Posts

NMB BUNGE BONANZA LAFANA JIJINI DODOMA

Image
Mchezaji wa timu ya Bunge, Dkt. Christina Mnzava, akipokea kikombe toka kwa Naibu Spika Daniel Sillo, baada ya timu ya wabunge kuibuka washindi wa Nmb Bunge Bonanza lililofanyika leo jijini Dodoma.   Bunge limewakutanisha washiriki 1,000 kutoka wizara 14 na taasisi 10  bonanza hilo limefayika katika viwanja vya Shule ya Sekondari John Merlini, jijini Dodoma, leo, Agosti 29, 2026. Ushindani mkali ulikuwa kutoka kwa timu za Bunge, wizara, Taasisi na NMB,  kujenga mshikamano na kuongeza uelewa kuhusu kinga dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza. Aidha kulikuwa na watu wa Damu Salama, walikuwa wakihitaji wananchi wa kuchangia damu. Aidha Naibu Spika Sillo, amewaasa  wabunge na wananchi kujitahidi kufanya mazoezi ili kujiepusha na magonjwa nyemelezi .Naibu aliyasema hayo wakati wa kufunga Bonanza hilo ambapo alimwakilisha Spika Mussa Azanni Zungu  

JAJI MKUU MASAJU AMWAPISHA NDEJEMBI LEO IKULU YA CHAMWINO JIJINI DODOMA

Image
J aji Mkuu wa Tanzania, George Masaju, akimwapicha   Deogratius John Ndejembi, kuwa   Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo asubuhi Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma. Kushoto anayeshuhudiam ni Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Ndejembi akitia sahihi kiapo chake  Vigogo ws Kamati ya Ulinzi na Usalama, wakiteta kabla ya kushuhudia kiapo  

MAKAMU WA RAIS MTALAJIWA NDEJEMBI APIGIWA KURA NA WABUNGE 324

Image
Mpambe wa Rais ( ADC) Brigedia Jenerali Nyamburi   Mashauri, akitoa heshima kwa wabunge  baada ya kutambulishwa bungeni na spika, mpambe huyo alileta barua yenye jina la Makamu wa Rais Mteuliwa  kwa ajili ya kujadiliwa na kupigiwa kura na wabunge Spika Mussa Azzan Zungu, akiwaonyesha wabunge barua toka kwa Rais Dkt. Sam,a Suluhu Hassan, yenye jina la Makamu wa Rais Mteuliwa  Ndejembi akionyesha unyenyekevu alipokuwa akijadiliwa na wabunge huku kulia rafiki yake Waziri Mavunde, akipiga makofi Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba, akitoa hoja bungeni kwa ajili ya kupigiwa kura Makamu wa Rais Mtalajiwa  Mbunge wa Mlalo Rashidi Shangazi, akimwelezea Ndejembi Wabunge 324 wamepiga kura za ndio kumthibitisha Makamu wa Rais Mteule Deogratius Ndejembi katika mchakato ambao umefanyika leo Bungeni jijini Dodoma. Katika uchaguzi huo hakukuwa na kura za hapana wala kura zilizoharibika, hakika wabunge waliosema hilo ni chaguo la Mungu na anayefatia ni Rais Dkt .Samia Suiluhu Has...

NMB BUNGE BONANZA KUFANYIKA KESHO JIJINI DODOMA

Image
Mkuu wa Idara ya Biashara za Serikali wa Benki ya NMB, Vicky Bishubo, akizungumza na wanahabari leo wakati wa kukabidhi vifaa vya michezo ya Bonanza la NMB Bunge Bonanza litakalofanyika jijini Dodoma kesho, Hafla ya makabidhiano hayo yalifanyika ukumbi wa Spika Dodoma , Bonanza hilo linatalajiwa kuongozwa na Spika wa Bunge Mussa Azzan Zungu. aliwaambia wanahabari benki hiyo imekuwa na kawaida ya kutoa asilimia ya faida yake kwa kutoa huduma kwa jamii na bunge ni sehemu ya jamii hiyo, amewaomba wananchi wa mkoa wa Dodoma na vitongoji vyake kujitokeza kwa wingi kuja kujionea bonanza la kukata na shoka kesho. Nae Mwenyekiti wa Kamati inayoratibu uendeshaji wa matamasha ya Bunge Bonanza,   Festo Sanga , ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Makete, aliwaambia wanahabri kwamba benki hiyo imekuwa ni mkombozi wa wabunhge wengi ambao hujitokeza kufanya mazoezi kwa kulinda afya za mili yao , alinainisha kwamba kesho kutakuwa na michezo mingi na wamealika Taasisi mbalimbai za serikali kuja kush...