WAZIRI UMMY AWATAKA WAGANGA WAKUU WA MIKOA KUANZISHA ZOEZI LA WAZI LA UCHUNGUZI WA SARATANI YA KIZAZI KWA WANAWAKE Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa kupokea vifaa vya kuchunguza saratani vyenye thamani ya shilingi milioni 98 leo jijini Dar es salaam . Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (kulia) akipokea moja ya vifaa vya uchunguzi wa saratani ya kizazi kutoka kwa Mkurugenzi Mkazi wa Jhpiego nchini Tanzania Bw. Jeremia Zoungran (kushoto) wakati wa makabidhiano ya vifaa vya kuchunguza saratani ya kizazi leo jijini Dar es salaam. Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (kulia) akipokea moja ya nyenzo za kufundishia juu ya uchunguzi wa saratani ya kizazi kutoka kwa Mkurugenzi Mkazi wa Jhpiego nchini Tanzania Bw. Jeremia Zoungran (kushoto) wakati wa makabidhiano ya vifaa vya kuchunguza saratani ya kizazi leo jijini Dar es salaam katikati ni Afisa Afya kutoka USAID Bi. Ananth Thambinygan . Mkurugenzi Mkazi wa Jhpiego nchini Tanzania Bw. Jeremia Zoungran akiongea na waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa kupokea vifaa vya kuchunguza saratani vyenye thamani ya shilingi milioni 98 leo jijini Dar es salaam . Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wa Wizara ya afya, Jpiego na USAID wakati wa kupokea vifaa vya kuchunguza saratani vyenye thamani ya shilingi milioni 98 leo jijini Dar es salaam wa tatu kushoto ni Mkurugenzi Mkazi wa Jhpiego nchini Tanzania Bw. Jeremia Zoungran na aliyevaa nguo ya pundamilia ni Afisa Afya kutoka USAID Bi. Ananth Thambinygan .picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii. NA WAMJW-DAR ES SALAAM. WAZIRI Wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu amewaelekeza waganga wakuu wa mikoa yote nchini kuanzisha zoezi la wazi la uchunguzi wa saratani ya kizazi angalau mara moja katika mwezi ili kusaidia kutokomeza tatizo kwa wanawake hilo nchini. Hayo amesema wakati wa kupokea vifaa vya kuchunguza saratani vyenye thamani ya shilingi milioni 98 ambavyo vimetolewa na Taasisi isiyo ya Kiserikali ya JHPIEGO kwa kushirikiana na USAID ili kusaidia kupambana na tatizo hilo nchini. “Angalau ifikapo Desemba 2018 nataka vituo vya Afya vya Serikali 524 viwe vinatoa huduma ya matibabu ya awali ya Saratani ya mlango wa kizazi na kufikia wanawake milioni 3 watakaopata huduma hii ili kuokoa wanawake wa vijijini kwani mpaka sasa hivi tunavyo vituo vya afya 265 vinavyotoa huduma hii ” alisema Waziri Ummy. Aidha Waziri Ummy amesema kuwa uchunguzi na kutoa chanjo ya Saratani ya mlango wa kikazi kwa wasichana kuanzia miaka 9 mpaka 14 ili kuweza kupunguza vifo vitokanavyo na tatizo hilo kwani katika kila wanawake 100 vifo vinavyotokana na ugonjwa huo ni 32. Mbali na hayo Waziri Ummy amesema kuwa katika kuongeza jitihada za kupambana na ugonjwa huo Serikali imeongeza vituo vya afya 100 kutoka 343 hadi kufikia 443 mwaka huu ili kutokomeza tatizo hilo nchini. Kwa upande wake Mkurugenzi Mkazi wa Jhpiego nchini Tanzania Bw. Jeremia Zoungran amesema kuwa walianzisha mpango wa kupambana na tatizo hilo na kufanikiwa kuwafikia wanawake elfu 75 kwa mikoa 4 tangu mwaka 2009. “Mbali na mikoa hiyo 4 bado tunalengo la kuongeza mikoa mingine 7 ili kuweza kutoa huduma hiyo kwa ajili ya kuunga mkono Juhudi za Serikali katika kupambana na Saratani ya mlango wa kizazi ili kuweza kuokoa wanawake wengi zaidi nchini” alisema Bw. Zoungran. Posted by MICHUZI BLOG at Monday, November 20, 2017 No comments: Links to this post Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to FacebookShare to Pinterest VODASTAR YAICHAKAZA NOKIA MAGOLI 8-1 MECHI YAKIRAFIKI Mshambuliaji wa timu ya VodaStar, ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Vodacom Tanzania PLC, Ian Ferrao (wapili kulia)akishangilia goli baada ya kuifungia timu yake wakati wa mchezo wakirafiki dhidi ya timu ya Nokia uliofanyika katika uwanja wa Gymkhana jijini Dar es Salaam,VodaStar iliiadhibu Nokia kwa magoli 8-1. Wachezaji wa timu ya VodaStar,wakiongozwa na Mkurugenzi mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC, Ian Ferrao (wapili kulia mwenye miwani) wakishangilia kombe lao baada ya kuihadabisha timu ya Nokia kwa magoli 8-1 wakati wa mchezo wakirafiki uliofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kikosi cha timu ya VodaStar kilichoisambaratisha timu ya Nokia kwa magoli 8-1 wakati wa mechi yakirafiki wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mechi hiyo kuisha iliyofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Mashabiki watimu ya VodaStar, wakifurahia kombe lao baada ya timu yao kiichakaza timu ya Nokia kwa magoli 8-1 wakati wamchezo wakirafiki uliofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC, Ian Ferrao (kushoto) akimshuhudia Mkurugenzi wa Nokia Tanzania,Martin Talbot ( kulia) akimvisha medali nahodha wa timu ya VodaStar, Ngayama Matongo baada ya kuilaza timu hiyo kwa magoli 8-1 wakati wa mechi yakirafiki uliofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Mshambuliaji wa timu ya VodaStar, Ian Ferrao ambaye pia ni Mkurugenzi mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC, (kushoto) akipongezwa na Mkurugenzi mtendaji wa Nokia Tanzania, Martin Talbot kwa kuchaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo wakati wa mchezo wa kirafiki kati ya kampuni hizo ambapo VodaStar iliichapa Nokia kwa magoli 8-1 mwishoni mwa wiki katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam. Nahodha wa timu ya Nokia Tanzania,Charles Domingos(kulia) akiachia shuti kali na kuifungia goli timu yake na lapekee wakati wa mechi yakirafiki iliyofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam kati ya timu yake na VodaStar ambapo VodaStar waliichakaza timu hiyo kwa magoli 8-1. Posted by MICHUZI BLOG at Monday, November 20, 2017 No comments: Links to this post Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to FacebookShare to Pinterest Mkurugenzi Mkazi wa USAID bwana Andy Karas atembelea walengwa wa TASAF mkoani Iringa. Na Estom Sanga – Iringa Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Misaada ya Kimataifa la Marekani –USAID-bwana Andy Karas amepongeza jitihada za serikali ya Tanzania kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF katika kuwafikia wananchi wanaokabiliwa na umasikini kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini ambao umeanza kuonyesha mafanikio makubwa katika maeneo mbalimbali nchini, jambo linalovutia wadau wa maendeleo kuendelea kusaidia jitihada hizo. Bwana Karas ameyasema hayo alipokutana na Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kijiji cha Igingilanyi kata ya Nduli katika halmashauri ya Wilaya ya Iringa ,mkoani Iringa ambako licha ya kuelezwa namna TASAF inavyoendelea kutekeleza Mpango huo, lakini pia alishuhudia namna walengwa wa mpango huo walivyoboresha maisha yao kwa kutumia fedha za ruzuku za mfuko huo. Amesema hamasa inayoonyeshwa na Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kujiletea maendeleo kwa kuanzisha miradi midogo midogo kwa kutumia fedha zinazotolewa na Serikali kupitia TASAF, imelivutia Shirika hilo na kuahidi kuwa litaendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania katika kuboresha utaratibu wa kuwainua wananchi kiuchumi . Bwana Karas amesema utaratibu wa kuwafikia na kuwasaidia moja kwa moja wananchi wanaoishi katika mazingira magumu ya kiuchumi umekuwa ukitumika katika nchi nyingi duniani na umeonyesha mafanikio makubwa kwa kusisimua shughuli za kiuchumi na kijamii kwa kaya masikini . Aidha Mkurugenzi Mkazi huyo wa USAID amevutiwa na masharti ya Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini kupitia TASAF hususani katika nyanja za elimu, afya, lishe na uwekezaji kwenye shughuli za kiuchumi kwa walengwa wa Mpango huo kuwa umeamusha ari ya kutokomeza umasikini miongoni mwao. Akiwa katika kijiji hicho cha Igingilanyi kata ya Nduli bwana Karas alitembelea baadhi ya kaya za Walengwa wa TASAF na kujionea namna walivyonufaika na ruzuku ya Mpango huo kwa kuanzisha miradi midogo midogo ya ufugaji wa kuku na nguruwe na kutumia sehemu ya mapato yao kuboresha makazi kwa kujenga nyumba za matofali na kuezeka kwa mabati. “ni jambo jema sana mnalolifanya kwa kuwekeza katika elimu ya watoto wenu na kuboresha makazi yenu kwa kutumia ruzuku mnayoipata” alisisitiza bwana Karas. Bwana Karas pia alionyesha kuvutiwa na utaratibu wa kuanzisha vikundi vya kuweka akiba na kukopeshana unaofanywa na Walengwa wa Mpango huo wa Kunusuru Kaya Maskini ambao alisema ukiimarishwa utatoa fursa kubwa zaidi kwa wananchi hao kukuza shughuli zao za kiuchumi kwa kukopeshana kwa riba ndogo ikilinganisha na ile inayotozwa na taasisi za kibenki. Kwa Upande wake Mkurugenzi wa Miradi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF,Bwana Amadeus Kamagenge alimweleza Mkurugenzi Mkazi huyo wa USAID kuwa licha ya Serikali kupitia Mfuko huo kuendelea kutoa ruzuku kwa Kaya Masikini sana katika mikoa yote nchni ,hivi sasa umeanza kujikita zaidi katika kuhamasisha walengwa kuanzisha vikundi vya kuweka akiba na kukopeshana kwa kuwatumia wataalamu walioko kwenye maeneo yao wakiwemo Maafisa wa Maendeleo ya Jamii, kilimo, Mifugo na biashara ili waweze kuboresha shughuli za kiuchumi kwa walengwa. “Mkakati huo umeanza kuonyesha mafanikio kwa kuwaongezea walengwa kwa Mpango huo kipato na kuwapa uwezo wa kubuni na kusimamia kwa ufanisi miradi yao midogo midogo wanayoianzisha. Hata hivyo bwana Kamagenge amesema mafanikio yaliyoanza kupatikana kwa kaya za walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini yameibua kilio kutoka kwa kaya nyingine ambazo hazikuingizwa kuingizwa kwenye Mpango huo kutaka nazo pia zijumuishwe kwenye utaratibu huo. Hadi sasa TASAF inatekeleza Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini katika vijiji 9,835 ambayo ni sawa na asilimia 70 ya vijiji na shehia zote Tanzania bara na Zanzibar. Mkurugenzi M kazi wa Shirika la Misaada la Marekani –USAID-bwana Andy Karas (wa tatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na mmoja wa walenwa wa TASAF katika kijiji cha Igingilanyi kata ya Nduli wilaya ya Iringa baada ya kutembelea nyumba aliyoijenga mlengwa huyo (nyuma yao ) baada ya kupata ruzuku kutoka TASAF. Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Misaada la Marekani USAID bwana Andy Karas akipokea zawadi ya kuku kutoka kwa mmoja wa walengwa wa Mpango wa kunusuru Kaya Masikini unaoratibiwa na TASAF katika kijiji cha Igingilanyi wilaya ya Iringa Vijijini ambako akutana na walengwa wa Mpango huo kuona namna wanavyonufaika na Mpango huo. Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Misaada la Marekani nchini USAID bwana Andy Karas akisoma taarifa kwenye mkutano wa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kijiji cha Igingilanyi kata ya Nduli wilaya ya Iringa Vijijini ambako alitembelea kuona namna walengwa wa Mpango huo wanavyonufaika na ruzuku inayotolewa na serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF. Baadhi ya Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kijiji cha Igingilanyi wilaya ya Iringa Vijijini wakiwaburudisha wageni kutoka Shirika la Misaada la Marekani –USAID waliotembelea kijiji hicho kuona shughuli za Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini unaoratibiwa na TASAF . Mkurugenzi mkazi wa Shirika la Misaada la Marekani Bwana Andy Karas akisalimiana na mmoja wa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kijiji cha Igingilanyi kata ya Nduli wilaya ya Iringa Vijijini wakati alipotembelea kijiji hicho.Katikati yao ni Mkurugenzi wa miradi wa TASAF bwana Amadeus Kamagenge. Posted by MICHUZI BLOG at Monday, November 20, 2017 No comments: Links to this post Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to FacebookShare to Pinterest BENKI YA KILIMO YATEMBELEA MIRADI YA JKT KITEULE CHA BULAMBA, BUNDA Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imetembelea mradi wa ufugaji wa vifaranga vya samaki unaotekelezwa na kikosi cha 822 Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Rwamkoma wilaya ya Butiama kupitia Kiteule chake cha Bulamba, wilayani Bunda. Akizungumza lengo la ziara hiyo, mkuu wa msafara huo ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki hiyo, Bibi Rosebud Kurwijila amesema lengo kubwa la kutembelea Mradi huo ni kujionea juhudi za serikali za kuchagiza mapinduzi ya kilimo hasa katika tasnia ya ufugaji na uvuvi wa samaki nchini. Bibi Kurwijila aliongeza kuwa tasnia ya ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba ni mojawapo ya minyororo ya mwanzo inayopatiwa mikopo kwa ajili ya uongezaji wa thamani mazao na mifugo mbalimbali hasa katika uongezaji wa thamani wa ufugaji wa samaki nchini. Aliongeza kuwa Benki ya Kilimo imejipanga kuendeleza uongezaji wa thamani wa Ufugaji wa Samaki na uvuvi nchini ili ziweze kuchangia ukuaji wa uchumi nchini. Mradi huo wa ufugaji wa samaki unaotekelezwa na JKT Wilaya ya Bunda, Kiteule cha Bulamba ulizinduliwa rasmi mwezi Novembea, 2014 kwa kupandikiza vifaranga vya samaki katika vizimba ndani ya Ziwa Victoria. Mradi huo unatekelezwa kwa ushirikiano na wadau mbalimbali wakiwemo Economic Social Research Foundation (ESRF) na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP). Ufugaji wa samaki kwa kutumia teknolojia ya vizimba ndani ya Ziwa Victoria, umekuwa maarufu zaidi katika nchi za Afrika Mashariki ikiwemo Uganda na Kenya ambapo umepunguza kwa kiasi kikubwa uvuvi haramu katika fukwe za ziwa hilo. Afisa Kilimo na Ufugaji wa kikosi cha 822 Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Rwamkoma, Kapteni M. Kinana (kulia) akiongea na Ujumbe kutoka Benki ya Kilimo (hawapo pichani) walipotembelea mradi huo uliopo wilayani Bunda. Kushoto ni Msimamizi wa Mradi wa Ufugaji wa Samaki wa JKT Kiteule cha Bulamba, Luteni Kelvin Gondo. Maafisa wa Jeshi la Kujenga Taifa wanaotekeleza Mradi wa Ufugaji wa Samaki kwa Vizimba Kiteule cha Bulamba wakifuatilia mkutano wa pamoja kati ya JKT na Ujumbe kutoka Benki ya Kilimo. Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), Bibi Rosebud Kurwijila (kulia) akizungumza wakati walipotembelea Mradi wa Ufugaji wa Samaki kwa Vizimba Kiteule cha Bulamba uliopo wilaya ya Bunda, Mkoani Mara. Kushoto ni Afisa Uvuvi wa wilaya ya Bunda, Bw. Steven Ochieng’. Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa TADB, Bw. Dome Malosha (kulia) akizungumza wakati walipotembelea Mradi wa Ufugaji wa Samaki kwa Vizimba Kiteule cha Bulamba uliopo wilaya ya Bunda, Mkoani Mara. Wengine pichani ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki hiyo, Bibi Rosebud Kurwijila (kushoto) na Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi, Bw. Joseph Mutashubilwa (katikati). Afisa Uvuvi wa wilaya ya Bunda, Bw. Steven Ochieng’ (kushoto) akichangia wakati wa mazungumzo hayo. Anayemsikiliza ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki hiyo, Bibi Rosebud Kurwijila (kulia). Msimamizi wa Mradi wa Ufugaji wa Samaki wa JKT Kiteule cha Bulamba, Luteni Kelvin Gondo akitoa maelezo juu ya maendeleo ya ufugaji wa samaki katika hatua mbalimbali. Posted by MICHUZI BLOG at Monday, November 20, 2017 No comments: Links to this post Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to FacebookShare to Pinterest MAHAFALI YA KWANZA YA CHUO CHA MANJANO BEAUTY ACADEMY YAFANYIKA JIJINI DAR Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh Mama Sophia Mjema Akizungumza Machache wakati wa Mahafali ya kwanza ya Chuo cha Manjano Beauty Academy .Ambapo amewataka Wanawake Kuchangamkia Fursa ya Urembo kwa kuwa ukuaji wake kwa sasa ni kubwa na inakabiliwa na Upungufu wa Wataalamu hivyo akiwashauri wanawake wengi Kujiunga na Kuiga Mambo Mazuri Yanayofanywa na Chuo cha Manjano Beauty Academy.Akieleza zaidi Alisema Sekta ya Urembo ina Fursa kubwa kwa Ajira kwa sasa,Katika Mahafali hayo Wahitimu 120 Wametunukiwa vyeti katika katika nyanja ya urembo. Mwanzilishi wa Chuo cha Manjano Beauty Academy Mama Shekha Nasser Akitoa Hotuba yake wakati wa mahafali ya kwanza ya chuo hicho yaliofanyika Kwenye Viwanja vya Kijiji cha Makumbusho Jijini Dar es salaam.Mama Shekha Nasser Amewashukuru wazazi na walezi kwa kuwapeleka Watoto wao kwenye chuo hicho kwa LengoKupata Ujuzi wa Maswala ya Urembo,Aidha Ametaja Changamoto kubwa Alizokabiliana nazo wakati anaanzishi Chuo hicho Ikiwemo ukosefu wa Wataalamu wazawa wa Maswala ya Urembo. Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh Mama Sophia Mjema Akiwa na Wageni Waalikwa wakati wa Mahafali ya Kwanza ya Chuo cha Manjano Beauty Academy Baadhi ya Wahitimu waliotunukiwa kwenye Mahafali ya Kwanza ya Chuo cha Manjano Beauty Academy yaliofanyika Kwenye Viwanja vya Kijiji cha Makumbusho Jijini Dar es salaam Mshauri wa Maswala ya Kisaikolojia Anti Sadaka Akitoa Neno la Shukrani kwenye Mahafali hayo Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh Mama Sophia Mjema Akitoa Cheti kwa Mmoja wa Wahitimu Kwenye Mahafali ya kwanza ya Chuo cha Manjano Beauty Academy.. Mgeni Rasmi,Uongozi wa Chuo cha Manjano Bauty Academy ,Wageni waalikwa na Wahitimu Wakiwa katika Picha ya Pamoja Chuo cha Manjano Beauty Academy kimetunuku Astashahada (Certificates) na Stashahada (Diploma) kwa wahitimu 120 wa kwanza wa chuo hicho katika nyanja ya urembo na utengenezaji wa nywele.Urembo na mitindo ni moja kati ya sekta zinazoajiri mamilioni ya wanawake kwa sasa, lakini bado sekta hiyo imeendelea kuwa isiyo rasmi. Wanawake wengi wanaofanya kazi kwenye saluni hawana utaalamu, lakini ndiyo wanaofuatwa na wanaume na wanawake kwa ajili ya kutengenezwa mionekano inayovutia, wanaishi kwa kufanya kazi kubahatisha. Akizungumza kwenye mahafali ya kwanza ya Manjano Beauty Academy iliyofanyika jijini Dar es Salaam, mwanzilishi wa Manjano Beauty Academy, Shekha Nasser alisema kuwa maono hayo ndiyo yaliyosababisha yeye kuanzisha Manjano Beauty Academy.Manjano Beauty Academy ni shule kwa ajili ya afya na urembo ambayo ina lengo la kuwawezesha wasichana wa Kitanzania. “Tunashauri, tunatoa mafunzo na kuwaandaa wanafunzi kwa ajili ya soko kwa kuwapatia ujuzi unaohitajika. Serikali haiwezi kuwaajiri wahitimu wote, hata sekta binafsi haiwezi kwa hivi sasa, kwa hiyo mafunzo haya yanawasaidia wasichana wadogo kuweza kujitengenezea soko kwenye sekta ya urembo,” alisema Shekha.Kwa mujibu wa Shekha, wasichana hao wamekuwa wakipewa mafunzo na wakufunzi bora wanaopatikana katika sekta ya urembo ambayo yatawatasaidia wao kutimiza malengo yao binafsi pamoja na malengo ya kitaasisi. “Naamini kuwa wahitimu hawa watabadilisha sekta ya urembo hapa nchini, kama Korea na Filipino wanavyotambulika ulimwenguni kwa kuwa na bidhaa bora za ngozi na wataalam wa matibabu wenye weledi, huko mbeleni Tanzania itajulikana ni nchi inayotoa bidhaa bora za urembo kwa ngozi za Kiafrika, kuanzia bidhaa za urembo wa uso zinazozalishwa kutokana na Mwani wa baharini toka Zanzibar mpaka bidhaa za poda ambazo zina virutubisho vya Manjano ya asili na vyakutosha,” alisema Shekha ambaye pia ni mwanzilishi wa Shear Illusions. Mwaka 2015, kupitia bidhaa za LuvTouch Manjano, Shekha alizindua kampeni inayoitwa Manjano Dream Makers iliyokuwa na lengo la kuwawezesha wasichana wenye mafunzo ya kijasiriamali kujikwamua kiuchumi ili kutimiza ndoto zao. “Katika miaka miwili tangu kuanzishwa kwa taasisi ya Manjano, mtandao wa wanawake wa Manjano Dream-Makers umeweza kuenea katika majiji na miji Saba nchini na kuwasaidia kutengeneza ajira na kutengeneza kipato kwa kuuza bidhaa zao kupitia mfumo wa nyumba kwa nyumba kwa wanawake wasio na ajira,” alisema Shekha. Aliongeza kuwa, “Leo tunajivunia kuwa na wasichana 360 katika mtandao wa ‘Manjano Dream-Makers’ wenye matumaini ya kuboresha maisha yao na familia zao kwa kuuza bidhaa za LuvTouch Manjano. Posted by MICHUZI BLOG at Monday, November 20, 2017 No comments: Links to this post Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to FacebookShare to Pinterest CHAMA CHA MBIO ZA MAGARI TANZANIA (AAT) CHAWAKUMBUKA WAATHIRIKA WA AJALI NA KUJADILIANA NA WADAU NAMNA YA KUZIPUNGUZA 1 Mgeni Rasmi Mwanasheria wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Afande Deus Sokoni akifungua mjadala katika Siku ya Kukumbuka waathirika wa Ajali Duniani (The World Day Of Remembrance For Road Traffic Victims 19 November 2017) iliyoandaliwa na kufanyika kwenye ofisi za Chama Cha Mbio za Magari Tanzania AAT Upanga jijini Dar es salaam ikishirikisha wadau kutoka taasisi mbalimbali nchini Tanzania. Wadau mbalimbali wamekutana na kujadiliana namna ya kupunguza ajali hasa katika kuzipitia sheria za usalama barabarani na kuzifanyia marekebisho pamoja na kuwakumbusha watumiaji wa Barabara kuzingatia sheria za usalama barabarani, Taasisi zilizoshiriki katika mjadala huo ni WHO, KIkosi Cha Usalama Barabarani, SUMATRA, Chama Cha Mbizo za Magari Tanzania AAT, Chama cha Kutetea Abiria Tanzania CHAKUA, TIRA na wawakilishi Idara ya Habari Maelezo. 2 Mratibu wa Semina hiyo Bw. Alferio Nchimbi akizungumza katika semina hiyo na kukaribisha wadau mbalimbai ili kuchangia michango yao katika mada mbalimbali zilizowasilishwa. 3 Mgeni Rasmi Mwanasheria wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Afande Deus Sokoni akisisitiza jambo wakati akijibu maswali katika semina hiyo kulia ni Mratibu wa Semina hiyo Bw. Alferio Nchimbi. 4 Bw. Monday Likwepa Katibu Mkuu wa Chama cha Kutetea Abiria akichangia mada katika semina hiyo. 5 Bi Mary Kessi Mratibu Programu ya Usalama Barabarani WHO akitoa mada katika semina hiyo iliyofanyika kwenye ofisi za Chama cha Mbio za Magari Tanzania (AAT) Upanga jijini Dar es salaam. 6 Afisa Leseni Mwandamizi kutoka SUMATRA Bw. Gabriel Anthony akitoa mada katika semina hiyo. 7 Daktari Bingwa wa Kitengo cha Magonjwa ya Dharura na Ajali Muhimbili Dk Juma Mfinanga akitoa ufafanuzi kwa upande wa hospitali ya Muhimbili wakati wa semina hiyo. 8 Baadhi ya washiriki wakiwa katika semiha hiyo 9 10 Posted by MICHUZI BLOG at Monday, November 20, 2017 No comments: Links to this post Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to FacebookShare to Pinterest KABURI LAFUKULIWA MOSHI KUONDOA UTATA WA MWILI WA MTU ALIYEZIKWA BAADA YA KUOKOTWA MTONI Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini. UTATA umeighubika familia ya Jackson Makundi ambayo kijana wake aliyetambulika kwa jina la Humphrey Makundi,Mwanafunzi wa shule ya Sekondari ya Scolastica iliyopo mji mdogo wa Himo kupotea katika mazingira tatanishi. Utata wa kupotea kwa mwanafunzi huyo unatiliwa shaka zaidi na familia hiyo baada ya kufukuliwa kwa kaburi ulimozikwa mwili uliookotwa mto Ghona mita 300 ,jirani na shule hiyo ukidaiwa kushabihiana na wa mwanafunzi huyo. Humphrey Makundi, mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari ya Scolastica anatajwa kupotea tangu Novemba 7 mwaka huu akiwa shuleni hapo huku wanafunzi wenzake wakiendelea na mitihani ya kidato cha Pili ya upimaji ya kitaifa . Familia ya kijana huyo yenye makazi yake mkoani Dodoma ikalazimika kutumia mitandao ya kijamii kutoa taarifa za kupotea kwake ikidai mazingira ya kutoweka kwake ni ya kutatanisha na baadae kuwasilisha taarifa katika kituo cha Polisi cha Himo . Kutokana na kuwepo kwa taarifa za kuokotwa kwa mwili huo ,familia iliwasilisha maombi katika mahakama ya Hakimu Mkazi, Moshi na mahakama ikaamuru kufukuliwa kwa Kaburi hilo zoezi lililoanza majira ya saa 8:30 mchana na kudumu kwa zaidi ya saa moja. Jeshi la Polisi liliongoza zoezi hilo katika makaburi ya Karanga huku likishuhudiwa na ndugu wa mtoto aliyepotea ambapo baada ya mwili kutolewa kaburini hali ya simanzi ilionekana katika nyuso za baadhi ya ndugu wa Mwanafunzi huyo akiwemo baba mzazi wa kijana huyo. Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Kamishna Msaidizi wa Polisi ,Hamis Issa akathibitisha uwepo wa tukio hilo huku akieleza kuwa tayari jeshi la Polisi linawashikilia wati 11 akiwemo mmiliki wa shule hiyo Edward Shayo huku likifanya uchunguzi wa kina kuhusu matukio hayo mawili. Mwili uliofukuliwa katika makaburi ya Karanga upande wa marehemu wasiokuwa na ndugu ulipelekewa katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya KCMC kwa uchunguzi zaidi chini ya uangalizi wa jeshi la Polisi wakishirikiana na madaktari kutoka KCMC. Jeshi la Polisi likiwa limezungushia utepe eneo ambalo kuna kaburi ulimozikwa mwili ambao familia ya Mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Scolastica iliyopo mji mdogo wa Himo aliyepotea ,Humphrey Makundi ulitilia shaka. Kaburi ulimozikwa mwili wa mtu aliyezikwa na Manispaa ya Moshi baada ya kuokotwa Mto Ghona jirani na ilipo shule ya Sekondari . Askari Polisi wakishirikiana na ndugu wa Mwanafunzi aliyepotea Humphrey Makundi wakifukua Kaburi ulimozikwa mwili wa mtu aliyeokotwa Mto Ghona katika wilaya ya Moshi. Kaburi likifukuliwa. Baba mzazi wa Mwanafunzi wa shule ya Sekondari ya Scolastica aliyepotea,Jackson Makundi (Katkati) akijadili jambo na wanandugu wakati zoezi la kufukua kaburi likiendelea. Baba mzazi wa Mwanafunzi Humphrey ,Jackson Makundi (Mwenye suti nyeupe) akitizama mwili (haupo pichani) baada ya kaburi kufukuliwa. Baba mzazi wa Mwanafunzi Humphrey ,Jackson Makundi (Mwenye suti nyeupe) akionekana akiwa amekaa chini baada ya kutizama mwili uliofukuliwa katika kaburi . Askari Polisi na Wanandugu wa kijana aliyepotea wakijaribu kusaidia kumnyanyua mzazi wa Mwanafunzi huyo kutoka katika eneo lilipo kaburi lililofukuliwa . Baba mzazi wa Mwanafunzi Humphrey ,Jackson Makundi (Mwenye suti nyeupe) akisindikizwa kutoka katika eneo la Makaburi ya Karanga katika manispaa ya Moshi. Mwili uliofukuliwa katika makaburi hayo ukiwekwa katika gari la Polisi kwa ajili ya kwenda kuhifadhiwa katika Hosptali ya Rufaa ya KCMC. Gari la Polisi likiwa na mwili uliofukuliwa katika Makaburi ya Karanga.
WAZIRI UMMY AWATAKA WAGANGA WAKUU WA MIKOA KUANZISHA ZOEZI LA WAZI LA UCHUNGUZI WA SARATANI YA KIZAZI KWA WANAWAKE
Waziri
wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu
akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa kupokea
vifaa vya kuchunguza saratani vyenye thamani ya shilingi milioni 98 leo
jijini Dar es salaam .
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy
Mwalimu (kulia) akipokea moja ya vifaa vya uchunguzi wa saratani ya
kizazi kutoka kwa Mkurugenzi Mkazi wa Jhpiego nchini Tanzania Bw.
Jeremia Zoungran (kushoto) wakati wa makabidhiano ya vifaa vya
kuchunguza saratani ya kizazi leo jijini Dar es salaam.
Waziri
wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu
(kulia) akipokea moja ya nyenzo za kufundishia juu ya uchunguzi wa
saratani ya kizazi kutoka kwa Mkurugenzi Mkazi wa Jhpiego nchini
Tanzania Bw. Jeremia Zoungran (kushoto) wakati wa makabidhiano ya vifaa
vya kuchunguza saratani ya kizazi leo jijini Dar es salaam katikati ni
Afisa Afya kutoka USAID Bi. Ananth Thambinygan .
Mkurugenzi
Mkazi wa Jhpiego nchini Tanzania Bw. Jeremia Zoungran akiongea na
waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa kupokea vifaa vya
kuchunguza saratani vyenye thamani ya shilingi milioni 98 leo jijini
Dar es salaam .
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy
Mwalimu (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya watendaji
wa Wizara ya afya, Jpiego na USAID wakati wa kupokea vifaa vya
kuchunguza saratani vyenye thamani ya shilingi milioni 98 leo jijini
Dar es salaam wa tatu kushoto ni Mkurugenzi Mkazi wa Jhpiego nchini
Tanzania Bw. Jeremia Zoungran na aliyevaa nguo ya pundamilia ni Afisa
Afya kutoka USAID Bi. Ananth Thambinygan .picha na Emmanuel
Massaka,Globu ya jamii.
NA WAMJW-DAR ES SALAAM.
WAZIRI
Wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu
amewaelekeza waganga wakuu wa mikoa yote nchini kuanzisha zoezi la wazi
la uchunguzi wa saratani ya kizazi angalau mara moja katika mwezi ili
kusaidia kutokomeza tatizo kwa wanawake hilo nchini.
Hayo
amesema wakati wa kupokea vifaa vya kuchunguza saratani vyenye thamani
ya shilingi milioni 98 ambavyo vimetolewa na Taasisi isiyo ya
Kiserikali ya JHPIEGO kwa kushirikiana na USAID ili kusaidia kupambana
na tatizo hilo nchini.
“Angalau
ifikapo Desemba 2018 nataka vituo vya Afya vya Serikali 524 viwe
vinatoa huduma ya matibabu ya awali ya Saratani ya mlango wa kizazi na
kufikia wanawake milioni 3 watakaopata huduma hii ili kuokoa wanawake
wa vijijini kwani mpaka sasa hivi tunavyo vituo vya afya 265
vinavyotoa huduma hii ” alisema Waziri Ummy.
Aidha
Waziri Ummy amesema kuwa uchunguzi na kutoa chanjo ya Saratani ya
mlango wa kikazi kwa wasichana kuanzia miaka 9 mpaka 14 ili kuweza
kupunguza vifo vitokanavyo na tatizo hilo kwani katika kila wanawake 100
vifo vinavyotokana na ugonjwa huo ni 32.
Mbali
na hayo Waziri Ummy amesema kuwa katika kuongeza jitihada za kupambana
na ugonjwa huo Serikali imeongeza vituo vya afya 100 kutoka 343 hadi
kufikia 443 mwaka huu ili kutokomeza tatizo hilo nchini.
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mkazi wa Jhpiego nchini Tanzania Bw. Jeremia
Zoungran amesema kuwa walianzisha mpango wa kupambana na tatizo hilo na
kufanikiwa kuwafikia wanawake elfu 75 kwa mikoa 4 tangu mwaka 2009.
“Mbali
na mikoa hiyo 4 bado tunalengo la kuongeza mikoa mingine 7 ili kuweza
kutoa huduma hiyo kwa ajili ya kuunga mkono Juhudi za Serikali katika
kupambana na Saratani ya mlango wa kizazi ili kuweza kuokoa wanawake
wengi zaidi nchini” alisema Bw. Zoungran.
VODASTAR YAICHAKAZA NOKIA MAGOLI 8-1 MECHI YAKIRAFIKI
Mshambuliaji
wa timu ya VodaStar, ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Vodacom Tanzania
PLC, Ian Ferrao (wapili kulia)akishangilia goli baada ya kuifungia timu
yake wakati wa mchezo wakirafiki dhidi ya timu ya Nokia uliofanyika
katika uwanja wa Gymkhana jijini Dar es Salaam,VodaStar iliiadhibu Nokia
kwa magoli 8-1.
Wachezaji
wa timu ya VodaStar,wakiongozwa na Mkurugenzi mtendaji wa Vodacom
Tanzania PLC, Ian Ferrao (wapili kulia mwenye miwani) wakishangilia
kombe lao baada ya kuihadabisha timu ya Nokia kwa magoli 8-1 wakati wa
mchezo wakirafiki uliofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es
Salaam mwishoni mwa wiki.
Kikosi
cha timu ya VodaStar kilichoisambaratisha timu ya Nokia kwa magoli 8-1
wakati wa mechi yakirafiki wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mechi
hiyo kuisha iliyofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es
Salaam mwishoni mwa wiki.
Mashabiki
watimu ya VodaStar, wakifurahia kombe lao baada ya timu yao kiichakaza
timu ya Nokia kwa magoli 8-1 wakati wamchezo wakirafiki uliofanyika
katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC, Ian Ferrao (kushoto) akimshuhudia
Mkurugenzi wa Nokia Tanzania,Martin Talbot ( kulia) akimvisha medali
nahodha wa timu ya VodaStar, Ngayama Matongo baada ya kuilaza timu hiyo
kwa magoli 8-1 wakati wa mechi yakirafiki uliofanyika katika viwanja
vya Gymkhana jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Mshambuliaji
wa timu ya VodaStar, Ian Ferrao ambaye pia ni Mkurugenzi mtendaji wa
Vodacom Tanzania PLC, (kushoto) akipongezwa na Mkurugenzi mtendaji wa
Nokia Tanzania, Martin Talbot kwa kuchaguliwa kuwa mchezaji bora wa
mchezo wakati wa mchezo wa kirafiki kati ya kampuni hizo ambapo
VodaStar iliichapa Nokia kwa magoli 8-1 mwishoni mwa wiki katika viwanja
vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
Nahodha
wa timu ya Nokia Tanzania,Charles Domingos(kulia) akiachia shuti kali
na kuifungia goli timu yake na lapekee wakati wa mechi yakirafiki
iliyofanyika katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam kati ya
timu yake na VodaStar ambapo VodaStar waliichakaza timu hiyo kwa magoli
8-1.
Mkurugenzi Mkazi wa USAID bwana Andy Karas atembelea walengwa wa TASAF mkoani Iringa.
Na Estom Sanga – Iringa
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Misaada ya Kimataifa la Marekani –USAID-bwana Andy Karas amepongeza jitihada za serikali ya Tanzania kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF katika kuwafikia wananchi wanaokabiliwa na umasikini kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini ambao umeanza kuonyesha mafanikio makubwa katika maeneo mbalimbali nchini, jambo linalovutia wadau wa maendeleo kuendelea kusaidia jitihada hizo.
Bwana Karas ameyasema hayo alipokutana na Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kijiji cha Igingilanyi kata ya Nduli katika halmashauri ya Wilaya ya Iringa ,mkoani Iringa ambako licha ya kuelezwa namna TASAF inavyoendelea kutekeleza Mpango huo, lakini pia alishuhudia namna walengwa wa mpango huo walivyoboresha maisha yao kwa kutumia fedha za ruzuku za mfuko huo.
Amesema hamasa inayoonyeshwa na Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kujiletea maendeleo kwa kuanzisha miradi midogo midogo kwa kutumia fedha zinazotolewa na Serikali kupitia TASAF, imelivutia Shirika hilo na kuahidi kuwa litaendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania katika kuboresha utaratibu wa kuwainua wananchi kiuchumi .
Bwana Karas amesema utaratibu wa kuwafikia na kuwasaidia moja kwa moja wananchi wanaoishi katika mazingira magumu ya kiuchumi umekuwa ukitumika katika nchi nyingi duniani na umeonyesha mafanikio makubwa kwa kusisimua shughuli za kiuchumi na kijamii kwa kaya masikini .
Aidha Mkurugenzi Mkazi huyo wa USAID amevutiwa na masharti ya Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini kupitia TASAF hususani katika nyanja za elimu, afya, lishe na uwekezaji kwenye shughuli za kiuchumi kwa walengwa wa Mpango huo kuwa umeamusha ari ya kutokomeza umasikini miongoni mwao.
Akiwa katika kijiji hicho cha Igingilanyi kata ya Nduli bwana Karas alitembelea baadhi ya kaya za Walengwa wa TASAF na kujionea namna walivyonufaika na ruzuku ya Mpango huo kwa kuanzisha miradi midogo midogo ya ufugaji wa kuku na nguruwe na kutumia sehemu ya mapato yao kuboresha makazi kwa kujenga nyumba za matofali na kuezeka kwa mabati.
“ni jambo jema sana mnalolifanya kwa kuwekeza katika elimu ya watoto wenu na kuboresha makazi yenu kwa kutumia ruzuku mnayoipata” alisisitiza bwana Karas.
Bwana Karas pia alionyesha kuvutiwa na utaratibu wa kuanzisha vikundi vya kuweka akiba na kukopeshana unaofanywa na Walengwa wa Mpango huo wa Kunusuru Kaya Maskini ambao alisema ukiimarishwa utatoa fursa kubwa zaidi kwa wananchi hao kukuza shughuli zao za kiuchumi kwa kukopeshana kwa riba ndogo ikilinganisha na ile inayotozwa na taasisi za kibenki.
Kwa Upande wake Mkurugenzi wa Miradi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF,Bwana Amadeus Kamagenge alimweleza Mkurugenzi Mkazi huyo wa USAID kuwa licha ya Serikali kupitia Mfuko huo kuendelea kutoa ruzuku kwa Kaya Masikini sana katika mikoa yote nchni ,hivi sasa umeanza kujikita zaidi katika kuhamasisha walengwa kuanzisha vikundi vya kuweka akiba na kukopeshana kwa kuwatumia wataalamu walioko kwenye maeneo yao wakiwemo Maafisa wa Maendeleo ya Jamii, kilimo, Mifugo na biashara ili waweze kuboresha shughuli za kiuchumi kwa walengwa.
“Mkakati huo umeanza kuonyesha mafanikio kwa kuwaongezea walengwa kwa Mpango huo kipato na kuwapa uwezo wa kubuni na kusimamia kwa ufanisi miradi yao midogo midogo wanayoianzisha.
Hata hivyo bwana Kamagenge amesema mafanikio yaliyoanza kupatikana kwa kaya za walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini yameibua kilio kutoka kwa kaya nyingine ambazo hazikuingizwa kuingizwa kwenye Mpango huo kutaka nazo pia zijumuishwe kwenye utaratibu huo. Hadi sasa TASAF inatekeleza Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini katika vijiji 9,835 ambayo ni sawa na asilimia 70 ya vijiji na shehia zote Tanzania bara na Zanzibar.

Mkurugenzi M kazi wa Shirika la Misaada la Marekani –USAID-bwana Andy Karas (wa tatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na mmoja wa walengwa wa TASAF katika kijiji cha Igingilanyi kata ya Nduli wilaya ya Iringa baada ya kutembelea nyumba aliyoijenga mlengwa huyo (nyuma yao ) baada ya kupata ruzuku kutoka TASAF.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Misaada la Marekani USAID bwana Andy Karas akipokea zawadi ya kuku kutoka kwa mmoja wa walengwa wa Mpango wa kunusuru Kaya Masikini unaoratibiwa na TASAF katika kijiji cha Igingilanyi wilaya ya Iringa Vijijini ambako akutana na walengwa wa Mpango huo kuona namna wanavyonufaika na Mpango huo.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Misaada la Marekani nchini USAID bwana Andy Karas akisoma taarifa kwenye mkutano wa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kijiji cha Igingilanyi kata ya Nduli wilaya ya Iringa Vijijini ambako alitembelea kuona namna walengwa wa Mpango huo wanavyonufaika na ruzuku inayotolewa na serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF.
Baadhi ya Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kijiji cha Igingilanyi wilaya ya Iringa Vijijini wakiwaburudisha wageni kutoka Shirika la Misaada la Marekani –USAID waliotembelea kijiji hicho kuona shughuli za Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini unaoratibiwa na TASAF .
Mkurugenzi mkazi wa Shirika la Misaada la Marekani Bwana Andy Karas akisalimiana na mmoja wa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kijiji cha Igingilanyi kata ya Nduli wilaya ya Iringa Vijijini wakati alipotembelea kijiji hicho.Katikati yao ni Mkurugenzi wa miradi wa TASAF bwana Amadeus Kamagenge.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Misaada ya Kimataifa la Marekani –USAID-bwana Andy Karas amepongeza jitihada za serikali ya Tanzania kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF katika kuwafikia wananchi wanaokabiliwa na umasikini kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini ambao umeanza kuonyesha mafanikio makubwa katika maeneo mbalimbali nchini, jambo linalovutia wadau wa maendeleo kuendelea kusaidia jitihada hizo.
Bwana Karas ameyasema hayo alipokutana na Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kijiji cha Igingilanyi kata ya Nduli katika halmashauri ya Wilaya ya Iringa ,mkoani Iringa ambako licha ya kuelezwa namna TASAF inavyoendelea kutekeleza Mpango huo, lakini pia alishuhudia namna walengwa wa mpango huo walivyoboresha maisha yao kwa kutumia fedha za ruzuku za mfuko huo.
Amesema hamasa inayoonyeshwa na Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kujiletea maendeleo kwa kuanzisha miradi midogo midogo kwa kutumia fedha zinazotolewa na Serikali kupitia TASAF, imelivutia Shirika hilo na kuahidi kuwa litaendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania katika kuboresha utaratibu wa kuwainua wananchi kiuchumi .
Bwana Karas amesema utaratibu wa kuwafikia na kuwasaidia moja kwa moja wananchi wanaoishi katika mazingira magumu ya kiuchumi umekuwa ukitumika katika nchi nyingi duniani na umeonyesha mafanikio makubwa kwa kusisimua shughuli za kiuchumi na kijamii kwa kaya masikini .
Aidha Mkurugenzi Mkazi huyo wa USAID amevutiwa na masharti ya Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini kupitia TASAF hususani katika nyanja za elimu, afya, lishe na uwekezaji kwenye shughuli za kiuchumi kwa walengwa wa Mpango huo kuwa umeamusha ari ya kutokomeza umasikini miongoni mwao.
Akiwa katika kijiji hicho cha Igingilanyi kata ya Nduli bwana Karas alitembelea baadhi ya kaya za Walengwa wa TASAF na kujionea namna walivyonufaika na ruzuku ya Mpango huo kwa kuanzisha miradi midogo midogo ya ufugaji wa kuku na nguruwe na kutumia sehemu ya mapato yao kuboresha makazi kwa kujenga nyumba za matofali na kuezeka kwa mabati.
“ni jambo jema sana mnalolifanya kwa kuwekeza katika elimu ya watoto wenu na kuboresha makazi yenu kwa kutumia ruzuku mnayoipata” alisisitiza bwana Karas.
Bwana Karas pia alionyesha kuvutiwa na utaratibu wa kuanzisha vikundi vya kuweka akiba na kukopeshana unaofanywa na Walengwa wa Mpango huo wa Kunusuru Kaya Maskini ambao alisema ukiimarishwa utatoa fursa kubwa zaidi kwa wananchi hao kukuza shughuli zao za kiuchumi kwa kukopeshana kwa riba ndogo ikilinganisha na ile inayotozwa na taasisi za kibenki.
Kwa Upande wake Mkurugenzi wa Miradi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF,Bwana Amadeus Kamagenge alimweleza Mkurugenzi Mkazi huyo wa USAID kuwa licha ya Serikali kupitia Mfuko huo kuendelea kutoa ruzuku kwa Kaya Masikini sana katika mikoa yote nchni ,hivi sasa umeanza kujikita zaidi katika kuhamasisha walengwa kuanzisha vikundi vya kuweka akiba na kukopeshana kwa kuwatumia wataalamu walioko kwenye maeneo yao wakiwemo Maafisa wa Maendeleo ya Jamii, kilimo, Mifugo na biashara ili waweze kuboresha shughuli za kiuchumi kwa walengwa.
“Mkakati huo umeanza kuonyesha mafanikio kwa kuwaongezea walengwa kwa Mpango huo kipato na kuwapa uwezo wa kubuni na kusimamia kwa ufanisi miradi yao midogo midogo wanayoianzisha.
Hata hivyo bwana Kamagenge amesema mafanikio yaliyoanza kupatikana kwa kaya za walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini yameibua kilio kutoka kwa kaya nyingine ambazo hazikuingizwa kuingizwa kwenye Mpango huo kutaka nazo pia zijumuishwe kwenye utaratibu huo. Hadi sasa TASAF inatekeleza Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini katika vijiji 9,835 ambayo ni sawa na asilimia 70 ya vijiji na shehia zote Tanzania bara na Zanzibar.

Mkurugenzi M kazi wa Shirika la Misaada la Marekani –USAID-bwana Andy Karas (wa tatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na mmoja wa walengwa wa TASAF katika kijiji cha Igingilanyi kata ya Nduli wilaya ya Iringa baada ya kutembelea nyumba aliyoijenga mlengwa huyo (nyuma yao ) baada ya kupata ruzuku kutoka TASAF.

Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Misaada la Marekani USAID bwana Andy Karas akipokea zawadi ya kuku kutoka kwa mmoja wa walengwa wa Mpango wa kunusuru Kaya Masikini unaoratibiwa na TASAF katika kijiji cha Igingilanyi wilaya ya Iringa Vijijini ambako akutana na walengwa wa Mpango huo kuona namna wanavyonufaika na Mpango huo.

Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Misaada la Marekani nchini USAID bwana Andy Karas akisoma taarifa kwenye mkutano wa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kijiji cha Igingilanyi kata ya Nduli wilaya ya Iringa Vijijini ambako alitembelea kuona namna walengwa wa Mpango huo wanavyonufaika na ruzuku inayotolewa na serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF.

Baadhi ya Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kijiji cha Igingilanyi wilaya ya Iringa Vijijini wakiwaburudisha wageni kutoka Shirika la Misaada la Marekani –USAID waliotembelea kijiji hicho kuona shughuli za Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini unaoratibiwa na TASAF .

Mkurugenzi mkazi wa Shirika la Misaada la Marekani Bwana Andy Karas akisalimiana na mmoja wa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kijiji cha Igingilanyi kata ya Nduli wilaya ya Iringa Vijijini wakati alipotembelea kijiji hicho.Katikati yao ni Mkurugenzi wa miradi wa TASAF bwana Amadeus Kamagenge.
BENKI YA KILIMO YATEMBELEA MIRADI YA JKT KITEULE CHA BULAMBA, BUNDA
Bodi
ya Wakurugenzi ya Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB)
imetembelea mradi wa ufugaji wa vifaranga vya samaki unaotekelezwa na
kikosi cha 822 Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Rwamkoma wilaya ya Butiama
kupitia Kiteule chake cha Bulamba, wilayani Bunda.
Akizungumza
lengo la ziara hiyo, mkuu wa msafara huo ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi
ya Wakurugenzi ya Benki hiyo, Bibi Rosebud Kurwijila amesema lengo kubwa
la kutembelea Mradi huo ni kujionea juhudi za serikali za kuchagiza
mapinduzi ya kilimo hasa katika tasnia ya ufugaji na uvuvi wa samaki
nchini.
Bibi
Kurwijila aliongeza kuwa tasnia ya ufugaji wa samaki kwa njia ya
vizimba ni mojawapo ya minyororo ya mwanzo inayopatiwa mikopo kwa ajili
ya uongezaji wa thamani mazao na mifugo mbalimbali hasa katika uongezaji
wa thamani wa ufugaji wa samaki nchini.
Aliongeza
kuwa Benki ya Kilimo imejipanga kuendeleza uongezaji wa thamani wa
Ufugaji wa Samaki na uvuvi nchini ili ziweze kuchangia ukuaji wa uchumi
nchini.
Mradi
huo wa ufugaji wa samaki unaotekelezwa na JKT Wilaya ya Bunda, Kiteule
cha Bulamba ulizinduliwa rasmi mwezi Novembea, 2014 kwa kupandikiza
vifaranga vya samaki katika vizimba ndani ya Ziwa Victoria.
Mradi
huo unatekelezwa kwa ushirikiano na wadau mbalimbali wakiwemo Economic
Social Research Foundation (ESRF) na Shirika la Maendeleo la Umoja wa
Mataifa (UNDP).
Ufugaji
wa samaki kwa kutumia teknolojia ya vizimba ndani ya Ziwa Victoria,
umekuwa maarufu zaidi katika nchi za Afrika Mashariki ikiwemo Uganda na
Kenya ambapo umepunguza kwa kiasi kikubwa uvuvi haramu katika fukwe za
ziwa hilo.
Afisa
Kilimo na Ufugaji wa kikosi cha 822 Jeshi la Kujenga Taifa (JKT)
Rwamkoma, Kapteni M. Kinana (kulia) akiongea na Ujumbe kutoka Benki ya
Kilimo (hawapo pichani) walipotembelea mradi huo uliopo wilayani Bunda.
Kushoto ni Msimamizi wa Mradi wa Ufugaji wa Samaki wa JKT Kiteule cha
Bulamba, Luteni Kelvin Gondo.
Maafisa
wa Jeshi la Kujenga Taifa wanaotekeleza Mradi wa Ufugaji wa Samaki kwa
Vizimba Kiteule cha Bulamba wakifuatilia mkutano wa pamoja kati ya JKT
na Ujumbe kutoka Benki ya Kilimo.
Mwenyekiti
wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB),
Bibi Rosebud Kurwijila (kulia) akizungumza wakati walipotembelea Mradi
wa Ufugaji wa Samaki kwa Vizimba Kiteule cha Bulamba uliopo wilaya ya
Bunda, Mkoani Mara. Kushoto ni Afisa Uvuvi wa wilaya ya Bunda, Bw.
Steven Ochieng’.
Mjumbe
wa Bodi ya Wakurugenzi wa TADB, Bw. Dome Malosha (kulia) akizungumza
wakati walipotembelea Mradi wa Ufugaji wa Samaki kwa Vizimba Kiteule cha
Bulamba uliopo wilaya ya Bunda, Mkoani Mara. Wengine pichani ni
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki hiyo, Bibi Rosebud Kurwijila
(kushoto) na Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi, Bw. Joseph Mutashubilwa
(katikati).
Afisa
Uvuvi wa wilaya ya Bunda, Bw. Steven Ochieng’ (kushoto) akichangia
wakati wa mazungumzo hayo. Anayemsikiliza ni Mwenyekiti wa Bodi ya
Wakurugenzi wa Benki hiyo, Bibi Rosebud Kurwijila (kulia).
Msimamizi
wa Mradi wa Ufugaji wa Samaki wa JKT Kiteule cha Bulamba, Luteni Kelvin
Gondo akitoa maelezo juu ya maendeleo ya ufugaji wa samaki katika hatua
mbalimbali.
MAHAFALI YA KWANZA YA CHUO CHA MANJANO BEAUTY ACADEMY YAFANYIKA JIJINI DAR
Mgeni
Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh Mama Sophia Mjema Akizungumza
Machache wakati wa Mahafali ya kwanza ya Chuo cha Manjano Beauty
Academy .Ambapo amewataka Wanawake Kuchangamkia Fursa ya Urembo kwa kuwa
ukuaji wake kwa sasa ni kubwa na inakabiliwa na Upungufu wa Wataalamu
hivyo akiwashauri wanawake wengi Kujiunga na Kuiga Mambo Mazuri
Yanayofanywa na Chuo cha Manjano Beauty Academy.Akieleza zaidi Alisema
Sekta ya Urembo ina Fursa kubwa kwa Ajira kwa sasa,Katika Mahafali hayo
Wahitimu 120 Wametunukiwa vyeti katika katika nyanja ya urembo.
Mwanzilishi
wa Chuo cha Manjano Beauty Academy Mama Shekha Nasser Akitoa Hotuba
yake wakati wa mahafali ya kwanza ya chuo hicho yaliofanyika
Kwenye Viwanja vya Kijiji cha Makumbusho Jijini Dar es salaam.Mama
Shekha Nasser Amewashukuru wazazi na walezi kwa kuwapeleka Watoto wao
kwenye chuo hicho kwa LengoKupata Ujuzi wa Maswala ya Urembo,Aidha
Ametaja Changamoto kubwa Alizokabiliana nazo wakati anaanzishi Chuo
hicho Ikiwemo ukosefu wa Wataalamu wazawa wa Maswala ya Urembo.
Mgeni
Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh Mama Sophia Mjema Akiwa na Wageni
Waalikwa wakati wa Mahafali ya Kwanza ya Chuo cha Manjano Beauty
Academy
Baadhi
ya Wahitimu waliotunukiwa kwenye Mahafali ya Kwanza ya Chuo cha
Manjano Beauty Academy yaliofanyika Kwenye Viwanja vya Kijiji cha
Makumbusho Jijini Dar es salaam
Mshauri wa Maswala ya Kisaikolojia Anti Sadaka Akitoa Neno la Shukrani kwenye Mahafali hayo
Mgeni
Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh Mama Sophia Mjema Akitoa Cheti kwa
Mmoja wa Wahitimu Kwenye Mahafali ya kwanza ya Chuo cha Manjano Beauty
Academy..
Mgeni Rasmi,Uongozi wa Chuo cha Manjano Bauty Academy ,Wageni waalikwa na Wahitimu Wakiwa katika Picha ya Pamoja
Chuo
cha Manjano Beauty Academy kimetunuku Astashahada (Certificates) na
Stashahada (Diploma) kwa wahitimu 120 wa kwanza wa chuo hicho katika
nyanja ya urembo na utengenezaji wa nywele.Urembo
na mitindo ni moja kati ya sekta zinazoajiri mamilioni ya wanawake kwa
sasa, lakini bado sekta hiyo imeendelea kuwa isiyo rasmi.
Wanawake
wengi wanaofanya kazi kwenye saluni hawana utaalamu, lakini ndiyo
wanaofuatwa na wanaume na wanawake kwa ajili ya kutengenezwa mionekano
inayovutia, wanaishi kwa kufanya kazi kubahatisha.
Akizungumza
kwenye mahafali ya kwanza ya Manjano Beauty Academy iliyofanyika
jijini Dar es Salaam, mwanzilishi wa Manjano Beauty Academy, Shekha
Nasser alisema kuwa maono hayo ndiyo yaliyosababisha yeye kuanzisha
Manjano Beauty Academy.Manjano Beauty Academy ni shule kwa ajili ya afya
na urembo ambayo ina lengo la kuwawezesha wasichana wa Kitanzania.
“Tunashauri,
tunatoa mafunzo na kuwaandaa wanafunzi kwa ajili ya soko kwa kuwapatia
ujuzi unaohitajika. Serikali haiwezi kuwaajiri wahitimu wote, hata sekta
binafsi haiwezi kwa hivi sasa, kwa hiyo mafunzo haya yanawasaidia
wasichana wadogo kuweza kujitengenezea soko kwenye sekta ya urembo,”
alisema Shekha.Kwa
mujibu wa Shekha, wasichana hao wamekuwa wakipewa mafunzo na wakufunzi
bora wanaopatikana katika sekta ya urembo ambayo yatawatasaidia wao
kutimiza malengo yao binafsi pamoja na malengo ya kitaasisi.
“Naamini
kuwa wahitimu hawa watabadilisha sekta ya urembo hapa nchini, kama
Korea na Filipino wanavyotambulika ulimwenguni kwa kuwa na bidhaa bora
za ngozi na wataalam wa matibabu wenye weledi, huko mbeleni Tanzania
itajulikana ni nchi inayotoa bidhaa bora za urembo kwa ngozi za
Kiafrika, kuanzia bidhaa za urembo wa uso zinazozalishwa kutokana na
Mwani wa baharini toka Zanzibar mpaka bidhaa za poda ambazo zina
virutubisho vya Manjano ya asili na vyakutosha,” alisema Shekha ambaye
pia ni mwanzilishi wa Shear Illusions.
Mwaka
2015, kupitia bidhaa za LuvTouch Manjano, Shekha alizindua kampeni
inayoitwa Manjano Dream Makers iliyokuwa na lengo la kuwawezesha
wasichana wenye mafunzo ya kijasiriamali kujikwamua kiuchumi ili
kutimiza ndoto zao.
“Katika
miaka miwili tangu kuanzishwa kwa taasisi ya Manjano, mtandao wa
wanawake wa Manjano Dream-Makers umeweza kuenea katika majiji na miji
Saba nchini na kuwasaidia kutengeneza ajira na kutengeneza kipato kwa
kuuza bidhaa zao kupitia mfumo wa nyumba kwa nyumba kwa wanawake wasio
na ajira,” alisema Shekha.
Aliongeza kuwa, “Leo tunajivunia kuwa na wasichana 360 katika mtandao wa ‘Manjano Dream-Makers’ wenye matumaini ya kuboresha maisha yao na familia zao kwa kuuza bidhaa za LuvTouch Manjano.
Aliongeza kuwa, “Leo tunajivunia kuwa na wasichana 360 katika mtandao wa ‘Manjano Dream-Makers’ wenye matumaini ya kuboresha maisha yao na familia zao kwa kuuza bidhaa za LuvTouch Manjano.
CHAMA CHA MBIO ZA MAGARI TANZANIA (AAT) CHAWAKUMBUKA WAATHIRIKA WA AJALI NA KUJADILIANA NA WADAU NAMNA YA KUZIPUNGUZA
Mgeni Rasmi Mwanasheria wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Afande Deus Sokoni akifungua
mjadala katika Siku ya Kukumbuka waathirika wa Ajali Duniani (The World
Day Of Remembrance For Road Traffic Victims 19 November 2017)
iliyoandaliwa na kufanyika kwenye ofisi za Chama Cha Mbio za Magari
Tanzania AAT Upanga jijini Dar es salaam ikishirikisha wadau kutoka
taasisi mbalimbali nchini Tanzania.
Wadau
mbalimbali wamekutana na kujadiliana namna ya kupunguza ajali hasa
katika kuzipitia sheria za usalama barabarani na kuzifanyia marekebisho
pamoja na kuwakumbusha watumiaji wa Barabara kuzingatia sheria za
usalama barabarani, Taasisi zilizoshiriki katika mjadala huo ni WHO,
KIkosi Cha Usalama Barabarani, SUMATRA, Chama Cha Mbizo za Magari
Tanzania AAT, Chama cha Kutetea Abiria Tanzania CHAKUA, TIRA na
wawakilishi Idara ya Habari Maelezo.
Mratibu
wa Semina hiyo Bw. Alferio Nchimbi akizungumza katika semina hiyo na
kukaribisha wadau mbalimbai ili kuchangia michango yao katika mada
mbalimbali zilizowasilishwa.
Mgeni Rasmi Mwanasheria wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Afande Deus Sokoni akisisitiza jambo wakati akijibu maswali katika semina hiyo kulia ni Mratibu wa Semina hiyo Bw. Alferio Nchimbi.
Bw. Monday Likwepa Katibu Mkuu wa Chama cha Kutetea Abiria akichangia mada katika semina hiyo.
Bi
Mary Kessi Mratibu Programu ya Usalama Barabarani WHO akitoa mada
katika semina hiyo iliyofanyika kwenye ofisi za Chama cha Mbio za Magari
Tanzania (AAT) Upanga jijini Dar es salaam.
Afisa Leseni Mwandamizi kutoka SUMATRA Bw. Gabriel Anthony akitoa mada katika semina hiyo.
Daktari
Bingwa wa Kitengo cha Magonjwa ya Dharura na Ajali Muhimbili Dk Juma
Mfinanga akitoa ufafanuzi kwa upande wa hospitali ya Muhimbili wakati wa
semina hiyo.
Baadhi ya washiriki wakiwa katika semiha hiyo
KABURI LAFUKULIWA MOSHI KUONDOA UTATA WA MWILI WA MTU ALIYEZIKWA BAADA YA KUOKOTWA MTONI
Na Dixon Busagaga wa Globu
ya Jamii Kanda ya Kaskazini.
UTATA
umeighubika familia ya Jackson Makundi ambayo kijana wake
aliyetambulika kwa jina la Humphrey Makundi,Mwanafunzi wa shule ya
Sekondari ya Scolastica iliyopo mji mdogo wa Himo kupotea katika
mazingira tatanishi.
Utata
wa kupotea kwa mwanafunzi huyo unatiliwa shaka zaidi na familia hiyo
baada ya kufukuliwa kwa kaburi ulimozikwa mwili uliookotwa mto Ghona
mita 300 ,jirani na shule hiyo ukidaiwa kushabihiana na wa mwanafunzi
huyo.
Humphrey
Makundi, mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari ya
Scolastica anatajwa kupotea tangu Novemba 7 mwaka huu akiwa shuleni hapo
huku wanafunzi wenzake wakiendelea na mitihani ya kidato cha Pili ya
upimaji ya kitaifa .
Familia
ya kijana huyo yenye makazi yake mkoani Dodoma ikalazimika kutumia
mitandao ya kijamii kutoa taarifa za kupotea kwake ikidai mazingira ya
kutoweka kwake ni ya kutatanisha na baadae kuwasilisha taarifa katika
kituo cha Polisi cha Himo .
Kutokana
na kuwepo kwa taarifa za kuokotwa kwa mwili huo ,familia iliwasilisha
maombi katika mahakama ya Hakimu Mkazi, Moshi na mahakama ikaamuru
kufukuliwa kwa Kaburi hilo zoezi lililoanza majira ya saa 8:30 mchana na
kudumu kwa zaidi ya saa moja.
Jeshi
la Polisi liliongoza zoezi hilo katika makaburi ya Karanga huku
likishuhudiwa na ndugu wa mtoto aliyepotea ambapo baada ya mwili
kutolewa kaburini hali ya simanzi ilionekana katika nyuso za baadhi ya
ndugu wa Mwanafunzi huyo akiwemo baba mzazi wa kijana huyo.
Kamanda
wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Kamishna Msaidizi wa Polisi ,Hamis Issa
akathibitisha uwepo wa tukio hilo huku akieleza kuwa tayari jeshi la
Polisi linawashikilia wati 11 akiwemo mmiliki wa shule hiyo Edward Shayo
huku likifanya uchunguzi wa kina kuhusu matukio hayo mawili.
Mwili
uliofukuliwa katika makaburi ya Karanga upande wa marehemu wasiokuwa na
ndugu ulipelekewa katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya KCMC kwa
uchunguzi zaidi chini ya uangalizi wa jeshi la Polisi wakishirikiana na
madaktari kutoka KCMC.
Jeshi
la Polisi likiwa limezungushia utepe eneo ambalo kuna kaburi ulimozikwa
mwili ambao familia ya Mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Scolastica
iliyopo mji mdogo wa Himo aliyepotea ,Humphrey Makundi ulitilia shaka.
Kaburi ulimozikwa mwili wa mtu aliyezikwa na Manispaa ya Moshi baada ya kuokotwa Mto Ghona jirani na ilipo shule ya Sekondari .
Askari
Polisi wakishirikiana na ndugu wa Mwanafunzi aliyepotea Humphrey
Makundi wakifukua Kaburi ulimozikwa mwili wa mtu aliyeokotwa Mto Ghona
katika wilaya ya Moshi.
Kaburi likifukuliwa.
Baba
mzazi wa Mwanafunzi wa shule ya Sekondari ya Scolastica
aliyepotea,Jackson Makundi (Katkati) akijadili jambo na wanandugu wakati
zoezi la kufukua kaburi likiendelea.
Baba
mzazi wa Mwanafunzi Humphrey ,Jackson Makundi (Mwenye suti nyeupe)
akitizama mwili (haupo pichani) baada ya kaburi kufukuliwa.
Baba
mzazi wa Mwanafunzi Humphrey ,Jackson Makundi (Mwenye suti nyeupe)
akionekana akiwa amekaa chini baada ya kutizama mwili uliofukuliwa
katika kaburi .
Askari
Polisi na Wanandugu wa kijana aliyepotea wakijaribu kusaidia kumnyanyua
mzazi wa Mwanafunzi huyo kutoka katika eneo lilipo kaburi
lililofukuliwa .
Baba
mzazi wa Mwanafunzi Humphrey ,Jackson Makundi (Mwenye suti nyeupe)
akisindikizwa kutoka katika eneo la Makaburi ya Karanga katika manispaa
ya Moshi.
Mwili
uliofukuliwa katika makaburi hayo ukiwekwa katika gari la Polisi kwa
ajili ya kwenda kuhifadhiwa katika Hosptali ya Rufaa ya KCMC.
Gari la Polisi likiwa na mwili uliofukuliwa katika Makaburi ya Karanga.
Comments
Post a Comment