Posts

CAG KICHERE AMKABIDHI RAIS SAMIA RIPOTI YA UKAGUZI KWA MWAKA 2024 NA 2425

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa Mwaka wa Fedha 2024/25 kutoka kwa Charles Kichere, Ikulu jijini Dar es Salaam, tarehe 30 Machi, 2026. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na  Ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa Mwaka wa Fedha 2024/25, Taarifa ya Mwaka ya Utendaji Kazi wa Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) pamoja na Taarifa ya Mwaka ya Utendaji Kazi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA),  baada ya kuzipokea leo Ikulu jijini Dar es Salaam. @@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@ Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Dkt. Charles Kichere, Machi 30, 2026, amewasilisha Ripoti Kuu ya mwaka wa fedha 2024/2025 kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Ikulu jijini Dar es Salaam ambapo amesema kuwa deni la Serikali bado ni himilivu na lipo ndani ya viwango salama...

MASHIMO KATIKA BARABARA YA DODOMA SINGIDA KAZI YA TANROADS KUYAZIBA----- MHANDISI MLAVI

Image
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Ephatar Mlavi (pichani),amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, itaendelea kuziba mashimo yaliyopo katika barabara ya kutoka Dodoma hadi Simgida, ambapo amebainisha kwamba Serikali ya Rais Samia   imeendelea kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika miundombinu ya barabara na madaraja ili kukuza uchumi wa taifa na kurahisisha usafirishaji. Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dodoma, katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO amesema kuwa uwekezaji huo umeimarisha kwa kiasi kikubwa kuchochea biashara za ndani na za kikanda. Aidha, amebainisha kuwa barabara ni mhimili mkuu wa uchumi kwani zaidi ya asilimia 80 ya usafirishaji wa mizigo na abiria hutegemea barabara, hali inayosukuma Serikali kuendelea kuimarisha sekta hiyo. Pia ameongeza kuwa hadi Desemba 2025, mtandao wa barabara nchini umefikia kilomita 182,164.41, huku TANROADS ikisimamia kilomita 37,734.4...

NAIBU WAZIRI WANU AGAWA VIFAA VYA TEHAMA JIJINI DODOMA LEO

Image
  Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir (kulia), akiwa ameongozana na katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Carolyne Nombo baada ya kugawa vifaa vya TEHAMA kwa wawakilishi wa shule za msingi na za Amali nchini. ambapo alisema kuwa jitihada za Serikali za kuimarisha elimu kwa baadhi ya shule nchini imekuwa ikipokelewa vyema na. alibainisha kwamba Vifaa hivyo vinatarajiwa kutumika kufundishia na kujifunzia, ili kusaidia wanafunzi kuendana na maendeleo ya sayansi na teknolojia. Aidha Wanu alitoa angalizo kwa walimu waliopokea vifaa hivyo kuhakikisha vifaa hivyo haviendi kukaa stoo bari viwe vya kujifunzia ili wanafunzi waendane na teknolojia ya sasa wasiachwe nyuma Hafla ya ugawaji wa vifaa hivyo imefanyika leo, Machi 30, 2026, katika viwanja vya ofisi ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mtumba jijini Dodoma. Vifaa hivyo vina thamani ya takribani shs milioni 769 na vitagawiwa katika shule 19 za msingi na sekondari, katika mikoa tisa ambayo ni Dodoma...

MWENYEKITI KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAJI NA MAZINGIRA JACKSON KISWAGA NA KAMATI YAKE WAKUTANA NA WATENDAJI WA WIZARA YA MAJI

Image
Mwenyekiti   wa   Kamati ya Kudumu ya Bunge ya   Maji na Mazingira Jackson Kiswaga (kushoto), akiongoza kikao cha Kamati yake ilipokutana na Maofisa wa Wizara ya maji wakiongozwa na Waziri wake Juma Aweso . Kikao hicho kilifanyikia katika  ukumbi za Mikutano ya Bunge jijini Dodoma.  Aidha  Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira wakiongozwa na Mwenyekiti wake wameridhishwa na utekelezaji wa majukumu ya usimamizi wake wa Watendaji wa Wizara ya Maji chini ya Waziri wa Jumaa Aweso Maofisa wa Wizara ya Maji Wabunge ambao ni wajumbe wa kamati hiyo wakipitia makablasha ya wizara ya Maji Mjumbe wa Kamati hiyo Mbunge Mwanaisha Ulenge, akichangia