RIDHIWANI AWASILISHA BAJETI YA WIZARA YAKE NA YAPITA BIRA KUPINGWA
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete leo, akiwasilisha bajeti ya wizara hiyo mbele ya wabunge jijini Dodoma Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete amesema Serikali kupitia Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma imeimarisha maadili ya viongozi wa umma ambapo asilimia 85 ya viongozi wamewasilisha matamko ya mali na madeni yao. Amebainisha kwamba hatua hiyo inaonyesha kuimarika kwa uwajibikaji wa viongozi na uaminifu wa wananchi kwa taasisi za umma, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kujenga Serikali inayowajibika, yenye uwazi na inayoaminika kwao. Pia Ridhiwani amesema wananchi 34,334 wamepatiwa elimu ya maadili, hatua inayochangia kukuza utamaduni wa uadilifu na uwajibikaji katika jamii. Aidha Waziri Ridhiwani amesema Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kusimamia maadili kwa vitendo kwa sababu uadilifu wa viongozi ndio msingi wa haki, maendele...