JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI


Simu:  +255-22-2112035/40
Nukushi: +255-2122617/2120486
Baruapepe: ps@moha.go.tz

       9 Barabaraya Ohio      
       S.L.P.  9223
11483 DAR ES SALAAM
                                                                                              
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dr. John Pombe Joseph Magufuli amewapandisha Cheo Maafisa sita wa Uhamiaji kuwa Makamishna wa Uhamiaji kuanzia tarehe  28 mwezi Februari mwaka 2017, Wakati huo huo amewateua kushika  nyadhifa  mbalimbali katika Jeshi la Uhamiaji.

Walioteuliwa kushika nyadhifa hizo ni Mrakibu wa Uhamiaji (SI) Edward Peter Chogero kuwa Kamishna wa Divisheni ya Fedha na Utawala, Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji (SSI) Samwel Rhobby Magweiga kuwa Kamishna wa Divisheni ya Udhibiti na Uongozi wa Mipaka, Mrakibu Mwandamizi (SSI) wa Uhamiaji Gerald John Kihinga kuwa Kamishna wa Divisheni ya Pasipoti na Uraia, Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji (SSI) Musanga Mbusuro Etimba kuwa Kamishna wa Divisheni ya Hati za Ukaazi na Pasi, Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji (SSI) Hannerole Morgan Manyanga kuwa Kamishna wa Divisheni ya Sheria.

Aidha Mh.Rais amemteua pia Naibu Kamishna wa Uhamiaji Mourice David Kitinusa kuwa Kamishna Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA).  Uteuzi huo unaanzia tarehe 28 mwezi Februari mwaka 2017.

Imetolewa na
Meja Jenerali Projest Rwegasira
Katibu Mkuu
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi  
26 Machi 2017

Comments

Popular posts from this blog

AMANI YETU TUILINDE NAIBU WAZIRI CHANDE AZUNGUMZA KATIKA IJITIMAI JIJINI DODOMA

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.