Posts

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE NISHATI NA MADINI YARIDHISHWA NA KIWANDA CHA NGUZO ZA ZEGE

Image
  *Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita  * Yaipongeza TANESCO kwa usimamizi wa Ujenzi wa Kiwanda hicho * Shilingi Bilioni 8 zawekezwa ujenzi wa Kiwanda  @@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@ Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeridhishwa na Ujenzi wa Kiwanda cha Zege kinachomilikiwa na kampuni tanzu ya TANESCO ya kuzalisha nguzo za zege kilichopo katika Mkoa wa Tabora wakati wa ziara yao ya kikazi Mkoani humo tarehe 12 Machi, 2026. Akizungumza baada ya ziara hiyo Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mwanamama shupavu Mbunge wa Bagamoyo, Subira Mgallu ameeleza kuridhishwa na hatua ya kukamilika kwa Kiwanda hicho kilichoanza uzalishaji na kuwaelekeza Wizara ya Nishati na TANESCO kukisimamia kiwanda hicho kiendelee kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa na kuzalisha faida. “Kwa niaba ya Kamati tumeridhika na kazi kubwa iliyofanyika katika kiwanda hiki ambacho kimekamilika na uzalishaji umeanza, tunatoa rai kwa Wizara na TANESCO kuendelea kusimamia kiwanda hiki ...

TANZANIA YAENDELEA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA

Image
  Na WMJJWM – New York, Marekani   Serikali ya Tanzania imesisitiza dhamira yake ya kuendelea kutekeleza kikamilifu makubaliano ya kimataifa yanayohusu usawa wa kijinsia na maendeleo, sambamba na kuimarisha juhudi za kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia katika jamii.   Akizungumza katika mkutano huo, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima, amesema Tanzania inaendelea kuthibitisha dhamira yake ya kutekeleza kikamilifu na kwa ufanisi hatua zilizowekwa katika makubaliano mbalimbali ya kimataifa kuhusu jinsia na maendeleo ambayo nchi imeridhia. Dkt. Gwajima amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizoingia katika makubaliano na maazimio mbalimbali ya kimataifa, ikiwemo Azimio na Jukwaa la Utekelezaji la Beijing, Mkataba wa Kutokomeza Aina Zote za Ubaguzi Dhidi ya Wanawake (CEDAW) pamoja na Malengo ya Maendeleo Endelevu ya mwaka 2030.   Ameeleza kuwa Serikali inaendelea kutekeleza mipango na mikakati mbalimbali yenye...

WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU AAGIZA WATENDAJI NCHINI WAJIPANGE KUHUSU UWEKEZAJI USIOKUWA NA UBABAISHAJI

Image
  WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewaagiza Wakuu wa Mikoa na watendaji wao katika mikoa yote nchini wajipange kutoa taarifa kuhusu uwekezaji na ukuzaji wa biashara kwenye mikoa  kila wanapotoa taarifa kwa viongozi wa kitaifa   Ametoa wito huo leo jioni (Jumatano, Machi 11, 2026) wakati akifunga Mkutano wa Kuhakiki Rasimu ya Pili ya Mpango wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji (Mkumbi II) uliofanyika katika ukumbi wa Kambarage, HAZINA, jijini Dodoma.   Alisema mapendekezo yote yaliyowasilishwa na washiriki wa mkutano huo ambao ni Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa pamoja na Wakurugenzi yaandaliwe katika mfumo wa mkakati wa utekelezaji ili kuwezesha kuwa wa ufanisi.    “Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala na Wakurugenzi wa Halmashauri mbebe jukumu la kuwa mabalozi wa kwanza wa uwekezaji katika maeneo yenu kwa kutambua na kutangaza fursa mbalimbali zilizopo katika maeneo yenu, “Tubebe hili jukumu, kila Mkuu wa Mkoa anapotoa taa...

VITUO 14 ZA KUJAZIA GESI VYA JIJINI DAR ES SALAAM ----- MKURUGENZI TPDC MAKAME

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC)   Mussa Makame, aakizungumza na wanahabari leo jijini Dodoma, akiwaeleza jinsi Shirika hilo lilivyojizatiti kutoa huduma kwa wananchi na kuhalakisha ucholongaji wa visima vya gesi drhrmu ambayo inapatikana. Aidha amesema mpaka sasa wameweza kuunganisha nyumba 2500 kwa wananchi  wa Mtwara kwa ajili ya huduma ya gesi wanataka kushirikiana na watu binafsi kwa ajili hya kusambaza gesi hiyo kuwafikia wananchi mikoani. Makame amebainisha kwamba shieika lake limeweza kufungua vituo 14 vya kujazia gesi jijini Dar es salaam  na wapo mbioni kusambaza mikoani sasa. Makame   amesema utekelezaji wa mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki ( EACOP), umefikia asilimia 43.5 huku baadhi ya kazi za ujenzi katika makambi na vituo vya kuhifadhia mabomba zikikamilika kwa asilimia 100.   Pia Wanatalajia kujenga bomba jipya kutoka Mtwara hadi Chalinze ,Tanga na hadi mikoa ya kati, wamo katika upembez...