Posts

BINGWA WA DUNIA WA MASUMBWI CRAWFORD KUITANGAZA SERENGETI KIMATAIFA

Image
  Na. Hance Mbena – Serengeti  Katika muendelezo wa kuitangaza Tanzania duniani kupitia utalii wa michezo, leo Mei 28, 2026, bingwa wa masumbwi duniani, Terence “Bud” Crawford, amekabidhiwa rasmi ubalozi wa utalii baada ya kukutana na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji. Tukio hilo limefanyika ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ikiwa ni siku ya tano ya ziara yake nchini. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Dkt. Kijaji alieleza kuwa Serikali ya Tanzania chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeendelea kuifungua na kuitangaza sekta ya utalii kimataifa kupitia kampeni mbalimbali za kuitangaza nchi, ikiwemo filamu za “Tanzania: The Royal Tour” na “Amazing Tanzania” ambazo zimeendelea kuvutia wageni na watu mashuhuri kutoka mataifa mbalimbali duniani kutembelea Tanzania. “Michezo ni sehemu muhimu ya ajira na maendeleo ya uchumi, lakini pia imekuwa daraja la kuunganisha Tanzania na watu mashuhuri duniani. Kupitia michezo tunaende...

JESHI LA KUJENGA TAIFA (JKT) LAWAITA KIDATO CHA SITA KUANZA MAFUNZO KWA MUJIBU WA SHERIA ZA NCHI

Image
MKUU wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele amewataka wahitimu wa kidato cha sita Tanzania Bara na Visiwani waliochaguliwa kujiunga na mafunzo ya Jeshi hilo kwa mujibu wa sheria kuripoti katika makambi waliyopangiwa  ili waweze kuanza mafunzo ya  uzalendo,ukakamavu ,kufundishwa nidhamu,Umoja wa Kitaifa,Stadi za kazi na utayari wa kulijenga na kulitumikia Taifa pasipo kulinyongonyesha. Akizungumza na Wanahabari kwa niaba yake leo katika ofisi za Makai Mkuu ya Jeshi hilo jijini Dodoma    Mkuu wa Tawi la Utawala JKT Brigedia Jenerali Hassan Mabena, amesema majina ya waliochaguliwa yanapatikana kwenye tovuti ya JKT ambayo ni  www.jkt.mil.tz. Hii hapa ni taarifa nzima ya Mkuu huyo.  TAARIFA KWA UMMA WITO WA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA JKT KUNDI LA LAZIMA (MUJIBU WA SHERIA) MWAKA 2026 Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Meja Jenerali Rajabu Nduku Mabele, anatoa wito kwa Vijana waliohitimu elimu y a sekondari kidato cha sita mwaka 2026, kutoka shule zo...

VIGOGO WA WIZARA YA ARDHI NA MAENDELEO YA MAKAZI WAPO UKUMBINI TAYARI KWA BAJETI

Image
Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Mhan disi Anthony Sanga (kulia), akisalimiana  na  Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Hamad Abdallah baada ya kukutana  katika ukumbi wa bunge wa Spika jijini Dodoma kwa ajili ya kusikiliza uwasilishwaji wa bajeti ya wizara hiyo leo utakaofanywa na  Waziri wa wizara hiyo Katibu Mkuu MMjhandi Sanga, akisalimiana na aliyewahi kuwa Waziri wa Wizara hioyo Angelina Mabula  

MBUNGE LUFUNGIJA ALILIA MAENDELEA JIMBONI KWAKE SERIKALI YAAHIDI KUMPELEKEA

Image
Mbunge wa jimbo la Ulyangulu CCM,  Masanja Lufungija (pichani) leo akichangia bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani, ameitaka Serikali kukamilisha ujenzi wa vituo vya Polisi vilivyojengwa na wananchi kwa kujitolea imebaki umaliziaji tuu wa kuezeka mabati na sakafu. Akijibu maswal ya wabuge  waliochangia  bajeti hiyo Waziri wa wizara hiyo Protas Katambi amemhakikishia mbunge huyo kwamba bajeti ya mwaka huu watahakikisha maboma hayo yanamaliziwa ili kuwe na vituo hivyo . Kabla ya hapo katika maswali ya asubuhi alimuuliza Waziri wa ujenzi ni lini Barabara ya  Kahama Ulyangulu Kaliua Mpanda itajengwa kwani tangu mwaka 2015 aliahidi mgombea urais pia na Mgombea Mwenza  kwamba ingejengwa hadi leo haijajengwa.  

WAZIRI KAPINGA ASOMA BAJETI YA WIZARA YAKE LEO. WABUNGE WAMSIFIA KWA UTENDAJI KAZI

Image
Waziri wa Viwanda na Biashara , Judith Kapinga, akiwasilisha Hotuba ya  Makadilio ya Bajeti ya Wizara yake kwa mwaka  2026 na 2027 bungeni Dodoma  leo. Soma hotuba yake yote hapa 1. Mheshimiwa Spika; kutokana na taarifa iliyowasilishwa leo hapa Bungeni na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo ambayo imechambua Bajeti ya Wizara ya Viwanda na Biashara tarehe 24 na 26 Machi, 2026, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu likubali kupokea na kujadili Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Mwaka 2025/2026. Aidha, ninaliomba Bunge lako likubali kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda na Biashara kwa Mwaka 2026/2027. 2. Mheshimiwa Spika; nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema, kwa afya njema na kuwepo hapa siku hii muhimu ya leo. 3. Mheshimiwa Spika; kwa unyenyekevu na moyo wa shukrani, nitumie nafasi hii kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, R...