Posts

WAZIRI DKT. NYANSAHO AWASILISHA BAJETI YA WIZARA YAKE LEO BUNGENI JIJINI DODOMA

Image
 Mheshimiwa Spika, kufuatia taarifa iliyowasilishwa leo hapa Bungeni na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) iliyochambua na kutoa ushauri ulioboresha Bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, ninaomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu likubali kupokea na kujadili Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2025/26. Aidha, ninaomba Bunge lako Tukufu lijadili na kupitisha Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2026/27 kwa mafungu yote matatu (Fungu 57 - Wizara, Fungu 38 - NGOME na Fungu 39 - JKT). 2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote nitumie fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema, kwa kuijalia Nchi yetu amani, utulivu na mshikamano na kutuwezesha kuendelea kutumikia Taifa letu kwa uaminifu na uadilifu tukiwa wenye afya njema. 3. Mheshimiwa Spika, napenda kuungana na waheshimiwa wabunge wenzangu waliot...

UCSAF YAWAKUTANISHA WAHARIRI NA WAANDISHI WA MAKAO MAKUU DODOMA

Image
Kaimu Mkurugenzi wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote UCSAF, Albart Richard, akifungua semina ya Wahariri na Wanahabari wa Makao Makuu Dodoma  iliyofanyika Makao Makuu ya Mamlaka hiyo yaliyopo  eneo la ndejengwa  leo pamoja na mambo mengine wandishi waliweza kufahamishwa kazi za Mamlaka hiyo zinavyoendelea kufanyika nchi nzima na  pia wakafahamishwa jinsi wanavyoendelea kusambaza mawasiliano hadi vijijini   na kufunga Internati za bure kwenye maeneo ya mkusanyiko ya watu wengi mijini na vijijini. Naye Mwenyekiti wa Chama cha Wanadishi wa habari Mkoa wa Dodoma Mussa Yusuf, aliushukuru uongozi wa mamlaka hiyo kwa kitendo chake cha kuita wanahabri wa mkoa huo kuwafahamisha mambo mbalimbali yanayofanywa na mfuko huo, alisema hapo mwanzo walikuwa wakipata tabu kuwafikia sasa imekuwa lahisi kwani wameweza kubadilishana hata mawasilian kitumambacho hakikuwepo hapo mwanzo. Wanahabari wakiwa katika semina hiyo  

MBUNGE WA MAGU KIDOGO AKWAMISHE BAJETI YA WIZARA YA UCHUKUZI

Mbunge wa Magu, Boniventura Kiswaga, kidogo akwamishe bajeti ya Wizara ya Uchukuzi pale alipoondoa shilingi akidai kutotendewa haki ujenzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza  ambapo umekuwa ukipigwa kalenda kila mwaka. Mbunge huyo aliungwa mkono na wabunge zaidi ya 10 kama kanuni za bunge zinavyotaka ndipo majadiliano yalianza bungeni  na kupelekea Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba kuingilia kati na kusema  Serikali inaendelea kuchukua hatua kuhakikisha Uwanja wa Ndege wa Mwanza unaboreshwa na kujengwa katika hadhi ya kimataifa ili kuendana na hadhi ya jiji la Mwanza kama kitovu muhimu cha shughuli za kiuchumi Kanda ya Ziwa. Amesema hayo bungeni jijini Dodoma wakati akitoa kauli ya Serikali kuhusu hoja ya maendeleo ya Uwanja wa Ndege wa Mwanza iliyowasilishwa na Mbunge wa Magu, Boniventura Kiswaga, katika mjadala wa bajeti ya Wizara ya Uchukuzi kwenye Kikao cha 28 cha Mkutano wa Tatu wa Bunge la 13, leo Mei 13, 2026. Waziri Mkuu amesema Serikali inatambua umuhimu wa Uwanja wa Nd...

TANZANIA MWENYEJI MKUTANO WA WABUNGE WANAWAKE WA MABUNGE UKANDA WA MAZIWA MAKUU

Image
Spika Mussa Azan Zungu , akizungumzia  Mkutano wa jukwaa la Mabunge la Kimataifa kuhusu Eneo la Maziwa Makuu (FP-ICGLR), kwa ushirikiano na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambapo leo limesaini Makubaliano ya Uenyeji kwa ajili ya Mkutano huo  wa kwanza wa Wabunge Wanawake (WPC) 2026 nchini. hafla ya kusaini ilifanyika ofisini kwake jijini Dodoma. Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Baraka Leonard, akizungumza  kuhusu mkutano wa wanawake wa mabunge ya nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu unaotarajiwa kufanyika nchini una lengo la kuwajengea wanawake uwezo katika masuala ya uongozi, maamuzi na maendeleo ya jamii, mazungumzo hayo yalifanyika Ofisi ya Spika jijini Doddoma leo