WAKULIMA TANZANIA CHANGAMKIENI MIKOPO KWENYE BENKI YAKE---NYABUNDEGE
Mkurugenzi Mwendeshaji, Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) Frank Nyabundege, akizungumza na wanahabri leo asubuhi katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO Mtumba jijini Dodoma, Mkurugenzi huyo, amewaomba wakulima wa tanzania kuchangamkia mikopo inayotolewa na benki hiyo ambayo liba yake ni kidogo, akawataka wajiepushe na mikopo ya kausha damu ambayo imekuwa ikiwafanya wananchi kudaiwa na wengine kupata presha na kupelekea vifo. Aidha alianza kuwaeleza wanahabri kwamba TADB ni benki ya Serikali iliyoanzishwa kuwezesha wakulima, wafugaji na wavuvi kupata huduma za kifedha. • Adhima kuu ya TADB ni kuchangia kuimarisha usalama wa chakula na kupunguza umaskini kupitia mageuzi ya sekta ya kilimo. • TADB inatekeleza dhamira hiyo kwa kutoa suluhisho bunifu za kifedha zinazojenga minyororo ya thamani ya kilimo iliyo endelevu na jumuishi. • Benki imeanzishwa pia kuhakikisha kilimo kinabadilika kutoka kilimo cha kujikimu kwenda k...