RAIS DKT MAGUFULI AKUTANA NA BILL GATES NA KAIMU BALOZI WA MAREKANI NCHINI


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe magufuli akisalimiana na Mwenyekiti wa  tasisi ya Bill and Melinda Gates Foundation Bw. Bill Gates aliyemtembelea na kufanya mazungumzo naye Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 10, 2017. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe magufuli akizungumza na Mwenyekiti wa  tasisi ya Bill and Melinda Gates Foundation Bw. ill Gates aliyemtembelea  Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 10, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe magufuli akiagana na Mwenyekiti wa  tasisi ya Bill and Melinda Gates Foundation Bw. Bill Gates aliyemtembelea na kufanya mazungumzo naye Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 10, 2017. Pamoja nao ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (kulia), Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mhe. Dk Charles Tizeba (wa tatu Kushoto), Msaidizi wa rais Masuala ya diplomasia Bi. Zuhura Bundala (kushoto)  pamoja na maafisa alioongozana nao Bw. Bill Gates
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe magufuli akisalimiana na  Kaimu Balozi wa  Marekani nchini Bi. Immi Patterson aliyemtembelea na kufanya mazungumzo naye Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 10, 2017.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe magufuli akiwa katika mazungumzo na   Kaimu Balozi wa  Marekani nchini Bi. Immi Patterson aliyemtembelea  Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 10, 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe magufuli akimsindikiza Kaimu Balozi wa  Marekani nchini Bi. Immi Patterson aliyemtembelea na kufanya mazungumzo naye Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 10, 2017

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe magufuli akiagana na  Kaimu Balozi wa  Marekani nchini Bi. Immi Patterson aliyemtembelea na kufanya mazungumzo naye Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 10, 2017.PICHA NA IKULU

HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YASHINDWA KUTEKELEZA AGIZO LA KAMATI YA LAAC

Na Jumbe Ismailly IRAMBA 

HALMASHAURI ya wilaya ya Iramba,Mkoani Singida imeshindwa kutekeleza agizo la kamati ya kudumu ya Bunge la kutenga asilimia kumi kutoka kwenye mapato yake ya ndani kwa ajili ya vikundi vya wanawake pamoja na vijana katika kipindi cha kuanzia mwaka wa fedha wa 2012/2013 hadi 2014/2015.

Kaimu Mweka Hazina wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba,CARROLINE DALULI aliyasema hayo kwenye taarifa aliyotoa kwenye mkutano wa Baraza maalumu la madiwani wa Halmashauri ya wilaya hiyo lilipokutana kujadili hoja za Ukaguzi na Mpangokazi wa utekelezaji wa maoni yaliyotolewa na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za serikali (CAG) kwa mwaka 2015/2016.

“Kamati iliagiza Halmashauri kuchangia asilimia kumi kutoka kwenye mapato ya ndani kwa ajili ya wanawake na vijana kwa miaka hiyo iliyotajwa na kiasi kilichoonekana”alifafanua kaimu Mweka Hazina huyo.

Kwa mujibu wa Kaimu Mweka hazina huyo kwa mwaka 2012/2013,2013/2014 na 2014/2015 Halmashauri ya wilaya ya Iramba haijatekeleza agizo la kamati ya kudumu ya Bunge kwani hakuna fedha yeyote ile iliyotengwa na iliyopelekwa kwenye vikundi hivyo.

Aidha Daluli aliweka bayana pia kwamba kwa mwaka 2016/2017 Halmashauri hiyo imechangia shilingi milioni mbili,zikiwemo shilingi milioni moja kwa Mazega Kisimba na shilingi zingine milioni moja kwa kikundi cha Maendeleo Shelui na itaendelea kuchangia kadri fedha zitakapopatikana.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Huduma za jamii wa Halmashauri hiyo,Hamisi Kinota akichangia hoja hiyo ya michango ya vikundi vya wanawake na vijana alisisitiza kwamba kutokana na uchangiaji wa Halmashauri hiyo unadhihirisha wazi kwamba Halmashauri haitaweze kuchangia michango hiyo kwa asilimia mia moja.

Hata hivyo Kinota huku akionyesha hofu ya utekelezaji wa agizo hilo la kamati ya kudumu ya Bunge alibainisha kuwa katika kipindi cha mwaka 2012/2013,2013/2014 na 2014/2015 kati ya shilingi milioni 109,819,388 zilizotarajiwa kutumika,ni shilingi milioni mbili tu ndizo zilizotolewa na hivyo kubakiza zaidi ya shilingi milioni 107,hali ambayo inaonyesha hakuna uwezekano kwa Halmashauri hiyo kumaliza deni hilo kwa asilimia mia moja.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Singida,Dk.Rehema Nchimbi alishauri kwamba njia pekee ya kumaliza deni hilo la michango ya vikundi vya wanawake na vijana ni kuandika maandiko mbali mbali na kusambaza kwa wafadhili na kudai kwamba kuna watu wenye fedha walio tayari kuwasaidia wanawake na vijana.

“Mtakapopata hizo fedha najua mnaweza kupata hata zaidi ya shilingi milioni mia mbili,mtakapopata hizo fedha mtaaandika kwamba ni fedha ambazo ninyi wenyewe Halmashauri mmezitafuta kwa hiyo itakuwa ni sehemu ya mapato yenu na mtazipeleka kwa wanawake na vijana”alisisitiza Dk.Nchimbi.
Mkuu wa Mkoa wa Singida,Dk.Rehema Nchimbi akimkabidhi mmoja wa madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba cheti cha mafunzo ya udiwani aliyopata na ambayo yatawawezesha madiwani wote kutambua majukumu pamoja na mipaka yao ya kazi.(Picha zote Na Jumbe Ismailly).
Mkuu wa Mkoa wa Singida,Dk.Rehema Nchimbi akisisitiza juu ya maafisa watendaji wa vijiji 30 walioiba fedha za chakula cha njaa kuhakikisha wanazirejesha ifikapo aug,30,mwaka huu na kupendekeza njia rahisi ya fedha hizo kurejeshwa kuwa ni kuanzishwa kwa Mahakama tembezi itakayomtembelea kila mdaiwa na kuuza mali alizonazo ili kulipia deni la chakula hicho cha njaa walizokula.

SERIKALI KUDHIBITI USAFIRISHAJI WA FEDHA TASLIMU MIPAKANI


Washiriki wa warsha ya siku mbili ya maandalizi ya utekelezaji wa Kanuni za Taarifa za Usafirishaji na uingizaji wa fedha tasilimu kutoka na kwenda nje ya nchi wakifuatilia kwa makini mjadala katika warsha hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu (BoT) jijini Dar es Salaam.
Washiriki wa warsha ya siku mbili ya maandalizi ya utekelezaji wa Kanuni za Taarifa za Usafirishaji na uingizaji wa fedha tasilimu kutoka na kwenda nje ya nchi wakiwa katika picha ya pamoja baada ya ufunguzi wa warsha hiyo iliyofanyika katika Ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), jijini Dar es Salaam.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Fedha na Mipango)


Na Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam

Wizara ya Fedha na Mipango imeandaa Kanuni za taarifa za Usafirishaji na uingizaji wa fedha taslimu kutoka na kwenda nje ya nchi (Crossborder Declaration of Currency and Bearer Negotiable Instruments Regulations) ambapo wasafirishaji wa fedha taslimu na wasafiri wote wanaotoka au kuingia nchini, watatakiwa kutoa taarifa za fedha taslimu wanazosafirisha ikiwa fedha hizo zinalingana au zinazidi kiasi cha dola za kimarekani elfu kumi (USD 10,000).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha ya siku mbili ya maandalizi ya utekelezaji wa Kanuni hizo, Kamishna na Mtendaji Mkuu wa Kitengo cha Kudhibiti Fedha Haramu (FIU) Ndugu Onesmo H. Makombe alisema utekelezaji wa kanuni hizi, pamoja na mambo mengine utaiwezesha nchi kuwa na takwimu za usafirishaji fedha taslimu.

“Takwimu hizo zitakazosaidia pamoja na mambo mengine kubaini vitendo vya kihalifu, kupunguza utoroshaji wa mitaji na kuhakikisha kuwa tunapunguza kama siyo kumaliza kabisa usafirishaji wa fedha zitokanazo na uhalifu au/na fedha kwa ajili ya kufadhili ugaidi” alisema Bw. Makombe

Aidha kanuni hizo zimeweka adhabu zitakazochukuliwa dhidi ya wale watakabainika kutaka kupita na fedha zinazolingana au zinazozidi kiwango kilichowekwa bila kutoa taarifa au watakaotoa taarifa za uongo. Alizitaja adhabu hizo kuwa ni pamoja na kukamatwa kwa fedha taslimu walizonazo na kuchukuliwa hatua nyingine za kisheria kama vile kufunguliwa mashtaka.

“Wahalifu pamoja na mambo mengine, wanapenda kusafiri na fedha taslimu kwani wanaogopa kutumia benki kutuma fedha kutokana na umakini unaoongezeka katika benki na udhaifu unaoweza kuwepo mipakani” Alisisitiza Bw. Makombe.Kamishna huyo amewaasa washiriki wa warsha hiyo kutekeleza jukumu hilo kwa uadilifu na uaminifu mkubwa ili kuziba mianya yote ambayo wahalifu wanaweza kuitumia kutimiza kusudi lao ovu na kuhatarisha usalama wa nchi.

Kutokana na umuhimu wa ushiriki wa wadau mbalimbali katika utekelezaji wa kanuni hizo warsha hiyo imejumuisha washiriki kutoka taasisi mbalimbali wengi wao wakiwa ni maafisa forodha.

Washiriki hao wametoka Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Fedha na Mipango-Zanzibar, Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki na kikanda, Mamlaka ya Mapato Tanzania na vikosi vya ulinzi na usalama

Wengine ni Bodi ya Mapato Zanzibar, Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo-Zanzibar, Shirika la Posta, Benki kuu ya Tanzania, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka-Zanzibar, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka-Tanzania Bara Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania Bara na Zanzibar, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, Idara ya uhamiaji na Kitengo cha Kudhibiti Fedha Haramu.

JK NA LOWASSA WAJUMUIKA NA MAMIA YA WANANCHI MAZISHI YA BILIONEA MREMA ARUSHA

 Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete akiweka shada la maua katika kaburi la Bilionea marehemu Maleu Mrema katika ibada ya mazishi yaliyofanyika jana katika hoteli yake ya Ngurudoto iliyopo nje kidogo ya jiji la Arusha(Habari Picha NA Pamela Mollel,Arusha)
Waziri Mkuu mstaafu,Edward  Lowassa akiweka shada la maua pamoja na mke wake  katika mazishi ya bilionea Maleu Mrema jana nje kidogo ya jiji la Arusha katika hoteli ya Ngurudoto
Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo akiweka shada la maua katika kaburi la marehemu Mrema katika ibada ya mazishi yaliyofanyika katika hoteli yake ya Ngurudoto iliyopo nje kidogo ya jiji la Arusha
 Baadhi ya wake za marehemu wakiweka udongo katika kaburi la mpendwa wao

 Waziri Mstaafu wa mambo ya nje Benard Membe akiweka shada la maua katika kaburi la Bilione Mrema

 Meneja mahusiano Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa)Pascal Shelutete akiweka shada la maua katika kaburi la Bilione Mrema.
 Watoto wa marehemu wakiwa wamebeba mashada ya maua

 Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete wakisalimiana na Waziri Mkuu mstaafu,Edward  Lowassa katika mazishi ya bilionea Maleu Mrema leo nje kidogo ya jiji la Arusha katika hoteli ya Ngurudoto
 Baadhi ya wanakamati wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa marehemu Mrema kuelekea katika eneo maalumu lililotengwa na familia kwaajili ya maziko
 Hapa watoto wakiwa wanaweka udongo katika kaburi la baba yao
 Wake wa marehemu wakiwa wanaingia katika eneo maalumu lililotengwa kwaajili ya maziko
 Kulia ni Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete,katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo pamoja na
Abdulrahman Omari Kinana wakiteta jambo katika msiba wa Mrema
 Wake wa marehemu Mrema wakiwa katika huzuni kulia aliyevalia suti nyeusi ni baba mzazi wa Bilionea huyo
 Mh Abdulrahman Omari Kinana mara baada ya kuweka shada la maua
 Jeneza la marehe Bilionea Maleu Mrema likiwa linashushwa katika nyumba yake ya milele

Wanafamilia wakiwa katika picha ya pamoja na Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete
Nyumba ya milele ya Bilionea Maleu Mrema 

Comments

Popular posts from this blog

AMANI YETU TUILINDE NAIBU WAZIRI CHANDE AZUNGUMZA KATIKA IJITIMAI JIJINI DODOMA

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.