Posts

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA AWASILISHA BAJETI YA WIZARA YAKE LEO BUNGENI JIJINI DODOMA

Image
Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Homera, akisoma bajeti ya wizara yake bungeni leo ambapo  pamoja na mambo mengine alisema  Waziri  utekelezaji wa Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026, Mpango wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara na Taasisi zilizoko chini ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2026/2027, tarehe 24 Aprili, 2026 Bungeni, Jijini Dodoma. Dkt. Homera amesema kuwa Upekuzi huo umeimarisha ulinzi wa maslahi ya Serikali, kupunguza hatari za hasara za kifedha, kuongeza uwajibikaji katika matumizi ya fedha za umma, na kuhakikisha miradi ya maendeleo inatekelezwa kwa kuzingatia sheria na mikataba yenye tija kwa Taifa. *“Mhe. Mwenyekiti vilevile, Ofisi ilikamilisha upekuzi wa Hati za Makubaliano (Memoranda of Understanding) 396.”* Amesema Dkt. Homera Aidha, Waziri wa Katiba na Sheria ameeleza kuwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imesimamia mikataba 2,821 iliyosainiwa kati ya Serikali na wadau mbalimbali. Pia Ofisi ilipokea maombi ya kuvunja mikataba saba (7) am...

BAJETI YA WIZARA YA NISHATI YAPITISHWA NA WABUNGE KWA FURAHA ZOTE

Image
Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, akihitimisha bajeti ya wizara yake leo bungeni jijini Dodoma ,amabapo aliwaambia wabunge wote kwamba maombi na maoni yao wakikutana mwakani yatakuwa yametekelezwa  yote, kwani dhamila  ya rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuona wananchi wa nchi hii wanapata umeme wa uhakika na kupikia nishati safi  

PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI LEO BUNGENI JIJINI DODOMA

Image
Spika wa Bunge  Mussa Azzan Zungu (kulia), akimsikiliza kwa makini  Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza  Johari, mazungumzo hayo yalifanyikia ndani ya ukumbi wa bunge leo. Bunge lilikuwa likisimamiwa na Mwenyekiti Deo Mwanyika Jesca Magufuli (kulia), akimweleza jambo Waziri Angella Kairuki Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira)  Reuben Kwagilwa, akijibu maswali ya wabunge  Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir, akijibu maswali ya wabunge Mkurugenzi   Mtendaji wa   CRDB   Bank Foundation   Tuli Mwambapa, akitambulishwa bungeni