Posts

UHURU WA HABARI HAUWEZI KUDUMU BILA UCHUMI IMARA KWA WANAHABARI. WAZIRI MAKONDA

Image
@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@ Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,  Paul Makonda, amesema uhuru wa vyombo vya habari hauwezi kuwa wa kweli kama wanahabari wenyewe hawana uhakika wa kiuchumi. Akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani jijini Arusha,  Makonda ameeleza kuwa hali ya kipato duni kwa wanahabari inawafanya kuwa rahisi kushawishiwa na maslahi ya wanasiasa au wafanyabiashara, hali inayohatarisha uadilifu wa taaluma hiyo. Amebainisha kuwa kuna baadhi ya mifumo isiyo rasmi ambapo watu wenye maslahi binafsi hufadhili wanahabari au vyombo vya habari ili kulinda taswira zao, jambo linalodhoofisha ukweli na kuathiri maamuzi ya wananchi. Aidha, amesisitiza haja ya kuhamisha mwelekeo wa vyombo vya habari kutoka kwenye “ku-brand watu” kwenda kwenye kuibua fursa za kiuchumi, hasa katika sekta zenye tija kama utalii, ili kujenga msingi imara wa mapato kwa tasnia ya habari. Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na M...

KATIBU WIZARA YA MAJI AWAFUNDA WABUNGE

Image
Katibu Mkuu   wa   Wizara ya Maji , Mhandisi Mwajuma Waziri, akitoa mada leo 30.4.2026,kwa wabunge iliyohusu upatikanani wa maji katika majimbo ya uchaguzi nchi nzima, Katibu huyo amewatoa wasi wasi wabunge kuhusu maji yanayotoka Ziwa Victoria yatapita kila sehemu kama ilivyopangwa. Spika Mussa Zungu, akifungua semina hiyo  Waziri Aweso amesema Serikali imelenga kufikisha huduma ya maji katika vijiji 1,575 vilivyosalia kufikia mwaka 2030, ikiwa ni mkakati wa kuhakikisha upatikanaji wa maji unakuwa wa uhakika na endelevu nchini kote, hakuna jimbo ambalo halitapata huduma za maji aliwahakikishia wabunge hao   

WAZIRI KAIRUKI AWASILISHA BAJETI YA MAWASILIANO 2026/2027 BUNGENI JIJINI DODOMA

Image
                                                                                                                                                                                                                                                          ...

WABUNGE WA CCM WAWACHAGUA WABUNGE WATATU KWENDA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI, YUMO MTOTO WA WASIRA

Image
  Katibu wa Bunge   Baraka I. Leonard   akizungumza na wanahabari baada ya kumalizika uchaguzi ndani ya CCM wa wabunge wa Tanzania watakaoingia katika Bunge la Afrika Mashariki kujaza nafasi tatu zilizokuwa wazi, Uchaguzi huo ulifanyika katika ukumbi wa Msekwa jijini Dodoma na mkutano huu wa wanahabari ulifanyika katika Ukumbi wa Spika. Katibu alibainisha haya,    nawajulisha  kuhusu Uchaguzi Mdogo utakaofanyika   tarehe 4 Mei 2026, kuchagua wajumbe watatu watakaowakilisha Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki . Hivyo, tunaomba mfikishe taarifa hii muhimu kwa wananchi.   Uchaguzi huu ni wa kujaza nafasi zilizoachwa wazi katika Bunge la Afrika Mashariki baada ya Mhe. James Kinyasi Millya (Mb), Mhe. Dkt. Ng’waru Jumanne Maghembe (Mb) na Mhe. Angela Charles Kizigha (Mb) kuchaguliwa kuwa Wabunge katika Bunge la Jamuhuri la Muungano wa Tanzania.   Ndugu Waandishi wa Habari Uchaguzi huu mdogo unafanyika kwa mujibu wa Kanuni ya ...