Posts

WANANCHI WAMIMINIKA BANDA LA BUNGE KATIKA MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

Image
Afisa wa Bunge Jeremia Wambura, akiwaeleza umuhimu wa Siwa wananchi waliotembelea banda la Bunge  katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa umma inayomalizika kesho. Wananchi mbalimbali walimiminika katika banda hilo kujionea mavazi yanayovaliwa na Spika, Naibu Spika na Wenyeviti wa Bunge, Aidha baadhi walipenda kufahamu ni nani anayetakiwa kutembelea bunge ambapo walijibiwa ni mwananchi yoyote yule  ilimladi aombe kulitembelea, waliweza kujionea majalida mbalimbali ya bunge  pia kujionea picha za maspika Naibu Spika Wenyeviti waliowahi waliongoza Bunge hilo Tangu mwanzo wa Uhuru hadi sasa. Afisa wa Bunge Debora Sanja, akiwaeleza jambo  wananchi waliofika katiba banda hilo Mavazi ya Spika, Naibu Spika na Wenyeviti wa Bunge  

MATUKIO YA PICHA KATIKA CRDB BUNGE BONANZA SHUHUDIA KATIKA VIWANJA VYA JAMHURI JIJINI DODOMA

Image
Washindi wa shindano la kukamata kuku wakionyesha baada ya kuwakamata na kuwazidi ujanja washindani wenzao Mbunge wa Monduli, Joseph Isack 'Mmasai' (AK .KADOGOO) WATATU TOKA KUSHOTO akishiriki shindano la kula wali maharage na kuibuka mshindi katika Bonanza la CRDB Bank Bunge lilioandaliwa na Wizara ya Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma leo Juni 20, 2026' Katika Bonanza hilo ambalo mgeni rasmi alikuwa Spika wa Bunge Mussa Azzan Zungu aliye wakilishwa na Naibu wake, Daniel Sillo ilishirikisha pia michezo ya kufukuza kuku, kukimbia na gunia, kunywa soda, pete, wavu, soka, riadha, bao na draft.  

MBUNGE WA MBOGWE FAGASON AONYESHA UFAHARI WA WATOTO WAKE BUNGENI. WABUNGE WAMSHANGILIA

Image
Mbunge wa Mbogwe mkoani Geita, Fagason Nkingwa, ameleta watoto wake leo bungeni wapata 15, amewataka vijana wasiogope kuzaa kwani Bara la Afrika ni kubwa linahitaji nguvu kazi. Mwenyekiti wa Bunge Deo Mwanyika,, akiwatambulisha watoto hao alisema alimwandikia barua kwamba watoto wake wapo 15 wamekuja kutembelea bunge kwa kujifunza, ilikuwa furaha na velegele vilitawala ukumbi wa wabunge  na badae walienda kutembelea maeneo mbalimbali ya bunge. Akizungumza na mwandishi wetu Fagason alisema anamkumbuka, marehemu Dkt. John Magufuli, aliwaomba Watanzania wazae yeye anajenga Mashule na Hospitali na kujenga Mabarabara, Fagason alitolea mfano wa baadhi ya nchi za Ulaya hivi sasa wanatoa zawadi kwa vijana wao kuzaana kwani wamebakia wazee nguvu kazi imeisha wanataka kutawaliwa na vijana kutoka mataifa mengine waliyoyatawala siku za nyuma.