Posts

WABUNGE WAMWAGIA SIFA KEDEKEDE WAZIRI MKENDA NA NAIBU WAKE WANU NA KATIBU MKUU WA WIZARA HIYO MAMA NOMBO

Image
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo wamemwagia sifa kemu kemu Waziri  wa Elimu, Sayansi na Teknolojia,  Profesa  Adolf  Mkenda,    Naibu Waziri wa Wizara hiyo . Wanu Hafidh Ameir, wakati wa kuchangia bajeti ya wizara hiyo aliyoiwasilisha leo asubuhi na kuanza kujadiliwa na wabunge hao kila mbunge aliyenyayuka kuchangia alisifu ufanyaji kazi wao pamoja na watendadi wengine wa wizara hiyo wakidai ni wasikivu wapigie simu muda wowote wanatatua shida yako hususani watendaji hao wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo  Profesa. Carolyne Nombo. "Hakika wizara hiyo imepata watendaji elimu ya amali itatufikisha mbali tumechelewa sana kwa watendaji hawa tutafika mbali sana ni waelewa wanaelimu ambayo inawafanya wanaweza kwenda sehemu yoyote na kuchota ujuzi na kuuleta hapa nchini ", alisema mbunge wa Msalala Mabula Magangila Waziri wa Elimu sayansi na Teknolojia, Profesa. Adolf Mkenda akiwasilisha hotuba ya bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka ...

WAZIRI AWESO AWAKILISHA BAJETI YA WIZARA YAKE

Image
Waziri wa Maji, Jumaa Aweso,  akiwasilisha bajeti ya Wizara yake leo Bungeni,  pamoja na mambo mengine  aliwabainishia wabungeni kuwa  familia yake, hususan wake zake, ndiyo uwekezaji wake mkubwa na wa thamani zaidi. Akimshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumwamini tena kuongoza wizara hiyo amesema atahakikisha hamwangushi Rais atahakikisha anafanya kazi kwa uwezo wake wote. Kila Mtanzania atapata maji chini ya uongozi wa Rais kipenzi  cha Watanzania Mawaziri wakijadiliana bungeni wakati wa majadiliano ya bajeti hiyo Naomba maji na mimi kwetu shida huenda akisema hivyo mbunge  Asenga  akizungumza na waziri Aweso  

BAJETI YA WIZARA YA MAKONDA YAPITISHWA KWA SHANGWE BUNGENI

Image
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,  Paul Makonda (pichani)  amewasilisha bajeti ya Wizara yake kwa mwaka wa fedha 2026/27 Bungeni jijini Dodoma ambapo paamoja na  mambo mengine, aliweza kuwa na wageni wengi mmoja wapo ni Mwanasoka maarufu barani Afrika , Drogba. Aidha wasanii mbalimbali nchini pamoja na walimbwende waliunakisisha ukumbi wa bunge, hakika waziri huyp kijana amekuja na ubunifu mkubwa katika usomaji wa bajeti yake na ndiyo maana bajeti yake imeweza kujadiliwa na wabunge na kueleweka na kupitishwa kwa idadi kubwa ya wabunge  huku akimwagiwa sifa kemukemu kwa uchapa kazi wake pamoja na watendaji wake.   Uwasilishaji huo ulifanyika leo, Mei 4, 2026, ambapo pamoja na mambo mengine, amezungumzia mikakati mbalimbali ya wizara ikiwa  pamoja na masuala ya klabu za Simba na Yanga ambapo sasa muda umefika wa kuwa na viwanja vyao kutokana na ukongwe wao na jinsi wanavyoiletea sifa nchi hii. Walimbwende wakiongozwa na kiongozi wao Mu...