Posts

RIDHIWANI AWASILISHA BAJETI YA WIZARA YAKE NA YAPITA BIRA KUPINGWA

Image
Waziri   wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,   Ridhiwani   Kikwete leo, akiwasilisha bajeti ya wizara hiyo mbele ya wabunge jijini Dodoma Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete amesema Serikali kupitia Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma imeimarisha maadili ya viongozi wa umma ambapo asilimia 85 ya viongozi wamewasilisha matamko ya mali na madeni yao. Amebainisha kwamba  hatua hiyo inaonyesha kuimarika kwa uwajibikaji wa viongozi na uaminifu wa wananchi kwa taasisi za umma, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kujenga Serikali inayowajibika, yenye uwazi na inayoaminika kwao. Pia Ridhiwani amesema wananchi 34,334 wamepatiwa elimu ya maadili, hatua inayochangia kukuza utamaduni wa uadilifu na uwajibikaji katika jamii. Aidha Waziri Ridhiwani amesema Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kusimamia maadili kwa vitendo kwa sababu uadilifu wa viongozi ndio msingi wa haki, maendele...

WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU AHITIMISHA BAJETI YAKE NA KUPITISHWA KWA KISHINDO NA WABUNGE

Image
Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba, akihitimisha bajeti ya Wizara yake leo bungeni jijini Dodoma ambapo iliweza kuchangiwa na wabunge kwa muda wa wiki moja  ambapo iligusa nyanja mbalimbali, wabunge walimpongeza kwa kazi anazozifanya  kwa kuweza kutembelea mikoani na kugusa majimbo yake ambapo aliweza kuzumngumza na wananchi moja kwa moja, akihitimisha amesema sasa ni muda wa kuwatumikia wananchi na siyo muda wa maneno sasa ni vitendo tuu asiyetaka kwenda na kasi yake ampishe ameapa kutumikia wananchi "Nimewasikia kwa masikio yangu mkitoa michango yenu sasa tukachape kazi fedha zitatoka kilambunge atapata kwenye jimbo lake ili tuweze kuletea mandeleo wananchi wanamatalajio makubwa na Chama cha  Mapinduzi walichokichagua kwa kishindo",alisema Nchemba. Wakuu wa Mikoa wakisikiliza bajeti ya Waziri Mkuu