Posts

WATOTO WA KIKE WAOMBA KUOLEWA IWE MIAKA 18 MPANJU ASEMA LINAZUNGUMZIKA

Image
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Amon Mpanju, akisoma Hotuba yake katika Jukwa la Baraza la Watoto kwenye uzinduzi wa Kanuni za Uanzishwaji na uendeshwaji wa Mabaraza ya Watoto kuanzia vitongojini hadi Taifa Tanzania Bara na Visiwani, Mpanju aliwahakikishia washiriki hao kwamba Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni sikivu hakuna kinachoshindikana , maombi yao yatafanyiwa kazi ili watoto wa Taifa hili wajione  nao wanahaki ya kufaidi matunda ya nchi hii. Watoto ni lazima wawe na jukwaa linalowakutanisha kutoka maeneo mbalimbali ya nchi. kuwe na mfumo unaowajengea uwezo wa kujieleza,kusikilizana, kuheshimiana, kujifunza uongozi na kuelewa nafasi yao katika familia, jamii na Taifa. Naibu Katibu Mkuu, Amon Mpanju, akikata utepe wenye vitabu vya kanuni za watoto nchini Wahiriki  wakimkalibisha mgeni rasmi Watoto wakisikiliza kwa makii hotuba Wadau wakimsikiliza mgeni rasmi Sheria ya ndoa ya Mwaka 1971 inayoruhusu mvulana kuo...

NYONGO AOMBA USHIRIKIANO KUTATUA MIGOGORO YA ARDHI, KUINUA UWEKEZAJI PWANI

Image
  @@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@ MKUU wa Mkoa wa Pwani, Stanslaus Nyongo, amesisitiza ushirikiano na viongozi na watendaji katika kutatua changamoto mbalimbali, ikiwemo migogoro ya ardhi, kwa kuzingatia haki, taratibu, kanuni na sheria ili kupata suluhu za kudumu. Nyongo amesema mkoa unapaswa kujipanga kukabiliana na migogoro hiyo na kuhakikisha inakua ikipungua, huku akisisitiza umuhimu wa kila kiongozi na mtendaji kutekeleza wajibu wake kwa kuzingatia sheria na haki. Aidha, amesema ataendelea kuweka na kuboresha mazingira wezeshi ya uwekezaji ili kuvutia wawekezaji zaidi na kuhakikisha Pwani inaendelea kuwa kinara katika sekta ya viwanda na uwekezaji nchini. Nyongo aliyasema hayo Septemba 8, 2026, wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani kati yake na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo, Abubakar Mussa Kunenge, ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Songwe. “Mkoa huu ni wa uwekezaji, dira naifahamu, Nimezunguka nje ya nchi na ndani ya nchi kutafuta wawekezaji, nime...