TARIMBA ANG’OLEWA UENYEKITI WA BUNGE SPOTS CLUB
Mbunge wa Kinondoni Abbas Tarimba leo ameondoshwa katika wadhifa wake wa Mwenyekiti wa Bunge Spots Club katika uchaguzi uliofanyika katika ukumbi wa Msekwa jijini Dodoma baada ya kuambulia kura 41 huku mpinzani wake Mbunge Mwanamama Rebeca Sanga Msemwa (Pichani), kujipatia kura 158. Wagombea katika nafasi hiyo walikuwa wawili tuu. Uchaguzi huo uliokuwa na bashasha kubwa huku wabunge na wafanyakazi wa bunge wakiwapigia kampeni wabunge walioonekana watawaogoza vyema kwa kipindi cha miaka mitano ijayo, aidha Makamu Mwenyekiti alichauguliwa Mbunge Thomas Maganga Kampala, aliyejinyakulia kura 135 huku akimwacha hoi mpinzani wake Mbunge Esther Matiko aliyeambulia kura 63. Uchaguzi huo ulisimamiwa na Mbunge Mashimba Ndaki ambapo pia alimtangaza Mbunge Festo Sanga,kwa wadhifa wa Meneja wa Timu , aliyejinyakulia kura 117 na kuwaacha hoi wapinzani wake watatu. Aidha Wabunge hao Viongozi wapya wa Bunge Spots Club wakiwa katika picha ya Pamoja baada ya kufan...