Posts

JWTZ LAWAAGA MAJENERALI 17 JIJINI DODOMA

Image
Magari maalumu  yaliyobeba  maafisa jenerali  17 wastaafu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), yakisukumwa katika hafla ya kuwaaga iliyoongozwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob Mkunda katika Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa Kikombo jijini Dodoma Julai 10, 2026. Askari wakiwa wamejipanga tayari kupita katikati magari maalumu yaliyowabeba maafisa Jrnrrali wastaafu Jenerali Mkunda akiagana na Meja Jenerali Mstaafu Suleiman Mungiya Mzee. Aidha Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob Mkunda amewaasa maafisa jenerali  17 Wastaafu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), kuacha kuhangaika na mambo ya siasa na mengineyo, bali watulie waishi vizuri na familia zao. Pamoja na mambo mengine Jenerali Mkunda ameyasema hayo wakati wa hafla ya kuwaaga maafisa Jenerali hao  katika Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa Kikombo jijini Dodoma Julai 10, 2026. Jenerali Mkunda (aliyekaa mbele katikati pamoja na viongozi wengine)  wakiwa katika picha ya kumbukumbu na  maaf...

WAZIRI MKUU MWIGULU ALIFUNGA BUNGE NA KUWATAKA WATANZANIA WATUNZE AMANI

Image
HOTUBA YA MHESHIMIWA DKT. MWIGULU LAMECK NCHEMBA (MB.), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUAHIRISHA MKUTANO WA TATU (3) WA BUNGE LA 13 LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAREHE 26 JUNI, 2026 JIJINI DODOMA   1.             Mheshimiwa Spika, awali ya yote ninamshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa fadhili zake zilizotuwezesha sote kuiona siku hii muhimu katika historia ya Bunge la 13. Kama mnavyofahamu, tumekutana leo kwa ajili ya kuhitimisha mkutano wa Tatu ambao ulikuwa mahsusi kwa ajili ya kupokea na kujadili bajeti ya serikali.   2.             Mheshimiwa Spika, nimesema leo ni siku muhimu na ya kihistoria kwa sababu, hii ni Bajeti ya kwanza ya Serikali kupitishwa na Bunge la 13 baada ya uchaguzi mkuu wa 2025. Hongereni sana waheshimiwa Wabunge!   3.             Mheshimiwa Spik...