TANZANIA YA TATU KWA UBORA WA MBEGU AFRIKA
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI ) ndugu Nyasebwa Chimagu, akizungumza na wanahabari katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO jijini Dodoma leo ,kuhusu huduma za mbegu zinazotolewa na Taasisi yake, Kwa Twakimu za Kimataifa Mkurugenzi huyo alisema Tanzania ni ya tatu kwa ubora wa mbegu barani Afrika ikitanguliwa na Afrika Kusini na Nigeria na Kidunia ni ya 15, Mkurugenzi huyo aliendelea kusema kwamba Mbegu ni bidhaa inayosimamiwa na Serikali (regulated product) duniani kote kutokana na umuhimu wake kwa usalama wa chakula na lishe, na ni mojawapo ya pembejeo muhimu katika kuleta mageuzi ya kilimo (Agricultural Transformation) kwa kuongeza tija au technical efficiency, mapato na ubora wa mazao. Aidha, biashara ya mbegu hufanyika pia kimataifa kwa kuzingatia viwango vya ubora vya kimataifa. Mathani, hadi mwaka 2026, thamani ya biashara ya mbegu duniani ilifikia Dola za Kimarekani Bilioni 67.2. Kutokana na umuhimu huo, nchi nyin...