KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE NISHATI NA MADINI YARIDHISHWA NA KIWANDA CHA NGUZO ZA ZEGE
*Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita * Yaipongeza TANESCO kwa usimamizi wa Ujenzi wa Kiwanda hicho * Shilingi Bilioni 8 zawekezwa ujenzi wa Kiwanda @@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@ Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeridhishwa na Ujenzi wa Kiwanda cha Zege kinachomilikiwa na kampuni tanzu ya TANESCO ya kuzalisha nguzo za zege kilichopo katika Mkoa wa Tabora wakati wa ziara yao ya kikazi Mkoani humo tarehe 12 Machi, 2026. Akizungumza baada ya ziara hiyo Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mwanamama shupavu Mbunge wa Bagamoyo, Subira Mgallu ameeleza kuridhishwa na hatua ya kukamilika kwa Kiwanda hicho kilichoanza uzalishaji na kuwaelekeza Wizara ya Nishati na TANESCO kukisimamia kiwanda hicho kiendelee kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa na kuzalisha faida. “Kwa niaba ya Kamati tumeridhika na kazi kubwa iliyofanyika katika kiwanda hiki ambacho kimekamilika na uzalishaji umeanza, tunatoa rai kwa Wizara na TANESCO kuendelea kusimamia kiwanda hiki ...