kwa taratibu zote na mfumo huo mpya wa utoaji wa leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii kwa njia ya mnada na maombi kuwasilishwa, mnada wa kwanza utaanza tarehe 1 Julai, 2018 kwa kuanza kunadi vitalu 61 ambavyo kwa sasa havina wawekezaji.

Mnada wa pili utafanyika mwaka 2020 baada ya kuisha kwa muda huo wa nyongeza wa miaka miwili ukihusisha vitalu 95 vilivyoongezewa muda wa umiliki wa leseni pamoja na vitalu vingine endapo vitabaki katika mnada huo wa kwanza kwa sababu mbalimbali.

Alisema sheria na kanuni zinazoandaliwa hivi sasa zitazingatia mambo muhimu ikiwemo kuwapa nafasi watanzania wenye mitaji midogo kuweza kuingia kwenye biashara hiyo pamoja na kuweka adhabu kali dhidi ya wafanyabiashara watakaohujumu biashara hiyo kwa makusudi.

Mkutano huo wa siku moja ulihudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Gaudence Milanzi, Naibu Katibu Mkuu, Dk. Aloyce Nzuki, wakurugenzi, wakuu wa vitengo na wakuu wa taasisi zilizopo chini ya wizara hiyo na waandhishi wa habari.

Oktoba 22 mwaka huu (2017) wakati akiongoza kikao cha wadau wa sekta ya Maliasili na Utalii mjini Dodoma, Waziri Kigwangalla alitangaza kufuta leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii zilizokuwa zianze mwezi Januari, 2018 ili kupisha utarartibu mpya wa utoaji wa leseni hizo kwa njia ya mnada ikiwa ni mkakati wa Serikali wa kuimarisha sekta hiyo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wadau wa sekta ya uwindaji wa kitalii katika mkutano uliondaliwa na Wizara yake mjini Dodoma jana kwa ajili ya kujadili mikakati mbalimbali ya kuimarisha sekta hiyo ikiwemo utekelezaji wa azma ya Serikali ya kuanzisha utaratibu mpya wa utoaji wa leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii kwa njia ya mnada. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Dk. Aloyce Nzuki.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi (kushoto) akizungumza katika mkutano huo. Kulia ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla.
Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Kampuni za Uwindaji wa Kitalii nchini, Michael Mantheakis (kulia) akiwasilisha mapendekezo yake katika mkutano wa wadau wa sekta ya uwindaji wa kitalii katika mkutano uliondaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii mjini Dodoma jana kwa ajili ya kujadili mikakati mbalimbali ya kuimarisha sekta hiyo ikiwemo utekelezaji wa azma ya Serikali ya kuanzisha utaratibu mpya wa utoaji wa leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii kwa njia ya mnada.
Mdau wa sekta ya uwindaji wa kitalii, Dk. Licky Abdallah akizungumza katika mkutano huo. 
Mdau wa sekta ya uwindaji wa kitalii ambaye pia ni mmilikia wa kampuni ya uwindaji wa kitalii ya Bushman Hunting Safaris, Talal Abood akiwasilisha mapendekezo yake katika mkutano huo. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akisikiliza kwa makini mapendekezo ya wadau wa sekta ya uwindaji wa kitalii katika mkutano uliondaliwa na Wizara yake mjini Dodoma jana. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Gaudence Milanzi.
Baadhi ya wadau wa sekta ya uwindaji wa kitalii wakiwa katika mkutano huo. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wadau wa sekta ya uwindaji wa kitalii katika mkutano uliondaliwa na Wizara yake mjini Dodoma jana kwa ajili ya kujadili mikakati mbalimbali ya kuimarisha sekta hiyo ikiwemo utekelezaji wa azma ya Serikali ya kuanzisha utaratibu mpya wa utoaji wa leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii kwa njia ya mnada. Kulia kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mej. Jen. Gaudence Milanzi na Naibu Katibu Mkuu, Dk. Aloyce Nzuki (kushoto kwake). 
Baadhi ya watendaji wa Wizara ya Maliasili na Utalii na Taasisi zake wakiwa katika mkutano huo. 

KAMPUNI YA PiMAK YAFUNGUA DUKA KUBWA LA KUUZA VYOMBO VYA MAHOTELINI JIJINI ARUSHA








Makamu Mwenyekiti TATO Henry Kimambo katikati akifungua duka kubwa lavifaa mbalimbali vya mapishi kwenye mahoteli linalomilikiwa na kampuni ya kimataifa ya PiMAK ambao ni watengenezaji na wauzaji wa bidhaa hiyo ,Duka hilo lilifunguliwa juzi eneo la njiro jijini Arusha,Kulia ni Meneja Mkuu wa kampuni hiyo, Ali Donmez ( Habari Picha na Pamela Mollel,Arusha)






Makamu Mwenyekiti TATO Henry Kimambo ambaye alikuwa mgeni rasmi akiingia katika duka kubwa lavifaa mbalimbali vya mapishi kwenye mahoteli linalomilikiwa na kampuni ya kimataifa ya PiMAKambao ni watengenezaji na wauzaji wa bidhaa hizo ,Duka hilo lilifunguliwa juzi eneo la njiro jijini Arusha,kulia ni Meya wa jiji la Arusha Kalist Lazaro






Kulia ni Mbunge wa Arusha Godbless Lema akiteta jambo na Mkurugenzi wa hoteli ya Gold Crest ya Mwanza na Arusha Mathias Manga mara baada ya kuwasili katika ufunguzi wa duka kubwa lavifaa mbalimbali vya mapishi kwenye mahoteli linalomilikiwa na kampuni ya kimataifa ya PiMAK







Meneja Mkuu wa kampuni ya PiMAK ya kimataifa inayojihusisha na utengenezaji na uuzaji wa vifaa mbalimbali vya mapishai kwenye mahoteli akitoa maelezo kwa mteja aliyetembelea duka hilo









Meneja Mkuu wa kampuni hiyo, Ali Donmez akimuonyesha bidhaa za kampuni ya PiMAK mtaja aliyetembelea duka hilo siku ya uzinduzi Bi.Mary Mbajo






Wahudumu wa duka hilo wakiwa na vepeperushi vya kampuni hiyo






Muonekano ndani ya duka hilo




Makamu Mwenyekiti TATO Henry Kimambo akizungumza mara baada ya kukata utepe,kushoto ni diwani wa kata ya Themi jijini Arusha ,Milance Kinabo










Naibu Meya wa jiji la Arusha,Viola Likindikok akiangalia baadhi ya vyombo vinavyopatikana dukani hapo anayefatia ni Meya wa jiji la Arusha Kalist Lazaro









Kulia Meneja Mkuu wa kampuni hiyo, Ali Donmez akipozi na wadau katikati ni Maya wa jiji Kalist Lazaro




Mbunge wa Arusha Godbless Lema akiteta jambo na wadau wa kampuni hiyo






























Meneja Mkuu wa kampuni hiyo, Ali Donmez akitoa maelezo kwa mteja






















Wageni waliofika katika uzinduzi huo wakibadilishana mawazo



Na Pamela Mollel,Arusha

KAMPUNI ya kimataifa ya PiMAK inayojihusisha na utengenezaji na uuzaji wa vifaa vya mbalimbali vya mapishi kwenye mahoteli , imefungua duka kubwa jijini Arusha kwaajili ya kuwarahisishia watumiaji wa vyombo hivyo kuvipata kwa wakati

Akizungumza katika uzinduzi wa duka hilo la kisasa Makamu Mwenyekiti TATO Henry Kimambo ambaye alikuwa mgeni rasmi alisema kuwepo kwa duka hilo hapa Tanzania tayari ni fursa kubwa kwa wafanyabiashara wa mahoteli

Kimambo alisema kuwa kampuni ya PiMAK kuja kuwekeza nchini itasaidia ajira lakini pia kuwainua wajasiriamali wadogo wenye ndoto ya kufika mbali.“Kuna hawa wajasiriamali wadogo ambao wanajihusisha na maswala ya upishi watapata fursa ya kutanua biashara zao kwa kuwa tayari vifaa vinapatikana kiurahisi”alisema Kimambo

Meneja Mkuu wa kampuni hiyo, Ali Donmez alisema, kampuni hiyo yenye makao yake Uturuki imeamua kufungua maduka hapa Nchini Tanzania kwaajili ya kuwarahisishia wateja wake ambao walikuwa wakiagiza vyombo hivyo nje ya nchi.

Akizungumzia kuhusiana na bidhaa hizo, alisema kuwa ni bidhaa kwa ajili ya matumizi ya hoteli, migahawa na huduma kubwa za mapishi vikiwamo vya kukatia nyama, kuhokea mikate, kuoshea vyombo, kupikia na huduma nyingine za kihoteli4

Comments

Popular posts from this blog

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

AMANI YETU TUILINDE NAIBU WAZIRI CHANDE AZUNGUMZA KATIKA IJITIMAI JIJINI DODOMA

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.