MATUKIO MBALIMBALI KATIKA PICHA


Mkurugenzi Mtendaji wa ForumCC, Rebecca Muna akiwasilisha mada kwa wadau kutoka kwenye asasi za kiraia, maafisa mipango wa wizara mbalimbali pamoja na watafiti kuhusu namna ya kuongeza jitihada katika kuingiza masuala ya kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi katika mipango na bajeti.

FORUMCC imeandaa mkutano na kukutanisha wadau kujadili namna ya kuongeza jitihada katika kuingiza masuala ya kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi katika mipango na bajeti ya serikali kuu na serikali za mitaa hapa nchini Tanzania. 

Mkutano huo umewakutanisha wadau mbalimbali kutoka sekta binafsi pamoja na serikali ili kuangalia njia nzuri zinazoweza kusadia Tanzania kuwa na mfuko wa Mabadiliko ya Tabianchi ili kupunguza kutegemea zaidi fedha kutoka kwa wafadhili.

Lengo la mkutano huu ni kuwakutanisha wadau kujadili na kuhamasisha jitihada za kuingiza masuala ya mabadiko ya Tabianchi katika mipango na bajeti ya Serikali katika kipindi hiki tunapoelekea katika Bunge la bajeti ya mwaka 2017/18.

Akizungumza kwenye mkutano huo Mkurugenzi Msaidizi, Sekta za Uchumi na Uzalishaji toka TAMISEMI, Dkt. Lucy Ssendi amesema serikali kupitia TAMISEMI iko karibu na wadau mbalimbali wa mabadiliko ya Tabianchi ili kuweza kupunguza majanga mbalimbali hapa nchini, na wao TAMISEMI wana jukumu la kubwa kwenye asasi za kiraia kuingia kwenye miradi inayohusu mabadiliko ya Tabianchi.

Pia Mwenyekiti wa bodi ya ForumCC, Euster Kibona aliwaomba wadau mbalimbali waliofika kwenye mkutano huo kushirikiana na FORUMCC ili kuweza kufikia malengo waliyojiwekea kwenye suala la mabadiliko ya Tabianchi linalotishia maendeleo ya jamii za mbalimbali na ukuaji wa uchumi nchini Tanzania.

Mkutano huo uliofanyika kwenye ukumbi wa COSTECH (Tume ya Sayansi na Teknolojia) leo uliwakutanisha wadau mbalimbali kutoka asasi za kiraia, maafisa mipango kutoka wizara mbalimbali, watafiti na waandishi wa habari. 
Mkurugenzi Msaidizi, Sekta za Uchumi na Uzalishaji toka TAMISEMI, Dkt. Lucy Ssendi akitoa mada kuhusu kazi za TAMISEMI pamoja na ushirikiano wake kwenye masuala ya mabadiliko ya Tabianchi kwenye mkutano uliofanyika leo kwenye kumbi wa COSTECH (Tume ya Sayansi na Teknolojia) jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa bodi ya ForumCC, Euster Kibona akitolea ufafanuzi baadhi ya maswali pamoja na kutoa maoni kwa maofisa wa wizara kuangalia namna ya kushirikiana ili kupunguza athari za mabadiliko ya Tabianchi.
Mkutano ukiendelea uliowakutanisha wadau mbalimbali uliowakutanisha ili kujadili namna ya kuongeza jitihada katika kuingiza masuala ya kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi katika mipango na bajeti.
Mtaalamu wa Masuala ya Nishati, Erneus Kaijage akiwasilisha mada kuhusu uwekezaji wa fedha katika sekta ya nishati kwenye mkutano uliowakutanisha wadau mbalimbali wa mabadiliko ya Tabianchi leo jijini Dar es Salaam






Baadhi ya wadau wa Mabadiliko ya Tabianchi wakichangia mada pamoja na kuuliza maswali kuhusu namna ya kuongeza jitihada katika kuingiza masuala ya kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi katika mipango na bajeti kwenye mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa COSTECH (Tume ya Sayansi na Teknolojia) leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Msaidizi, Sekta za Uchumi na Uzalishaji toka TAMISEMI, Dkt. Lucy Ssendi akijibu maswali yaliyokuwa yanaulizwa na wadau mbalimbali wa masuala ya mabadiliko ya Tabianchi kwenye mkutano uliowakutanisha wadau hao kwenye ukumbi wa Chuo cha Sayansi jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi Mtendaji wa ForumCC, Rebecca Muna akijibu maswali yaliyokuwa yakiulizwa na wadau mbalimbali waliokutana ili kujadili namna ya kuongeza jitihada katika kuingiza masuala ya kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi katika mipango na bajeti.
Mwezeshaji wa Mkutano wa FORUMCC, Abdallah Henku akizungumza jambo kwenye mkutano huo uliowakutanisha wadau mbalimbali wa Mabadiliko ya Tabianchi.



Baadhi ya wadau mbalimbali walioshiriki kutoka asasi za kiraia, maafisa mipango kutoka wizara, watafiti na waandishi wa habari wakifuatilia mada zilizokuwa zikiendelea kwenye ukumbi wa COSTECH (Tume ya Sayansi na Teknolojia) mkutano ulipofanyika leo ulioandaliwa na FORUMCC.

Picha ya Pamoja

BALOZI WA KOREA AKABIDHI MAKTABA YA KISASA KWA SERIKALI YA TANZANIA

Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Serikali ya Korea kupitia mradi wa ''Thank you Small Ribray program'' leo imekabidhi Vifaa na kuzindua maktaba ndogo ya kisasa katika ofisi za makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo balozi wa Korea nchini Song Geum Young amesema kuwa serikali yake licha ya kusaidia serikali katika miradi mingi lakini kwa sasa wameamua kusaidia katika kuwawezesha watoto kupata elimu inayoendana na wakati.

"sisi kama korea tunaamini kuwa ukimpa mtoto elimu umeweza kumpa maisha ya kesho, hivyo vifaa hivi vitaweza kuwasaidia katika kukuza taaluma yao " amesema Balozi.Balozi ametoa wito kwa wazazi kuwaleta watoto waweze kutumia maktaba hiyo kwa kutumia sehemu hiyo kwa ajili kukuza taaluma yao .
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Dk Leonard Akwilapo akiwa na Balozi wa Korea nchini , Song Geum Young na Mama Anna Abdalah Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi ya Makumbusho ya Taifa wakikata utepekuashiria uzinduzihuo.

Balozi wa Korea nchini , Song Geum Young akizungumza kabla ya uzinduzi wa wa Maktaba ya kisasa ambayo imetolewa na Serikali ya korea.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Dk Leonard Akwilapo, akikabidhi vitabu kwa Mwenyekiti wa bodi ya Makumbusho ya Taifa , Mama Anna Abdalah
Mkurugenzi Mtendaji wa Makumbusho ya Taifa , Audax Mabula akizungumza kabla ya uzinduzi wa Maktaba ya Kisasa katika Makumbusho ya Taifa.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Dk Leonard Akwilapo akizungumza kabla ya uzinduzi wa Maktaba ya Kisasa katika ukumbi wa Makumbusho ya taiafa kwa msaada wa Serikali ya watu wa Korea.
Baadhi ya wadau walioshiriki tukio hilo
Viongozi mbalimbali akiwemo na balozi mteule wa korea wakifatia hotuba ya balozi
Wanafunzi wa shule ya Msingi Bunge wakishuhudia tukio hilo
Mwenyekiti wa bodi ya Makumbusho ya Taifa , Mama Anna Abdalah akizungumza na waandishi wa habari 

Wanafunzi wa shule ya Msingi Bunge wakitumia baadhi ya vifaa vilivyopo katika Maktaba ya Kisasa ndani ya ukumbi huo wa makumbusho ya Taifa

Wanafunzi wa shule ya Msingi Bunge wakitumia baadhi ya vifaa vilivyopo katika Maktaba ya Kisasa ndani ya ukumbi huo wa makumbusho ya Taifa

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Dk Leonard Akwilapo akiwa na Balozi wa Korea nchini , Song Geum Young wakipata maelekezo jinsi ya namna vifaa vya kielektronic vinavyofanya kazi katikakutoa elimu kwa watoto ndani ya maktaba hiyo ambayo imefadhiliwa na serikali ya Korea

Picha ya pamoja ya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Dk Leonard Akwilapo akiwa na Balozi wa Korea nchini , Song Geum Young na Mama Anna Abdalah wageni waalikwa wengine waliohudhuria katika hafla hiyo

COCA-COLA YAZIDI KUHAMASISHA WANAFUNZI KUTAMBUA NA KUKUZA VIPAJI VYAO

Wafanyakazi wa Coca-Cola wakiwagawia wanafunzia wa Shule ya Sekondari ya Olorieni Vinywaji vya Coca-Cola katika eneo la shule hiyo. 
Mwanafunzi wa Shule ya sekondari ya Olorieni akionyesha kipaji cha kucheza na Baiskeli kupitia promosheni inayoendeshwa na Coca-Cola ya Onja msisimko katika shule mbalimbali. 
Wanafunzi wa Shule ya sekondari ya Olorieni wakionyesha kipaji cha kucheza na baiskeli kupitia promosheni inayoendeshwa na Coca-Cola ya Onja msisimko katika shule mbalimbali. 
Wanafunzi wa Shule ya sekondari ya Olorieni wakicheza wimbo wa Kijuso (jukwaani) huku wenzao wakiwatazama kwenye promosheni inayoendeshwa na Coca-Cola ya Onja msisimko katika shule mbalimbali jijini Arusha.
Wanafunzi wa wawili wa Shule ya sekondari ya Olorieni wakionyesha kipaji cha kucheza muziki kupitia promosheni inayoendeshwa na Coca-Cola katika shule mbalimbali. 
Mwongozaji wa Promosheni (Supervisor) Onesmo Swila Akimkabidhi zawadi ya mipira ya miguu mwalimu wa michezo wa shule ya Sekondari ya Olorieni katika promosheni yao ya Onja msisimko na Coca-ola inayoendeshwa katika shule mbalimbali jijjini Arusha. 
Wanafunzi wa Shule ya sekondari ya Olorieni wakionyesha kipaji cha kuimba kupitia promosheni inayoendeshwa na Coca-Cola ya Onja msisimko katika shule mbalimbali. 
Wanafunzi wa Shule ya sekondari ya Olorieni wakicheza wimbo wa Kijuso (jukwaani) huku wenzao wakiwatazama kwenye promosheni inayoendeshwa na Coca-Cola ya Onja msisimko katika shule mbalimbali jijini Arusha. 
Wanafunzi wa Shule ya sekondari ya Olorieni wakigongeana sheazi mara baada ya kugawiwa vinywaji kwenye promosheni inayoendeshwa na Coca-Cola ya Onja msisimko katika shule mbalimbali jijini Arusha. (Picha na Ferdinand Shayo). 

Kampuni ya Bonite Bottlers Kupitia kinywaji chake cha Coca-Cola imezidi kuhamsisha wanafunzi kutambua na kukuza vipaji vyao kupitia Promotioni ya Onja Msisimko na Coca-Cola wanayoiendesha katika shule mbalimbali jijini Arusha. Cocacola imefanya hayo katika shule Sekondari ya Olorieni jijini Arusha ambapo baadhi ya wanafunzi walipata Fursa ya kuonyesha vipaji vyao ikiwemo kucheza na baiskeli katika jukwaa, kucheza muziki pamoja na kuimba. Msimamizi wa promosheni hiyo Onesmo Swila amewataka wanafunzi katika shule hizo wanazotembelea ikiwemo Sekondari ya Olorieni ambayo wameitembelea, kuendeleza vipaji vyao kwa kila fursa wanayopata kwa kuwa kipaji ni hazina.

 “wanafunzi acheni kuficha vipaji vyenu, vionyesheni, ili mpate fursa ya kuvikuza, sisi Coca-Cola tumeamua kuwahamasisha kwa lengo kuwatia moyo ili mfikie malengo yenu.” Alisema Onesmo Aidha licha ya kuwashukuru walimu wa shule hiyo kwa kuwakubalia kutembelea shule hiyo na kuwagawia wanafunzi zawadi ikiwemo ya kinywaji cha Coca-Cola, amesema ziara hiyo wataendelea nayo katika shule mbalimbali jiji Arusha ili kuwaonjesha wanafunzi Msisimko wa Coca-Cola. 

Mwalimu wa Michezo katika Shule ya Sekondari ya Olorieni, Haroon Maluli akipokea zawadi ya Mipira kutoka Coca-Cola, Ameshukuru kwa zawadi hiyo huku akiwasihi wanafunzi kutoficha vipaji vyao, bali wavionyeshe kwa kila fursa inayopatikana ili kuvikuza zaidi. “Tunashukuru kwa zawadi ya mipira, ila nawasihi wanafunzi kutumia fursa kama hii iliyoletwa na Coca-Cola kuonyesha vipawa vyenu, kwani hata sisi tulivyokuwa tunasoma hatukuvificha ndio maana tupo hapa” alisema Mwalimu Haroon.

MUWSA WATUMIA MAADHIMISHO YA WIKI YA MAJI KUOTESHA MITI KATIKA VYANZO VYAKE VYA MAJI.

Baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) wakishusha miti tayari kwa ajili ya kuotesha kando ya vyanz vya maji vinavyosimamiwa na mamlaka hiyo.
Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) John Ndetiko akiwa amebeba mti tayari kwa ajili ya kuotesha kando ya chanzo cha maji cha Shiri kilichopo wilayani Hai.
Baadhi ya wanafunzi wa shule za msingi wakisaidia katika zoezi la ubebabji miti kwa ajili ya kuotesha.
Wafanyakazi wa MUWSA wakiwa wamebeba mit kwa ajili ya kuotesha katika chanzo cha maji cha Shiri.
Kaimu Mkurugenzi wa MUWSA,John Ndetiko akiotesha mti katika eneo la chanzo cha maji cha Shiri.

Baadhi ya wafanyakazi wa MUWSA wakiotesha miti katika chanzo hicho.
Hii ni sehemu ya mitiiliyooteshwa Mwaka jana katika eneo hilo zoezi lililooongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimajaro Saidi Mecky Sadicki.
Huu ndio mti uliooteshwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Saidi Mecky Sadicki katika eneo hilo.
Chanzo cha maji cha Shiri kilichopo wilayani Hai kinachoimamiwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi.(MUWSA.)
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuotesha miti katika chanzo hicho.


Chanzo kipya cha maji cha Mkashilingi kilichopo jirani na chanzo cha chemichei cha Shiri.

Comments

Popular posts from this blog

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

AMANI YETU TUILINDE NAIBU WAZIRI CHANDE AZUNGUMZA KATIKA IJITIMAI JIJINI DODOMA

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.