Posts

NDEJEMBI AONGOZA KIKAO ILI KUWEKA MIKAKATI YA UTEKELEZAJI WA BAJETI NA HOJA ZA WABUNGE

Image
  Waziri wa Nishati,  Deogratius  Ndejembi, pamoja na Naibu Waziri wa Nishati,  Salome Makamba wamekutana na Viongozi wa Wizara pamoja na Taasisi zilizo chini ya Wizara kuweka mikakati mahsusi ya kuanza utekelezaji wa hoja na mapendekezo yaliyotolewa na Wabunge, pamoja na kujipanga kwa utekelezaji wa Bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2026/27. Waziri Ndejembi na Naibu Waziri Salome wamekutana na Viongozi hao katika kikao cha kwanza cha kimkakati mara baada ya Bajeti kupitishwa, kilichowashirikisha Makatibu Wakuu, Makamishna, Wakurugenzi, Wakuu wa Vitengo, Wenyeviti wa Bodi za Taasisi zilizo chini ya Wizara, Wakuu wa Taasisi na baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Nishati. Katika kikao hicho, Waziri Ndejembi amewataka viongozi wa kila idara na vitengo vya Wizara pamoja na Taasisi zake, kila mmoja kujipanga kimkakati katika utekelezaji wa mambo yote yaliyoahidiwa kupitia Bajeti, pamoja na kutafuta majawabu na utekelezaji wa maoni na mapendekezo ya Waheshimiwa Wabunge yali...

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA AWASILISHA BAJETI YA WIZARA YAKE LEO BUNGENI JIJINI DODOMA

Image
Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Homera, akisoma bajeti ya wizara yake bungeni leo ambapo  pamoja na mambo mengine alisema  Waziri  utekelezaji wa Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026, Mpango wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara na Taasisi zilizoko chini ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2026/2027, tarehe 24 Aprili, 2026 Bungeni, Jijini Dodoma. Dkt. Homera amesema kuwa Upekuzi huo umeimarisha ulinzi wa maslahi ya Serikali, kupunguza hatari za hasara za kifedha, kuongeza uwajibikaji katika matumizi ya fedha za umma, na kuhakikisha miradi ya maendeleo inatekelezwa kwa kuzingatia sheria na mikataba yenye tija kwa Taifa. *“Mhe. Mwenyekiti vilevile, Ofisi ilikamilisha upekuzi wa Hati za Makubaliano (Memoranda of Understanding) 396.”* Amesema Dkt. Homera Aidha, Waziri wa Katiba na Sheria ameeleza kuwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imesimamia mikataba 2,821 iliyosainiwa kati ya Serikali na wadau mbalimbali. Pia Ofisi ilipokea maombi ya kuvunja mikataba saba (7) am...

BAJETI YA WIZARA YA NISHATI YAPITISHWA NA WABUNGE KWA FURAHA ZOTE

Image
Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, akihitimisha bajeti ya wizara yake leo bungeni jijini Dodoma ,amabapo aliwaambia wabunge wote kwamba maombi na maoni yao wakikutana mwakani yatakuwa yametekelezwa  yote, kwani dhamila  ya rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuona wananchi wa nchi hii wanapata umeme wa uhakika na kupikia nishati safi