Posts

NEEMA YA KIDIJITALI: Serikali Yashusha Ada kwa Wanablogu, TCRA Yazindua Redio ya Kisasa 'DSB'

Image
SERIKALI imetangaza neema ya kihistoria kwa wanablogu, vijana wabunifu, na watoa maudhui mtandaoni nchini kwa kupunguza ada za leseni kwa kiwango kikubwa, hatua inayolenga kuchochea ukuaji wa uchumi wa kidijitali na kurasimisha shughuli za wahabarishaji wa mitandao. Hatua hiyo imekuja kufuatia utafiti wa kina na mikutano ya kimkakati ya takribani mwaka mzima kati ya mtandao wa Tanzania Bloggers Network (TBN) na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), ikielezea vikwazo vya gharama vilivyokuwa vikikwaza uandishi wa habari za kidijitali nchini. Akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano wa Mwaka wa Watoa Huduma za Utangazaji (ABC 2026) jijini Dodoma leo, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamisi Mwinjuma, amesema ada ya leseni kwa watoa maudhui mtandaoni imeshushwa kutoka Sh500,000 hadi Sh50,000 tu, huku ada ya maombi ikiwa ni Sh10,000 pekee. Mageuzi hayo pia yamegusa kundi la wakusanyaji wa maudhui (Online Content Aggregators), ambao ada yao imeshushwa kutoka Sh1,000,0...

TCRA YAWAKUTANISHA WANAHABARI JIJIJINI DODOMA

Image
Meneja wa Huduma za Utangazaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA),   Mhandisi Andrew Kisaka , akiwasilisha mada kuhusu Kanuni za wanahabari kwa washiriki wa Mkutano  Mkuu wa mwaka wa Vyombo vya Utangazaji, b      

SERIKALI YALIPA ASILIMIA 95 YA DENI LA KIHISTORIA MIFUKO YA HIFADHI, WAZIRI SANGU AIPONGEZA AWAMU YA SITA

Image
  S WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu akiwa katika picha ya pamoja ya Viongozi mara baada ya kuzindua Sera ya Taifa ya Kinga ya Jamii Jijini Arusha. @@@@@@@@@@@@@@ Na OWM-KAM,Arusha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mheshimiwa Deus Clement Sangu, ametoa shukrani za dhati kwa Serikali ya Awamu ya Sita kwa utaratibu wake wa kishujaa wa kulipa deni la kihistoria la shilingi trilioni 4 nukta 46 lililokuwa linaikabili mifuko ya hifadhi ya jamii nchini.  Akizungumza jijini Arusha wakati wa uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Kinga ya Jamii ya Mwaka 2023, Waziri Sangu amebainisha kuwa hadi sasa Serikali imefanikiwa kulipa asilimia 95 ya deni hilo ambalo lilirithiwa kutoka kipindi cha kabla ya mwaka 1999, hatua ambayo imesaidia kuimarisha ukwasi na ufanisi wa mifuko hiyo katika kuwahudumia wanachama. Mheshimiwa Sangu ameeleza kuwa hatua hiyo ni sehemu ya safari ndefu ya maboresho ya Sekta ya Kinga ya Jamii yaliyoanza ...

WAZIRI RIDHIWANI KIKWETE AWATAKA WAAJIRI NCHINI KUZINGATIA SHERIA NA KANUNI KATIKA USIMAMIZI WA RASILIMALIWATU

Image
  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Tume ya Utumishi wa Umma baada ya Waziri huyo kufungua kikao kazi cha mafunzo ya Tume ya Utumishi wa Umma kwa Mamlaka za Maji Tanzania cha Utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma na Matumizi ya Mfumo wa kielektroniki wa kushughulikia Rufaa na uwasilishwaji wa taarifa za masuala ya kiutumishi leo tarehe 9 Februari. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akisaini kitabu cha wageni baada ya kuwasili katika Ofisi za NSSF Mkoani Morogoro katika Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Na. Antonia Mbwambo, Ofisi ya Rais   Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora-Morogoro Tarehe: 9 Februari, 2026 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Jakaya Kikwete amez...