WAZIRI MKUU MWIGULU ALIFUNGA BUNGE NA KUWATAKA WATANZANIA WATUNZE AMANI
HOTUBA YA MHESHIMIWA DKT. MWIGULU LAMECK NCHEMBA (MB.), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUAHIRISHA MKUTANO WA TATU (3) WA BUNGE LA 13 LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAREHE 26 JUNI, 2026 JIJINI DODOMA 1. Mheshimiwa Spika, awali ya yote ninamshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa fadhili zake zilizotuwezesha sote kuiona siku hii muhimu katika historia ya Bunge la 13. Kama mnavyofahamu, tumekutana leo kwa ajili ya kuhitimisha mkutano wa Tatu ambao ulikuwa mahsusi kwa ajili ya kupokea na kujadili bajeti ya serikali. 2. Mheshimiwa Spika, nimesema leo ni siku muhimu na ya kihistoria kwa sababu, hii ni Bajeti ya kwanza ya Serikali kupitishwa na Bunge la 13 baada ya uchaguzi mkuu wa 2025. Hongereni sana waheshimiwa Wabunge! 3. Mheshimiwa Spik...