CHUO CHA IAA ARUSHA KUFUNGUA MATAWI MIKOANI ----PROFESA SEDOYEKA
Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Profesa. Eliamani Sedoyeka, akizungumza na wanahabari katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO jijini Dodoma. akizungumzia kuazishwa kwa masomo mbalimbali yatakayokidhi kiu ya vijana kujitegemea ambapo chuo hicho kinafungua matawi mikoani ili kuondoa kasumba ya vijana wengi kukimbilia mijini kufuata masomo. Amempongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kukipa nyezo za kukidhi mahitaji ya chuo ambapo kinasomesha walimu wake wengi kwa kiwango cha PHD ili wakilejea weweze kuboresha elimu inayotolewa hapo. Aidha chuo hicho kimetenga Shilingi bilioni 2 kupitia Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) kwa ajili ya kuimarisha miundombinu ya kiteknolojia na kidijitali, hatua inayolenga kubadili mfumo wa utoaji elimu na kuendana na mahitaji ya dunia ya sasa. Mkuu wa Chuo huyo amesema uwekezaji huo unahusisha uanzishwaji wa Madarasa Mahiri yanayotumia Akili Unde (AI Smart Classrooms) katika kampasi za chuo hicho. Amesema madar...