Mabinti 11 wa marais wa Afrika wanaoongoza kwa urembo



Bona Mugabe
 


Faith Elizabeth Sakwe


Zahra Buhari


Isabel dos Santos

Brenda Biya

Thuthukile Zuma

Aya Abdel Fattah al-Sisi
 Ngina Kenyatta


Malika Bongo Ondimba
 



Ange Kagame
 



Princess Sikhanyiso Dlamini



BARA la Afrika licha ya matatizo lukuki yanayolikabili kijamii, uchumi na kisiasa bado limebarikiwa na vitu vingi ikiwamo wingi wa maliasili kuliko mabara yote duniani.
Ukiachana na maliasili, miongoni mwa vitu hivyo vingi ilivyobarikiwa ni urembo wa mabinti zake na ambao wana sifa tofauti tofauti zilizo maalumu na kuwafanya wavutie mbele ya macho ya hadhara.
Hata hivyo, ni watu wachache wanaotambua kuwa baadhi ya wakuu wa nchi pia wamebarikiwa kuwa na mabinti warembo na wasomi.
Hiyo ni pamoja na kwamba inafahamika wazi katika nafasi zao za uongozi hata kabla hawajawa marais huwawia rahisi kupata wake warembo wanaokuwa chimbuko la mabinti hao.
Wafuatao ni miongoni mwa mabinti 10 wa viongozi wakuu wa nchi za Afrika wanaotamba kwa urembo barani humu:
1. Bona Mugabe
Bona ni binti wa Rais wa Zimbabwe na Mwenyekiti wa sasa wa Umoja wa Afrika (AU), Robert Mugabe. Ameolewa kwa Simba Chikore. Alisomea uhasibu na masuala ya fedha katika Chuo Kikuu cha City cha Hong Kong na aliendelea na masomo yake katika masuala ya kibenki na fedha katika Taasisi ya Usimamizi ya Singapore. Kwa sasa anafanya kazi katika kampuni ya maziwa ya Alpha & Omega huko Mazowe, Zimbabwe.

2. Faith Elizabeth Sakwe
Ni binti mkubwa wa aliyekuwa Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan na Dame Patience. Kwa sasa ameolewa na Godswill Osim Edward. Wenzi hao wachanga walichumbiana mwaka jana.
3. Zahra Buhari
Huku akiingia madarakani rasmi Ijumaa iliyopita, Rais mpya wa Nigeria, Muhammadu Buhari naye ni miongoni mwa viongozi waliobarikiwa mabinti warembo-Zahra Buhari, ambaye ni mwanafunzi wa Utabibu katika Chuo Kikuu cha Surrey nchini Uingereza.
 4. Isabel dos Santos
Ni binti wa Rais wa Angola, José Eduardo dos Santos. Akiwa katika umri wa miaka 40, Dos Santos aliwahi kutajwa kama mwanamke pekee barani Africa aliye bilionea na pia mwenye umri mdogo; hii ni kwa mujibu wa Forbes. Serikali huhesabu taarifa hizo kama suala la ufahari wa taifa na ushahidi kwamba taifa hilo lenye watu milioni 21.47 kwa idadi ya mwaka 2013, limefika mahali pazuri baada ya kutokea katika vita ndefu ya wenyewe kwa wenyewe.

5. Brenda Biya
Binti wa Rais wa Jamhuri ya Cameroon pia anasifiwa katika mitandao maarufu ya jamii na hufuatiliwa na kundi la wafuasi 3,000. Brenda alifungua akaunti yake ya Instagram mwaka 2012 na huchangia picha zake za uanafunzi kila siku na maisha ya familia, mawazo na mitazamo.

6. Thuthukile Zuma
Ni binti mdogo kati ya wanne wa Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma kutoka kwa aliyekuwa mkewe Nkosazana Dlamini-Zuma, ambaye kwa sasa ni Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika (AU). Thuthukile ni mnadhimu mkuu katika Idara ya Mawasiliano na Huduma za Posta Afrika Kusini.  Anaonekana mrembo kwa staili yake ya ukataji nywele fupi.
7. Aya Abdel Fattah al-Sisi
Ni binti pekee wa Abdel Fattah al-Sisi, mkuu wa zamani wa jeshi la Misri, ambaye kwa sasa ni Rais wa Misri. Ni mwenye mvuto, heshima na adabu.

8. Ngina Kenyatta
Ni binti wa Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta. Mrembo huyo, ambaye mara nyingi hugonganisha vichwa katika mitandao ya kijamii nchini Kenya kuhusu mahusiano yake ya kimapenzi. Alichukua jina hilo kutoka kwa bibi yake, Mama Ngina Kenyatta. Anahesabiwa sana kama mtu mwenye kujichanganya mno na jamii na mwingi wa utata.
9. Malika Bongo Ondimba
Malika Bongo Ondimba(32), ni binti pekee wa Rais wa Gabon, Ali Bongo Ondimba. Msichana huyo anaelezwa kama ‘mwenye bidii ya kazi’ na familia yake.

10. Ange Kagame
Ange ni mtoto wa pili na binti pekee wa Rais wa Rwanda, Paul Kagame. Ni mhisani na amekuwa akihusika na shughuli za uwezeshaji wanawake, elimu, upunguzaji umasikini na kinga za maradhi.
Ange alichomoza zaidi akiteka vichwa vya habari duniani wakati alipoambatana na baba yake wakati wa mkutano wa Marekani na viongozi wa Afrika mwaka jana kwa urembo na urefu kumzidi baba yake. Ange alizaliwa Septemba 8, 1993, mjini Brussels, Ubelgiji.
11. Princess Sikhanyiso Dlamini
Binti mfalme Sikhanyiso, alizaliwa Septemba Mosi 1987, ni binti mkubwa wa Mfalme Mswati III wa Swaziland. Ni mtoto wake wa kwanza kati ya



Comments

Popular posts from this blog

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.

AMANI YETU TUILINDE NAIBU WAZIRI CHANDE AZUNGUMZA KATIKA IJITIMAI JIJINI DODOMA