STAMICO YAANZA UZALISHAJI MAKAA YA MAWE KABULO-KIWIRA

STAMICO YAANZA UZALISHAJI MAKAA YA MAWE KABULO-KIWIRA

 Wataalam wa STAMICO wakiendelea na kazi ya uchimbaji makaa ya mawe katika Mlima wa Kabulo uliopo Kiwira wilayani Ileje mkoa wa Songwe.
 Shughuli za uchimbaji wa Makaa ya Mawe zinazofanywa na STAMICO, zikiendelea katika Mlima Kabulo-Kiwira.

Na Koleta Njelekela-STAMICO
Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limeanza uchimbaji wa makaa ya mawe katika mlima wa Kabulo uliopo Kiwira katika wilaya ya Ileje Mkoa wa Songwe.

Mratibu wa Mradi wa Uchimbaji Makaa ya Mawe-Kiwira, Mjiolojia Alex Rutagwelela ambaye pia ni Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti na Uchorongaji wa STAMICO amesema kazi ya uchimbaji iliyoanza tarehe 30/04/2017 inaendelea vizuri na tayari tani 100 zimechimbwa katika siku ya kwanza. Lengo la mradi ni kuchimba tani 200-300 kwa siku.

“Tumeanza uchimbaji na tani hizo, kama njia mojawapo ya kujaribu mitambo ya uchimbaji, kabla ya uzinduzi rasmi ambao unatarajiwa kufanyika hivi karibuni, baada ya Shirika na wadau wake, kukamilisha maandalizi ya uzinduzi.” Alifafanua Mjiolojia Rutagwelela. 

Aidha Rutagwelela amesema matarajio ya STAMICO ni kuchimba kati ya tani 6000 hadi tani 9000 za makaa ya mawe kwa mwezi kwa kuanzia, kiwango ambacho kinatarajiwa kuongezeka kadiri kazi ya uchimbaji inavyoendelea.

Mratibu huyo amesema awamu ya kwanza ya Mradi wa uchimbaji makaa ya mawe inatekelezwa kupitia leseni zake mbili za uchimbaji mdogo wa madini Primary Mining Licences (PMLs) zilizopo ndani ya leseni ya utafiti ya Kabulo zenye ukubwa wa Hecta 16.52. 

Leseni hizo mbili za Uchimbaji wa Awali wa Madini katika eneo hilo la Kabulo zina tani zipatazo 241,865 za mashapo ya makaa ya mawe yaliyoko karibu na uso wa ardhi ambayo yataruhusu Uchimbaji wa Mgodi wa Wazi (Open pit mining) kufanyika. 

“Uchimbaji huu, ambao umeanzia kwenye mlima wa Kabulo na baadae mlima wa Ivogo, utaiwezesha STAMICO kuzalisha makaa ya mawe na hivyo kupunguza uhaba wa madini hayo nchini ambayo ni moja ya vyanzo vya nishati ya umeme. Makaa ya mawe hutumika kama moja ya vyanzo vya Nishati katika shughuli za uzalishaji viwandani vikiwemo viwanda vya Saruji nchini” alifafanua Rutagwelela.

WAKAZI 122 MKOANI SIMIYU WAPEWA HATI NA WAZIRI LUKUVI AGAWA HATI 122 LAMADI

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi amegawa hati miliki za ardhi 122 kwa wananchi wa Lamadi Mkoa wa Simiyu wakati alipofanya ziara yake mikoa ya kanda ya ziwa kuhamasisha ulipaji kodi ya pango la ardhi na suala la urasimishaji wa makazi holela.

Wananchi hao 122 ni wale waliofanikiwa kulipia michango yote, hivyo kuondokana na makazi holela na kuishi katika makazi rasmi. Hata hivyo jumla ya wananchi 5,200 wa Lamadi Mkoa wa Simiyu washapimiwa maeneo yao kwa ajili ya urasimishaji, na watapatiwa hati zao mara tu baada ya kukamilisha michango stahili.

Katika ziara hiyo, waziri Lukuvi amefika wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza na kufanya ukaguzi wa mfumo wa ulipaji kodi ya pango la ardhi wilayani hapo na kugundua kati ya wakazi 35,000 wanaotakiwa kulipa kodi ya ardhi 28,000 wameishapelekewa hati ya madai.

Waziri Lukuvi pia ametembelea Idara ya Ardhi ya wilayani Nyamagana na kukagua mafaili ya kumbukumbu za wananchi kuhusu taarifa za ardhi ikiwemo masuala ya hati na kukugundua baadhi ya viongozi hawajalipa kodi ya pango la ardhi. Mmoja ya viongozi hao ni Mbunge wa Kwimba Shannif Mansoor ambaye hajalipa kodi ya pango la ardhi tangu 2010 kiasi cha shilingi milioni 529.

Aidha katika wilaya hiyo ameongea na wananchi wa Nundu kata ya Meko, mbali ya kusikiliza kero zao na kuzipatia ufumbuzi papo hapo, amewahimiza kuchamkia fursa ya kurasimisha makazi yao na kupata hati ili kuzipa thamani ardhi zao na kujitanulia fursa za uchumi.
Magere Mugeta mkazi wa Lamadi mkoani Simiyu akipokea hati ya kumuliki ardhi kutoka kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi.
Janet Magige mkazi wa Lamadi mkoani Simiyu akipokea hati ya kumuliki ardhi kutoka kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi akiwasisitiza wakazi Lamadi mkoani Simiyu umuhimu wa kumiliki ardhi kwa hati kwa kuwaonesha moja ya hati zinazotolewa kwa wananchi.
Wakazi wa Lamadi mkoani Simiyu wakishangilia pamoja na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi kwa kuwawezesha kupata Hati za kumiliki Ardhi.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi akikagua moja ya faili katika masijala ya Ardhi ya Ilemela Mkoani Mwanza akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongela (mwenye kofia).
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi akikagua mfumo wa kodi wa manispaa ya Nyamagana mkoani Mwanza ili kubaini wadaiwa wa kodi ya Ardhi.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi akiongea na wakazi wa Ilemela mkoani Mwanza.
Baadhi ya wakazi wa Ilemela mkoani Mwanza wakimsikiliza kwa makini Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi alipokuja kusikiliza kero zao za ardhi.

DKT. SHEIN AONGOZA SHEREHE ZA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI (MEI MOSI) MAHONDA, ZANZIBAR

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akisalimiana na Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto, Mhe. Maudline Cyrus Castico alipowasili katika viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja leo katika Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akisalimiana na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Zanzibar Maalim Khamis Mwinyi alipowasili katika viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja leo katika Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akiwapungia Mkono Wafanyakazi mbali mbali waliopita mbele yake kwa Maandamano wakati wa Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja.
Baadhi ya wafanyakazi wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba,Sheria,Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakipita kwa Maandamano mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) wakati wa Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja.
Wafanyakazi na Wananchi kutoka shehia mbali mbali za Unguja walijumuika kwa pamoja katika Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja,wakipita kwa maandamano mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) akiwa mgeni rasmi katika sherehe hizo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akiwapungia Mkono Wafanyakazi mbali mbali waliopita mbele yake kwa Maandamano wakati wa Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja akiwa na Viongozi mbali mbali.
Wafanyakazi na Wananchi kutoka shehia mbali mbali za Unguja walijumuika kwa pamoja katika Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja,wakipita kwa maandamano mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) akiwa mgeni rasmi katika sherehe hizo.
Wafanyakazi wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar wakibeba Bango lenye Nembo la Idara yao wakati wa maandamano katika Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja,ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani).
Wafanyakazi wa Benki ya Tanzania BOT wakibeba Bango lenye Nembo la Idara yao wakati wa maandamano katika Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja,ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani).
​Wafanyakazi wa ​Idara ya Uhamiaji Zanzibar wakimpungia Mkono ​Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani),​alipokuwa akipokea ​​maandamano katika Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja.Picha na Ikulu, Zanzibar.

SMZ YAAHIDI KUUNGA MKONO JUHUDI ZA ZANUSO KATIKA SEKTA YA UJASIRIAMALI

Mshiriki wa Mashindano ya ujasiriamali kwa Vyuo vikuu, Tahani Said akipokea zawadi kutoka kwa Mgeni rasmi ambaye ni Mkurugenzi wa Viwanda Zanzibar, Saleh Suleiman Hamad katika mashindano hayo yaliyoandaliwa na jumuiya ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu Zanzibar(ZANUSO).
Mshiriki wa Mashindano ya ujasiriamali kwa Vyuo vikuu, Issah Eugenio ambaye mradi wake wa Handbags made in Jeans umechukua nafasi ya mwanzo, akipokea zawadi kutoka kwa Mgeni rasmi ambaye ni Mkurugenzi wa Viwanda Zanzibar, Saleh Suleiman Hamad katika mashindano hayo yaliyoandaliwa na jumuiya ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu Zanzibar(ZANUSO).
Mgeni rasmi Mkurugenzi wa Viwanda Zanzibar, Saleh Suleiman Hamad akiutubia wakati wa kufunga mashindano yaliyoandaliwa na jumuiya ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu Zanzibar(ZANUSO) huko ZU kampasi kuu ya Tunguu.
Mlezi wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Zanzibar(ZU), Mhadhiri wa Chuo hicho Juma Rashid Khamis wakati akizungumza katika uzinduzi wa mashindano ya miradi ya Ujasiriamali kwa wanafunzi wa vyuo vikuu Zanzibar yaliyofanyika katika kampasi ya chuo hicho huku Tunguu, Unguja.
Mkurugenzi wa Kampuni ya SISI Consultants, Mohamed Wario ambayo ni miongoni mwa wadhamini akitoa nasaha zake kwa wanafunzi walioshiriki katika mashindano hayo yaliyoandaliwa na jumuiya ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu Zanzibar(ZANUSO) huko ZU kampasi kuu ya Tunguu.
Picha ya pamoja ya washiriki wa mashindano hayo pamoja na Viongozi wa ZANUSO na ZU pamoja na mgeni rasmi.

Na Juma Farid, Zanzibar.

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar  imeahidi kuendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na baadhi ya Jumuiya za wanafunzi wa Vyuo Vikuu nchini zinazoonyesha nia ya kuthamini  fani ya Ujasiriamali kama chanzo mbadala cha kupunguza tatizo la Ajira nchini.

Ahadi hiyo imetolewa na  Mkurugenzi  wa Viwanda Zanzibar, Saleh Suleiman Hamad  kwa Niba ya  Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko  Balozi Amina Salum Ali Wakati akifunga warsha ya Mashindano ya miradi ya Ujasiriamali kwa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Zanzibar yaliyoandaliwa na Jumuiya ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu Zanzibar ( ZU) huko Kampasi Kuu ya Chuo hicho Tunguu.

Amesema ubunifu ulionyeshwa na wanafunzi hao katika uandishi, mikakati na bidhaa  za miradi ya Ujasiriamali waliyoiwasilisha katika Mashindao hayo inajenga ushawishi kwa serikali na mashirika mengine ya kimataifa kuwaunga mkono ili wafikie malengo yao ya kujiajiri na kuwaajiri vijana wengine wasiokuwa na ajira.

Amesema bado wanafunzi wengi wanaohitimu elimu ya ngazi ya vyuo vikuu nchini hawajatumia fursa zinazopatikana katika fani ya Ujasiriamali ambayo imekuwa ikitegemewa na mataifa mbali mbali duniani kupunguza  tatizo la ajira hasa kwa vijana.

“ Nasaha zangu kwenu kabla ya kuanzisha mradi wowote fanyeni tathimini na utafti wa kitaalamu kubaini aina ya ujasiriamali unaotaka kufanya una maslahi gani na wateja wako wahitaji bidhaa za aina gani sambamba na kuwa wabunifu wa kufanya miradi isiyofanana.”, alisema Katibu huyo.

Aidha alieleza kwamba kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Masoko, Balozi Amina Salum Ali serikali itaendelea kudhamini miradi itakayoonyesha ustawi na maendeleo endelevu.

Pia  katika juhudi za kuwajengea uwezo wajasiriamali hao alieleza kwamba serikali itashawishi makampuni na mashirika ya kimaita ya kibiashara kufanya kazi kwa karibu na jumuiya hizo ili zipate soko la uhakika la kuuzia bidhaa zao.

Hata  hivyo ametoa nasaha zake kwa wajasiriamali hao kutengeneza bidhaa bora zitakazokubalika katika soko la kimataifa pamoja na kujiongeza kitaaluma kupitia mafunzo mbali mbali ya fani hiyo.

Mapema  akizungumza  Mlezi wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Zanzibar(ZU), Bw. Juma Rashid Khamis  ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo hicho aliwasihi washiriki wa mashindao hayo kuendelea kujifunza zaidi kupitia kwa wajasiria mali wakongwe ili wapate ujuzi wa ziada wa kukabiliana na ushindani wa bidhaa na miradi ya ujasiriamali ndani na nje ya Zanzibar.

Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya SISI Consultants, Mohamed  Wario  aliwataka Wasomi hao kutumia  vizuri  fursa hiyo ya ujasiria mali kwa kuangazia  sehemu tofauti  ambazo bado hazijatumiwa  vizuri  kibiashara  zikiwemo  Sekta ya Utalii, Uvuvi na Ufugaji ili kuzalisha bidhaa bora zinazotokana na rasilimali hizo na kuzishindanisha katika soko la ndani na nje ya nchi.

“ Kampuni  ipo tayari kushirikiana na nyinyi  wakati wowote  lakini lazima mjiongeze zaidi kufikia lengo la kufanya miradi bora na inayoendana na mahitaji ya sasa ili mpate mafanikio zaidi”, alisisitiza Mkurugenzi huyo.

Kwa upande wake mshiriki wa mashindano hayo aliyeshindanisha mradi wa usindikaji wa bidhaa aina ya Jam inayotumia kwa chakula cha mkate iliyotengenezwa kwa matunda ya Maembe, Ehlam Ali Khamis alisema wazo la kutengeza bidhaa hizo ni kutokana na kukosekana kwa matumizi mazuri ya matunda hayo hasa wakati wa msimu wake hali inayosababisha kuharibika kwa kukosekana kwa viwanda vya kusindika matunda hayo.

Akitoa ufafanuzi juu ya  Warsha hiyo,  Mwanzilishi na Msimamizi  wa Mashindano hayo  Jumuiya ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Zanzibar  ZANUSO,  Mohamed Omar  alifafanua kwamba awali mchakato huo ulishirikisha jumla ya vyuo Sita na ulipopita mchujo vikabaki vitatu ambavyo ni Zanzibar University (ZU), State University  of Zanzibar(SUZA) na Summait University.

Mashindano hayo wamepatikana washindi saba ambao wamepewa Zawadi mbali mbali zikiwemo simu za Adroid, lakini nafasi ya kwanza ambayo imeshikiliwa na Issah Eugenio kwa mradi wa Handbags Made in Jeans, nafasi ya pili ni Ehlam Ali Khamis kwa mradi wa Mango Jam na Tatu Ibrahim ahmad abdalla na Sabrina  Khamis Machano wa mradi wa Teke knowlge solutions company  wote kutoka vyuo tofauti vilivyoshiriki kwa awatua hiyo.

Comments

Popular posts from this blog

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.

AMANI YETU TUILINDE NAIBU WAZIRI CHANDE AZUNGUMZA KATIKA IJITIMAI JIJINI DODOMA