Posts

MOI SASA KIMBILIO LA WENGI ----------DKT MPOKI

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI),  Balozi Dkt Mpoki Ulisubisya ,  akizungumza leo  na wanahabari katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO  jijini Dodoma,  akisema Amelenga kuboresha huduma kwa kuanzisha mfumo wa miadi ya kidijitali ili kupunguza msongamano na kupendekeza huduma za saa 24.  Aidha amebainishwa kwamba kuwahi foleni usiku wa maneno kwa ajili ya kutibiwa hivi sasa haipo mgonjwa anaweza kuweka ahadi na Daktari wake  kwa kumpigia simu ukifika moja kwa moja unaenda kumuona, Hosptali ya moi imekuwa kimbilio la wengi tena baadhi kutoka nchi za nje. Amempongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha kutoa huduma hizo bora  ambapo sasa wanaweza kumtibu mgoja wa kichwa bila kumpasua vifaa vingi vya kisasa vipo vya kutosha  Huo ni uwezeshwaji wa Rais.   Wanahabari wakichukua habari kutoka kwa Dkt Mpaki alipokuwa akizungumza nao  

WANANCHI PERAMIHO, SHIWINGA KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MBUNGE, DIWANI

Image
  @@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@ Wapiga Kura 127,632 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura watashiriki katika uchaguzi wa kuchagua Mbunge katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mkoa wa Ruvuma na Kata ya Shiwinga iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe. Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele ameyasema hayo leo Februari 25, 2026 mjini Songea Mkoani Ruvuma wakati akisoma risala maalum kuhusu uchaguzi katika jimbo na kata husika utakao fanyika kesho Februari 26, 2026 na kusema kuwa jumla ya vituo 373 vya Kupigia Kura vitatumika. “Kati yao wapiga kura 120,780 ni wa Jimbo la Peramiho na wapiga kura 6,852 wapo katika kata ya shiwinga na jumla ya vituo 373 vya Kupigia Kura vitatumika, ambapo vituo 354 vipo Jimbo la Peramiho na vituo 19 vipo katika Kata ya Shiwinga Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi,”amesema Jaji Mwambegele. Aidha, amesema kwa uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Peramiho vyama vya sia...

KATIBU MTENDAJI MAMLAKA YA RUFANI YA ZABUNI ZA UMMA NCHINI NCHINI AZUNGUMZA NA WANAHABARI DODOMA

Image
Katibu Mtendaji wa   Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA)   nchini Tanzania ni   James Sando , akizungumza na wanahabari leo katika ukumbi wa Idara ya habari MAELEZO jijini Dodoma , akielezea utendaji kazi wa Mamlaka yake.   Aidha amebainisha kwamba  Mamlaka imefungua fursa kwa vijana 878 kwa kuwapatia mafunzo ya kuwajengea uwezo ili waweze kudai haki zao kwa ufanisi katika michakato ya ununuzi wa umma. ‎ Amesema kuwa mafunzo hayo yametolewa katika mikoa ya Dodoma, Dar es Salaam, Mwanza na Mbeya ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa azma ya Serikali ya kuwawezesha vijana na makundi maalum kushiriki kikamilifu katika sekta ya ununuzi wa umma. Wanahabari wakiwajibika katika mkutano huo  

WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO MKOANI ARUSHA

Image
  Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo tarehe 24 Februari, 2026 akifungua Semina ya Bodi za Wakurugenzi wa Mamlaka za Maji nchini unaofanyika katika hoteli ya Ngurdoto, jijini Arusha. Mkutano huo wa kitaifa unawakutanisha viongozi wakuu wa usimamizi wa Mamlaka 85 za maji nchini. PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo tarehe 24 Februari, 2026 akizungumza na Washirki wa Semina ya Bodi za Wakurugenzi wa Mamlaka za Maji nchini unaofanyika katika hoteli ya Ngurdoto, jijini Arusha. Mkutano huo wa kitaifa unawakutanisha viongozi wakuu wa usimamizi wa Mamlaka 85 za maji nchini. PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU Muonekano wa ujenzi wa Stendi Kuu ya Mabasi yaendayo mikoani unaotekelezwa katika eneo la Bondeni City kwenye Halmashauri ya Jiji la Arusha kwa gharama ya sh. bilioni 14.3 ambao leo tarehe 24 Februari, 2026 Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba alifanya ziara ya kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi huo. Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo tarehe 24 Februari,...

MARAIS DKT.JOHN MAGUFULI NA DKT.SAMIA SULUHU HASSAN WALIHESHIMISHA J W T Z.

Image
Helkopta  zikilipamba jengo jipya la Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT) lililopo eneo la Kikombo  Mkoani Dodoma, awali Makao Makuu hayo yalikuwa Upanga jijini Dar es Salaam. Jengo hilo la kisasa liliasisiwa na Rais wa awamu ya Tano marehemu  Dkt. John Pombe Magufuli  na kumaliziwa ujenzi wake na Rais wa Awamu ya Sita Dkt. Samia Suluhu Hassan.   Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo, Rais Samia amesema hakuna uwekezaji unaoweza kuja bila kuwepo mazingira salama, na kwamba haiwezekani kujenga ustawi wa wananchi bila amani. Ameeleza kuwa hivi karibuni shirika la kimataifa la tathmini ya ukuaji wa uchumi duniani, The Modes, limeipa nchi daraja la I, kiwango alichokieleza kuwa ni kizuri kwa mustakabali wa ukuaji wa uchumi. Ameongeza kuwa kadri taifa linavyoimarika kiuchumi, uwekezaji katika sekta ya ulinzi unakuwa jambo lisiloepukika kutokana na umuhimu wake kwa maendeleo na ustawi wa wananchi. Amesema Serikali itaendelea kuliwezesha Jeshi kuwa na mazingira bor...