Posts

KUPANDA KWA MAFUTA NI DUNIA NZIMA WANANCHI WAJIHADHARI NA WAPOTOSHAJI

Image
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Kenan Kihongosi, amezungumza na wanahabari leo jijini Dodoma na kuwahakikishia  wananchi kwamba Serikali imeanzisha mfuko maalum kwa ajili ya kukabiliana na uhaba wa mafuta. Aidha Chama cha Mapinduzi kimeitaka Serikali kuhakikisha  inalitumia shirika la TPDC  kuwa muagizaji mafuta mkuu ili kuwauzia wananchi kwa bei ya soko kwani baadhi ya wafanyabishara huwa na mambo yao kwa kujali faida zaidi. Kihongosi amebainisha kwamba hakuna nchi ambayo haijaguswa na kupanda kwa mafuta hata kule ulaya mafuta yamepanda kuliko  Tanzania hata majirani wa Tanzania mfano hapo Kenya na Uganda bei ipo juu sana kuliko hapa nchini "Mafuta yamepanda kwenye soko la Dunia kutokana na vita vya mashariki ya kati  kati ya Marekani, Israel na Irani tuombee vita viishe ili hali ilejee kama kawaida", alisema Kihongosi. Aidha mewataka wanasiasa kuaacha kutumia uhaba wa mafuta kujitafutia umaarufu   

TUMWAMINI MUNGU TUACHANE NA MAUVUMI YA KUGUSANA MABEGA..... ASKOFU

Image
Askofu wa Kanisa la Pentecostal Evangelical of Africa (PEFA) la Sayuni City Charch lililopo eneo la Ntyuka jijini Dodoma........akitoa mahubilia kwa waumini wa kanisa hilo leo katika kuanzimisha sikukuu ya Pasaka, amabapo aliwaambia katika kuadhimisha sherehe hiyo watanzania hawana budi kumwamini mungu na mwanae Yesu Kristo, wajiepushe na mambo ya uvumi ,wapendane  kufanya hivyo watakuwa wanatenda haki katika nchi hii kutofanya hivyo ni kutakiana mabaya kila uchwao", oneni sasa mauvumi kila kona mara mtu kageuka chatu namara mtu akikushika bega sehemu zako za siri zinatoweka  nani siri zake zimetowe mbona hatumuoni  atoe ushahidi", alisema Askofu huyo na kuongeza kwamba maandiko yanasema kutakuwa na taabu nyingi, njaa ,matetemeka na manabii wa uongo ambao hivi sasa wanazusha kila balaa sasa ni wakati wa kumrudia mungu hayo yote yatakuwa hayanatija kwa binadamu wapendane waasche kuzuliana. ..  

WAZRI MKUU MWIGULU AWASILISHA BAJETI YAKE BUNGENI MNA KUSEMA WATALII WAMEONGEZEKA NA KUCHECHEMUA UCHUMI

Image
Jitihada kubwa zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi mahiri wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambazo zimetambuliwa kitaifa, kikanda na kimataifa zimechechemua kwa kiasi kikubwa kuongezeka kwa watalii nchini. Hayo yamebainishwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (pichani), Bungeni Jijini Dodoma kwenye hotuba yake kuhusu Mapato na Mwelekeo wa Kazi za Serikali na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na Ofisi ya Bunge kwa Mwaka 2026/2027. Dkt. Mwigulu amesema kutokana na uhuhimu wa Sekta ya Maliasili na Utalii katika ukuaji wa uchumi, ajira na pato la Taifa, Serikali imeendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ili kuinua sekta hiyo muhimu kwa uchumi wa nchi yetu. “Mikakati hiyo imeongeza idadi ya watalii wanaotembelea hifadhi za Taifa kwa asilimia 10.73 kutoka watalii 5,360,247 mwaka 2024 hadi 5,935,561 mwaka 2025 na hivyo kuongeza mapato yatoka...

LUKUVI ATAKUMBUKWA KWA MENGI-------WAZIRI MKUU: MWIGULU

Image
WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) na Mbunge wa Isimani, Mheshimiwa William Lukuvi atakumbukwa kwa mengi na Watanzania kutokana na utumishi wake uliotukuka katika nafasi mbalimbali alizohudumu. “Mheshimiwa Lukuvi atakumbukwa kwa mengi na Watanzania kutokana na utumishi wake uliotukuka katika nafasi mbalimbali. Mchango wake kwa Jamii na Watanzania kwa ujumla katika nafasi mbalimbali alizotumikia kuanzia Chama, Jimboni na Serikalini umekuwa chachu katika kuleta maendeleo kwa wananchi,” amesema Waziri Mkuu ambaye ameongoza mazishi hayo kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan. Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumanne, Machi 31, 2026) wakati akizungumza katika ibada ya mazishi ya marehemu iliyofanyika nyumbani kwake kwenye kijiji cha Idodi, wilayani Iringa, mkoani Iringa. “Kwa niaba ya Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan nitumie nafasi hii kuwahah...

CAG KICHERE AMKABIDHI RAIS SAMIA RIPOTI YA UKAGUZI KWA MWAKA 2024 NA 2425

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa Mwaka wa Fedha 2024/25 kutoka kwa Charles Kichere, Ikulu jijini Dar es Salaam, tarehe 30 Machi, 2026. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na  Ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa Mwaka wa Fedha 2024/25, Taarifa ya Mwaka ya Utendaji Kazi wa Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) pamoja na Taarifa ya Mwaka ya Utendaji Kazi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA),  baada ya kuzipokea leo Ikulu jijini Dar es Salaam. @@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@ Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Dkt. Charles Kichere, Machi 30, 2026, amewasilisha Ripoti Kuu ya mwaka wa fedha 2024/2025 kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Ikulu jijini Dar es Salaam ambapo amesema kuwa deni la Serikali bado ni himilivu na lipo ndani ya viwango salama...

MASHIMO KATIKA BARABARA YA DODOMA SINGIDA KAZI YA TANROADS KUYAZIBA----- MHANDISI MLAVI

Image
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Ephatar Mlavi (pichani),amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, itaendelea kuziba mashimo yaliyopo katika barabara ya kutoka Dodoma hadi Simgida, ambapo amebainisha kwamba Serikali ya Rais Samia   imeendelea kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika miundombinu ya barabara na madaraja ili kukuza uchumi wa taifa na kurahisisha usafirishaji. Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dodoma, katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO amesema kuwa uwekezaji huo umeimarisha kwa kiasi kikubwa kuchochea biashara za ndani na za kikanda. Aidha, amebainisha kuwa barabara ni mhimili mkuu wa uchumi kwani zaidi ya asilimia 80 ya usafirishaji wa mizigo na abiria hutegemea barabara, hali inayosukuma Serikali kuendelea kuimarisha sekta hiyo. Pia ameongeza kuwa hadi Desemba 2025, mtandao wa barabara nchini umefikia kilomita 182,164.41, huku TANROADS ikisimamia kilomita 37,734.4...