Posts

MIFUGO KUINGIA KWENYE VYANZO VYA MAJI NI TATIZO----- DKT. SHINHU

Image
Mkurugenzi wa Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria (LVBWB) nchini Tanzania   Dkt. Renatus Shinhu , akizungumza na wanahabari katika ukumbi wa Idara ya Habari MA EKLEZO jijini Dodoma leo akizungumzia  utendaji kazi wa bodi hiyo  akifafanua Ofisi yake inawajibika na usimamizi wa rasilimali za maji katika bonde hilo, ikijumuisha kuhakikisha upatikanaji endelevu wa maji na kushirikiana na wadau mbalimbali kuongoza miradi ya maendeleo ya maji  

TUME YA USHINDANI FCC INAMENO -----NGASONGWA

Image
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Khadija Ngasongwa ,akizungumza na wanahabari katika ukumbi wa mikutano wa Idara ya habari MAELEZO jijini Dododoma leo, akiwaeleza kuhusu majukumu ya tume hiyo na utekelezaj wake kwa siku 100 za Rais Dkt. Samia Suhuhu Hassan, Kaimu huyo alibainisha kwamba tume yake   ya Ushindani   ( FCC ) ni Taasisi   ya   Umma iliyoanzishwa kwa mujibu wa kifungu cha 62(1) cha Sheria   ya Tume ya Ushindani   Na. 8   ya   mwaka 2003 (FCA). Aidha Ngasongwa amebainishwa kwamba  TCC   ina "meno" (uwezo wa kisheria na nguvu) ya kudhibiti biashara, ina mamlaka ya kukuza ushindani wa haki, kuzuia mienendo ya kibiashara inayohadaa, kudhibiti bidhaa bandia, na kuilinda haki ya mlaji Baadhi ya maofisa wa Tume hiyo na waidara ya habari maelezo wakiwa katika mkutano huo Wanahabari wqakiwjibika  

MOI SASA KIMBILIO LA WENGI ----------DKT MPOKI

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI),  Balozi Dkt Mpoki Ulisubisya ,  akizungumza leo  na wanahabari katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO  jijini Dodoma,  akisema Amelenga kuboresha huduma kwa kuanzisha mfumo wa miadi ya kidijitali ili kupunguza msongamano na kupendekeza huduma za saa 24.  Aidha amebainisha kwamba kuwahi foleni usiku wa maneno kwa ajili ya kutibiwa hivi sasa haipo mgonjwa anaweza kuweka ahadi na Daktari wake  kwa kumpigia simu ukifika moja kwa moja unaenda kumuona, Hosptali ya moi imekuwa kimbilio la wengi tena baadhi kutoka nchi za nje. Amempongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha kutoa huduma hizo bora  ambapo sasa wanaweza kumtibu mgoja wa kichwa bila kumpasua vifaa vingi vya kisasa vipo vya kutosha  Huo ni uwezeshwaji wa Rais.   Wanahabari wakichukua habari kutoka kwa Dkt Mpaki alipokuwa akizungumza nao  

WANANCHI PERAMIHO, SHIWINGA KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MBUNGE, DIWANI

Image
  @@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@ Wapiga Kura 127,632 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura watashiriki katika uchaguzi wa kuchagua Mbunge katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mkoa wa Ruvuma na Kata ya Shiwinga iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe. Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele ameyasema hayo leo Februari 25, 2026 mjini Songea Mkoani Ruvuma wakati akisoma risala maalum kuhusu uchaguzi katika jimbo na kata husika utakao fanyika kesho Februari 26, 2026 na kusema kuwa jumla ya vituo 373 vya Kupigia Kura vitatumika. “Kati yao wapiga kura 120,780 ni wa Jimbo la Peramiho na wapiga kura 6,852 wapo katika kata ya shiwinga na jumla ya vituo 373 vya Kupigia Kura vitatumika, ambapo vituo 354 vipo Jimbo la Peramiho na vituo 19 vipo katika Kata ya Shiwinga Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi,”amesema Jaji Mwambegele. Aidha, amesema kwa uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Peramiho vyama vya sia...

KATIBU MTENDAJI MAMLAKA YA RUFANI YA ZABUNI ZA UMMA NCHINI NCHINI AZUNGUMZA NA WANAHABARI DODOMA

Image
Katibu Mtendaji wa   Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA)   nchini Tanzania ni   James Sando , akizungumza na wanahabari leo katika ukumbi wa Idara ya habari MAELEZO jijini Dodoma , akielezea utendaji kazi wa Mamlaka yake.   Aidha amebainisha kwamba  Mamlaka imefungua fursa kwa vijana 878 kwa kuwapatia mafunzo ya kuwajengea uwezo ili waweze kudai haki zao kwa ufanisi katika michakato ya ununuzi wa umma. ‎ Amesema kuwa mafunzo hayo yametolewa katika mikoa ya Dodoma, Dar es Salaam, Mwanza na Mbeya ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa azma ya Serikali ya kuwawezesha vijana na makundi maalum kushiriki kikamilifu katika sekta ya ununuzi wa umma. Wanahabari wakiwajibika katika mkutano huo