WAKILI ALIYEGHUSHI MHURI WA BENKI YA NMB APANDISHWA KIZIMBANI KISUTU
Mshtakiwa ambaye ni wakili wa kujitegemea, Godwin Muganyizi (kulia), akitoka kusikiliza kesi yake anayodaiwa kughushi mhuri wa Benki ya NMB na kujipatia kiasi cha Sh milioni 51.640 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. wakili huyu alitumia uwezo wake wa fedha kwa kuwashawish baadhi ya askari wa mahakama hiyo kumlinda ili picha yake isipatikane kwa usahihi alipokuwa akiingia mahakamani na wakati wa kusikilizwa kesi yake ambapo wapambe wake waliziba mlango wa kuingia kwenye chumba cha mahakama na kuwawia vigumu wapasha habari kuingia humu na kuwa kazi ya kuviziana kwenye kulido za mahakama hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella(kulia) akikimbia kwenye mashindano ya Rock City Marathon yaliyofanyika jijini Mwanza jana. Kulia ni Mameneja Masoko wa NMB – Josephine Kulwa na Mercy Nyange. NMB imetoa udhamini wa shilingi million 10 kwaajili ya kufanikisha mashindano hayo.
Msindi wa Kilometer 21 - Boy Chacha kutoka Mkoa wa Mara,akimaliza masindano ya Rock City Marathon,jijini Mwanza jana. NMB imetoa udhamini wa shilingi million 10 kwaajili ya kufanikisha mashindano hayo.
Wanafunzi wa shule mbalimbali za
msingi katika kanda ya ziwa wakiwa kwenye mbio za mashindano ya Rock City
Marathon yaliyofanyika jana Jijini Mwanza. NMB imetoa udhamini wa shilingi
million 10 kwaajili ya kufanikisha mashindano hayo.
Afisa Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa NMB –
Augustino Mbogella akinyanyua juu ufunguo wa Trekta tayari kabisa kumkabidhi
Mkuu wa Mkoa wa Mara – Dr Charles Mlingwa kwa niaba ya Wilaya ya Ushetu ya
Mkoani Shinyanga ambao ndio washindi wa zawadi ya meya ya mwaka 2016, zawadi
hiyo hutolewa kila mwaka na mkutano mkuu wa ALAT kwaajili ya meya aliyewaletea
wananchi wakje maendeleo zaidi. Trekta hilo limetolewa na NMB na lina thamani
ya shilingi Milioni 56 huku nia ikiwa kuchochea shgughuli za maendeleo katika
halmashauri mbalimbali huku faida ikiwa ni kuwanufaisha watanzania ambao ni
wateja wa NMB.
Afisa Mkuu wa Ukaguzi wa Ndani wa NMB – Augustino Mbogella akimkabidhi ufunguo wa trekta Mkuu wa Mkoa wa Mara – Dr Charles Mlingwa kwa niaba ya mshindi wa zawadi ya Meya bora wa Mwaka 2016 ambayo ni Halmashauri ya Ushetu Mkoani Shinyanga. Trekta hilo lililotolewa na NMB lina thamani ya shilingi Milioni 56 huku nia ikiwa kuchochea shgughuli za maendeleo katika halmashauri mbalimbali huku faida ikiwa ni kuwanufaisha watanzania ambao ni wateja wa NMB.
Mkuu wa Mkoa wa Mara – Dr Charles
Mlingwa akijaribu kuwasha trekta lililokabidhiwa kwake na benki ya NMB kwa
niaba ya Halmashauri ya Ushetu ya mkoani shinyanga ambao ndio washindi wa mwaka
huu wa zawadi ya meya bora. Trekta hilo lililotolewa na NMB lina thamani ya
shilingi Milioni 56 huku nia ikiwa kuchochea shgughuli za maendeleo katika
halmashauri mbalimbali huku faida ikiwa ni kuwanufaisha watanzania ambao ni
wateja wa NMB.
Comments
Post a Comment