TUME YA MAWASILIANO NCHINI TANZANIA YAWAANDALIA SEMINA WAMILIKI WA BLOG


 Afisa Habari wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mabel Masasi, akizungumza kabla ya kuwakalibisha viongo wa Mamlaka ya Mawasilano kuongea na Wamiliki wa Blog nchini warsha hiyo ya siku moja ilifanyika  jijini Dar es Salaam leo . Warsha hiyo ilihusu kuelemisha wasiokuwa na ujuzi wa uandishi wa habari kwenda shule kujiendelea na mambo wanayoyaweka katika blog zao. pia  zizingatie utaifa kwanza na uzingatie maadili ya kitanzania. hiyo yote kujiepusha na kushtakiwa huku tuendako
 Mkurugenzi wa Utangazaji wa Mamlaka hiyo Habby Gunze, Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo Profesa John Nkhoma na Mwakilishi kutoka Idara ya habari Maelezo Mr Msigwa.

 Maofisa wa Tume ya Mawasiliano wakimsikiliza mkurugenzi alipokuwa akifungua warsha hiyo




Waalikwa wakimsikiliza mkurugenzi alipokuwa akifunguwa warsha hiyo



 Habby Gunze, akitoa mada yake


Mkurugenzi Profesa John Nkhoma, akifungua warsha hiyo ya siku moja, waliomzunguka ni wanablog na waandishi wa habari, unaweza kujionea baadhi ya wanablog wanatumia simu kuchukua tukio 




Na Oliver Oswald, Dar es Salaam

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imesema haina mpango wa kuwaumiza au kuwawekea vikwazo vya kuandika na kuripoti taarifa za uchaguzi waandishi wa habari, bali itaendelea kuwasisitiza kuzingatia maadili na ukomo wa uandishi.

Kauli hiyo ilitolewa jijini Dar es Salaam jana na Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Profesa John Nkoma katika mkutano na wamiliki wa mitandao ya kijamii nchini (Blogger’s) kuhusu namna ya kuripoti habari kuelekea uchaguzi mkuu ujao hapo mwakani.
Alisema dhumuni la kukutana na wamiliki hao ni kuendelea kuwakumbusha kuzingatia maadili ya uandishi kabla ya kutangaza au kuripoti taarifa zao katika mitandao.

“Unajua kipindi cha uchaguzi mambo mengi yanajitokeza na kila mwandishi hususani wana blogg huwa katika changamoto kubwa ya kuhakikisha anapata taarifa mpya ili kuwavuta wasomaji ukizingatia mawasiliano ya habari kwa njia ya mitandao imezidi kukua kila siku.

“Kutokana na hilo TCRA tumeona tunakila sababu ya kukutana na wenzetu ili kuwapa elimu ya kuandika habari zao katika kipindi hicho kwa kuzingatia ukweli halisi wa habari anayo iripoti na ukomo wa kiuandishi,”alisema Nkoma.
Wakati huohuo Nkoma aliwasisitiza wamiliki hao kuzingatia suala la ulinganifu wa habari kabla haijasambaa kwenye mitandao ili kuepusha manung’uniko kutoka kwa wahusika.

“Uhuru wa uandishi utaendelea kuzingatiwa ila tahadhari iliyopo ni kukumbuka kulinganisha taarifa zenu kabla hamjazisambaza kwabi vinginevyo mnaweza kuibua malalamiko kwa wahusika,”alisema Nkoma.

Wakizungumzia kuhusu suala la ukomo wa uandishi na ulinganifu wa habari, baadhi ya wamiliki wa blogg waliohudhuria katika mkutano huo wamesema jambo hilo ni muhimu kwa kila mwandishi kulitambua na kulifanyia kazi ili kuepuka madhara ya kushtakiwa.

Dues Mhagale ni mmiliki wa Mhagalle Blogg, alisema ipo haja kwa wamiliki wa blog wasiokuwa na taaluma ya habari kujifunza ili kutambua na kuelewa kwa umakini maadili ya uandishi, kwani kutampa mwongozo katika kutoa taarifa sahihi zisizo na upendeleo.
Alisema sambamba na hilo pia kila mmiliki wa blog anapaswa kueleza chanzo cha habari anayoitoa ili kuepuka madhara ya kujumuishwa katika malalamiko.

“Baadhi ya wanablogg wamekuwa na kawaida ya kuchukua habari kutoka blog nyingine bila kueleza taarifa hizo amezitoa kutoka kwa nani, hawajui mwisho wa siku anaweza kujikuta matatizoni bila kuwa na hatia,”alisema Mhagalle.
Mwisho.

Comments

Popular posts from this blog

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

KADA MGEJA AHUDHURIA MAZIKO YA MAMA MZAZI WA MWANDISHI MWANDAMIZI WA HABARI KAHAMA