MBUNGE WA MAGU KIDOGO AKWAMISHE BAJETI YA WIZARA YA UCHUKUZI
Mbunge wa Magu, Boniventura Kiswaga, kidogo akwamishe bajeti ya Wizara ya Uchukuzi pale alipoondoa shilingi akidai kutotendewa haki ujenzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza ambapo umekuwa ukipigwa kalenda kila mwaka. Mbunge huyo aliungwa mkono na wabunge zaidi ya 10 kama kanuni za bunge zinavyotaka ndipo majadiliano yalianza bungeni na kupelekea Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba kuingilia kati na kusema Serikali inaendelea kuchukua hatua kuhakikisha Uwanja wa Ndege wa Mwanza unaboreshwa na kujengwa katika hadhi ya kimataifa ili kuendana na hadhi ya jiji la Mwanza kama kitovu muhimu cha shughuli za kiuchumi Kanda ya Ziwa. Amesema hayo bungeni jijini Dodoma wakati akitoa kauli ya Serikali kuhusu hoja ya maendeleo ya Uwanja wa Ndege wa Mwanza iliyowasilishwa na Mbunge wa Magu, Boniventura Kiswaga, katika mjadala wa bajeti ya Wizara ya Uchukuzi kwenye Kikao cha 28 cha Mkutano wa Tatu wa Bunge la 13, leo Mei 13, 2026. Waziri Mkuu amesema Serikali inatambua umuhimu wa Uwanja wa Nd...