Posts

WAZIRI MKUU MWIGULU AKAGUA MRADI WA UJENZI WA BOMBA LA MAFUTA MKOANI TANGA

Image
  Aonya wageni wanaoanzisha makampuni kwa kutumia kivuli cha wazawa WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Jumatatu (Februari 16, 2026) amekagua mradi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima (Uganda) hadi Chongoleani mkoani Tanga na amesema kuwa amefurahishwa na utekelezaji wake. Amesema kuwa mradi huo ni wa kimkakati ambao utagharimu Dola za Marekani bilioni 5.65 ni kielelezo cha undugu kati ya Tanzania na Uganda. “Ninatambua msisitizo uliowekwa na viongozi wetu, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Mheshimiwa Rais Yoweri Kaguta Miseveni katika utekelezaji wa mradi huu.” Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ambaye yuko mkoani Tanga kwa ziara ya kikazi amesema kuwa Serikali itaendelea kuweka uzito unaostahili katika kutekeleza mradi huo ambao umefikia asilimia 81 ya utekelezaji kwa heshima ya undugu kati ya Tanzania na Uganda. “Lakini tutaendelea kuweka uzito unaostahili kwa heshima ya kulinda uhuru wetu kwa kuwa ni nchi huru ambayo inaweza kujitegemea kuteke...

KOCHA GAMONDI RASMI SASA KUINOA STARS

Image
  Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Paul Makonda, ameweka wazi kuwa, Kocha Miguel Gamondi amesaini rasmi mkataba wa miaka miwili wa kuifundisha timu ya Taifa ya soka ya Tanzania (Taifa Stars).   Waziri Makonda amesema hayo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam leo Februari 16, 2026, wakati wa Hafla ya Utiaji Saini Mkataba wa Kocha huyo iliyofanyika katika Uwanja wa Benjamin Mkapa.   Amesema Gamondi amestahili mkataba huo baada ya kuonesha uwezo wa hali ya juu katika michuano ya AFCON 2025 iliyofanyika Morocco hivi karibuni na kuingoza Taifa Stars kufika hatua ya 16 ya michuano hiyo kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania akiwa kocha wa muda.   Serikali sasa imeamua kumwajiri rasmi ili aiongoze timu hiyo katika jitihada za kunyakua ubingwa wa AFCON 2027, ambapo Tanzania itakuwa mwenyeji wa mashindano hayo.

MKURUGENZI MKUU WA VETA, CPA ANTHONY MZEE KASORE KATIKA MKUTANO NA WANAHABARI LEO JIJINI DODOMA

Image
  Ndugu Wanahabari, Awali ya yote napenda kuwashukuru kwa kuitikia wito wa kushiriki mkutano huu muhimu unaolenga kuhabarisha Watanzania kuhusu jitihada za Serikali katika uendelezaji ufundi stadi nchini n a furs a zi lizopo VETA kwa ajili ya kuwawezesha vijana na wananchi kwa ujumla kuajirika na kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi . Leo hatuzungumzii nadharia. Tunazungumzia maisha ya vijana kubadilika ; Tunazungumzia ajira kuundwa ; Tunazungumzia uchumi kujengwa kwa mikono ya Watanzania wenye ujuzi. KUHUSU VETA Ndugu wanahabari, Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) ni Wakala wa Serikali iliyoanzishwa kwa Sheria ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Sura ya 82 ikiwa na majukumu ya utoaji, ugharamiaji na uratibu wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi nchini. Kwa lugha rahisi zaidi , VETA ndiyo inazalisha watu wanaojenga Tanzania kwa vitendo. Nyumba tunazoishi, barabara tunazopita, umeme tunaotumia, mashine viwandani, huduma za utalii, tekn...