WABUNGE WAMWAGIA SIFA KEDEKEDE WAZIRI MKENDA NA NAIBU WAKE WANU NA KATIBU MKUU WA WIZARA HIYO MAMA NOMBO
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo wamemwagia sifa kemu kemu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, Naibu Waziri wa Wizara hiyo . Wanu Hafidh Ameir, wakati wa kuchangia bajeti ya wizara hiyo aliyoiwasilisha leo asubuhi na kuanza kujadiliwa na wabunge hao kila mbunge aliyenyayuka kuchangia alisifu ufanyaji kazi wao pamoja na watendadi wengine wa wizara hiyo wakidai ni wasikivu wapigie simu muda wowote wanatatua shida yako hususani watendaji hao wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa. Carolyne Nombo. "Hakika wizara hiyo imepata watendaji elimu ya amali itatufikisha mbali tumechelewa sana kwa watendaji hawa tutafika mbali sana ni waelewa wanaelimu ambayo inawafanya wanaweza kwenda sehemu yoyote na kuchota ujuzi na kuuleta hapa nchini ", alisema mbunge wa Msalala Mabula Magangila Waziri wa Elimu sayansi na Teknolojia, Profesa. Adolf Mkenda akiwasilisha hotuba ya bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka ...