Posts

WACHIMBAJI MADINI WACHANGA WAJIUNGE KWENYE VIKUNDI ILI WAWEZE KUPATA MIKOPO

Image
Mkaguzi Mkuu wa Migodi na Mazingira Tume ya Madini Mhandisi Hamis kamando, akizungumza na wanahabari kuhusu utendaji kazi wa Tume hiyo. Mazungumzo hayo yalifanyika Idara ya habari MAELEZO jijini Dodoma. Wachimbaji wadogo wa madini nchini wametakiwa kujiunga katika vikundi vya watu kumi ili kukidhi kiwango cha kuo,ba mikopo katika mabenki nchini, gharama ya kuomba mmoja mmoja ni kubwa, hayo yameelezwa na Mkaguzi Mkuu wa Migodi na Mazingira wa tume ya Madini nchini Hamis Kamando alipokuwa akizungumza na wanahabri leo.  

AMINI USIAMINI JENGO HILI INADAIWA LIMEUZWA SH BILIONI 6 JIJINI DODOMA

Image
Jengo hili lililopo katika makutano ya barabara za Oney Way na Sido jijini Dodoma ,inadaiwa limeuzwa kwa fedha za Kitanzania Bilioni 6 na dalali aliyefanikisha mpango huo kajipatia Sh Milioni 200. Je jengo hili linastahili kwa fedha hiyo na aliyenunua  anadaiwa ni kijana wa kijiweni   

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE NISHATI NA MADINI YARIDHISHWA NA KIWANDA CHA NGUZO ZA ZEGE

Image
  *Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita  * Yaipongeza TANESCO kwa usimamizi wa Ujenzi wa Kiwanda hicho * Shilingi Bilioni 8 zawekezwa ujenzi wa Kiwanda  @@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@ Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeridhishwa na Ujenzi wa Kiwanda cha Zege kinachomilikiwa na kampuni tanzu ya TANESCO ya kuzalisha nguzo za zege kilichopo katika Mkoa wa Tabora wakati wa ziara yao ya kikazi Mkoani humo tarehe 12 Machi, 2026. Akizungumza baada ya ziara hiyo Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mwanamama shupavu Mbunge wa Bagamoyo, Subira Mgallu ameeleza kuridhishwa na hatua ya kukamilika kwa Kiwanda hicho kilichoanza uzalishaji na kuwaelekeza Wizara ya Nishati na TANESCO kukisimamia kiwanda hicho kiendelee kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa na kuzalisha faida. “Kwa niaba ya Kamati tumeridhika na kazi kubwa iliyofanyika katika kiwanda hiki ambacho kimekamilika na uzalishaji umeanza, tunatoa rai kwa Wizara na TANESCO kuendelea kusimamia kiwanda hiki ...

TANZANIA YAENDELEA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA

Image
  Na WMJJWM – New York, Marekani   Serikali ya Tanzania imesisitiza dhamira yake ya kuendelea kutekeleza kikamilifu makubaliano ya kimataifa yanayohusu usawa wa kijinsia na maendeleo, sambamba na kuimarisha juhudi za kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia katika jamii.   Akizungumza katika mkutano huo, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima, amesema Tanzania inaendelea kuthibitisha dhamira yake ya kutekeleza kikamilifu na kwa ufanisi hatua zilizowekwa katika makubaliano mbalimbali ya kimataifa kuhusu jinsia na maendeleo ambayo nchi imeridhia. Dkt. Gwajima amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizoingia katika makubaliano na maazimio mbalimbali ya kimataifa, ikiwemo Azimio na Jukwaa la Utekelezaji la Beijing, Mkataba wa Kutokomeza Aina Zote za Ubaguzi Dhidi ya Wanawake (CEDAW) pamoja na Malengo ya Maendeleo Endelevu ya mwaka 2030.   Ameeleza kuwa Serikali inaendelea kutekeleza mipango na mikakati mbalimbali yenye...

WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU AAGIZA WATENDAJI NCHINI WAJIPANGE KUHUSU UWEKEZAJI USIOKUWA NA UBABAISHAJI

Image
  WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewaagiza Wakuu wa Mikoa na watendaji wao katika mikoa yote nchini wajipange kutoa taarifa kuhusu uwekezaji na ukuzaji wa biashara kwenye mikoa  kila wanapotoa taarifa kwa viongozi wa kitaifa   Ametoa wito huo leo jioni (Jumatano, Machi 11, 2026) wakati akifunga Mkutano wa Kuhakiki Rasimu ya Pili ya Mpango wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji (Mkumbi II) uliofanyika katika ukumbi wa Kambarage, HAZINA, jijini Dodoma.   Alisema mapendekezo yote yaliyowasilishwa na washiriki wa mkutano huo ambao ni Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa pamoja na Wakurugenzi yaandaliwe katika mfumo wa mkakati wa utekelezaji ili kuwezesha kuwa wa ufanisi.    “Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala na Wakurugenzi wa Halmashauri mbebe jukumu la kuwa mabalozi wa kwanza wa uwekezaji katika maeneo yenu kwa kutambua na kutangaza fursa mbalimbali zilizopo katika maeneo yenu, “Tubebe hili jukumu, kila Mkuu wa Mkoa anapotoa taa...