Wateja wa Tigo Kushinda Mamilioni ya Fedha Katika Promosheni ya Msimu wa Sikukuu

 Mkuu wa Malaipo ya Simu wa Kampuni ya Tigo Tanzania, Hussein Sayed, akizungunza na waandishi wa habari wakati akitangaza Promosheni ya msimu  wa Sikukuu ya Krismas kwa wateja wa kampuni hiyo watakaofanya malipo kwa kutumia Tigo Pesa, mamzungumzo hayoi yalifanyika jijini Dar es Salaam leo. (kulia ni Mkuu wa Bidhaa za Tigo James Sumali





                                                           PRESS RELEASE
Tigo Customers to Win Millions of Shillings with Tigo Pesa in new Festive Season Campaign
·         Massive prizes up for grabs for transactions done via Tigo Pesa
Dar es Salaam, 30th November, 2017- Tanzania’s leading mobile money service, Tigo Pesa is set to reward its customers with millions of shillings this Christmas and New Year season through an exciting new promotion dubbed ‘Transact and Win With Tigo Pesa.’

The one month-long promotion will see three grand prize winners lining their pockets with TZS 15 million, TZS 10 million and TZS 5 million each. Additionally every day, one lucky Tigo Pesa customer will scoop the daily prize of TZS 1million, with four others filling their pockets with daily prizes of TZS 500,000 each.

‘We expect a total of 153 winners in the one-month duration of this promotion,’ Tigo’s Chief Officer - Financial Services, Hussein Sayed revealed while unveiling the campaign to the media in Dar es Salaam today.

Customers will qualify for entry to the daily and monthly draws by simply doing any outgoing transaction via Tigo Pesa. ‘The more transactions you make on Tigo Pesa, the more your chances to win,’ Sayed elaborated. No conditions apply.

‘We are proud of our contribution in driving the financial inclusion agenda through Tigo Pesa.  Tigo pesa is more than a payment solution. It’s a lifestyle. Hence we take all possible measures to empower our customers. We are therefore delighted to once again offer our Tigo customers these prizes, which will enable them to enjoy their festive season as they continue to benefit from our digital lifestyle services,” he added.

These exciting prizes comes against the backdrop of Tigo’s modernized network infrastructure, with Tigo’s key priority hinged on listening to customer’s needs and always providing innovative and relevant solutions to address those needs.

Tigo Pesa is Tanzania’s second largest mobile money service provider that boasts a large network of over 70,000 merchants and agents countrywide. The mobile money service transacts over TZS 1.7bn every month.
                                                                                     -Ends-

About Tigo:
Tigo Tanzania is Tanzania's leading digital lifestyle telecommunications company. Tigo started its operations in Tanzania in 1995.  

Through its distinctive and diverse product portfolio in voice, SMS, high-speed internet and mobile financial services, Tigo has pioneered digital innovations such as the first Smartphone in Swahili, Free Facebook in Swahili, TigoPesa App, Tigo Mobile App as well as the first East African cross-border mobile money transfer with currency conversion.     

For 3 consecutive years, Tigo has dominated market growth, becoming the second largest operator in Tanzania.   With an aggressive expansion plan, Tigo launched 4G LTE network in Dar es Salaam and 24 cities around the country between 2015 and 2017. Tigo boasts a loyal 10 million registered subscribers, and directly and indirectly employs over 300,000 Tanzanians including, an extended network of customer service representatives, mobile money merchants, sales agents and distributors.  

Tigo is the commercial brand of a Swedish company Millicom, a multinational firm championing digital lifestyle in 13 countries worldwide; with commercial operations in Africa and Latin America and corporate offices in Europe and the US.

Millicom’s footprint in Africa spans 25 years and our Swedish DNA means we are transparent, always act with integrity and abide to the highest ethical standards.

Millicom has invested over US$1,690, million in Tigo Tanzania since 2007 and is listed on the Swedish Stock Exchange
………………………………………………………………………………………………………………
For further information visit: www.tigo.co.tz or contact:
Woinde Shisael – Corporate Communications Manager
Mobile: +255 713 123 431. Woinde.shisael@tigo.co.tz
…………………









Mary Rutta, akizungumza kwa wanahabari


 
Wateja wa Tigo Kushinda Mamilioni ya Fedha Katika Promosheni ya Msimu wa Sikukuu
Promosheni hiyo itakayodumu kwa kipindi cha mwezi mmoja itashuhudia washindi watatu wa jumla wakijinyakulia vitita vya TZS 15 millioni, TZS 10 millioni na TZS 5 millioni kila mmoja. Pamoja na hayo, kutakuwa na washindi wa kila siku ambapo mmoja atalamba donge nono la TZS 1millioni, huku wengine wanne wakijinyakulia TZS 500,000 kila mmoja, kila siku.

‘Tunatarajia kupata jumla ya washindi 153 katika kipindi cha mwezi mmoja wa promosheni hii,’ Afisa Mkuu wa Huduma za Kifedha wa Tigo, Hussein Sayed alisema akizindua promosheni hiyo mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.

Wateja watapata nafasi ya kushinda kwa kufanya miamala yoyote kutoka kwa simu zao kupitia Tigo Pesa. ‘Kadri ya unavyofanya miamala mingi zaidi ndivyo unavyojiongezea nafasi ya kushinda ,’ Sayed alifafanua. Hakuna masharti.

 “Tunajivunia mchango wetu katika kupanua wigo wa upatikanaji wa huduma za kifedha nchini kupitia Tigo Pesa. Tigo Pesa ni zaidi ya huduma ya kutuma na kupokea pesa. Ni sehemu ya maisha. Kwa hiyo tuna furaha kubwa kuwapa fursa ya kujishindia zawadi hizi nono ambazo zitawawezesha kufurahia msimu hu wa sikukuu huku wakiendelea kufaidika na huduma zetu bora za kidigitali,’ aliongeza.

Zawadi hizi murwa zinakuja kwa nguvu ya mtandao mpana na ulioboreshwa wa Tigo, huku lengo kuu la Tigo likiwa ni kuwasikiliza wateja wake na kuwapa huduma za kisasa zinazoendana na mahitaji yao.

Tigo Pesa ni huduma ya fedha ya simu za mkononi ya pili kwa ukubwa nchini yenye mtandao mpana wa mawakala zaidi ya 70,000 waliosambaa kote nchini. Miamala ya takriban TZS 1.7bn inafanyika kupitia Tigo Pesa kila mwezi.
-Mwisho-



Kuhusu Tigo:

Tigo Tanzania ni kampuni ya simu inayotoa huduma bora za maisha ya kidigitali nchini Tanzania. Tigo ilianza kuendesha shughuli zake nchini Tanzania mwaka 1995.
Kupitia huduma zake za kipekee za sauti, ujumbe mfupi, intaneti yenye kasi na huduma za kifedha kupitia simu za mikononi, Tigo inaongoza kwa ubunifu wa kidigitali kwa kuwa kampuni ya kwanza Tanzania kuzindua facebook na smartphone zenye lugha ya Kiswahili, huduma ya TigoPesa, pamoja na huduma ya kwanza inayowezesha wateja kufanya miamala ya fedha kupitia simu za mkononi kwenda nje ya nchi yenye uwezo wa kubadili thamani ya fedha kwa sarafu ya nchi husika Afrika Mashariki.     
Tigo ni kampuni ya pili kwa ukuwa nchini na imekuwa kampuni ya simu inayokuwa kwa kasi zaidi nchini kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo. Kupitia mkakati mkubwa wa kupanua na kuboresha huduma zake, kati ya mwaka 2015 hadi 2016, Tigo  ilizindua mtandao wa 4G LTE jijini Dar es Salaam na katika miji mingine 22 nchini
Tigo inajivunia jumla ya watumiaji milioni 10 wa simu waliosajiliwa, na imetoa nafasi za ajira za moja kwa moja na zile zisizokuwa na moja kwa moja kwa Watanzania wapatao 300,000; hii ikiwa ni pamoja na wawakilishi wa huduma kwa wateja, wafanyabiashara wakubwa wa fedha kupitia simu za mikononi, mawakala wa mauzo na wasambazaji.  
Tigo ni nembo ya kibiashara ya Millicom, kampuni ya kimataifa inayoongoza mageuzi ya maisha ya kidigitali katika nchi 13 duniani. Ikiwa inaendesha shughuli zake za kibiashara katika bara la Afrika na Amerika ya Kusini, Ofisi kuu za Millicom zipo Ulaya na Marekani.
………………………………………………………………………………………………………
Kwa taarifa zaidi tembelea: www.tigo.co.tz au wasiliana na: 
Woinde Shisael – Meneja Mawasiliano
Simu: +255 713 123431            Barua pepe: Woinde.shisael@tigo.co.tz
……………………………………………………………………………………………………..




Comments

Popular posts from this blog

AMANI YETU TUILINDE NAIBU WAZIRI CHANDE AZUNGUMZA KATIKA IJITIMAI JIJINI DODOMA

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.