Posts

WAZIRI DKT. GWAJIMA AWASILISHA BAJETI YA WIZARA YAKE SHANGWE ZALINDIMA BUNGENI DODOMA

Image
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Dkt. Dorothy Gwajima amenena kwamba ukatili wa kijinsia bado ni changamoto kubwa inayokwamisha wanawake na wanaume kufikia ndoto zao za maendeleo na ustawi wa maisha yao, licha ya juhudi mbalimbali zinazo chukuliwa na Serikali. Akisoma bajeti ya Wizara yake kwa mwaka wa fedha 2026/2027 Bungeni jijini Dodoma, Dkt. Gwajima amesema takwimu kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Jeshi la Polisi zinaonyesha kuwa matukio ya ukatili wa kingono kwa jinsia zote yamepungua kutoka 12,749 mwaka 2024 hadi matukio 11,625 mwaka 2025.  Ameeleza kuwa kupungua kwa matukio hayo kunadhihirisha mafanikio ya kampeni za uhamasishaji, elimu kwa umma na hatua za kisheria zinazochukuliwa dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia nchini. Hata hivyo, amesema wanawake bado ndio waathirika wakuu wa ukatili wa kingono ikilinganishwa na wanaume. Takwimu zinaonyesha wanawake 10,976 walifanyiwa ukatili wa kingono mwaka 2024 na 10,057 mwaka 2...

BAJETI YA WIZARA YA ARDHI YAPITA LAKINI.......

Image
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt. Leonard Akwilapo, akihitimisha bajeti ya wizara yake baada ya kujadiliwa kwa siku mbili na wabunge kisha kupitishwa kwa kauli moja ya ndiyoooo.  Pamoja na kupitishwa bajeti hiyo wabunge wengi waliochangia walionyesha kutolidhishwa na utendaji kazi wa maofisa ardhi majimboni kwao na baadhi yao kudiliki kusema wizara hiyo bora ifutwe kutokana na migogoro mingi kusababishwa na watendaji wa wizara hiyo. Wananchji wamefikia kuuana kwa kugombea ardhi iliyogawiwa mara mbili na watendaji hao . hata mabaraza ya Ardhi nayo yanachangia migogoro na kusaababisha wananchi kutoyaamini ndiyo maana viongozi wa kitaifa wanapotembelea mikoani hawaishi kupokelewa kwa  kunyayuliwa mabango. Naibu Waziri wa Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Kaspar Muya, akichangia hotuba ya Wizara hiyo na kujibu hoja za wabunge mbalimbali zilizotolewa kwenye bajeti hiyo Mbunge wa Jimbo la Misungwi,  Silvery Luboja Salvatory, akichagia bajeti hiyo Naibu ...