STAMICO YAANZA UZALISHAJI MAKAA YA MAWE KABULO-KIWIRA
STAMICO YAANZA UZALISHAJI MAKAA YA MAWE KABULO-KIWIRA
Wataalam
wa STAMICO wakiendelea na kazi ya uchimbaji makaa ya mawe katika Mlima
wa Kabulo uliopo Kiwira wilayani Ileje mkoa wa Songwe.
Shughuli za uchimbaji wa Makaa ya Mawe zinazofanywa na STAMICO, zikiendelea katika Mlima Kabulo-Kiwira.
Na Koleta Njelekela-STAMICO
Shirika
la Madini la Taifa (STAMICO) limeanza uchimbaji wa makaa ya mawe katika
mlima wa Kabulo uliopo Kiwira katika wilaya ya Ileje Mkoa wa Songwe.
Mratibu
wa Mradi wa Uchimbaji Makaa ya Mawe-Kiwira, Mjiolojia Alex Rutagwelela
ambaye pia ni Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti na Uchorongaji wa STAMICO
amesema kazi ya uchimbaji iliyoanza tarehe 30/04/2017 inaendelea vizuri
na tayari tani 100 zimechimbwa katika siku ya kwanza. Lengo la mradi ni
kuchimba tani 200-300 kwa siku.
“Tumeanza
uchimbaji na tani hizo, kama njia mojawapo ya kujaribu mitambo ya
uchimbaji, kabla ya uzinduzi rasmi ambao unatarajiwa kufanyika hivi
karibuni, baada ya Shirika na wadau wake, kukamilisha maandalizi ya
uzinduzi.” Alifafanua Mjiolojia Rutagwelela.
Aidha
Rutagwelela amesema matarajio ya STAMICO ni kuchimba kati ya tani 6000
hadi tani 9000 za makaa ya mawe kwa mwezi kwa kuanzia, kiwango ambacho
kinatarajiwa kuongezeka kadiri kazi ya uchimbaji inavyoendelea.
Mratibu
huyo amesema awamu ya kwanza ya Mradi wa uchimbaji makaa ya mawe
inatekelezwa kupitia leseni zake mbili za uchimbaji mdogo wa madini
Primary Mining Licences (PMLs) zilizopo ndani ya leseni ya utafiti ya
Kabulo zenye ukubwa wa Hecta 16.52.
Leseni
hizo mbili za Uchimbaji wa Awali wa Madini katika eneo hilo la Kabulo
zina tani zipatazo 241,865 za mashapo ya makaa ya mawe yaliyoko karibu
na uso wa ardhi ambayo yataruhusu Uchimbaji wa Mgodi wa Wazi (Open pit
mining) kufanyika.
“Uchimbaji
huu, ambao umeanzia kwenye mlima wa Kabulo na baadae mlima wa Ivogo,
utaiwezesha STAMICO kuzalisha makaa ya mawe na hivyo kupunguza uhaba wa
madini hayo nchini ambayo ni moja ya vyanzo vya nishati ya umeme. Makaa
ya mawe hutumika kama moja ya vyanzo vya Nishati katika shughuli za
uzalishaji viwandani vikiwemo viwanda vya Saruji nchini” alifafanua
Rutagwelela.
WAKAZI 122 MKOANI SIMIYU WAPEWA HATI NA WAZIRI LUKUVI AGAWA HATI 122 LAMADI
Waziri
wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi amegawa hati
miliki za ardhi 122 kwa wananchi wa Lamadi Mkoa wa Simiyu wakati
alipofanya ziara yake mikoa ya kanda ya ziwa kuhamasisha ulipaji kodi ya
pango la ardhi na suala la urasimishaji wa makazi holela.
Wananchi
hao 122 ni wale waliofanikiwa kulipia michango yote, hivyo kuondokana
na makazi holela na kuishi katika makazi rasmi. Hata hivyo jumla ya
wananchi 5,200 wa Lamadi Mkoa wa Simiyu washapimiwa maeneo yao kwa ajili
ya urasimishaji, na watapatiwa hati zao mara tu baada ya kukamilisha
michango stahili.
Katika
ziara hiyo, waziri Lukuvi amefika wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza na
kufanya ukaguzi wa mfumo wa ulipaji kodi ya pango la ardhi wilayani hapo
na kugundua kati ya wakazi 35,000 wanaotakiwa kulipa kodi ya ardhi
28,000 wameishapelekewa hati ya madai.
Waziri
Lukuvi pia ametembelea Idara ya Ardhi ya wilayani Nyamagana na kukagua
mafaili ya kumbukumbu za wananchi kuhusu taarifa za ardhi ikiwemo
masuala ya hati na kukugundua baadhi ya viongozi hawajalipa kodi ya
pango la ardhi. Mmoja ya viongozi hao ni Mbunge wa Kwimba Shannif
Mansoor ambaye hajalipa kodi ya pango la ardhi tangu 2010 kiasi cha
shilingi milioni 529.
Aidha
katika wilaya hiyo ameongea na wananchi wa Nundu kata ya Meko, mbali ya
kusikiliza kero zao na kuzipatia ufumbuzi papo hapo, amewahimiza
kuchamkia fursa ya kurasimisha makazi yao na kupata hati ili kuzipa
thamani ardhi zao na kujitanulia fursa za uchumi.
Magere
Mugeta mkazi wa Lamadi mkoani Simiyu akipokea hati ya kumuliki ardhi
kutoka kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa
William Lukuvi.
Janet
Magige mkazi wa Lamadi mkoani Simiyu akipokea hati ya kumuliki ardhi
kutoka kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa
William Lukuvi.
Waziri
wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi
akiwasisitiza wakazi Lamadi mkoani Simiyu umuhimu wa kumiliki ardhi kwa
hati kwa kuwaonesha moja ya hati zinazotolewa kwa wananchi.
Wakazi
wa Lamadi mkoani Simiyu wakishangilia pamoja na Waziri wa Ardhi, Nyumba
na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi kwa kuwawezesha kupata
Hati za kumiliki Ardhi.
Waziri
wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi
akikagua moja ya faili katika masijala ya Ardhi ya Ilemela Mkoani Mwanza
akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongela (mwenye kofia).
Waziri
wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi
akikagua mfumo wa kodi wa manispaa ya Nyamagana mkoani Mwanza ili
kubaini wadaiwa wa kodi ya Ardhi.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi akiongea na wakazi wa Ilemela mkoani Mwanza.
Baadhi
ya wakazi wa Ilemela mkoani Mwanza wakimsikiliza kwa makini Waziri wa
Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa William Lukuvi alipokuja
kusikiliza kero zao za ardhi.
DKT. SHEIN AONGOZA SHEREHE ZA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI (MEI MOSI) MAHONDA, ZANZIBAR
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
(kushoto) akisalimiana na Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana,
Wanawake na Watoto, Mhe. Maudline Cyrus Castico alipowasili katika
viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja leo katika
Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
(kushoto) akisalimiana na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya
Wafanyakazi Zanzibar Maalim Khamis Mwinyi alipowasili katika viwanja vya
Mpira Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja leo katika Sherehe za
Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
(kushoto) akiwapungia Mkono Wafanyakazi mbali mbali waliopita mbele yake
kwa Maandamano wakati wa Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya
Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika viwanja vya Mpira Mahonda
Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja.
Baadhi
ya wafanyakazi wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba,Sheria,Utumishi wa Umma na
Utawala Bora wakipita kwa Maandamano mbele ya Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani)
wakati wa Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi
Duniani zilizofanyika leo katika viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya
Kaskazini "B" Unguja.
Wafanyakazi
na Wananchi kutoka shehia mbali mbali za Unguja walijumuika kwa
pamoja katika Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi
Duniani zilizofanyika leo katika viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya
Kaskazini "B" Unguja,wakipita kwa maandamano mbele ya Rais wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo
pichani) akiwa mgeni rasmi katika sherehe hizo.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
(kushoto) akiwapungia Mkono Wafanyakazi mbali mbali waliopita mbele yake
kwa Maandamano wakati wa Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya
Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika viwanja vya Mpira Mahonda
Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja akiwa na Viongozi mbali mbali.
Wafanyakazi
na Wananchi kutoka shehia mbali mbali za Unguja walijumuika kwa
pamoja katika Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi
Duniani zilizofanyika leo katika viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya
Kaskazini "B" Unguja,wakipita kwa maandamano mbele ya Rais wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo
pichani) akiwa mgeni rasmi katika sherehe hizo.
Wafanyakazi
wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar wakibeba Bango lenye Nembo la Idara
yao wakati wa maandamano katika Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya
Siku ya Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika viwanja vya Mpira
Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja,ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
(hayupo pichani).
Wafanyakazi
wa Benki ya Tanzania BOT wakibeba Bango lenye Nembo la Idara yao wakati
wa maandamano katika Sherehe za Kilele cha maadhimisho ya Siku ya
Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika viwanja vya Mpira Mahonda
Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja,ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
(hayupo pichani).
Wafanyakazi
wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar wakimpungia Mkono Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo
pichani),alipokuwa akipokea maandamano katika Sherehe za Kilele cha
maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika
viwanja vya Mpira Mahonda Wilaya ya Kaskazini "B" Unguja.Picha na Ikulu,
Zanzibar.
SMZ YAAHIDI KUUNGA MKONO JUHUDI ZA ZANUSO KATIKA SEKTA YA UJASIRIAMALI
Mshiriki
wa Mashindano ya ujasiriamali kwa Vyuo vikuu, Tahani Said akipokea
zawadi kutoka kwa Mgeni rasmi ambaye ni Mkurugenzi wa Viwanda Zanzibar,
Saleh Suleiman Hamad katika mashindano hayo yaliyoandaliwa na jumuiya
ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu Zanzibar(ZANUSO).
Mshiriki
wa Mashindano ya ujasiriamali kwa Vyuo vikuu, Issah Eugenio ambaye
mradi wake wa Handbags made in Jeans umechukua nafasi ya mwanzo,
akipokea zawadi kutoka kwa Mgeni rasmi ambaye ni Mkurugenzi wa Viwanda
Zanzibar, Saleh Suleiman Hamad katika mashindano hayo yaliyoandaliwa na
jumuiya ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu Zanzibar(ZANUSO).
Mgeni
rasmi Mkurugenzi wa Viwanda Zanzibar, Saleh Suleiman Hamad akiutubia
wakati wa kufunga mashindano yaliyoandaliwa na jumuiya ya Wanafunzi wa
Chuo Kikuu Zanzibar(ZANUSO) huko ZU kampasi kuu ya Tunguu.
Mlezi
wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Zanzibar(ZU), Mhadhiri wa Chuo
hicho Juma Rashid Khamis wakati akizungumza katika uzinduzi wa
mashindano ya miradi ya Ujasiriamali kwa wanafunzi wa vyuo vikuu
Zanzibar yaliyofanyika katika kampasi ya chuo hicho huku Tunguu, Unguja.
Mkurugenzi
wa Kampuni ya SISI Consultants, Mohamed Wario ambayo ni miongoni mwa
wadhamini akitoa nasaha zake kwa wanafunzi walioshiriki katika
mashindano hayo yaliyoandaliwa na jumuiya ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu
Zanzibar(ZANUSO) huko ZU kampasi kuu ya Tunguu.
Picha ya pamoja ya washiriki wa mashindano hayo pamoja na Viongozi wa ZANUSO na ZU pamoja na mgeni rasmi.
Na Juma Farid, Zanzibar.
SERIKALI
ya Mapinduzi ya Zanzibar imeahidi kuendelea kuunga mkono juhudi
zinazofanywa na baadhi ya Jumuiya za wanafunzi wa Vyuo Vikuu nchini
zinazoonyesha nia ya kuthamini fani ya Ujasiriamali kama chanzo mbadala
cha kupunguza tatizo la Ajira nchini.
Ahadi
hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Viwanda Zanzibar, Saleh Suleiman Hamad
kwa Niba ya Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko Balozi Amina Salum
Ali Wakati akifunga warsha ya Mashindano ya miradi ya Ujasiriamali kwa
Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Zanzibar yaliyoandaliwa na Jumuiya ya Wanafunzi
wa Chuo Kikuu Zanzibar ( ZU) huko Kampasi Kuu ya Chuo hicho Tunguu.
Amesema
ubunifu ulionyeshwa na wanafunzi hao katika uandishi, mikakati na
bidhaa za miradi ya Ujasiriamali waliyoiwasilisha katika Mashindao hayo
inajenga ushawishi kwa serikali na mashirika mengine ya kimataifa
kuwaunga mkono ili wafikie malengo yao ya kujiajiri na kuwaajiri vijana
wengine wasiokuwa na ajira.
Amesema
bado wanafunzi wengi wanaohitimu elimu ya ngazi ya vyuo vikuu nchini
hawajatumia fursa zinazopatikana katika fani ya Ujasiriamali ambayo
imekuwa ikitegemewa na mataifa mbali mbali duniani kupunguza tatizo la
ajira hasa kwa vijana.
“
Nasaha zangu kwenu kabla ya kuanzisha mradi wowote fanyeni tathimini na
utafti wa kitaalamu kubaini aina ya ujasiriamali unaotaka kufanya una
maslahi gani na wateja wako wahitaji bidhaa za aina gani sambamba na
kuwa wabunifu wa kufanya miradi isiyofanana.”, alisema Katibu huyo.
Aidha
alieleza kwamba kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Masoko, Balozi Amina
Salum Ali serikali itaendelea kudhamini miradi itakayoonyesha ustawi na
maendeleo endelevu.
Pia
katika juhudi za kuwajengea uwezo wajasiriamali hao alieleza kwamba
serikali itashawishi makampuni na mashirika ya kimaita ya kibiashara
kufanya kazi kwa karibu na jumuiya hizo ili zipate soko la uhakika la
kuuzia bidhaa zao.
Hata
hivyo ametoa nasaha zake kwa wajasiriamali hao kutengeneza bidhaa bora
zitakazokubalika katika soko la kimataifa pamoja na kujiongeza kitaaluma
kupitia mafunzo mbali mbali ya fani hiyo.
Mapema
akizungumza Mlezi wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha
Zanzibar(ZU), Bw. Juma Rashid Khamis ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo
hicho aliwasihi washiriki wa mashindao hayo kuendelea kujifunza zaidi
kupitia kwa wajasiria mali wakongwe ili wapate ujuzi wa ziada wa
kukabiliana na ushindani wa bidhaa na miradi ya ujasiriamali ndani na
nje ya Zanzibar.
Naye
Mkurugenzi wa Kampuni ya SISI Consultants, Mohamed Wario aliwataka
Wasomi hao kutumia vizuri fursa hiyo ya ujasiria mali kwa kuangazia
sehemu tofauti ambazo bado hazijatumiwa vizuri kibiashara zikiwemo
Sekta ya Utalii, Uvuvi na Ufugaji ili kuzalisha bidhaa bora
zinazotokana na rasilimali hizo na kuzishindanisha katika soko la ndani
na nje ya nchi.
“
Kampuni ipo tayari kushirikiana na nyinyi wakati wowote lakini lazima
mjiongeze zaidi kufikia lengo la kufanya miradi bora na inayoendana na
mahitaji ya sasa ili mpate mafanikio zaidi”, alisisitiza Mkurugenzi
huyo.
Kwa
upande wake mshiriki wa mashindano hayo aliyeshindanisha mradi wa
usindikaji wa bidhaa aina ya Jam inayotumia kwa chakula cha mkate
iliyotengenezwa kwa matunda ya Maembe, Ehlam Ali Khamis alisema wazo la
kutengeza bidhaa hizo ni kutokana na kukosekana kwa matumizi mazuri ya
matunda hayo hasa wakati wa msimu wake hali inayosababisha kuharibika
kwa kukosekana kwa viwanda vya kusindika matunda hayo.
Akitoa
ufafanuzi juu ya Warsha hiyo, Mwanzilishi na Msimamizi wa Mashindano
hayo Jumuiya ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Zanzibar ZANUSO, Mohamed
Omar alifafanua kwamba awali mchakato huo ulishirikisha jumla ya vyuo
Sita na ulipopita mchujo vikabaki vitatu ambavyo ni Zanzibar University
(ZU), State University of Zanzibar(SUZA) na Summait University.
Mashindano
hayo wamepatikana washindi saba ambao wamepewa Zawadi mbali mbali
zikiwemo simu za Adroid, lakini nafasi ya kwanza ambayo imeshikiliwa na
Issah Eugenio kwa mradi wa Handbags Made in Jeans, nafasi ya pili ni
Ehlam Ali Khamis kwa mradi wa Mango Jam na Tatu Ibrahim ahmad abdalla na
Sabrina Khamis Machano wa mradi wa Teke knowlge solutions company
wote kutoka vyuo tofauti vilivyoshiriki kwa awatua hiyo.
Comments
Post a Comment