WAFANYAKAZI WASHAURIWA KUPIMA AFYA MARA BAADA YA KUSTAAFU.
Na: Lilian Lundo – MAELEZO Dodoma.
Wafanyakazi
nchini wameshauriwa kupima afya zao mara tu wanapostaafu ili
kujihakikishia ikiwa hawajaathirika na kazi ambazo wamekuwa wakizifanya.
Hayo
yameelezwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira, Vijana na
Wenye Ulemavu Eric Shitindi alipokuwa akifungua semina ya viongozi wa
Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) na viongozi wa
Vyama vya Wafanyakazi juu ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, leo Mjini
Dodoma.
“Kumekuwa
na mazoea kwa wafanyakazi kupima Afya pale tu wanapoajiriwa na
kutotilia maanani upimaji afya zao mara wanapostaafu ili kujua ikiwa
kazi wanazozifanya zimewaathiri kwa kiasi gani,” amesema Shitindi.
Ameendelea
kwa kusema kuwa, upimaji wa afya mara baada ya kustaafu utasaidia
watumishi kujua afya zao na ikiwa watakuwa wameathirika upitia kazi
walizokuwa wakizifanya basi mwajiri atawajibika mkulipa fidia mtumishi
huyo.
Aidha
amesema kuwa licha ya juhudi za Serikali katika kusimamia Usalama na
Afya maeneo mengi ya kazi sio ya kuridhisha kutokana na waajiri wengi
kutokuzingatia sheria na kanuni mbalimbaliza Usalama na Afya.
Hivyo
basi kutokana na waajiri hao kutofuata sheria na kanuni hizo
kumesababisha maeneo mengi ya kazi kulalamikiwa kutokana na ukiukwaji wa
sheria hizo.
Vile
vile amesema kuwa baadhi ya waajiri na wafanyakazi wana uelewa mdogo
kuhusu kuzingatia maelekezo ya Usalama na Afya Mahali pa kazi ikiwemo
matumizi sahihi ya vifaa kinga.
Kwa
upande wake Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa
Kazi (OSHA) Khadija Mwenda amesema kuwa, wameamua kuandaa semina hiyo
kwa viongozi wa vyama vya wafanyakazi hapa nchini ili na wao wakatoe
elimu hiyo kwa wafanyakazi wote nchini kutokana na wafanyakazi hao
kutokuwa na uelewa mzuri juu ya masuala ya Usalama na Afya Mahali pa
Kazi.
Kaimu
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) Bi.
Khadija Mwenda akiongea na Viongozi wa Shirikisho la Vyama vya
Wafanyakazi Tanzania(TUCTA) na Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi wakati
wa Ufunguzi wa Semina kuhusu masuala ya usalama na afya mahala pa kazi
Leo Mjini Dodoma.Kulia ni Makamu wa Rais wa Shirikisho la Vyama vya
Wafanyakazi (TUCTA) Bw.Qambos Sule
Katibu
Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu Bw.
Eric Shitindi akiongea na Viongozi wa Shirikisho la Vyama vya
Wafanyakazi Tanzania(TUCTA) na Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi wakati
wa Ufunguzi wa Semina kuhusu masuala ya usalama na afya mahala pa kazi
ambapo aliwashauri wafanyakazi nchini kupima afya mara wanapostaafu ili
kujihakikishia kama hawajaathirika na kazi walizokuwa wanafanya.Katikati
ni Makamu wa Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA)
Bw.Qambos Sule na Kushoto ni Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na
Afya Mahala pa Kazi (OSHA) Bi. Khadija Mwenda
Makamu
wa Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw.Qambos Sule
akiongea naViongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi
Tanzania(TUCTA) na Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi wakati wa Ufunguzi
wa Semina kuhusu masuala ya usalama na afya mahala pa kazi, kulia ni
Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu
Bw. Eric Shitindi na kushoto ni Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama
na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) Bi. Khadija Mwenda
Makamu
wa Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw.Qambos Sule
(KUSHOTO) na Katibu Mkuu Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw.
Jones Majura(KULIA) wakiteta jambo na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri
Mkuu-Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu Bw. Eric Shitindi baada ya
ufunguzi wa Semina kuhusu masuala ya usalama na afya mahala pa kazi leo
Mjini Dodoma
Katibu
Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu Bw.
Eric Shitindi akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Semina kuhusu
masuala ya usalama na afya mahala pa kazi Leo Mjini Dodoma. PICHA NA
IDARA YA HABARI-MAELEZO,DODOMA
HOSPITALI YA TEULE MUHEZA YAPATIWA MSAADA WA MASHUKA
HOSPITALI
ya Teule wilayani Muheza Mkoani Tanga imepata msaada wa mashuka 50 kwa
ajili ya kukabiliana na uhaba uliopo kutokana na kuwepo kwa idadi kubwa
ya wagonjwa wanao kwenda kupata matibabu kutoka maeneo mbalimbali hasa
vijijini.
Hatua ya uhaba huo unatokana na uchakavu wa wa mashuka unaotokana na kufubaa unaosababishwa na maji wanayotumia kufulia kutokana na uhaba wa maji hali iliyopelekea kuwepo uhitaji kila wakati ili kuweza kukithi mahitaji ya wagonjwa wanaokwenda kupata matibabu.
Hayo yalibainishwa jana na Kaimu Mganga Mkuu wa wilaya ya Muheza, Boniphace Mhabe wakati akipokea msaada wa mashuka 50 kutoka kampuni ya Suba Agro Trading na Engineering ambao ni mzalishaji wa mbegu bora zamahindi kwa kushirikiana na Cimmity taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mahindi na Ngano.
Shuka hilo zilitolewa kwa ajili ya wodi ya wakina mama wajawazito kwenye hosptali ya Teule Muheza,Hospitali ya wilaya ya korogwe na ile ya wilaya ya Handeni lengo kubwa likiwa kuwaondolea changamoto zinazowakabili.
"Vitanda vipo vingi lakini tatizo kubwa ni mashuka na hili linatokana na asilimia kub wa kuchakaa kutokana na maji lakini pia wakati mwengine yanabadilika rangi jambo ambalo limekuwa changamoto kwao.
Aidha alisema wanaishukuru kampuni hiyo kwa kuona umuhimu wa kusaidia msaada huo ambao umefika wakati muafaka kwa kusadia baadhi ya vikwazo wanazokutana navyo wakati wa utoaji wa huduma za afya.
Awali akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo,Afisa Masoko na Mauzo wa Kampuni hiyo,Neema Ng'unda alisema alisema wamekuwawakishiriki katika kuhamasisha kilimo Tanzania hususani kwa wakina mama ambao ndio nguzo kubwa hapa nchini kufikia mafanikio.
Alisema wamelenga wanawake kwa sababu ndio muhimili muhimu kwenye jamii wa kuwawezesha wakina baba kwenye kulima kilimo bora ambapo kinaweza kuwainua kiuchumi.
"Lakini pia tunawashukuru wakulima wote Tanzania kwa kutumia mbegu zao kwa kulima kilimo cha kisasa ambacho kinaweza kuwa mkombozi kijiinuakimaendeleo na kukuza mitaji yao "Alisema.
Naye kwa upande wake,Afisa Mauzo wa Suba Agro Trading yenye makao makuu yake mjini Arusha,Shillaga Samweli alisema zoezi hili limelenga kurudisha fadhila kwa wakina mama wa Tanzania maana ndio wamekuwa wakishiriki kikamilifu katika kilimo.
Hatua ya uhaba huo unatokana na uchakavu wa wa mashuka unaotokana na kufubaa unaosababishwa na maji wanayotumia kufulia kutokana na uhaba wa maji hali iliyopelekea kuwepo uhitaji kila wakati ili kuweza kukithi mahitaji ya wagonjwa wanaokwenda kupata matibabu.
Hayo yalibainishwa jana na Kaimu Mganga Mkuu wa wilaya ya Muheza, Boniphace Mhabe wakati akipokea msaada wa mashuka 50 kutoka kampuni ya Suba Agro Trading na Engineering ambao ni mzalishaji wa mbegu bora zamahindi kwa kushirikiana na Cimmity taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mahindi na Ngano.
Shuka hilo zilitolewa kwa ajili ya wodi ya wakina mama wajawazito kwenye hosptali ya Teule Muheza,Hospitali ya wilaya ya korogwe na ile ya wilaya ya Handeni lengo kubwa likiwa kuwaondolea changamoto zinazowakabili.
"Vitanda vipo vingi lakini tatizo kubwa ni mashuka na hili linatokana na asilimia kub wa kuchakaa kutokana na maji lakini pia wakati mwengine yanabadilika rangi jambo ambalo limekuwa changamoto kwao.
Aidha alisema wanaishukuru kampuni hiyo kwa kuona umuhimu wa kusaidia msaada huo ambao umefika wakati muafaka kwa kusadia baadhi ya vikwazo wanazokutana navyo wakati wa utoaji wa huduma za afya.
Awali akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo,Afisa Masoko na Mauzo wa Kampuni hiyo,Neema Ng'unda alisema alisema wamekuwawakishiriki katika kuhamasisha kilimo Tanzania hususani kwa wakina mama ambao ndio nguzo kubwa hapa nchini kufikia mafanikio.
Alisema wamelenga wanawake kwa sababu ndio muhimili muhimu kwenye jamii wa kuwawezesha wakina baba kwenye kulima kilimo bora ambapo kinaweza kuwainua kiuchumi.
"Lakini pia tunawashukuru wakulima wote Tanzania kwa kutumia mbegu zao kwa kulima kilimo cha kisasa ambacho kinaweza kuwa mkombozi kijiinuakimaendeleo na kukuza mitaji yao "Alisema.
Naye kwa upande wake,Afisa Mauzo wa Suba Agro Trading yenye makao makuu yake mjini Arusha,Shillaga Samweli alisema zoezi hili limelenga kurudisha fadhila kwa wakina mama wa Tanzania maana ndio wamekuwa wakishiriki kikamilifu katika kilimo.
Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha
RAIS ABBAS: AIDHA UHURU AU HAKI KAMILI KWA WOTE, KATIKA NCHI YA PALESTINA YA KIHISTORIA
Rais
wa Palestina “Mahmoud Abbas” amesisitiza kuwa uhuru wa nchi yake upo
karibu hauepukiki na kwamba uvamizi wa Israeli unafikia mwisho, akisema:
"Aidha upatikane uhuru au haki kamili ya wote katika nchi ya Palestina
ya kihistoria."
Rais
Abbas Jumatano jioni akihutubia Mkutano wa 72 wa Umoja wa Mataifa,
ameongeza kusema kwamba, imepita miaka ishirini na minne tangu kusainiwa
kwa Mikataba ya mpito ya Oslo, ambayo ilionesha ukomo wa uvamizi wa
Israeli na kuwapa matumaini Wapalestina, ya kuanzishwa kwa Dola yao
huru, huku akihoji " Tuko wapi sasa na matumaini haya?."
Amesema:"Tumekubali
uwepo wa Dola ya Israeli kupitia mipaka ya mwaka 1967, lakini Israeli
kutokubali uwepo wa Dola ya Palestina kunatupa maswali mengi. Badala ya
kuzingatia sababu, inafanya juhudi kuteka misimamo ya kimataifa kwa
masuala yasiyo na uzito wowote, yatokanayo na sera zake za kikoloni.
Tunapoitaka na kutakiwa na jumuiya ya kimataifa kukomesha uvamizi wake,
inadai ni uchochezi na kukosekana ushiriki wa Palestina na kuwekwa kwa
masharti yasiyowezekana."
Rais
Abbas ameongeza kusema kuwa,anaelea machafuko ni Utawala wa kivamizi wa
Israeli katika ardhi yetu,uvamizi ambao umefikia zaidi ya nusu
karne,huku zaidi ya miaka kumi sasa tumekubaliana kuunda kamati ya
pande tatu ambazo ni Marekani,Israeli na Palestina, ili kumaliza suala
la uchochezi.Kamati imefanya kazi kwa muda, lakini tumekuwa tunatoa
wito wa kufufuliwa wa kamati hiyo hatupati mrejesho. Hivi ni nani
anaekaribisha hilo na kufanya juhudi ya kulifanya liwepo?.
Amesema
pia,kuendelea kwa uvamizi ni aibu kwa Israeli na Jumuiya ya
Kimataifa,ni wajibu wa Umoja wa Mataifa kumaliza uvamizi huo ili
kuwezesha jamii ya Palestina kuishi kwa uhuru na ustawi katika ardhi
yake,huku mji mkuu wake ukiwa ni Jerusalemu ya Mashariki.
"Kukomesha uvamizi na vitendo vyake vya kidhalimu, vitakuwa na athari kubwa mno katika kupambana na udaidi pia mashirika yake kukosa karatasi muhimu ambazo huzitumia kwa kuuza fikra zao."Tunatilia mkazo la kukaliza uvamizi ili kukamilisha juhudi zetu katika kukabiliana na mashirika hayo ya kigaidi,kwani Wapalestina wapo dhidi ya ugaidi wa ndani,kikanda na wa kimataifa.
"Kukomesha uvamizi na vitendo vyake vya kidhalimu, vitakuwa na athari kubwa mno katika kupambana na udaidi pia mashirika yake kukosa karatasi muhimu ambazo huzitumia kwa kuuza fikra zao."Tunatilia mkazo la kukaliza uvamizi ili kukamilisha juhudi zetu katika kukabiliana na mashirika hayo ya kigaidi,kwani Wapalestina wapo dhidi ya ugaidi wa ndani,kikanda na wa kimataifa.
"Tuliwasilisha
mpango wa amani wa Kiarabu unaoitaka Israeli kuondoka katika maeneo ya
Palestina yanayokaliwa kimabavu tangu mwaka 1967 lakini Israeli
haikujibu,kama ilivyoufanyia ule mpango ujulikanao kama “Road Map”
uliowasilishwa na pande nne na kupitishwa na Baraza la Usalama la Umoja
wa Mataifa,hali inayoonekana kana kwamba Israeli ipo juu ya sheria.
Vilevile ukaja mpango wa amani wa Ufaransa ukifuatiwa na mkutano husika
mjini Paris,lakini juhudi zote hizi zilikataliwa na kupigwa na Israeli."
Ameongeza
kusema:”Tulimuomba Waziri Mkuu wa Israeli akubali ufumbuzi wa dola
mbili, kisha tukae kuzungumzia suala la mipaka akakataa,licha ya
jitihada zetu kufikia amani ya kweli, lakini Israeli inaendelea kuvuruga
na kuendeleza ujenzi wa makazi ya walowezi Ukingo wa Magharibi na kila
mahali, hatimae hakuna tena nafasi kwa ajili ya taifa la Palestina.
"Vitendo viovu vya Israeli katika mji mtakatifu, vitachochea hisia za uadui wa kidini, ambao unaweza kugeuka mgogoro mkubwa wa kidini, tumeiomba serikali ya Israeli kuheshimu sheria na historia ya sehemu hizo takatifu lakini Israel tangu ilipoikalia kimabavu Jerusalemu mwaka 1976, imekuwa ikiihodhi kwa azimio la upande mmoja.
"Vitendo viovu vya Israeli katika mji mtakatifu, vitachochea hisia za uadui wa kidini, ambao unaweza kugeuka mgogoro mkubwa wa kidini, tumeiomba serikali ya Israeli kuheshimu sheria na historia ya sehemu hizo takatifu lakini Israel tangu ilipoikalia kimabavu Jerusalemu mwaka 1976, imekuwa ikiihodhi kwa azimio la upande mmoja.
Rais
Abbas amesema kuwa, “Jerusalemu imekaliwa kimabavu na hatua zote za
Israeli ni batili kama ilivyo katika ujenzi wake wa makazi ya walowezi
Jerusalemu ya Mashariki na maeneo mengine ya Palestina. Ieleweke wazi
kuwa,ubadilishaji wa historia ya Jerusalemu na kuuchafua Msikiti wa
Aqswa ni kuchezea hatari,pia ni kushambulia majukumu ya Palestina na
yale ya Jordan.Tunaitahadharisha hilo, isijaribu kusababisha vita vya
kidini wakati mgogoro wetu ni wa kisiasa”.
"Chaguo
letu kama Waarabu na chaguo la dunia ni sheria za kimataifa, uhalali wa
kimataifa na uwepo wa dola huru ya Palestina kwa mujibu wa mipaka ya
1967.Tutatoa ushirikiano wote katika kufanikisha hilo la kihistoria,ili
tupate kuishi kwa amani pamoja na Israeli. Lakini kama ufumbuzi wa dola
mbili utaharibiwa na kuimarisha dola moja yenye serikali
mbili,hapatakuwa na linguine kwetu wala kwenu ila mapambano na kutaka
kupata haki zetu kamili ndani ya Palestina ya kihistoria. Hivi si
vitisho ila ni kutaka haki zetu kama wapalestina”.
Tatizo
letu kwa utawala wa kivamizi wa Israeli sio Uyahudi kama dini, kwani
hiyo ni dini ya Mungu kama Uislamu na Ukristo.Tumebeba majukumu yetu
katika Ukanda wa Gaza,ambayo haiwezekani kuwepo Palestina bila
hiyo,ninafarijika leo kuona kufikiwa kwa makubaliano mjini Cairo
kufuatia juhudi nzuri za Misri.Yamekomesha vitendo vya Hamas vilivyoleta
mgawanyiko na hatimae kufanyika kwa uchaguzi mkuu,hatimae serikali yetu
mwisho wa wiki ijayo itakwenda Ukanda wa Gaza ili kufanya kazi huko.
"Ukimya
wa jumuiya ya kimataifa juu ya vitendo dhalimu vya Israeli,ndio
uliohamasisha vitendo hivyo tangu awali hadi inakiuka maazimio ya Umoja
wa Mataifa tangu kuanzishwa kwake, uko wapi Umoja huo na maazimio
yake?Vipi unatendea mataifa kwa viwango tofauti? Basi huu ni wajibu wa
Umoja wa Mataifa." Aidha ameuomba kumaliza uvamizi wa Israeli ndani ya
muda maalumu,kwani haiwezi tena kutoa data huru kuhusu mpango wa amani
wa kiarabu,hasa kuhusiana na faili wakimbizi kwa mujibu wa azimio la
Umoja wa Mataifa 194,huku akiashiria kuwa maazimio ya Umoja wa Mataifa
yanaendelea kupuuzwa na Israeli”.
Rais
Abbas amesisitiza haja ya kusitisha shughuli za ujenzi wa makazi ya
walowezi katika maeneo ya Palestina,kwani hatuna uwezo wa kulinda raia
zetu chini ya utawala wa mabavu,Umoja wa Mataifa uitake Israeli kutambua
mipaka Palestina ya mwaka 1967 na kupunguza mpaka na kuomba wajumbe
wote wa Umoja wa Mataifa kutangaza kwamba kutambuliwa kwao kwa msingi wa
mipaka ya 1967,pia wanachama wote wa Umoja huo kutambua mipaka hiyo ili
kutilia mkazo maazimio ya sheria za kimataifa.
Amesema:"Iko
wapi mipaka ya Israeli mlioitambua wakati Israeli yenyewe
haijaikubali,sheria za kimataifa zinaitaka dunia kuweka hiyo mipaka".
Aidha Rais ametoa wito kwa nchi zote duniani kutoshiriki katika ujenzi
wa makazi ya kikoloni ulio kinyume na sheria,huku zikichukua hatua
stahiki dhidi yake kama ilivyofanya jumuiya ya kimataifa dhidi ya
utawala wa kibaguzi wa Afrika ya kusini na tunataka kutangaza habari
mbaya za mashirika ambayo yanafanya kinyume cha sheria na makazi."
Hivyo,
amezihimiza nchi wanachama kuitambua dola ya Palestina kwa mujibu wa
mipaka ya mwaka 1967,huku akitilia mkazo kuwa hatua hiyo haitoathiri
mpango wa amani,hasa hasa ikiwa Wapalestina wanaitambua dola ya Israeli.
Tunauhimiza Umoja wa Mataifa kuikubali Palestina kama mwanachama wake
kamili,huku tukiiomba jumuiya ya kimataifa kuendelea kuisaidia kiuchumi
na kifedha ili iweze kujitegemea na kujiamini.
Aidha
Rais Abbas, ametahadharisha juhudi za kutaka kubadilisha majukumu ya
shirika la misaada UNRWA na kanuni zake,pia kufuta kipengele cha saba
katika Baraza la haki za binaadamu au kuzuia kutoa orodha chafu ya
mashirika yanayofanya kazi katika makazi ya walowezi wa Israeli nchini
Palestina inayokaliwa kimabavu.
Rais
Abbas amehitimisha hotuba yake kwa kutilia mkazo msimamo wa nchi
yake,katika kuheshimu haki za binaadamu na kutekeleza mikataba ya Umoja
wa Mataifa na ile yote iliyosaini,kwani Palestina ni sehemu ya jumuiya
ya kimataifa na si vingine. Huku nchi yake pia itaandaa matakwa hayo kwa
maazimio yatayokwenda sambamba na misingi husika,kisha kuyawasilisha
kwa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
TIMU YA NDANTO FC YATWAA KOMBE LA MICHUANO YA 'TULIA CUP 2017'
Mkuu
wa Majeshi Mstaafu, Davis Mwamunyange, akimkabidhi Kombe Nahodha wa
timu ya Ndanto Fc, Peter Mwakingwa, baada ya kushika nafasi ya nafasi ya
kwanza na kutwaa kombe la fainali za 'Tulia Cup 2017' kwenye uwanja wa
Tandale Tukuyu Wilayani Rungwe mkoa wa Mbeya. Picha na Muhidin Sufiani
(MAFOTO MEDIA GROUP)
Mkuu
wa Majeshi Mstaafu, Davis Mwamunyange, akimkabidhi Kombe Nahodha wa
timu ya Isange, Frank Asilih, baada ya kushika nafasi ya pili katika
fainali za 'Tulia Cup'kwenye uwanja wa Tandale Tukuyu Wilayani Rungwe
mkoa wa Mbeya.
Beki
wa timu ya Isange Fc, Zawadi Andombwisye (kushoto) akichuana kuwania
mpira na mshambuliaji wa Ndanto Fc, Erick Mwangoye, wakati wa mchezo wa
Fainali za 'Tulia Cup' uliochezwa jana Sept 21, 2017 kwenye Uwanja wa
Tandale Tukuyu Wilayani Rungwe Mkoani Mbeya. Katika mchezo huo Ndanto
walishinda kwa mabao 2-1 na kutwaa kombe hilo kwa mwaka huu 2017 na
kitita cha sh. milioni 1.5.
Beki
wa timu ya Ndanto Fc,Fidelis Yeo (kulia) akiwania mpira na mshambuliaji
wa Isange Fc, Hussein Thom, wakati wa mchezo wa Fainali za 'Tulia Cup'
uliochezwa jana Sept 21, 2017 kwenye Uwanja wa Tandale Tukuyu Wilayani
Rungwe Mkoani Mbeya. Katika mchezo huo Ndanto walishinda kwa mabao 2-1
na kutwaa kombe hilo kwa mwaka huu 2017 na kitita cha sh. milioni 1.5.
Wachezaji wa Isange Fc, Shadrack Kandrum (kushoto) na Hussein Thom
(kulia) wakimdhibiti Mandela Chaile, wakati wa mchezo wa Fainali za
'Tulia Cup' uliochezwa jana Sept 21, 2017 kwenye Uwanja wa Tandale
Tukuyu Wilayani Rungwe Mkoani Mbeya. Katika mchezo huo Ndanto walishinda
kwa mabao 2-1 na kutwaa kombe hilo kwa mwaka huu 2017 na kitita cha sh.
milioni 1.5.
Beki
wa timu ya Isange Fc, Shadrack Kandrum (kulia) akimdhibiti mshambuliaji
wa Ndanto Fc, Julius Mtawala, wakati wa mchezo wa Fainali za 'Tulia
Cup' uliochezwa jana Sept 21, 2017 kwenye Uwanja wa Tandale Tukuyu
Wilayani Rungwe Mkoani Mbeya. Katika mchezo huo Ndanto walishinda kwa
mabao 2-1 na kutwaa kombe hilo kwa mwaka huu 2017 na kitita cha sh.
milioni 1.5.
Luteni
General, James Mwakibolwa, akiongozana na Mkurugenzi wa Taasisi ya
Tulia Trust na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Tulia
Ackson, kukagua timu ya Ndanto fc kabla ya mchezo wa fainali dhidi ya
Isande Fc, katika mchezo wa fainali wa 'Tulia Cup' kwenye uwanja wa
Tandale Tukuyu Wilayani Rungwe mkoa wa Mbeya.
Luteni
General, James Mwakibolwa, akimkabidhi Kombe Nahodha wa timu ya
Netiboli ya Kimo,Salome Sanyondo, baada ya kushika nafasi ya pili katika
fainali za 'Tulia Cup'kwenye uwanja wa Tandale Tukuyu Wilayani Rungwe
mkoa wa Mbeya.
Luteni
General, James Mwakibolwa, akimkabidhi Kombe Nahodha wa timu ya
Netiboli ya Wizara ya Mambo ya Ndani, baada ya kushika nafasi ya kwanza
katika fainali za 'Tulia Cup'kwenye uwanja wa Tandale Tukuyu Wilayani
Rungwe mkoa wa Mbeya.
WAZIRI KAIRUKI AZINDUA BODI YA PILI YA UONGOZI INSTITUTE
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Angellah Kairuki
amesema kuwa wakurugenzi walioteuliwa katika bodi ya Taasisi ya Uongozi
ni watu makini na wenye uzoefu wa muda mrefu katika nafasi mbalimbali
hivyo watatoa ushauri mzuri kwenye taasisi hiyo.
Waziri
Angellah aliyasema hayo katika uzinduzi wa bodi ya pili ya Taasisi ya
Uongozi uliofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es
Salaam. Amesema bodi ya wakurugenzi wa taasisi hiyo wamepita katika
utumishi na wazalendo katika sehemu zao mbalimbali ambapo watakuwa
msaada mkubwa kwa taasisi hiyo katika kutoa ushauri.
Amesema
kuwa Uongozi Institute ilianzishwa kwa ajili ya kuwajengea uwezo
viongozi wa Afrika katika kuangalia maendeleo endelevu ya bara la Afrika
hivyo wajumbe wa bodi ni wa kimataifa na wanatambulika.
Angellah
amesema kuwa walioteuliwa na Rais Dk.John Pombe Magufuli watatimiza
majukumu yao na wataendelea kupewa ushirikiano pamoja na viongozi
wengine wa Afrika katika kuwa na ajenda ya kuandaa viongozi.
Amesema
uongozi Institute inatakiwa kutimiza mambo matatu moja ni bidhaa ya
huduma iliyo na kiwango bora, kuangalia rasilimali ya kuweza kufanya
taasisi hiyo ikue katika kuangalia vyanzo vya mapato pamoja na kujengea
uwezo wa kuendelea kutekeleza ajenda ambazo zimeibuliwa.
Walioteuliwa
katika bodi hiyo Mwenyekiti ni Balozi wa Finland Inchini Afrika Kusini,
Kari Alanko , Makamu wa Rais Profesa Idris Kikula wengine ni Katibu
Mkuu wa Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Dk. Laureane Ndumbaro,
Katibu Mtendaji wa SADC Dk. Stergomena Tax, Profesa Penina Mlama wa
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Christina Duarte Waziri wa Zamani wa
Fedha , Mipango na Utumishi wa Cape Verde, Mkurugenzi wa Nodic Afrika ya
nchini Sweeden Lina Soiri, pamoja Mkurugenzi wa zamani wa shule ya
utawala ya nchini Uingereza , David Walker.
Nae
Afisa Afisa Mtendaji Mkuu wa Uongozi Institute, Profesa Joseph Semboja
amesema kuwa chombo hicho kilianzishwa katika kuwajengea viongozi wa
Afrika ambao waliridhia kuundwa kwa chombo hicho.
Amesema kuwa Taasisi hiyo imetoa mafunzo mbalimbali tangu kuanzishwa kwake na itaendelea kutoa mafunzo kwa watumishi.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Angellah Kairuki
akizungumza katika uzinduzi wa bodi ya pili ya Wakurugenzi wa Uongozi
Institute , uliofanyika katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es
Salaam.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Uongozi Insitute, Profesa Joseph Semboja akizungumza
katika uzinduzi wa bodi ya Uongozi Institute juu ya taasisi hiyo
inavyofanya kazi katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti
wa Bodi ya Wakurugenzi wa Uongozi Institute ,Balozi wa Finland Inchini
Afrika Kusini, Kari Alanko akitoa shukurani kwa Waziri Kairuki mara
baada ya kuzinduliwa bodi hiyo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Angellah Kairuki akigawa vitabu vya miongozo kwa wajumbe wa Bodi hiyo.
Sehemu watendaji mbalimbali wa serikali waliohudhuria uzinduzi wa bodi ya pili ya oungozi institute.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Angellah Kairuki akiwa
katika picha ya pamoja na bodi ya ya wakurugenzi ya Uongozi Institute,
jijini Dar es Salaam.
HAFLA YA CHAKULA CHA JIONI ILIOANDALIWA NA KINANA KWA AJILI YA KIONGOZI WA CHAMA CHA KIKOMUNISTI CHA VIETNAM MJINI DODOMA JANA SEPTEMBER 21,2017
Mwenyekiti
wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dodoma Alhaj Adamu Kimbisa akimtolea
ufafanuzi wa zawadi ya kinyango Mjumbe wa kamati kuu ya chama cha
kikomunisti cha vietnam (VCP) Comred Chau Van Lam uku katibu Mkuu wa
(CCM) akishuhudia zoezi hilo,wakati wa hafla ya Chakula cha Jion
ilioandaliwa na kinana.
Katibu
mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Comred Abdurahman Kinana akizungumza kabla
ya Mjumbe wa kamati kuu ya chama cha kikomunisti cha vietnam (VCP)
Comred Chau Van Lam kukabidhiwa zawadi na Mwenyekiti wa Chama Cha
Mapinduzi Mkoa wa Dodoma Alhaj Adamu Kimbisa wakati wa hafla ya Chakula
cha Jion.
Katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Comred Abdurahman Kinana akizungumza na balozi wa Vietnam Nguyen kim Doanh.
Katibu
mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Comred Abdurahman Kinana akifurahia jambo
na wageni wake toka chama cha Kikomunisti cha Vietnam (VCP) jana wakati
wa hafla ya chakula cha jion.
Katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Comred Abdurahman Kinana akizungumza wakati wa hafla ya chakula cha jion.
Wajumbe
wa Chama cha kikomunisti cha Vietnam (VCP) pamoja na Katibu mkuu wa
Jumuiya ya Umoja wa Wazaza CCM wa (pili toka kushoto) wakifuatilia
mazungumzo ya Katibu mkuu wa CCM katika hafla ya chakula cha jion.
Baadhi Wajumbe wa Sekretariet wakifuatilia mazungumzo ya Katibu mkuu wa CCM katika hafla ya chakula cha jion.
Katibu
Mkuu wa CCM Comred Abdurahman Kinana na Mjumbe wa kamati kuu ya chama
cha kikomunisti cha vietnam (VCP) Comred Chau Van Lam wakinyanyua glasi
kabla ya kuzigonganisha kutakiana heri kabla ya chakula cha jion alicho
mwandalia Mjumbe wa kamati kuu ya chama cha kikomunisti cha vietnam
(VCP) Comred Chau Van Lam Mjini dodoma.
Mwenyekiti
wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Dodoma Alhaj Juma Kimbisa pamoja na
Katibu wa idara ya SUKI kanal mstaaf Ngemela Rubiga wakinyanyua glasi
kabla ya kuzigonganisha kutakiana heri kabla ya chakula cha jion Katibu
mkuu wa CCM alicho mwandalia Mjumbe wa kamati kuu ya chama cha
kikomunisti cha vietnam (VCP) Comred Chau Van Lam Mjini dodoma.
Naibu
Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar DKT.Abdallah Mabodi akiagana na Mjumbe wa
kamati kuu ya chama cha kikomunisti cha vietnam (VCP) Comred Chau Van
Lam mara baada ya kumalizika hafla ya chakula cha Usiku ilioandaliwa na
Katibu mkuu wa CCM Comred Abdulrahman kinana Mjini dodoma.
Katibu
Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Comred Abdulrahman Kinana akiagana na Mgeni
wake Mjumbe wa kamati kuu ya chama cha kikomunisti cha vietnam (VCP)
Comred Chau Van Lam mara baada ya kumalizika kwa hafla ya chakula cha
jion aliomwandalia mgeni wake Mjini dodoma.
(PICHA ZOTE NA FAHADI SIRAJI)
Comments
Post a Comment