Posts

WAZIRI WA AFYA MOHAMED MCHENGERWA AWASILISHA BAJETI YA WIZARA LEO BUNGENI

Image
Wageni wa Waziri kutoka jimboni kwake wakipiga picha na mwenyeji wao baada ya kuwasilisha bajeti yake Waziri wa Afya Mohamed Mchengerwa, akiomba Sh Trioni  1.8 kwa ajili ya Bajeti ya Wizara ya Afya kwa Mwaka 2026 na 2027, wabunge wengi wakichangia bajeti ya wizara yake wameonyesha nia ya kumuunga mkono kutokana na  juhudi anazozichukua  kuhudumia wananchi wa Tanzania pamoja na ujenzi wa hospitali mpya mikoani na juhudi yake ya kuonyesha nia ya ujenzi wa Hospitali  ya Taifa ya Muhimbili ambayo itakuwa ya Mfano nchini,  iliyopo sasa imepitwa na wakati. Hata hivyo baadhi ya wabunge wakichangia wameomba sasa muda umefika wa kuanza kujengwa Hospitali za rufaa kwa kanda ili kupunguza misongamano katika Hiospitali ya Muhimbili  

WABUNGE WAPONGEZA UJENZI WA MUHIMBILI MPYA NA MFUKO WA BIMA YA AFYA

Image
Mwenyekiti wa Bunge Deo Mwanyika, akifungua semina ya wabunge iliyokuwa ikizungumzia ujenzi wa Hospitaliu ya  Taifa ya Muhimbili kando kando mwa majengo ya zamani yaliyodumu kwa muda wa miaka zaidi ya 100 na Mfuko wa Bima ya Afya kuanza kwake.  Waziri wa Afya Mohamed Mchengelwa, akisoma hotuba  katika semina ya wabunge  iliyofanyika ukumbi wa Msekwa jijini Dodoma.     Wabunge wakisikiliza wachangiaji Ramani inayoonyesha majengo yatakavyokuwa baada ya kukamilika ujenzi wake Mbunge wa Misungwi, Silvery Luboja, akichangia katika semina hiyo akisema ujenzi wa Hospitali hiyo hauepukiki lakini muda umefika sasa wa kujenga Muhimbili zingine katika mikoa ili kuepusha msongamano katika hospitali hiyo, kuhusu Bima ya Afya kunahitajika marekebisho makubwa nianzuri  ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni njema lakini kunaupigaji sana kwa baadhi ya watumishi na wenye hospitali ambao hupokea wagonjwa wa bima ya afya Mbunge Mariam Kisanji, akiitaka Serikali kuchuk...