Posts

Showing posts from October, 2025

MGEJA ASEMA URAIS SI MAJARIBIO, DKT. SAMIA ANATOSHA

Image
  Na Mwandishi Wetu, Kahama na Nzega Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na mwanasiasa mkongwe nchini, Ndugu Khamisi Mgeja (anayeongea pichani), amewatahadharisha Watanzania kutofanya makosa kwa kuchagua wagombea wa urais wasiokuwa na uzoefu wa kiuongozi na ambao hawajawahi kufanya kazi yoyote ya serikali, hata katika ngazi za mitaa, akisema kufanya hivyo ni kosa la kujitakia. Mgeja alikumbusha usia wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, aliyewahi kusema kuwa kiongozi bora wa nchi hii hatatoka nje ya CCM, bali atatoka ndani ya CCM. Amesema kuwa kiongozi huyo si mwingine bali ni Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye ni chaguo sahihi la Watanzania. Mgeja alitoa kauli hiyo katika mikutano ya kampeni iliyofanyika katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Nzega mkoani Tabora na Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, alipokuwa akinadi wagombea wa ubunge akiwemo Hussein Bashe (Nzega) na Benjamini Ng’ayiwa (Kahama Mjini). Akiwa katika vijiji vya Nyanhembe na Ufala wilayani Kahama, Mgeja aliw...

WATANZANIA WATAKIWA KUIUNGA MKONO JKT QUEENS

Image
Mkuu wa JKT Meja Jenerali Rajabu Mabele amewataka watanzania kuiunga mkono timu ya JKT Queens inayokwenda kuliwakilisha Taifa na ukanda wa CECAFA katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika kwa upande wa soka la wanawake. Meja Jenerali Mabele ameyasema hayo mara baada kumalizika kwa zoezi la upangaji wa makundi liliofanyika Cairo nchini Misri Octoba 27, 2025 ambapo JKT Queens imepangwa Kundi B likijumuisha Bigwa mtetezi TP Mazembe kutoka DR Congo, Asec Mimosas kutoka Ivory Coast na Gaborone United kutoka Botswana. Michuano hiyo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Novemba 8, 2025 hadi Novemba 21, 2025. Aidha Meja Jenerali Mabele ametoa wito kwa watanzania kushabikia timu hiyo ya kizalendo yenye wachezaji wazawa kama inavyofanyika mara zote kwa kwa timu za Simba na Yanga zinapowakilisha nchi. JKT Queens inawakilisha Tanzania na Ukanda wa CECAFA kwa ujumla kwenye michuano hiyo ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa upande wa Wanawake ambapo jumla ya timu 8 zitashiriki. Wachezaji wa timu hiyo w...

PROFESA MWAMFUPE AHITIMISHA KAMPENI KWA KUWAOMBA WANANCHI WAKAPIGE KURA

Image
Mgombea Udiwani Kata ya Madukani Dodoma mjini  profesa Davis  Mwamfupe    ambaye pia alikuwa Mstahiki Meya wa jiji hilo , akizungumza na wanahabari baada ya kuhitimisha kampeni zake alizofanya leo kutembelea wapiga kura katika eneo lake  lote ambalo sehemu kubwa ni sehemu ya biashara na makazi kidogo. Akizungumza kwa kujiamini aliwaomba wananchi wa kata yake wajitokeze kwa wingi mapema kwenda kupiga kura  baada ya kupiga na kulejea majumbani mwao kusubili matokeo, hakuna wa kuwazuia kupiga kura vyombo vya ulinzi na usalama vipo macho kwa lolote. "Nawaombeni wananchi wenzagu tujitokeze kwa wingi kwenda kukitendea haki chama chetu kuwachagua wagombea wote kwa kipindi cha miaka mitano  tena ni CCM inayoaminika".alisema Mwamfupe.  Profesa Mwamfupe, akizungumza huku akiwa amezungukwa na baadhi ya viongozi wa kata hiyo Mwenyekiti wa CCM Kata hiyo, a,izungumza na wanahabari  baada ya kuhitimishwa kampeni  

RIDHIWANI AENDELEA NA MIKUTANO YA KAMPENI JIMBONI KWAKE

Image
Kampeni zimeendelea kata ya Kiwangwa ambapo Mgombea Ubunge Wa CCM jimbo la Chalinze Ndg. Ridhiwani Kikwete amenadi Ilani ya CCM ya Mwaka 2025/30 ambapo pia amemuombea kura Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Samia Suluhu Samaha na Diwani wa kata hiyo Ndugu Malota Hussein Kwaga. Katika mikutano hiyo, mgombea Ubunge wa Chalinze ndg. Ridhiwani Kikwete alimuelezea Dr. Samia kuwa ni mtu mwenye maono na mwanamapinduzi wa kweli ambaye amefanikisha yale ambayo wengi walidhani yasingewezekani. Amefanikisha usambazaji wa Umeme Chalinze kwa vijiji vyote na vitongoji zaidi ya asilimia 75, maji zaidi ya asilimia 94, Elimu bure,kilimo na mengineyo mengi.  Kampeni zinaendelea katika jimbo la Chalinze.# KaziNaUtuTunasongaMbele  

MWAMBEGELE ATEMBELEA VITUO VYA KUPIGIA KURA NCHINI

Image
KATAVI                   UCHAGUZI                               OKTOBA 27, 2025 Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, MHE. JAJI WA RUFANI JACOBS MWAMBEGELE ametembelea na kujionea maandalizi ya ujenzi wa vituo 83 kati ya 90 vya Wapiga Kura vilivyotengwa maalum kwaajili ya wakazi wa zilizokuwa Kata za Ilangu, Ipwaga, Bulamata na Mishamo zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi ambazo zilifutwa na Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa kwa mujibu wa Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya), Sura 287.  Jaji Mwambegele alitembelea eneo hilo la Kata ya Tongwe katika Kitongoji cha Luhafwe akiwa ameambatana na Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Katavi, Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Tanganyika na watendaji wengine wa uchaguzi kuangalia maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani uliopangwa kufanyika Oktoba 29, 2025 nch...

Rais Samia Suluhu Hassan apokea Ujumbe Maalum kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Mhe. Felix Antoine Tshisekedi, Ikulu Jijini Dar es Salaam

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Mjumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mhe. Felix Antoine Tshisekedi, na Waziri wa Ushirikiano wa Kikanda wa Nchi hiyo Mhe. Floribert Anzuluni, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 24 Oktoba, 2025.        Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akipokea Ujumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Congo (DRC) Mhe. Felix Antoine Tshisekedi, uliowasilishwa kwake na Mjumbe Maalum na Waziri wa Ushirikiano wa Kikanda wa Nchi hiyo Mhe. Floribert Anzuluni, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 24 Oktoba, 2025. 1   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika Picha ya pamoja na Mjumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mhe. Felix Antoine Tshisekedi, na Waziri wa Ushirikiano wa Kikanda wa Nchi hiyo Mhe. Floribert Anzuluni, mara baada ya mazungumzo yao Ikulu Jijini Dar es Sala...

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAELEKEZO YA KISERA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

Image
 Mkurugenzi wa tume huru ya uchaguzi  Kailima

Mjumbe wa Kamati ya Ushindi UWT (Nyanda za Juu Kusini) 🌿 Sophia Mwakagenda akiwa mzigoni🌿

Image
  Mjumbe wa Kamati ya Ushindi ya UWT (Nyanda za Juu Kusini) 🌿 Sophia Mwakagenda , akiwa na Mgombea ubunge jimbo la Njombe mjini  Deo Mwanyika  akiwa Katika mwendelezo wa kampeni za elimu na uhamasishaji zilizofanyika Jimbo la Njombe Mjini , Sophia Mwakagenda amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi kwa amani na umoja, kwa kumpigia kura Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , pamoja na Mhe. Deo Mwanyika, Mgombea Ubunge wa Njombe Mjini, na wagombea wote wa chama katika ngazi mbalimbali. Amesisitiza kuwa kura ni silaha ya maendeleo na chachu ya kuendeleza amani na ustawi wa taifa, akiwataka wananchi kuendeleza imani kwa viongozi wanaothibitisha kwa vitendo dhamira ya kuwatumikia wananchi. 🤜 “Tumuunge mkono Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan na Mhe. Deo Mwanyika ; viongozi wanaosimamia maendeleo ya watu kwa vitendo.” alisema Mwakagenda

WADAU WA ELIMU WAKUTANA JIJINI DODOMA KUJADILI MAGEUZI YA SEKTA HIYO

Image
Serikali ya Awamu ya Sita chini  imepiga hatua kubwa katika mageuzi ya sekta ya elimu nchini, baada ya kutangaza rasmi kuwa elimu ya lazima sasa itakuwa miaka 10 kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne. Hatua hiyo inalenga kuhakikisha kila mtoto wa Kitanzania anapata fursa sawa ya kujifunza, kukuza maarifa na kupata ujuzi utakaomwezesha kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa. Akizungumza  Oktoba 22, 2025, jijini Dodoma katika mkutano wa mwaka wa tathmini ya pamoja ya sekta ya elimu, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu, Prof. Daniel Mushi (pichani juu), alisema kuwa maboresho hayo makubwa yatahitaji ushirikiano wa karibu kati ya serikali, wadau wa elimu na jamii kwa ujumla. “Mageuzi haya ni ya kimkakati. Tunataka elimu ya lazima iwe jumuishi, yenye ubora na inayomwandaa mwanafunzi kuwa mbunifu na mwenye mchango chanya katika maendeleo ya taifa. Tunatambua ipo haja ya kuongeza miundombinu, walimu na sera shirikishi,” amesema Pro...

📌 SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI.

Image
  Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano, ambapo baadhi ya minara hiyo itajengwa katika maeneo ya mipakani, mbuga za wanyama, na njia kuu za reli za SGR na TAZARA. Hatua hii inalenga kuhakikisha huduma za mawasiliano zinapatikana katika maeneo yote yenye umuhimu wa kimkakati kwa usalama, utalii na maendeleo ya Taifa. Mtendaji Mkuu wa UCSAF, Mhandisi Peter Mwasalyanda, amesema utekelezaji wa awamu hiyo mpya unafuatia mafanikio makubwa ya mradi wa awali wa minara 758, ambao umefikia zaidi ya asilimia 98 ya utekelezaji. Ameeleza kuwa kukamilika kwa mradi huo kumechangia kupunguza kwa kiasi kikubwa pengo la mawasiliano katika maeneo ya vijijini na pembezoni. Jumla ya vijiji 1,407 ambavyo awali havikuwa na mawasiliano, sasa vinafikishiwa huduma hiyo muhimu, hatua inayoboresha maisha ya wananchi na kuongeza fursa za kiuchumi. Aidha, Mhandisi Mwasalyanda ameongeza kuwa utekelezaji wa miradi ...

MWAKAGENDA AKISAKA KURA ZA WAGOMBEA WA CCM JIMBONI MAKAMBAKO

Image
Mbunge  Mstaafu Sophia Mwakagenda, akiwa jukwaani akimuombea kura   Mgombea   Ubunge Jimbo la Makambako   Daniel Godfrey Chongolo, pamoja na kura za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na madiwani wa jimbo hilo. Akizungumza kwa kujiamini huku akishangiliwa na wananchi waliojitokeza katika mkutano huo aliwaomba wanamakambako kutofanya kosa siku ya 29.10.2025 kujihimu mapema kwenda kupiga kura kuwapa kura za ndiyo wagombea wote wa Chama cha Mapinduzi, aliwaambia kelele za mpangaji hazimzuii mwenye nyumba kulala alibainisha kuwa kelele za wapinzani zisiwababaishe nchi ipo salama  na maendeleo makubwa yanakuja  wakiamini chama CCM.  "Nawaombeni wanaccm wenzangu na wasiokuwa wanaccm Mgombea Dkt. Samia, hatanii akisema atawaletea mandelea makubwa wananchi wa Tanzania  anasema kweli hebu tumwamini muone kazi yake mwanamama yoyote hawi muomgo hebu tujitokeze tumpe kura zote",alisema Mwakagenda. Kuhusu Chongolo, aliwaomba waanamakambako wasipoteze muda kufi...

TAARIFA AYA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI LEO 18.10.2025

Image
Mkurugenzi wa Tume hiyo  

DODOMA WASEMA AMANI KWANZA

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rose-Mary Senyamule, akiongoza Matembezi ya Kuhamasisha Amani na kuliombea Taifa, matembezi hayo yalianza leo asubuhi  Lango la Bunge Mkabala na  Shule ya Sekondari Dodoma  hadi viwanja vya Nyerere Square. Matembezi hayo pia  yaliambatana na uchunguzi wa matibabu ya magonjwa ya Moyo, Macho, Figo, Saratani na Selimundo. Uchunguzi huo uliendeshwa na madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Benjamini Mkapa wakiongozwa na Mkurugenzi wake Profesa Abel Makubi..Makundi yote ya jumuiya ya Wanadodoma  yakiongozwa na viongozi wake au wawakilishi wao kila aliyesimama alikuwa akiomba uchaguzi Mkuu  uwe wa amani, bila amani hakitafanyika kitu. Akihitimisha Mkuu wa Mkoa alisema Serikali ipo makini wananchi mtoe taarifa  kama kuna mtu au kikundi cha watu watakachokibaini kwamba kinataka kuhatarisha amani ili washugulike naye serikali imejipanga  ipo makini na wasithumubu chamoto watakiona watakaothubutu, alibainisha Senyamule.