Posts

WAZIRI ULEGA APITISHIWA BAJETI YAKE AWAAHIDI KUJENGA BARABARA ZAO WALIZODAI HAZIPITIKI.

Image
Waziri wa Ujenz,i Abdallah Ulega, akihitimisha bajeti ya wizara yake baada ya wabunge kuwaomba waipitishe kwa nguvu moja ili aende akajipange kuwapelekea barabara majimboni kwani, Ulenga akijibu kwa mbwe mbwe za kujiamini alisababisha mpaka Waziri Mkuu Dkt . Mwigulu kumpigia makofi akijibu maswali ya wabunge ambao  baadhi walikuwa na jaziba ya kutaka kushika  shilingi kwa majibu yake waliachia shilingi yake  na kupitisha bajeti hiyo. Amewaambia wakutane mwakani atakuwa ametimiza ahadi zake kwao  amewaomba  wabunge na wananchi wamuombee Rais Dkt . Samia Suluhun Hassan, mungu ammpe maisha marefu atimize ndoto zake za kuwaletea wananchi maisha mazuri na barabara nzuri na uchumi upae. Barabara zinapopitikia ndipo uchumi nao unapaa kwani wananchi itakuwa rahisi kuwafikishia mazao kila sehemu ya nchi mijini na vijijini.  Wazirai Mkuu Dkt.Mwigulu Nchemba, na wabunge pamona na mawaziri wakimpongeza Ulega na naibu wake baada ya kupita bajeti hiyo  

WAZIRI DKT. NYANSAHO AWASILISHA BAJETI YA WIZARA YAKE LEO BUNGENI JIJINI DODOMA

Image
 Mheshimiwa Spika, kufuatia taarifa iliyowasilishwa leo hapa Bungeni na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) iliyochambua na kutoa ushauri ulioboresha Bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, ninaomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu likubali kupokea na kujadili Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2025/26. Aidha, ninaomba Bunge lako Tukufu lijadili na kupitisha Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2026/27 kwa mafungu yote matatu (Fungu 57 - Wizara, Fungu 38 - NGOME na Fungu 39 - JKT). 2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote nitumie fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema, kwa kuijalia Nchi yetu amani, utulivu na mshikamano na kutuwezesha kuendelea kutumikia Taifa letu kwa uaminifu na uadilifu tukiwa wenye afya njema. 3. Mheshimiwa Spika, napenda kuungana na waheshimiwa wabunge wenzangu waliot...