WAFADHILI WARIDHISHWA NA MRADI NA MAENDELEO YA MRADI WA MAJARIBIO WA KUTUMIA TEKNOLOJIA KWA WATOTO WALIO NA FUSA NDOGO





 Katibui Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi kulia akiwaonyesha mmoja ya sehemu zinazotunzwa tablets ambazo zinatumiwa kufundishia wanafunzi akiwa na wafadhili wa mradi huo


Katibui Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi akiwaongoza wafadhili wa mradi huo kutembelea maeneo mbalimbali unapotekelezwa wilayani Pangani
  Katibui Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi kushoto akiwa na wafadhili wa mradi huo wakiangalia namna wanafunzi wanavyojifunza kutumia teknolojia ya Tablets
Katibui Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi kulia akiteta jambo na wafadhili wa mradi huo
Wadau wa mradi  wa  miaka mitano wenye lengo la kutumia  teknolojia ya kisasa kuwawezesha watoto waliona fursa ndogo ya kupata elimu katika umri wa miaka tisa hadi kumi na mmoja, kujifunza wenyewe stadi za msingi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) wameeleza kuridhishwa kwao na maendeleo ya majaribio hayo.

Wadau ambao walikuwa na ziara ya siku moja kutembelea vijiji mbalimbali vya nradi huo katika wilaya za Muheza na Pangani wadau aho ambao walikuwa pamoja na Mwakilishi wa Mpango wa Chakula Duniani (WFP) nchini Tanzania, Michael Dunford, Mkurugenzi wa Ofisi ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) ya Kanda ya Afrika Mashariki, Anne Ndong-Jatta wakiambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga, Mhandisi Zena Said.
Wakitoa maoni wakati wakipewa maelezo walisema ni wazi mradi umeanza kuonyesha uwezo wa teknolojia kuamsha ari ya kujifunza na kusoma.
Taarufa za awali za mradi na ushuhuda tuliouona inaonyesha kuwa mpango huu wa kiteknolojia una uwezo wa kuwasha mwamko wa elimu miongoni mwa watoto na wazazi na unapaswa kutiliwa maanani, alieleza  Mhandisi Said wakat wa ziara hiyo.
Pia Mhandisi Said alisema kuwa ni wazi pia kuwa kuwatambulisha wananchi katika teknolojia ya kisasa wakiwa na umtri mdogo kunawahakikishia  watoto hao kuwa hawawezi kunyanyaswa hapo baadaye wakiwa wakubwa.
Naye Ndong-Jatta alisema kuwa mradi unaonyesha haja ya kuangalia uwezekano wa kupunguza tatizo la kutojua kusoma na kuandika kwa wazazi kama njia mojawapo ya kuamsha mwamko wa elimu miongoni mwao na kuwawezesha kuwasukuma watoto kwenda shule.
Zaidi ya watoto 2,500 kutoka katika vituo 142 vilvyopo katika wilaya za Handeni, Korogwe, Lushoto, Mkinga, Muheza na Pangani walipewa tablet mpya aina ya Google Pixel C, zilizotolewa kwa hisani ya Google. Tableti hizo zimewekewa mifumo ya elimu kutoka kwa washindi watano wa mwisho wa Global Learning XPRIZE. Washindi hawa walichaguliwa kutoka katika timu 198 napaneli ya majaji 11 wa kujitegemea na walio wataalamu na kutangazwa mwezi September, 2017 wakati wa wiki ya BarazaKuu la Umoja wa Mataifa
Mradi huo wa miaka mitano uliotokana na mashindano duniani yenye thamani ya Dola za Mareka ni milioni 15. Mradihuu wa dunia unatoa changamoto kwa timu za wa bunifu kubuni na kuandaa zana za kusaidia kuondoa ujinga duniani na kuwasaidia watoto ambao hawajapata fursa ya kwenda shule kujifunza wakiwa nyumbani (Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha)

HALMASHAURI YA MJI GEITA YAPITISHA BILIONI 44.9 MWAKA WA FEDHA 2018/19

Mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Geita,Mhandisi Modest Aporinaly Akizungumza wakati wa kikao cha kupitisha Bajeti ya fedha ya mwaka 2018/19. 
Baadhi ya watumishi na wakuu wa idara wakiwa kwenye Kikao cha kupitisha Bajeti ya fedha ya mwaka 2018/19. 
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Geita Mheshimiwa Leonard Kiganga Bugomola,akizungumza wakati wa kikao cha kupitisha bajeti ya mwaka wa fedha 2018/19. 
Meza kuu ikiwa na viongozi mbali mbali wa Serikali na chama cha mapinduzi.


Na,Consolata Evarist,Geita
Baraza la madiwani wa halmashauri ya mji wa Geita,Wilayani Halmashauri ya Mji Geita limepitisha makadirio ya bajeti ya matumizi ya ya mwaka wa fedha 2018/2019 kiasi cha shilingi Bilioni 44,983,764,197.00 katika shughuli mbalimbali za Halmashauri. Kati ya Fedha hizo Jumla ya Tsh 15,585,248,344.00 ni kwa ajili ya shughuli za Maendeleo ikiwa ni Mapato ya Ndani, Ruzuku ya Serikali na Wahisani mbalimbali. Tshs. 4,765,976,688.00 kwa ajili ya matumizi ya kawaida ikiwa ni Ruzuku kutoka Serikali kuu na Mapato ya ndani na Tshs. 24,632, 539,165.00 kwa ajili ya mishahara.
Aidha Halmashauri imekisia kukusanya Jumla ya Tsh 5,114,157,735.00 toka vyanzo vya ndani ambayo fedha hii imejumuishwa katika jumla ya Bajeti ya mwaka 2018/2019. Jumla ya Tsh. 3,030,016,641.00 sawa na 60% zimetengwa kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo.
Akiongeza katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Geita kwenye kikoa cha kupitisha bajeti ya Mwaka wa fedha 2018/2019,Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya mji wa Geita,Mhandisi Modest Aporinali alisema Bajeti hyo imezingatia vipaumbele vilivyoainishwa kwenye Mwongozo wa kuandaa Bajeti uliotolewa na Wizara ya Fedha Mwezi, Novemba 2016, Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs 2030); Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015-2020, Mpango wa Pili wa miaka Mitano (FDYPII) 2016/17-2020/21 na Lengo likiwa ni kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2030.
“Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019,kwenye halmashauri hiyo kuwa imejielekeza katika kufikia vipaumbele vyenye shabaha na malengo yafuatayo Kuendelea kuboresha na kuimarisha mfumo wa makusanyo ya mapato ya ndani ili kuongeza mapato ya Halmashauri. Kuboresha Sekta za huduma za jamii, hususan, Elimu, Afya, Maji, Barabara, Mifugo, Uvuvi, Kilimo, Misitu, Maendeleo ya Jamii, Ushirika.Kusaidi Sera ya Taifa kufikia Uchumi wa kati wa uendelezaji wa viwanda.Kuimarisha Utawala bora”Alisema Modest
Aidha ameongeza kuwa Halmashauri inategemea kukusanya mapato yake kutoka kwenye vyanzo mbalimbali kama kodi ya huduma( service levy) kutoka kampuni ya Mgodi wa Dhahabu Geita na Kampuni nyingine zinazofanya kazi na Mgodi huo, kodi ya nyumba za kulala wageni, Leseni za biashara,faini mbalimbali, upigaji chapa mifugo na ushuru wa mifugo, ushuru wa mazao mbalimbali na matunda.
“Katika Bajeti ya mwaka 2018/2019. Jumla ya Shilingi 15,585,248,344 zimetengwa kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo, Kiasi cha shilingi 24,632,539,165 kwa ajili ya mishahara ya watumishi na Shilingi 4,765,976,688 kwa ajili ya matumizi mengineyo”. Aliongeza Mhandisi Aporinaly
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Geita Mheshimiwa Leonard Kiganga Bugomola alisema kwa mwaka wa fedha uliopita Halmashauri ilipanga kukusanya zaidi ya Shilingi Bilioni 5, ambapo hadi kufikia mwezi Disemba 2017 Halmashauri imeweza kukusanya kiasi cha Shilingi 2,868,353,850.15 sawa na asilimia 52.
Mh. Bugomola ameongeza kuwa kutokana na mafanikio ya ukusanyaji uliofikia nusu ya makadirio ana imani kuwa mpaka kukamilisha mwaka wa fedha 2017/2018 mwezi Juni mwaka huu, Halmashauri itakuwa imefikisha lengo la makusanyo. Aidha makusanyo hayo yanatoa mwanga wa mafanikio katika bajeti iliyopitishwa kwa mwaka wa fedha 2018/2019.
Kwa upande wake Mkuu wa wilaya hiyo,Mwl Herman Kapufi amewasisitiza wajumbe kuwa na ukusanyaji mzuri wa mapato hili kuweza kutekeleza bajeti kwa uzuri zaidi.
Katika Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019, Halmashauri ya Mji Geita imejielekeza katika kufikia vipaumbele vyenye shabaha na malengo ambayo ni Kuendelea kuboresha na kuimarisha mfumo wa makusanyo ya mapato ya ndani ili kuongeza mapato ya Halmashauri, Kuboresha Sekta za huduma za jamii, hususan, Elimu, Afya, Maji, Barabara, Mifugo, Uvuvi, Kilimo, Misitu, Maendeleo ya Jamii, Ushirika,
Kusaidia Sera ya Taifa kufikia Uchumi wa kati wa uendelezaji wa viwanda na Kuimarisha Utawala bora.

TGNP Mtandao wakutanisha madiwani 20 kujadili kushirikiana

Zaidi ya madiwani 20, kutoka mikoa mitano na wilaya Nane wamekutana jijini Dar Es Salaam, kubadilishana uzoefu na kujifunza jinsi ya kushirikiana na wananchi katika kuleta maendeleo katika kata zao.

Madiwani hao ni kutoka Halmashauri za wilaya za Kishapu (Shinyanga), Tarime (Mara), Mbeya (Mbeya), Morogoro Vijijini (Morogoro) na manispaa za Ilala, Kinondoni na Ubungo (Dar es salaam).

Madiwani hao ambao walikutana katika ofisi za TGNP Mtandao, zilizopo Mabibo Dar Es Salaam, pia walipata nafasi ya kutembelea Kipunguni na kujionea mradi unaotekelezwa katika eneo hilo.

Pamoja na kujifunza masuala mbalimbali, Madiwani hao walipata fursa ya kushirikisha masuala ya kijinsia ambayo bajeti za Halmashauri zao zimezingatia na jinsi walivyofanikiwa kutenga rasilimali za kuhakikisha bajeti zao zinakidhi mahitaji ya kijinsia.

Wakiwa kata ya Kipunguni iliyopo manispaa ya Ilala madiwani hao walikutana na Diwani wa Kata hiyo na kujifunza jinsi ambavyo wananchi waliopo katika Kituo cha Taarifa na Maarifa walivyofanikiwa kuleta maendeleo kwa kushirikiana na viongozi ikiwepo kupambana na ukatili wa kijinsia hasa ukeketaji.Eneo hilo maarufu kwa wakazi wa kutoka mikoa ya kaskazini ambako yapo makabila yanayofanya ukeketaji nalo limekumbwa na tatizo hilo.

Aidha katika ziara hiyo, waheshimiwa madiwani walipata nafasi ya kujifunza, faida za mabunge ya jamii, na kujifunza miradi ya maendeleo ya kuwezesha wananchi kiuchumi ambayo inatekelezwa na TGNP Mtandao kwa kushirikiana na wananchi wa Kipunguni.

Katika mabadilishano ya uelewa mmoja wa wajumbe ambaye ni Diwani wa Ijombe wilayani Mbeya, Stimar Hepa John alisema kwamba wakati umefika kwa wananchi wengi kutambua shughuli za TGNP Mtandao.

Alisema awali alikuwa akidhani kwamba asasi hiyo ina mlengo wa kisiasa kiasi cha kushindwa kutoa ushirikiano wa kutosha kwao lakini baada ya elimu hii amebadili uelekeo na kuitaka taasisi hiyo kupeleka elimu Tanzania nzima.

Alisema, "Anaona kwamba TGNP ina jukumu kubwa nchini Tanzania na hivyo inastahili kuwa kila mahali kuwasaidia watanzania kujiimarisha katika nyanja zote."Diwani huyo wa Ijombe ambaye pia ni Mkuu wa shule ya sekondari Igawii alisema pamoja na kubadili mwelekeo aliwataka wabunge kuona kwamba wanapoandaa miradi hawaandai mbunge mpya bali kusaidia wananchi kujiinua kiuchumi.

Katika mkutano huo walitoa maazimio kadhaa ya kufanyiwa kazi katika halmashauri.Miongoni mwa maazimio hayo ni namna ya kusimamia Mfuko wa Maendeleo wa wanawake kuhusu ile asilimia 5 na kutekeleza dhana ya viwanda.

Kwa mujibu wa Ofisa Programu uchechemuzi wa TGNP Mtandao, Deo Temba mambo mengine waliyokubaliana ni kushawishi na kufuatilia ongezeko kila zahanati na vifaa vya kujifungulia na kuhimiza uwekaji wa mikakati ya kupambana na ukatili wa jinsia na kuunda kamati za ulinzi za mtoto.

Pia imeelezwa haja ya TGNP Mtandao kuendelea kutoa elimu kwa kusaidiwa na mabaraza ya halmashauri kuhusu rasilimali fedha na kufuatilia uwekezaji katika ujenzi wa hosteli kupunguza umbali wa watoto wa kike kutembea kufuata shule.Mambo mengine ni kuona kwamba uandaazi wa bajeti unaanzia ngazi ya kijiji au mtaa badala ya kata na kukosekana kwa sauti za wananchi katika bajeti.

TGNP Mtandao ni asasi ya kiraia inayo fanya kazi na wanajamii kwa kipindi cha miaka 25 sasa, kwa kipindi chote hicho kimeshirikiana na taasisi za serikali, Wizara, Halmashauri na Kamati za Bunge za kisekta kwa ajili ya majadiliano, mashauriano na mafunzo ya namna ya kuboresha huduma za jamii kwa kuzingatia usawa wa kijinsia.

 Ofisa Programu uchechemuzi wa TGNP Mtandao, Deo Temba akifafanua jambo wakati akiendesha mjadala kwa Madiwani 20 kutoka mikoa 5 na wilaya 8 walioshiriki mkutano wa kubadilishana uzoefu na kujifunza jinsi ya kushirikiana na wananchi katika kuleta maendeleo katika kata zao uliondaliwa na TGNP Mtandao na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi hizo jijini Dar es Salaam.  Diwani wa Kata ya Songwa wilayani Kishapu, Shinyanga, Ngoromole Abdul akibadilishana uzoefu na madiwani wenzake wakati wa mkutano wa kubadilishana uzoefu na kujifunza jinsi ya kushirikiana na wananchi katika kuleta maendeleo katika kata zao uliondaliwa na TGNP Mtandao na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi hizo jijini Dar es Salaam. Diwani wa Ijombe wilayani Mbeya ambaye pia ni Mkuu wa shule ya sekondari Igawii, Stimar Hepa John akichangia kwenye mjadala wakati wa mkutano wa kubadilishana uzoefu na kujifunza jinsi ya kushirikiana na wananchi katika kuleta maendeleo katika kata zao uliondaliwa na TGNP Mtandao na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi hizo jijini Dar es Salaam.Diwani wa Kata ya Mshewe ya Wilaya ya Mbeya vijijini, mkoani Mbeya, Esther Mbega akishiriki kwenye mjadala wakati wa mkutano wa kubadilishana uzoefu na kujifunza jinsi ya kushirikiana na wananchi katika kuleta maendeleo katika kata zao uliondaliwa na TGNP Mtandao na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi hizo jijini Dar es Salaam. Diwani wa Kata ya Ukenyenge ya wilaya Kishapu mkoani Shinyanga, Anderson Mandia akisisitiza jambo wakati wa mkutano wa kubadilishana uzoefu na kujifunza jinsi ya kushirikiana na wananchi katika kuleta maendeleo katika kata zao uliondaliwa na TGNP Mtandao na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi hizo jijini Dar es Salaam. Pichani juu na chini ni washiriki wakiendelea kujadiliana wakati wa kipindi cha maswali na majibu katika mkutano wa kubadilishana uzoefu na kujifunza jinsi ya kushirikiana na wananchi katika kuleta maendeleo katika kata zao uliondaliwa na TGNP Mtandao na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi hizo jijini Dar es Salaam. Sehemu ya Madiwani 20 kutoka mikoa 5 na wilaya 8 walioshiriki mkutano wa kubadilishana uzoefu na kujifunza jinsi ya kushirikiana na wananchi katika kuleta maendeleo katika kata zao uliondaliwa na TGNP Mtandao na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi hizo jijini Dar es Salaam.

SERIKALI IMETENGA SHILINGI BILIONI 11.4 KUBORESHA WAKALA WA NDEGE ZAKE

Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye akiongea na wajumbe wa Menejimenti ya Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA) (hawapo pichani) wakati wa ziara yake kwenye taasisi hiyo jijini Dar es Salaam. Anayemsikiliza ni Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa taasisi hiyo Bwana Tito Kasambala
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Richard Mayongela (kushoto) akimkaribisha Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (kulia) kwenye uwanja wa ndege wa Dar es Salaam wakati wa ziara yake ya kutembelea na kukagua Wakala wa Ndege za Serikali
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye akipanda kukagua mojawapo ya ndege za Wakala wa Ndege za Serikali inayosafirisha viongozi wa ngazi ya juu wa Serikali wakati wa ziara yake kwa Wakala hiyo kwenye uwanja wa ndege wa Dar es Salaam
Mkaguzi Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali Mhandisi Bernard Mayila akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye wakati akifanya ukaguzi ndani ya ndege mojawapo inayosafirisha viongozi wa ngazi za juu wa Serikali wakati wa ziara yake alipotembelea Wakala hiyo kwenye uwanja wa ndege wa Dar es Salaam
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye akiteremka baada ya kukagua mojawapo ya ndege za Wakala wa Ndege za Serikali wakati wa ziara yake kwenye Wakala hiyo kwenye uwanja wa ndege wa Dar es Salaam

……………….

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imejipanga kuboresha Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA) ambayo inasimamia na kuendesha ndege ambazo zinasafirisha viongozi wa kitaifa wa Serikali

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye wakati wa ziara yake ya kikazi alipotembelea na kukagua utekelezaji wa majukumu ya Wakala wa Ndege za Serikali ambayo inasimamia na kuendesha ndege ambazo zinasafirisha viongozi wa kitaifa wa Serikali ambapo alizungumza na Menejimenti na wafanyakazi na kuwaeleza kuwa Serikali imejipanga kuboresha Wakala hiyo

Mhandisi Nditiye alisema kuwa azma ya Serikali ya Awamo ya Tano inayosimamiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ni kuhakikisha kuwa Taasisi za Serikali zinafanya kazi zake kwa weledi na uadilifu ili kufanikisha malengo ya Serikali ya kuwatumikia wananchi. “Serikali inatambua umuhimu wa Wakala hii na ina imani kubwa nanyi katika kuhakikisha kuwa mnafanya kazi zenu za kusafirisha viongozi kwa usalama na kwa uhakika ili waweze kutimiza majukumu yao ya kuwatumikia wananchi na tayari ina nia ya kuboresha taasisi hii”, amesema Mhandisi Nditiye.

Naye Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa TGFA Bwana Tito Kasambala amemueleza Mhandisi Nditiye kuwa taasisi yake ina ndege nne ambazo zinatumika kusafirisha viongozi wa kitaifa wa Serikali katika kutimiza majukumu yao ya kuwatumikia watanzania na tayari Serikali imetenga shilingi bilioni 11.4 kwenye bajeti ya mwaka wa fedha wa 2017/18 kwa ajili ya shughuli mbali mbali za Wakala ikiwemo matengenezo ya ndege, mafunzo kwa wanahewa na ukarabati wa karakana.
Mhandisi Nditiye amewaeleza wajumbe wa Menejimenti na wafanyakazi wa Wakala hiyo kuwa Serikali inatambua na kuthamini mchango wao na umuhimu wa wahandisi wa ndege na marubani wa kupata nafasi ya kuendesha ndege na kozi za mafunzo mbali mbali kuendana na taaluma zao ambapo tayari makubaliano yamefanyika baina ya Wizara na Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) ya kuwapatia nafasi marubani wa ndege za Wakala wa Ndege za Serikali nafasi ya kurusha ndege mara kwa mara ili kuendana na matakwa ya taaluma zao.

Ameongeza kuwa Serikali inashughulikia suala la miundo ya watumishi wa umma ambapo Wakala wa Ndege za Serikali ni mojawapo ya taasisi ambayo muundo wake unafanyiwa kazi ili kuweza kuzingatia taaluma, kada za watumishi na maslahi yao. “Natumaini wote mnatambua na kuelewa kuwa kipindi cha hapo nyuma kidogo utumishi wa umma uliingiwa na baadhi ya watu wachache ambao walikuwa wanafanya ujanja ujanja na kuharibu utumishi wa umma ambapo Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wetu, imelifanyia kazi jambo hili na ameunda bodi maalumu ambayo inafanyia kazi suala la muundo, kada na maslahi ya watumishi wa umma,” amesema Mhandisi Nditiye.

Aidha, wafanyakazi wa Wakala wa Ndege za Serikali wamemuomba Mhandisi Nditiye kuwasilisha ombi lao kwa Serikali la kuwaongezea mishahara yao kuendana na hali ya soko la ajira ya marubani ilivyo nchini kwa sasa.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,

Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

DC MATIRO AWARUDISHA KAZINI WATUMISHI WA AFYA WALIOTUMBULIWA ZIARA YA NAIBU WAZIRI MAVUNDE

Watumishi wa afya 22 katika hospitali ya Kolandoto manispaa ya Shinyanga wamerudishwa kazini na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro mara baada ya kutumbuliwa na uongozi wa hospitali hiyo kutokana na kutoa malalamiko yao mbele  Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Vijana Athony Mavunde alipofanya ziara yake Februari 27,2018.


Watumishi hao walifukuzwa kazi siku moja baada ya ziara ya Naibu Waziri huyo kwenye hospitali hiyo ambayo aliifanya  Februari 27 mwaka huu mara baada ya kutoa malalamiko yao juu ya kunyanyaswa na hospitali hiyo ambapo kesho yake wale waliojifanya wazungumzaji 'kiherehere' wakatimuliwa kazi na kutolipwa stahiki zao zote.


Akiongea Machi 1, 2018 na uongozi wa hospitalini hapo mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro alisema mara baada ya kupewa taarifa hizo juu ya watumishi hao kuwa wametimuliwa kazi baada ya kusema ukweli kwenye ziara ya Naibu Waziri huyo, jambo hilo limemkera na kuamua kufika kwenye hospitali hiyo kuwarudisha kazini.

“Kuanzia sasa watumishi wote mliowafukuza kazi wanarudi kazini na ninatoa siku 14 wawe wameshalipwa haki zao zote wanazodai, ikiwamo malimbikizo ya mishahara, makato ya NSSF,TUGHE, pamoja na kulipwa mishahara kiwango cha serikali, na msipofanya hivyo ndani ya siku hizo tutawachukulia hatua,”alisema.
"Kwanza hospitali hii mmeidharau serikali kwa sababu haiwezekani kiongozi mkubwa kama yule Naibu waziri anafanya ziara ya kusikiliza na kutatua kero za watumishi, halafu ninyi kesho yake mnawafukuza kazi, huo ni utovu wa nidhamu”,alisema Matiro.
Naye mmoja wa watumishi hao walifukuzwa kazi Elizabeth Zabron alisema baada ya kutoa malalamiko yao juu ya kunyanyaswa kwenye mishahara na madai mbalimbali, muda mfupi tu baada ya kuondoka Naibu Waziri huyo wakaona majina ya watu 22 yakiwa yamebandikwa kwenye ubao wa matangazo wakiitwa kesho kuonana na uongozi wa hospitali hiyo.
Alisema baada ya kwenda kuonana na uongozi huo wakajua tayari kilio chao kimesikika cha kulipwa mishahara na madai yao, ambapo wakashangaa wanaambiwa kuwa wamefukuzwa kazi na wanatakiwa kusaini barua hizo bila ya kuzisoma, ndipo wakagoma na kuamua kwenda kushitaki kwa mkuu huyo wa wilaya ili wapate haki zao.
Barua hizo kwa ndani zilikuwa zimeandikwa kuwa "unafukuzwa kazi na hutakiwa kulipwa haki yako yoyote na kutakiwa kuondoka eneo la kazi mara moja".
Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo Dkt .Maganga Dohoi alikiri kuwafukuza kazi watumishi hao na kudai kuwa bodi ya hospitali hiyo ilikaa na kuagiza watumishi wote wasio na sifa ya kuwa na vyeti vya kidato cha nne lakini wana taaluma ya uuguzi wafukuzwe kazi, ndipo naye akafuata maagizo hayo.
Hata hivyo mmoja wa wajumbe wa Bodi ya hospitali hiyo Magezi Magedi ambaye pia ni ofisa utumishi wa halmashauri ya manispaa ya Shinyanga, alikana kukifahamu kikao cha kufukuza watumishi hao , na kudai kama suala la kufukuza kazi kuna taratibu zake zinatakiwa kufuatwa na siyo kuwafukuza hovyo hovyo. 
Alisema  hospitali hiyo isitumie kivuli cha serikali kufukuza watumishi hao ikiwa suala la vyeti vya darasa la Saba lilikuwa la watumishi tu wa serikali.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza na watumishi wa afya katika hospitali ya Kolandoto waliotimuliwa kazi.-Picha na Marco Maduhu - Shinyanga News blog & Malunde1 blog
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akionyesha masikitiko namna walivyotendewa ndivyo sivyo watumishi hao wa afya katika hospitali ya Kolandoto kwa kutimuliwa kazi kisa wametoa malalamiko yao mbele ya Naibu waziri wa Kazi,Ajira na Vijana Anthony Mavunde.
Mmoja wa watumishi waliofukuzwa kazi Elizabeth Zabroni akielezea kisa cha kufukuzwa kazi
Emmanuel Makungu naye alidai wamekuwa wakilipwa mishahara lakini hawapewi Salary Slip wala kusaini popote na kutokujua umeingia mshahara wa mwezi gani na pia michango ya NSSF wamekuwa wakiambiwa imeingizwa lakini wakifuatilia hakuna pesa yoyote iliyowekwa pamoja na fedha za likizo kutopewa, na kubainisha kuwa walipotoa malalamiko yao mbele ya Naibu Waziri wa Kazi,Ajira na Vijana Antony Mavunde iliwapate haki zao wakaonekana kuwa kikwazo na kutimuliwa kazi.
Sara Mkem akionyesha kusikitishwa na uongozi wa hospitali hiyo kwa kuwafukuza kazi kisa wametoa matatizo yao mbele ya Naibu Waziri huyo ili yapate ufumbuzi, na kuonekana kuwa kero na kutimuliwa kazi, bila hata ya kujali utu wao pamoja na kulazimishwa kusaini barua bila ya kuzisoma  na kudai uongozi huo una roho ya kinyama kwani huenda ina dhamira ya kutaka arudi uraiani akauawe na watu wabaya kwa kumkata viungo vyake.
Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo Dkt Maganga Dohoi akijitetea kwa mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro
Baadhi ya watumishi waliofukuzwa kazi na uongozi wa hospitali ya Kolandoto wakiwa kwenye kikao na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro na uongozi wa hospitali hiyo kutatua suala lao la kufukuzwa kazi mara baada ya kutoa kilio chao kwa Naibu Waziri wa Kazi,Ajira na Vijana Antony Mavunde juu ya manyanyaso wanaoyapata .
Watumishi wa afya waliofukuzwa kazi katika hospitali ya Kolandoto wakiwa kwenye kikao cha kutatuliwa matatizo yao na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro mara baada ya kumpelekea matatizo yaliyowakumba ya kutimuliwa kazi kinyemela bila ya kufuata sheria za kazi.
Kikao kikiendelea.
Watumishi wa afya katika hospitali ya kolandoto waliofukuzwa kazi kenyemela wakiwa wameshika bango la kutaka haki yao
 Ofisa utumishi wa halmashauri ya manispaa ya Shinyanga,Magezi Magedi ambaye pia ni mjumbe wa bodi ya hospitali hiyo ya Kolandoto akikana kukifahamu kikao cha kufukuza kazi watumishi hao na wala tangu achaguliwe kuwa mjumbe wa bodi hiyo hajawahi kuitwa hata kikao kimoja  na kudai kama suala la kufukuza kazi watumishi hao kuna taratibu zake zinatakiwa kufuatwa, na siyo kuwafukuza hovyo hovyo na kuwalazimisha kusaini barua bila ya kuzisoma. 
 Ofisa kazi mkoa wa Shinyanga Revocatus Mabula alisema taratibu za kuwafukuza kazi watumishi hao zilikiukwa ambapo hawakupewa notes na walistahili kupewa haki zao zote ndani ya siku 14,kulipwa kiinua mgongo,malimbikizo ya likizo zao zote pamoja na kusafirishwa mahali walipotoka makwao na siyo kuambiwa tu wamefukuzwa kazi na hawatolipwa pesa yoyote.
Katibu wa Chama Cha Wafanyakazi TUGHE, Tabu Mambo alisema hawajahi kuona mchango wowote wa watumishi hao waliofukuzwa kazi licha ya kuambiwa kuwa wanalipiwa na kubainisha kuwa walipokuwa wakifika kuzungumza na watumishi hao walikuwa wakikosa ushirikiano kutoka kwa viongozi wao, na wale watumishi ambao walioonekana kuwa wanajua kuongea ndiyo kidogo walikuwa wakitolewa michango hiyo.
Picha na Marco Maduhu - Shinyanga News blog & Malunde1 blog

Ziara ya Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mkoani Njombe.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage akimsikiliza mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka alipomtembelea ofisini kwake kupata taarifa ya Viwanda na uwekezaji katika mkoa huo, leo tarehe 1 Machi, 2018.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage akizungumza jambo na Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bibi. Ruth Blasio Msafiri walipofika ofisi za SIDO Mkoa wa Njombe kuona utendaji wake.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji,. Charles Mwijage akikagua eneo litakalojengwa majengo makubwa kwa ajili ya wajasiriamali na wafanyabiashara wadogo, Mkoani Njombe leo tarehe 1 Machi, 2018.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage, akimsikiliza meneja wa Wakala wa Vipimo Mkoa wa Njombe kuhusu utaratibu wanaotumia katika kupima mizigo ya wakulima na wafanyabiashara mkoani Njombe.
Muonekano wa Kiwanda cha kuchakata Chai cha Unilever kilichopo mkoani Njombe ambacho kipo katika hatua za mwisho kukamilika kwa ujenzi wake.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage akikagua uenzi wa kiwanda cha Chai cha Unilever, Mkoani Njombe leo tarehe 1 Machi, 2018.
Wadau na wafanyabiashara wa Mkoa wa Njombe waliokusanyika kumsikiliza Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage (Hayupo pichani) na baadae kuuliza maswali kutokana na changamoto wanazokutana nazo na kupatiwa majibu.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage akizungumza wakati wa mkutano na wafanyabiashara kujadili changamoto zianazowakabili wafanyabiashara katika mkoa wa Njombe Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka na kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bibi. Ruth Blasio Msafiri.

TACAIDS KUANZA KAMPENI YA KUHAMASISHA WANAUME KUPIMA AFYA ZAO-MABOKO

Mratibu wa mtandao wa viongozi wa dini wanaoishi na virusi vya ukimwi ,(TANERELA),mchungaji Amin Sandewa pichani .(picha na Mwamvua Mwinyi)
Mkurugenzi mtendaji wa Tume ya Taifa ya kudhibiti ukimwi (TACAIDS ) ,Leonard Maboko akizungumza jambo ,mjini Kibaha ,Mkoani Pwani ,katika mkutano ulioandaliwa na tume hiyo ,kupitia mipango ya utekelezaji wa afua za ukimwi kwa asasi mwamvuli ya mwaka 2018/2019 .(picha na Mwamvua Mwinyi)

Na Mwamvua Mwinyi,Pwani

TUME ya Taifa ya kudhibiti ukimwi (TACAIDS), inatarajia kuanza kampeni za kitaifa kuhamasisha wanaume kupima afya zao ,ili kujenga tabia ya kujitokeza kujua afya zao kwani ni asilimia 45 pekee ya kundi hilo walioaminika kuwa na VVU ndio waliopima kujua hali zao.
Aidha imeeleza ,kati ya watu kumi wenye maambukizi mapya kwa mwaka ,vijana wanne sawa na asilimia 40 ugundulika kupata maambukizi hayo.

Pamoja na hayo ,kati ya vijana kumi waliopata maambukizi mapya kila mwaka nane huwa vijana wa kike na wawili ni vijana wa kiume.Mkurugenzi mtendaji wa TACAIDS ,Leonard Maboko aliyaeleza hayo mjini Kibaha ,Mkoani Pwani ,katika mkutano ulioandaliwa na tume hiyo ,kupitia mipango ya utekelezaji wa afua za ukimwi kwa asasi mwamvuli ya mwaka 2018/2019 .

Alisema ,kampeni hiyo itakuwa ya miezi sita na itakuwa endelevu hadi hapo watakapohakikisha wanatokomeza ama kupunguza gonjwa hilo .Maboko alisema ,wale watakaobainika kuwa na maambukizi mapya watatakiwa kuanza tiba ya dawa za kufubaza virusi vya ukimwi (ARVs) mapema ili kuondoa vifo vinavyotokana na virusi hivyo .

Alielezea ,wanaandaa kampeni hizo kutokana na takwimu za utafiti wa viashiria vya ukimwi ya mwaka 2016/2017 inayoonyesha idadi ya watu wanaopima na wanaogundulika kuambukizwa wanaoanza kutumia dawa ni wanawake kuliko wanaume.

“Asilimia 45 ya wanaume ndio wanaoaminika kuwa wamepima na kujua hali zao ,hali ambayo inaonyesha ni kiwango cha chini “.“Simaanishi wenye ukimwi wote wameshapima kujitambua ,lakini inahitajika hamasa ili tufikie malengo”alisema Maboko.

Hata hivyo Maboko alisema ,maambukizi mapya ya ukimwi yanaongezeka zaidi kwa kundi la vijana hususan wa kike .“Hii inaonyesha huko kipindi cha nyuma hakukuwa na hali hiyo hivyo haina budi kundi hilo likatiliwa mkazo ,ili kupunguza ongezeko hilo ” 

“Hali ya maambukizi ya ukimwi Tanzania kwasasa ni asilimia 4.7 kutoka asilimia 5.1 ,hali inapungua lakini inatakiwa tuendelee kupambana na maambukizi mapya ,na Tanzania bila ukimwi inawezekana” alisema Maboko.Aliwaambia wajumbe wa mkutano huo ,kuwa asasi mwamvuli zinarahisisha kazi ya uratibu kwa TACAIDS lakini changamoto waliyonayo ni kutopata ripoti za asasi hizo .

Nae mratibu wa mtandao wa viongozi wa dini wanaoishi na virusi vya ukimwi ,(TANERELA),mchungaji Amin Sandewa alisema wanawajengea uwezo wa kielimu viongozi wa dini wanaoishi na virusi hivyo ili kupambana na ukimwi na kuwa vielelezo kwa wengine.

Sandewa alisema, ugonjwa huo hauchagui ,muumini,viongozi wa dini wala mwalimu hivyo aliiomba jamii kuachana na unyanyapaa.Meneja ufuatiliaji na takwimu ,kutoka baraza la Taifa la watu wanaoishi na virusi vya ukimwi (NACOPHA) ,Rachel Jacob alifafanua wanaratibu shughuli za masuala ya ukimwi kwa kulenga mtu mmoja mmoja,kundi na mtandao .

Kwa mujibu wake ,katika kufanikisha shughuli hizo wameshafikia halmashauri 154 nchini kwa kushirikiana na viongozi walioteuliwa ambao wana maambukizi kwa ajili ya kusaidia kuwafikia watu na vikundi hivyo .

Rachel alibainisha ,kwasasa wana wajumbe 616,984 miongoni mwao asilimia 44 ni wanaume waliojitokeza kuweka wazi afya zao .Alifafanua zoezi hilo nao wanaendelea nalo ,kuhakikisha kufikia halmashauri zote hasa kundi la wanaume ambalo bado halina mwamko huo.

Katika mkutano huo ,asasi mwamvuli zilizoshiriki ni pamoja na NACOPHA,TAIFO,BAKWATA,FAJISAM-PENTECOSTE,TANERELA,TEC,BAHAI,National Steering Committe, na TIENAI.

SERIKALI YAAGIZA OPERESHENI YA KUONDOA WAVAMIZI WA KIGENI KATIKA KISIWA CHA IZINGA MKOANI KAGERA


.........................................................................................
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla ametoa siku 7 kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA  kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Karagwe kufanya Operesheni ya kuwaondoa wavamizi wa nchi jirani wanaodaiwa kulima na kufiga ndani kisiwa cha Izinga kilichopo ndani ya Pori la Akiba la Kimisi mkoani Kagera.
Ametoa agizo hilo jana wakati wa ziara yake wilayani Karagwe mkoa wa Kagera muda mfupi baada ya kupokea taarifa na malalamiko ya kukamatwa kwa mifugo ya Watanzania ndani ya kisiwa cha Mubali huku kukiwepo mazao yanayodaiwa kulimwa na wananchi wa Rwanda katika kisiwa kingine cha Izinga.

“Ndani ya siku saba hicho kisiwa cha Zinga msafishe kila kitu, Mkuu wa Wilaya msaidie mtengeneze kikosi kiende kule kitoe takataka zote zilizoko kule, inakua ngumu kuadministrate (kutawala) wengine wa kwetu tunawatoa alafu wa nchi nyingine wamekaa, unatawalaje?”. Aliuliza kwa mshangao Dk. Kigwangalla.

Alisema watanzania wakienda upande wa Rwanda kuvua samaki ziwa Ihema wanauawa mara moja bila mjadala, wakati kwa upande wa Tanzani raia wa nchi hiyo wapo wengi na wengine wamepewa Uraia wa Kuasili (Citizenship by Naturalisation, CN) na huwa hawafanyiwi vitendo vya unyanyasaji wala mauaji  jambo ambalo alisema  ipo haja kama nchi kuchukua hatua ili kukomesha vitendo hivyo.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania, David Kenyata alisema atatekeleza agizo hilo la Waziri Kigwangalla kwa haraka ndani ya muda uliotolewa ili kumaliza mgogoro huo.

Katika hatua nyingine Waziri Kigwangalla alikataa ombi la Mbunge wa Jimbo la Karagwe, Innocent Bashugwa la kuiomba Serikali iwamegee wananchi wa vijiji jirani sehemu ya eneo katika Pori la Akiba Kimisi kwa ajili ya shughuli za kilimo na ufugaji.

“Ardhi mimi sitatoa, sjui mlima sjui nini, siwezi kwenda kupeleka hilo ombi kwa Mhe. Rais, kabisa, hicho ni kitu ambacho hatuwezi kufanya kwa sasa’,” Alisisitiza Dk. Kigwangalla.

Mbunge huyo pia aliiomba Serikali kuweka uzio wa waya kwa ajili ya kutenganisha mpaka wa hifadhi hiyo na vijiji kwa madai ya kuepuka ukamataji wa mifugo ya wananchi unaofanywa na askari wa wanyamapori kwenye ardhi za vijiji na kuingizwa hifadhini na kutozwa faini, hoja iliyopigwa vikali na Mkuu wa Wilaya ya Karagwe, Godfrey Mheluka.

Hata hivyo, Dk. Kigwangalla alikataa ombi hilo na kusema kuwa mipaka ya hifadhi hiyo ni mikubwa kuwezesha utekelezaji wa ombi hilo. Alisema Serikali itatengeneza mtandao wa barabara zinazounganisha hifadhi hiyo na vijiji kwa ajili ya kuimarisha doria na shughuli za utalii pamoja na kujenga ofisi ndogo za pori hilo katika kila wilaya inayohusika na pori hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Karagwe, Godfrey Mheluka aliwataka wananchi wanaofanya vitendo vya kuingiza mifugo kwenye pori hilo wakati wa usiku kuacha mara moja kwa kuwa wakimatwa watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Alisema malalamiko ya wananchi hao kuwa askari wa wanyamapori wanakamata mifugo yao kwenye maeneo ya vijiji na kuiingiza hifadhini kwa lengo la kuwatoza faini kuwa sio ya kweli na kwamba malalamiko yanakuja kwakuwa hukamatwa asubuhi wakiwa wameshatoka kulisha mifugo hifadhini.
Kisiwa hicho cha Izinga ambacho kipo katika wilaya ya Karagwe mkoani Kagera kina ukubwa wa Kilomita za Mraba 12 na kinapakana na nchi Rwanda.
Pori la Akiba Kimisi liliqnzishwa mwaka 2003 kwa Tangazo la Serikali na 116 na lina ukubwa wa kilomita za mraba 1,030. Pori hilo lina wanyamapori mbalimbali wakiwemo Tembo, Twiga, Simba na Chui. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiongozana na Mbunge wa Jimbo la Karagwe, Innocent Bashugwa kukagua Pori la Akiba Kimisi wakati wa ziara yake ya kutatua migogoro ya ardhi kwenye maeneo ya hifadhi katika Wilaya ya Karagwe mkoani Kagera jana. 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na baadhi ya viongozi wa kijiji cha Mwisheni alipofika kukagua Pori la Akiba Kimisi wakati wa ziara yake ya kutatua migogoro ya ardhi kwenye maeneo ya hifadhi katika Wilaya hiyo mkoani Kagera jana.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiongozana na Mbunge wa Jimbo la Karagwe, Innocent Bashugwa kukagua Pori la Akiba Kimisi wakati wa ziara yake ya kutatua migogoro ya ardhi kwenye maeneo ya hifadhi katika Wilaya ya Karagwe mkoani Kagera jana. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Karagwe, Godfrey Mheluka wakati akikagua Pori la Akiba Kimisi akiwa kwenye ziara yake ya kutatua migogoro ya ardhi kwenye maeneo ya hifadhi katika Wilaya hiyo mkoani Kagera jana.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akionyesha mpaka wa Pori la Akiba Kimisi wakati wa ziara yake ya kutatua migogoro ya ardhi kwenye maeneo ya hifadhi katika Wilaya hiyo mkoani Kagera jana. Kulia ni Mkuu wa Karagwe, Godfrey Mheluka na Mbunge wa Karagwe, Innocent Bashungwa (kulia kwake).
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Ngara, Lut. Col. Michael Mutenjele (kushoto) wakati wakivuka kivuko cha Ruvuvu wakati wa ziara yake ya kutembelea na kutatua migogoro ya ardhi kwenye maeneo ya hifadhi katika Wilaya hiyo mkoani Kagera jana. 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiangalia baadhi ya mifugo iliyokamatwa ndani ya Pori la Akiba Kimisi wakati wa ziara yake ya kutatua migogoro ya ardhi kwenye maeneo ya hifadhi katika Wilaya Ngara mkoani Kagera jana. (Picha na Wizara ya Maliasili na Utalii).

Comments

Popular posts from this blog

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.

AMANI YETU TUILINDE NAIBU WAZIRI CHANDE AZUNGUMZA KATIKA IJITIMAI JIJINI DODOMA