PROF. SHEMDOE: SERIKALI IMEWEKEZA BILIONI 2.8 KUBORESHA AFYA, BARABARA, ELIMU YA AMALI GAIRO
Na. OWM–TAMISEMI, Gairo Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imewekeza Shilingi bilioni 2.8 katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya Kituo cha Afya Chanjale, Barabara ya Confort Pub–Magoweko na Shule ya Amali Kwipipa, hatua iliyoboresha upatikanaji wa huduma za afya, kurahisisha usafiri na usafirishaji pamoja na kupanua fursa za elimu ya amali kwa wananchi wa wilaya ya Gairo. Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, Julai 17, 2026 katika kijiji cha Kwipipa, kata ya Rubeho, wilaya ya Gairo, baada ya kukagua na kuweka mawe ya msingi katika miradi hiyo ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma. Prof. Shemdoe amesema miradi hiyo inaonesha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora karibu na maeneo wanayoishi kupitia uwekezaji unaogusa m...