Posts

PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI LEO BUNGENI JIJINI DODOMA

Image
Spika wa Bunge  Mussa Azzan Zungu (kulia), akimsikiliza kwa makini  Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza  Johari, mazungumzo hayo yalifanyikia ndani ya ukumbi wa bunge leo. Bunge lilikuwa likisimamiwa na Mwenyekiti Deo Mwanyika Jesca Magufuli (kulia), akimweleza jambo Waziri Angella Kairuki Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira)  Reuben Kwagilwa, akijibu maswali ya wabunge  Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir, akijibu maswali ya wabunge Mkurugenzi   Mtendaji wa   CRDB   Bank Foundation   Tuli Mwambapa, akitambulishwa bungeni  

RIDHIWANI AWASILISHA BAJETI YA WIZARA YAKE NA YAPITA BIRA KUPINGWA

Image
Waziri   wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,   Ridhiwani   Kikwete leo, akiwasilisha bajeti ya wizara hiyo mbele ya wabunge jijini Dodoma Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete amesema Serikali kupitia Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma imeimarisha maadili ya viongozi wa umma ambapo asilimia 85 ya viongozi wamewasilisha matamko ya mali na madeni yao. Amebainisha kwamba  hatua hiyo inaonyesha kuimarika kwa uwajibikaji wa viongozi na uaminifu wa wananchi kwa taasisi za umma, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kujenga Serikali inayowajibika, yenye uwazi na inayoaminika kwao. Pia Ridhiwani amesema wananchi 34,334 wamepatiwa elimu ya maadili, hatua inayochangia kukuza utamaduni wa uadilifu na uwajibikaji katika jamii. Aidha Waziri Ridhiwani amesema Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kusimamia maadili kwa vitendo kwa sababu uadilifu wa viongozi ndio msingi wa haki, maendele...