Posts

MATUKIO YA PICHA ZA MKUTANO MKUU WA MWAKA WA VYOMBO VYA UTANGAZAJI NCHINI.

Image
Mchoya Group wakionyesha ufundi wao katika mkutano huo Dkt.Albart Mkoko, akitoa mada yake  katika mkutano huo Kipangula, akitoa mada yake katika mkutano huo ambapo anasema kila mwandishi anatakiwa kuwa na JAB Indrisa Majura, akizungumza katika mkutano huo Bety Chalamila Mkwasa, akiwa katika mkutano huo Penzi Nyamungumi, akizungumza katika mkutano huo  

NEEMA YA KIDIJITALI: Serikali Yashusha Ada kwa Wanablogu, TCRA Yazindua Redio ya Kisasa 'DSB'

Image
SERIKALI imetangaza neema ya kihistoria kwa wanablogu, vijana wabunifu, na watoa maudhui mtandaoni nchini kwa kupunguza ada za leseni kwa kiwango kikubwa, hatua inayolenga kuchochea ukuaji wa uchumi wa kidijitali na kurasimisha shughuli za wahabarishaji wa mitandao. Hatua hiyo imekuja kufuatia utafiti wa kina na mikutano ya kimkakati ya takribani mwaka mzima kati ya mtandao wa Tanzania Bloggers Network (TBN) na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), ikielezea vikwazo vya gharama vilivyokuwa vikikwaza uandishi wa habari za kidijitali nchini. Akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano wa Mwaka wa Watoa Huduma za Utangazaji (ABC 2026) jijini Dodoma leo, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamisi Mwinjuma, amesema ada ya leseni kwa watoa maudhui mtandaoni imeshushwa kutoka Sh500,000 hadi Sh50,000 tu, huku ada ya maombi ikiwa ni Sh10,000 pekee. Mageuzi hayo pia yamegusa kundi la wakusanyaji wa maudhui (Online Content Aggregators), ambao ada yao imeshushwa kutoka Sh1,000,0...