Posts

WANANCHI PERAMIHO, SHIWINGA KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MBUNGE, DIWANI

Image
  @@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@ Wapiga Kura 127,632 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura watashiriki katika uchaguzi wa kuchagua Mbunge katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mkoa wa Ruvuma na Kata ya Shiwinga iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe. Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele ameyasema hayo leo Februari 25, 2026 mjini Songea Mkoani Ruvuma wakati akisoma risala maalum kuhusu uchaguzi katika jimbo na kata husika utakao fanyika kesho Februari 26, 2026 na kusema kuwa jumla ya vituo 373 vya Kupigia Kura vitatumika. “Kati yao wapiga kura 120,780 ni wa Jimbo la Peramiho na wapiga kura 6,852 wapo katika kata ya shiwinga na jumla ya vituo 373 vya Kupigia Kura vitatumika, ambapo vituo 354 vipo Jimbo la Peramiho na vituo 19 vipo katika Kata ya Shiwinga Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi,”amesema Jaji Mwambegele. Aidha, amesema kwa uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Peramiho vyama vya sia...

KATIBU MTENDAJI MAMLAKA YA RUFANI YA ZABUNI ZA UMMA NCHINI NCHINI AZUNGUMZA NA WANAHABARI DODOMA

Image
Katibu Mtendaji wa   Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA)   nchini Tanzania ni   James Sando , akizungumza na wanahabari leo katika ukumbi wa Idara ya habari MAELEZO jijini Dodoma , akielezea utendaji kazi wa Mamlaka yake.   Aidha amebainisha kwamba  Mamlaka imefungua fursa kwa vijana 878 kwa kuwapatia mafunzo ya kuwajengea uwezo ili waweze kudai haki zao kwa ufanisi katika michakato ya ununuzi wa umma. ‎ Amesema kuwa mafunzo hayo yametolewa katika mikoa ya Dodoma, Dar es Salaam, Mwanza na Mbeya ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa azma ya Serikali ya kuwawezesha vijana na makundi maalum kushiriki kikamilifu katika sekta ya ununuzi wa umma. Wanahabari wakiwajibika katika mkutano huo  

WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO MKOANI ARUSHA

Image
  Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo tarehe 24 Februari, 2026 akifungua Semina ya Bodi za Wakurugenzi wa Mamlaka za Maji nchini unaofanyika katika hoteli ya Ngurdoto, jijini Arusha. Mkutano huo wa kitaifa unawakutanisha viongozi wakuu wa usimamizi wa Mamlaka 85 za maji nchini. PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo tarehe 24 Februari, 2026 akizungumza na Washirki wa Semina ya Bodi za Wakurugenzi wa Mamlaka za Maji nchini unaofanyika katika hoteli ya Ngurdoto, jijini Arusha. Mkutano huo wa kitaifa unawakutanisha viongozi wakuu wa usimamizi wa Mamlaka 85 za maji nchini. PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU Muonekano wa ujenzi wa Stendi Kuu ya Mabasi yaendayo mikoani unaotekelezwa katika eneo la Bondeni City kwenye Halmashauri ya Jiji la Arusha kwa gharama ya sh. bilioni 14.3 ambao leo tarehe 24 Februari, 2026 Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba alifanya ziara ya kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi huo. Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo tarehe 24 Februari,...

MARAIS DKT.JOHN MAGUFULI NA DKT.SAMIA SULUHU HASSAN WALIHESHIMISHA J W T Z.

Image
Helkopta  zikilipamba jengo jipya la Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT) lililopo eneo la Kikombo  Mkoani Dodoma, awali Makao Makuu hayo yalikuwa Upanga jijini Dar es Salaam. Jengo hilo la kisasa liliasisiwa na Rais wa awamu ya Tano marehemu  Dkt. John Pombe Magufuli  na kumaliziwa ujenzi wake na Rais wa Awamu ya Sita Dkt. Samia Suluhu Hassan.   Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo, Rais Samia amesema hakuna uwekezaji unaoweza kuja bila kuwepo mazingira salama, na kwamba haiwezekani kujenga ustawi wa wananchi bila amani. Ameeleza kuwa hivi karibuni shirika la kimataifa la tathmini ya ukuaji wa uchumi duniani, The Modes, limeipa nchi daraja la I, kiwango alichokieleza kuwa ni kizuri kwa mustakabali wa ukuaji wa uchumi. Ameongeza kuwa kadri taifa linavyoimarika kiuchumi, uwekezaji katika sekta ya ulinzi unakuwa jambo lisiloepukika kutokana na umuhimu wake kwa maendeleo na ustawi wa wananchi. Amesema Serikali itaendelea kuliwezesha Jeshi kuwa na mazingira bor...

CHUO CHA IAA ARUSHA KUFUNGUA MATAWI MIKOANI ----PROFESA SEDOYEKA

Image
Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Profesa. Eliamani Sedoyeka, akizungumza na wanahabari katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO jijini Dodoma. akizungumzia kuazishwa kwa masomo mbalimbali yatakayokidhi kiu ya vijana kujitegemea ambapo chuo hicho kinafungua matawi mikoani ili kuondoa kasumba ya vijana wengi kukimbilia mijini kufuata masomo. Amempongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kukipa nyezo za kukidhi mahitaji ya chuo ambapo kinasomesha walimu wake wengi kwa kiwango cha PHD  ili wakilejea weweze kuboresha  elimu inayotolewa hapo.   Aidha chuo hicho kimetenga Shilingi bilioni 2 kupitia Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) kwa ajili ya kuimarisha miundombinu ya kiteknolojia na kidijitali, hatua inayolenga kubadili mfumo wa utoaji elimu na kuendana na mahitaji ya dunia ya sasa. Mkuu wa Chuo huyo amesema uwekezaji huo unahusisha uanzishwaji wa Madarasa Mahiri yanayotumia Akili Unde (AI Smart Classrooms) katika kampasi za chuo hicho. Amesema madar...

WAZIRI MKUU MWIGULU AKAGUA MRADI WA UJENZI WA BOMBA LA MAFUTA MKOANI TANGA

Image
  Aonya wageni wanaoanzisha makampuni kwa kutumia kivuli cha wazawa WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Jumatatu (Februari 16, 2026) amekagua mradi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima (Uganda) hadi Chongoleani mkoani Tanga na amesema kuwa amefurahishwa na utekelezaji wake. Amesema kuwa mradi huo ni wa kimkakati ambao utagharimu Dola za Marekani bilioni 5.65 ni kielelezo cha undugu kati ya Tanzania na Uganda. “Ninatambua msisitizo uliowekwa na viongozi wetu, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Mheshimiwa Rais Yoweri Kaguta Miseveni katika utekelezaji wa mradi huu.” Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ambaye yuko mkoani Tanga kwa ziara ya kikazi amesema kuwa Serikali itaendelea kuweka uzito unaostahili katika kutekeleza mradi huo ambao umefikia asilimia 81 ya utekelezaji kwa heshima ya undugu kati ya Tanzania na Uganda. “Lakini tutaendelea kuweka uzito unaostahili kwa heshima ya kulinda uhuru wetu kwa kuwa ni nchi huru ambayo inaweza kujitegemea kuteke...