Posts

BAJETI YA WIZARA YA ARDHI YAPITA LAKINI.......

Image
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt. Leonard Akwilapo, akihitimisha bajeti ya wizara yake baada ya kujadiliwa kwa siku mbili na wabunge kisha kupitishwa kwa kauli moja ya ndiyoooo.  Pamoja na kupitishwa bajeti hiyo wabunge wengi waliochangia walionyesha kutolidhishwa na utendaji kazi wa maofisa ardhi majimboni kwao na baadhi yao kudiliki kusema wizara hiyo bora ifutwe kutokana na migogoro mingi kusababishwa na watendaji wa wizara hiyo. Wananchji wamefikia kuuana kwa kugombea ardhi iliyogawiwa mara mbili na watendaji hao . hata mabaraza ya Ardhi nayo yanachangia migogoro na kusaababisha wananchi kutoyaamini ndiyo maana viongozi wa kitaifa wanapotembelea mikoani hawaishi kupokelewa kwa  kunyayuliwa mabango. Naibu Waziri wa Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Kaspar Muya, akichangia hotuba ya Wizara hiyo na kujibu hoja za wabunge mbalimbali zilizotolewa kwenye bajeti hiyo Mbunge wa Jimbo la Misungwi,  Silvery Luboja Salvatory, akichagia bajeti hiyo Naibu ...

MAPAMBANO YA DAWA ZA KULEVYA BANGI YAONGOZA KUKAMATWA NCHINI======PROFESA KABUDI

Image
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Uremavu) Profesa Palamagamba Kabudi, akizungumza na wanahabari leo katika ukujmbi wa Bune jijini Dopdoma pale alipookuwa akizungjmzia Taarifa ya hali ya Dawa za Kulevya kwa mwaka 2025. Akiwa ameambatana na Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, Aretas Lyimo, alisema mapambano dhidi ya dawa za kulevya yanaendelea kuimarika nnchini kwa mwaka 2025, hiyo ni kutokana na uwezeshwaji mkubwa uliofanywa na Serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Rais huyu ameimalisha utekelezaji wa mikakati ya Kitaifa kupambana na dawa za kulevya pale alipoiwezesha tume hiyo kuendesha oporesheni zake za mara kwa mara kudhibidi ukamataji na uteketezaji wa mara kwa mara unapojitokeza. Mwaka 2025 jumla ya tani 1,074.74 za dawa za kulevya zilikamatwa katika oporesheni  zilizofanyika katika maeneo mbalimbnali nchini. Hebu soma taarifa hiyo ya waziri ujionee mwenyewe, TAARIFA YA WAZIRI...

BINGWA WA DUNIA WA MASUMBWI CRAWFORD KUITANGAZA SERENGETI KIMATAIFA

Image
  Na. Hance Mbena – Serengeti  Katika muendelezo wa kuitangaza Tanzania duniani kupitia utalii wa michezo, leo Mei 28, 2026, bingwa wa masumbwi duniani, Terence “Bud” Crawford, amekabidhiwa rasmi ubalozi wa utalii baada ya kukutana na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji. Tukio hilo limefanyika ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ikiwa ni siku ya tano ya ziara yake nchini. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Dkt. Kijaji alieleza kuwa Serikali ya Tanzania chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeendelea kuifungua na kuitangaza sekta ya utalii kimataifa kupitia kampeni mbalimbali za kuitangaza nchi, ikiwemo filamu za “Tanzania: The Royal Tour” na “Amazing Tanzania” ambazo zimeendelea kuvutia wageni na watu mashuhuri kutoka mataifa mbalimbali duniani kutembelea Tanzania. “Michezo ni sehemu muhimu ya ajira na maendeleo ya uchumi, lakini pia imekuwa daraja la kuunganisha Tanzania na watu mashuhuri duniani. Kupitia michezo tunaende...

JESHI LA KUJENGA TAIFA (JKT) LAWAITA KIDATO CHA SITA KUANZA MAFUNZO KWA MUJIBU WA SHERIA ZA NCHI

Image
MKUU wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele amewataka wahitimu wa kidato cha sita Tanzania Bara na Visiwani waliochaguliwa kujiunga na mafunzo ya Jeshi hilo kwa mujibu wa sheria kuripoti katika makambi waliyopangiwa  ili waweze kuanza mafunzo ya  uzalendo,ukakamavu ,kufundishwa nidhamu,Umoja wa Kitaifa,Stadi za kazi na utayari wa kulijenga na kulitumikia Taifa pasipo kulinyongonyesha. Akizungumza na Wanahabari kwa niaba yake leo katika ofisi za Makai Mkuu ya Jeshi hilo jijini Dodoma    Mkuu wa Tawi la Utawala JKT Brigedia Jenerali Hassan Mabena, amesema majina ya waliochaguliwa yanapatikana kwenye tovuti ya JKT ambayo ni  www.jkt.mil.tz. Hii hapa ni taarifa nzima ya Mkuu huyo.  TAARIFA KWA UMMA WITO WA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA JKT KUNDI LA LAZIMA (MUJIBU WA SHERIA) MWAKA 2026 Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Meja Jenerali Rajabu Nduku Mabele, anatoa wito kwa Vijana waliohitimu elimu y a sekondari kidato cha sita mwaka 2026, kutoka shule zo...