WAZIRI DKT. NYANSAHO AWASILISHA BAJETI YA WIZARA YAKE LEO BUNGENI JIJINI DODOMA
Mheshimiwa Spika, kufuatia taarifa iliyowasilishwa leo hapa Bungeni na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) iliyochambua na kutoa ushauri ulioboresha Bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, ninaomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu likubali kupokea na kujadili Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2025/26. Aidha, ninaomba Bunge lako Tukufu lijadili na kupitisha Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2026/27 kwa mafungu yote matatu (Fungu 57 - Wizara, Fungu 38 - NGOME na Fungu 39 - JKT). 2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote nitumie fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema, kwa kuijalia Nchi yetu amani, utulivu na mshikamano na kutuwezesha kuendelea kutumikia Taifa letu kwa uaminifu na uadilifu tukiwa wenye afya njema. 3. Mheshimiwa Spika, napenda kuungana na waheshimiwa wabunge wenzangu waliot...