Posts

MAKAMU WA RAIS DKT. NCHIMBI ATEMBELEA MAONESHO YA KIMATAIFA YA NANE NANE - DODOMA

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ameitaka Tume ya Maendeleo ya Ushirika kuendelea kufanya usimamizi wa vyama vya ushirika na kutoa miongozo ya kitaalamu kwa vyama vyote nchini.   Makamu wa Rais ametoa wito huo, wakati wa Siku Maalum ya Ushirika katika Maonesho ya Kimataifa ya Nane Nane kwa mwaka 2026, yanayofanyika katika Viwanja vya John Malecela, Nzuguni mkoani Dodoma. Amesisitiza Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO) kuhakikisha linaendelea kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwa vyama vya ushirika kwa lengo la kuhakikisha nidhamu ya matumizi ya fedha, kuzuia ubadhirifu na kuongeza uwazi katika uendeshaji wa vyama hivyo.   Makamu wa Rais, amesema Ushirika wenye uadilifu ni muhimu sana katika kujenga imani kwa wanachama na kuvutia uwekezaji zaidi. Amesema kuimarika kwa ushirika kunategemea uwajibikaji, uaminifu na uadilifu wa wanachama, viongozi na watendaji wa vyama vya ushirika.   Makamu wa Rais ...

SERIKALI YATOA MSIMAMO MGOGORO WA ARDHI NGETA

Image
 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi  Dkt Leonard Akwilapo akizungumza na wananchi Ngeta, Kata ya Kikongo katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani tarehe 1 Agosti 2026. @@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@ Na Munir Shemweta, Kibaha Serikali imesema shauri la mgogoro wa ardhi unaowahusu baadhi ya wananchi wa Ngeta, Kata ya Kikongo katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani, limefungwa katika ngazi ya Wizara baada ya kubainika kuwa madai yao hayana msingi wa kuendelea kushughulikiwa kwa mujibu wa sheria. Msimamo huo umetolewa wakati Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, alipokutana na kuzungumza na wananchi hao kufuatia malalamiko yao ya muda mrefu kuhusu umiliki wa ardhi katika eneo la Makazi Mapya. Wananchi hao wanadai kuwa walihamishwa kutoka katika maeneo yao wakati wa Operesheni Vijiji na kuacha mashamba pamoja na mazao ya kudumu, yakiwemo ya mikorosho, lakini baadaye maeneo hayo yakamilikishwa kwa watu wengine bila ...

WAZIRI WA FEDHA OMAR ASISITIZA USHIRIKIANO KUCHOCHEA MAPINDUZI YA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI NCHINI

Image
  Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar (MB), akipokelewa na Naibu Waziri wa Kilimo,  David Silinde, wakati alipowasili katika Viwanja vya Dk. John Samwel Malecelaa kwa ajili ya kujionea shughuli mbalimbali za kilimo, mifugo na uvuvi, zinazotekelezwa katika Maonesho ya 33 ya Kimataifa ya Kilimo 2026, yanayofanyika katika viwanja hivyo Nzuguni, jijini Dodoma. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mhe. Jabir Shekimweri. Maonesho hayo yana kauli mbiu ya ‘‘Tambua soko, Ongeza Tija kutekeleza Dira 2050’’. Waziri wa Fedha,  Balozi Khamis Mussa Omar (MB), na Naibu Waziri wa Kilimo,  David Silinde, wakioneshwa moja ya bidhaa zinazozalishwa na wajasiriamali, wakati alipotembelea katika Viwanja vya Dk. John Samwel Malecelaa kwa ajili ya kujionea shughuli mbalimbali za kilimo, mifugo na uvuvi, zinazotekelezwa katika Maonesho ya 33 ya Kimataifa ya Kilimo 2026, yanayofanyika katika viwanja hivyo Nzuguni, jijini Dodoma. Maonesho hayo yana kauli mbiu ya ‘‘Tambua soko, Ongeza Tija ...

NAIBU WAZIRI WANU ATOA WITO WA KUIMARISHA USHIRIKI WA WANAWAKE KATIKA STEM

Image
  Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia,  Wanu Hafadh Ameir, amesisitiza nafasi muhimu ya wanawake wanataaluma katika kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Akizungumza jijini Dar es Salaam katika hafla ya Inclusive Mwalimu Gala 2026, Naibu Waziri amesema kuwa kauli mbiu ya hafla hiyo, “The Contribution of Women Professionals to the Implementation of Tanzania Development Vision 2050”, imeakisi mchango wa wanawake katika kujenga uchumi wa maarifa, ubunifu na teknolojia. Ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika sekta ya elimu. Hatua zilizotekelezwa ni pamoja na maboresho ya sera na sheria, ujenzi wa miundombinu ya kufundishia na kujifunzia, pamoja na kuimarisha matumizi ya teknolojia katika ufundishaji na ujifunzaji. Aidha, amesisitiza kuwa mchango wa wanawake hauwezi kupuuzwa na kwamba Serikali ikiendelea kuimarisha usawa wa kijinsia, kuongeza ushiriki wa wanawake katika fani za ST...