Posts

Showing posts from October, 2025

Rais Samia Suluhu Hassan apokea Ujumbe Maalum kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Mhe. Felix Antoine Tshisekedi, Ikulu Jijini Dar es Salaam

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Mjumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mhe. Felix Antoine Tshisekedi, na Waziri wa Ushirikiano wa Kikanda wa Nchi hiyo Mhe. Floribert Anzuluni, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 24 Oktoba, 2025.        Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akipokea Ujumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Congo (DRC) Mhe. Felix Antoine Tshisekedi, uliowasilishwa kwake na Mjumbe Maalum na Waziri wa Ushirikiano wa Kikanda wa Nchi hiyo Mhe. Floribert Anzuluni, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 24 Oktoba, 2025. 1   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika Picha ya pamoja na Mjumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mhe. Felix Antoine Tshisekedi, na Waziri wa Ushirikiano wa Kikanda wa Nchi hiyo Mhe. Floribert Anzuluni, mara baada ya mazungumzo yao Ikulu Jijini Dar es Sala...

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAELEKEZO YA KISERA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

Image
 Mkurugenzi wa tume huru ya uchaguzi  Kailima

Mjumbe wa Kamati ya Ushindi UWT (Nyanda za Juu Kusini) 🌿 Sophia Mwakagenda akiwa mzigoni🌿

Image
  Mjumbe wa Kamati ya Ushindi ya UWT (Nyanda za Juu Kusini) 🌿 Sophia Mwakagenda , akiwa na Mgombea ubunge jimbo la Njombe mjini  Deo Mwanyika  akiwa Katika mwendelezo wa kampeni za elimu na uhamasishaji zilizofanyika Jimbo la Njombe Mjini , Sophia Mwakagenda amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi kwa amani na umoja, kwa kumpigia kura Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , pamoja na Mhe. Deo Mwanyika, Mgombea Ubunge wa Njombe Mjini, na wagombea wote wa chama katika ngazi mbalimbali. Amesisitiza kuwa kura ni silaha ya maendeleo na chachu ya kuendeleza amani na ustawi wa taifa, akiwataka wananchi kuendeleza imani kwa viongozi wanaothibitisha kwa vitendo dhamira ya kuwatumikia wananchi. 🤜 “Tumuunge mkono Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan na Mhe. Deo Mwanyika ; viongozi wanaosimamia maendeleo ya watu kwa vitendo.” alisema Mwakagenda

WADAU WA ELIMU WAKUTANA JIJINI DODOMA KUJADILI MAGEUZI YA SEKTA HIYO

Image
Serikali ya Awamu ya Sita chini  imepiga hatua kubwa katika mageuzi ya sekta ya elimu nchini, baada ya kutangaza rasmi kuwa elimu ya lazima sasa itakuwa miaka 10 kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne. Hatua hiyo inalenga kuhakikisha kila mtoto wa Kitanzania anapata fursa sawa ya kujifunza, kukuza maarifa na kupata ujuzi utakaomwezesha kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa. Akizungumza  Oktoba 22, 2025, jijini Dodoma katika mkutano wa mwaka wa tathmini ya pamoja ya sekta ya elimu, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu, Prof. Daniel Mushi (pichani juu), alisema kuwa maboresho hayo makubwa yatahitaji ushirikiano wa karibu kati ya serikali, wadau wa elimu na jamii kwa ujumla. “Mageuzi haya ni ya kimkakati. Tunataka elimu ya lazima iwe jumuishi, yenye ubora na inayomwandaa mwanafunzi kuwa mbunifu na mwenye mchango chanya katika maendeleo ya taifa. Tunatambua ipo haja ya kuongeza miundombinu, walimu na sera shirikishi,” amesema Pro...

📌 SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI.

Image
  Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano, ambapo baadhi ya minara hiyo itajengwa katika maeneo ya mipakani, mbuga za wanyama, na njia kuu za reli za SGR na TAZARA. Hatua hii inalenga kuhakikisha huduma za mawasiliano zinapatikana katika maeneo yote yenye umuhimu wa kimkakati kwa usalama, utalii na maendeleo ya Taifa. Mtendaji Mkuu wa UCSAF, Mhandisi Peter Mwasalyanda, amesema utekelezaji wa awamu hiyo mpya unafuatia mafanikio makubwa ya mradi wa awali wa minara 758, ambao umefikia zaidi ya asilimia 98 ya utekelezaji. Ameeleza kuwa kukamilika kwa mradi huo kumechangia kupunguza kwa kiasi kikubwa pengo la mawasiliano katika maeneo ya vijijini na pembezoni. Jumla ya vijiji 1,407 ambavyo awali havikuwa na mawasiliano, sasa vinafikishiwa huduma hiyo muhimu, hatua inayoboresha maisha ya wananchi na kuongeza fursa za kiuchumi. Aidha, Mhandisi Mwasalyanda ameongeza kuwa utekelezaji wa miradi ...

MWAKAGENDA AKISAKA KURA ZA WAGOMBEA WA CCM JIMBONI MAKAMBAKO

Image
Mbunge  Mstaafu Sophia Mwakagenda, akiwa jukwaani akimuombea kura   Mgombea   Ubunge Jimbo la Makambako   Daniel Godfrey Chongolo, pamoja na kura za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na madiwani wa jimbo hilo. Akizungumza kwa kujiamini huku akishangiliwa na wananchi waliojitokeza katika mkutano huo aliwaomba wanamakambako kutofanya kosa siku ya 29.10.2025 kujihimu mapema kwenda kupiga kura kuwapa kura za ndiyo wagombea wote wa Chama cha Mapinduzi, aliwaambia kelele za mpangaji hazimzuii mwenye nyumba kulala alibainisha kuwa kelele za wapinzani zisiwababaishe nchi ipo salama  na maendeleo makubwa yanakuja  wakiamini chama CCM.  "Nawaombeni wanaccm wenzangu na wasiokuwa wanaccm Mgombea Dkt. Samia, hatanii akisema atawaletea mandelea makubwa wananchi wa Tanzania  anasema kweli hebu tumwamini muone kazi yake mwanamama yoyote hawi muomgo hebu tujitokeze tumpe kura zote",alisema Mwakagenda. Kuhusu Chongolo, aliwaomba waanamakambako wasipoteze muda kufi...

TAARIFA AYA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI LEO 18.10.2025

Image
Mkurugenzi wa Tume hiyo  

DODOMA WASEMA AMANI KWANZA

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rose-Mary Senyamule, akiongoza Matembezi ya Kuhamasisha Amani na kuliombea Taifa, matembezi hayo yalianza leo asubuhi  Lango la Bunge Mkabala na  Shule ya Sekondari Dodoma  hadi viwanja vya Nyerere Square. Matembezi hayo pia  yaliambatana na uchunguzi wa matibabu ya magonjwa ya Moyo, Macho, Figo, Saratani na Selimundo. Uchunguzi huo uliendeshwa na madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Benjamini Mkapa wakiongozwa na Mkurugenzi wake Profesa Abel Makubi..Makundi yote ya jumuiya ya Wanadodoma  yakiongozwa na viongozi wake au wawakilishi wao kila aliyesimama alikuwa akiomba uchaguzi Mkuu  uwe wa amani, bila amani hakitafanyika kitu. Akihitimisha Mkuu wa Mkoa alisema Serikali ipo makini wananchi mtoe taarifa  kama kuna mtu au kikundi cha watu watakachokibaini kwamba kinataka kuhatarisha amani ili washugulike naye serikali imejipanga  ipo makini na wasithumubu chamoto watakiona watakaothubutu, alibainisha Senyamule.