Posts

TARIMBA ANG’OLEWA UENYEKITI WA BUNGE SPOTS CLUB

Image
Mbunge wa Kinondoni Abbas Tarimba leo ameondoshwa katika wadhifa wake wa Mwenyekiti wa Bunge Spots Club katika uchaguzi uliofanyika katika ukumbi wa Msekwa jijini Dodoma baada ya kuambulia kura 41 huku mpinzani wake   Mbunge Mwanamama Rebeca   Sanga Msemwa (Pichani),   kujipatia kura 158. Wagombea katika nafasi hiyo walikuwa wawili tuu. Uchaguzi huo uliokuwa na bashasha kubwa huku wabunge na wafanyakazi wa bunge wakiwapigia kampeni wabunge walioonekana watawaogoza vyema kwa kipindi cha miaka mitano ijayo, aidha Makamu Mwenyekiti alichauguliwa Mbunge Thomas Maganga Kampala, aliyejinyakulia kura 135 huku akimwacha hoi mpinzani wake Mbunge Esther Matiko aliyeambulia kura 63. Uchaguzi huo ulisimamiwa na Mbunge Mashimba Ndaki ambapo pia alimtangaza   Mbunge Festo Sanga,kwa wadhifa wa Meneja wa Timu   , aliyejinyakulia kura 117 na kuwaacha hoi wapinzani wake watatu. Aidha Wabunge hao Viongozi wapya wa Bunge Spots Club wakiwa katika picha ya Pamoja baada ya kufan...

MAWASILIANO SASA KUWA KARIBU NA BURE ASEMA WAZIRI -----KAIRUKI MAWASILIANO SASA KUWA MARIBU NA BURE__________________________________________________________________________________________MAWASLIANO SASA KUWA KARIBU NA BURE _-------WAZIRI KARIUKI_______________________________________________________________________________________________________________________________

Image
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Angellah  Kairuki (Pichani) amesema kuwa Serikali imeendelea kudhibiti gharama za mawasiliano nchini ambapo gharama za kupiga simu ndani ya nchi zimeendelea kubaki shilingi 9 kwa dakika huku wastani wa bei ya data bila kifurushi ukiendelea kubaki shilingi 9.31 kwa MB moja, hali inayorahisisha wananchi wengi zaidi kumudu matumizi ya intaneti na huduma za kidigitali. ‎Akizungumza leo Februari 4, 2026 jijini Dodoma wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa ahadi za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ndani ya siku 100 kwa waandishi wa habari, Waziri Kairuki amesema mafanikio hayo yanatokana na uwekezaji unaoendelea kufanywa na Serikali katika miundombinu ya mawasiliano ikiwemo minara na Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano. ‎ Amebainisha kuwa hali ya upatikanaji wa mawasiliano imeendelea kuimarika ambapo laini za simu zilizosajiliwa zimeongezeka kutoka milioni 99.3 Oktoba 2025 hadi milioni 106.9 Januari 2026 sawa na ongezeko la asilimia 7, huku w...

WAZIRI PROFESA MAKAME AKEMEA MAKONDA WA DARADARA WANAONYAYASA WANAFUNZI

Image
Waziri  wa Uchukuzi  Profesa Makame Mbarawa  ametaka  hatua kali za kinidhamu zichukuliwe kudhibiti vitendo vya unyanyasaji dhidi ya wanafunzi wanaotumia usafiri wa mabasi ya mijini maarufu kama Daladala.  ‎ ‎Ameyasema hayo Waziri Profesa Mbarawa jijini Dodoma, wakati akizungumza na wanahabari kufuatia video iliyoenea mitandaoni ya mwanafunzi wa kidato cha kwanza, Mariana Eric Mirindima wa Shule ya Sekondari Jangwani, aliyewasilisha barua ya kueleza changamoto wanazokumbana nazo wanafunzi wanapotumia daladala. ‎Katika barua hiyo, ambayo mwanafunzi huyo alieleza kuwa baadhi ya makondakta wamekuwa wakigoma kuwabeba wanafunzi kwa madai kuwa hawalipi nauli kamili, hali inayowasababisha wanafunzi kusimama vituoni kwa muda mrefu, kuchelewa kufika shuleni au kushindwa kabisa kuhudhuria masomo. ‎ Prof. Mbarawa amempongeza mwanafunzi huyo pamoja na wazazi wake kwa ujasiri wa kutoa taarifa, na kubainisha  kuwa Serikali imeisikiliza sauti ya wanafunzi na itachukua hat...

LEO WABUNGE BUNGENI

Image
 

WAZIRI MKUU MCHEMBA AONGOZA AZANIA BENK BONANZA JIJINI DODOMA

Image
Waziri Mkuu Mwigulu Nchemba, akisani mpira wa miguu uliochezewa mechi ya watani wa jadi wbungeni wa Yanga na Simba katika Bonanza hilo aliyeshika mpira mhuo ni Mwamuzi Mstaafu wa Kimataifa Othamn Kazi(Mzee wa Kipenga cha Mwisho).