MAWASILIANO SASA KUWA KARIBU NA BURE ASEMA WAZIRI -----KAIRUKI MAWASILIANO SASA KUWA MARIBU NA BURE__________________________________________________________________________________________MAWASLIANO SASA KUWA KARIBU NA BURE _-------WAZIRI KARIUKI_______________________________________________________________________________________________________________________________
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Angellah Kairuki (Pichani) amesema kuwa Serikali imeendelea kudhibiti gharama za mawasiliano nchini ambapo gharama za kupiga simu ndani ya nchi zimeendelea kubaki shilingi 9 kwa dakika huku wastani wa bei ya data bila kifurushi ukiendelea kubaki shilingi 9.31 kwa MB moja, hali inayorahisisha wananchi wengi zaidi kumudu matumizi ya intaneti na huduma za kidigitali. Akizungumza leo Februari 4, 2026 jijini Dodoma wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa ahadi za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ndani ya siku 100 kwa waandishi wa habari, Waziri Kairuki amesema mafanikio hayo yanatokana na uwekezaji unaoendelea kufanywa na Serikali katika miundombinu ya mawasiliano ikiwemo minara na Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano. Amebainisha kuwa hali ya upatikanaji wa mawasiliano imeendelea kuimarika ambapo laini za simu zilizosajiliwa zimeongezeka kutoka milioni 99.3 Oktoba 2025 hadi milioni 106.9 Januari 2026 sawa na ongezeko la asilimia 7, huku w...