Posts

MBUNGE WA MBOGWE FAGASON AONYESHA UFAHARI WA WATOTO WAKE BUNGENI. WABUNGE WAMSHANGILIA

Image
Mbunge wa Mbogwe mkoani Geita, Fagason Nkingwa, ameleta watoto wake leo bungeni wapata 15, amewataka vijana wasiogope kuzaa kwani Bara la Afrika ni kubwa linahitaji nguvu kazi. Mwenyekiti wa Bunge Deo Mwanyika,, akiwatambulisha watoto hao alisema alimwandikia barua kwamba watoto wake wapo 15 wamekuja kutembelea bunge kwa kujifunza, ilikuwa furaha na velegele vilitawala ukumbi wa wabunge  na badae walienda kutembelea maeneo mbalimbali ya bunge. Akizungumza na mwandishi wetu Fagason alisema anamkumbuka, marehemu Dkt. John Magufuli, aliwaomba Watanzania wazae yeye anajenga Mashule na Hospitali na kujenga Mabarabara, Fagason alitolea mfano wa baadhi ya nchi za Ulaya hivi sasa wanatoa zawadi kwa vijana wao kuzaana kwani wamebakia wazee nguvu kazi imeisha wanataka kutawaliwa na vijana kutoka mataifa mengine waliyoyatawala siku za nyuma.  

DIWANI WA CCM ZUZU ADAIWA KUWALIZA WANACCM WENZAKE WAPAZA SAUTI KWA RAIS SAMIA AWASAIDIE

Image
Katibu Uenezi wa  Chama cha Maopinduzi Kata ya Zuzu jijini Dodoma ambaye pia ni mjasiliamali katika eneo la uchimbaji kokoto  wa machimbo ya kokoto na mchanga mtaa wa Mazengo Zuzu, Noel Chalres, akizungumza na wanahabari leo katika eneo la machimbo hayo akiwa na wenzake zaidi ya wajasiliamali zaidi ya 200 waliokusanyika katika eneo hilo kutoa kilio chao kwa wanahabari hao wakida kiongozi wao waliyemwamini wakamfanyia kampeni za udiwani na kisha kupata leo hii ameamua kuwageuka na kuwafukuza katika eneo lao ambalo wanalimiliki zaidi ya miaka 10 sasa. Kwa kushirikiana na baadhi ya watendaji wa jiji la Dodoma wameamua kufikisha kilio chao kwa wanahabari na katika vikao vya chama  wanasiku ya 8 sasa hawaingizi kipato chochote. Happines Joseph Luswaga, aliyejitambulisha kuwa ni mzaliwa wa Zuzu amemuomba Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuwasaidi yeye akiwa mwanamke siyo rais tu naanahuruma na watu wake awasaidie kulejeshewa eneo lao ambalo kiongozi wao wa CCM Diwani wao waliyemf...