BINGWA WA DUNIA WA MASUMBWI CRAWFORD KUITANGAZA SERENGETI KIMATAIFA
Na. Hance Mbena – Serengeti Katika muendelezo wa kuitangaza Tanzania duniani kupitia utalii wa michezo, leo Mei 28, 2026, bingwa wa masumbwi duniani, Terence “Bud” Crawford, amekabidhiwa rasmi ubalozi wa utalii baada ya kukutana na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji. Tukio hilo limefanyika ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ikiwa ni siku ya tano ya ziara yake nchini. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Dkt. Kijaji alieleza kuwa Serikali ya Tanzania chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeendelea kuifungua na kuitangaza sekta ya utalii kimataifa kupitia kampeni mbalimbali za kuitangaza nchi, ikiwemo filamu za “Tanzania: The Royal Tour” na “Amazing Tanzania” ambazo zimeendelea kuvutia wageni na watu mashuhuri kutoka mataifa mbalimbali duniani kutembelea Tanzania. “Michezo ni sehemu muhimu ya ajira na maendeleo ya uchumi, lakini pia imekuwa daraja la kuunganisha Tanzania na watu mashuhuri duniani. Kupitia michezo tunaende...