Ubalozi wa Libya wavunja ukimya biashara ya utumwa

 Naibu Balozi wa Libya nchini, Saleh Kosa, akizungumza na waandishi wa habari, akikanusha nchi yake kufanya biashara ya binadamu na kudai kwamba kinachofanyika ni utozaji wa fedha za ajili ya kuwasafirisha binadamu waliokimbia katika nchi zao ili wavuke kwenda nchi za Ulaya na Marekani. Mazunghumzo hayo yalifanyika Ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana




Na MWANDISHI WETU

SERIKALI ya Libya imekanusha taarifa iliyosambaa katika mitandao na vyombo mbalimbali vya habari kuwa mamia ya watu wanauzwa kama mnada katika soko la utumwa nchini humo kwa kiasi kidogo cha chini ya dola 400.
Akizungumza na waandishi wa habari Kaimu Balozi wa Libya, Saleh Kosa alisema mapatano yale yalikuwa ni gharama za kuwasafirisha na wala si gharama za kuuza uhuru wao ili wawe watumwa.
“Serikali ya Libya, mara tu baada ya kupata taarifa hizo ilivituma vyombo husika kufanya uchunguzi jumuishi na wa kina kuhusu madai hayo ambayo ni makosa kwa mujibu wa sheria za Libya na baadaye isambaze kwa watu wote na pia kuwachukulia hatua za kisheria wote wanaohusika bila ya kujali kama makosa yenyewe yamefanywa kwa lengo la kuvukisha wahamiaji au utumwa,”alisema Kosa.
Alisema Libya inaamini kwamba mambo kama hayo, huwa ni sehemu yanayofungamana na uhamiaji haramu ambao Libya ndiyo nchi iliyodhurika zaidi na kwamba imekataa kuwajibika peke yake kubeba jukumu la kukomesha uhamiaji haramu.
“Libya inapenda kuhakikisha kwamba katika kukomesha suala la uhamiaji haramu na mambo yanayohusiana nayo inalazimu kuwapo kwa juhudi za pamoja za kimataifa na zilizoratibiwa ili kupambana na hali hiyo.
“Kwa kigezo hiki, Libya inaomba kuwepo na mikakati kivitendo na yenye athari kubwa baina ya nchi wanazotoka wahamiaji haramu, nchi wapitiazo na waendazo na pia kushirikisha taasisi husika za kimataifa na za kikanda,”alisema kaimu balozi huyo.
Kosa alisema Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Libya inaweka upya msisitizo wake kuiunga mkono serikali ya nchi hiyo, kwa kuipa uwezo wa kiufundi na kilojistiki ili kuisaidia katika kudhibiti mipaka yake.
“Kuuhimiza Umoja wa nchi za Ulaya na jumuiya ya kimataifa kushirikiana na nchi watokazo wahamiaji ili kufanya miradi ya maendeleo ya kudumu kwa lengo la kukomesha suala hili na athari zake hatari.
“Pia kutekeleza vifungu vya tamko la pamoja kuhusu uhamiaji na maendeleo lililokubaliwa katika vikao vya Novemba 22 na 23 mwaka 2006 mjini Tripoli, Libya.
“Kuisaidia Libya kumudu gharama za kujenga na kuendesa vituo vya kuwaweka wahamiaji na kutoa misaada kusaidia maeneo yote yaliyodhurika na uhamiaji nchini Libya na pia kuvisaidia vyombo vya usalama vya Libya kuwa na uwezo unaohitajika,”alisema.
Aidha alisema kwa mara nyingine serikali ya Libya inalaani biashara ovu ya uuzaji na usafirishaji binadamu ikiwa ni ya kimataifa au ya kikanda.
Alisema endapo kuna lililotokea kuhusu hilo la wahamiaji basi itakuwa jambo alilolitenda mtu binafsi na wala si suala la kuratibiwa.
“Sisi tunalikana na kulilaani vikali kwa imani kwamba kushughulikia suala la wahamiaji ni lazima kuwe ni kwa kuzingatia heshima yao kama wanadamu.
“Serikali ya Umoja wa Kitaifa inawahakikishia kuwapo kwa mahusiano ya kindugu baina ya walibya na ndugu zao waafrika ambao kwa karne nenda rudi wamekuwa wakiunganishwa na mashikamano ya urafiki na kuwa malengo yanayofanana,”alisema.







Akisisitiza ajambo kwa waandishi wa habari

Comments

Popular posts from this blog

AMANI YETU TUILINDE NAIBU WAZIRI CHANDE AZUNGUMZA KATIKA IJITIMAI JIJINI DODOMA

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.