WAZIRI PROFESA MAKAME AKEMEA MAKONDA WA DARADARA WANAONYAYASA WANAFUNZI
Waziri wa Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa imetaka hatua kali za kinidhamu zichukuliwe kudhibiti vitendo vya unyanyasaji dhidi ya wanafunzi wanaotumia usafiri wa mabasi ya mijini maarufu kama Daladala. Ameyasema hayo Waziri Profesa Mbarawa jijini Dodoma, wakati akizungumza na waandishi wa habari kufuatia video iliyoenea mitandaoni ya mwanafunzi wa kidato cha kwanza, Mariana Eric Mirindima wa Shule ya Sekondari Jangwani, aliyewasilisha barua ya kueleza changamoto wanazokumbana nazo wanafunzi wanapotumia daladala. Katika barua hiyo, ambayo mwanafunzi huyo alieleza kuwa baadhi ya makondakta wamekuwa wakigoma kuwabeba wanafunzi kwa madai kuwa hawalipi nauli kamili, hali inayowasababisha wanafunzi kusimama vituoni kwa muda mrefu, kuchelewa kufika shuleni au kushindwa kabisa kuhudhuria masomo. Prof. Mbarawa amempongeza mwanafunzi huyo pamoja na wazazi wake kwa ujasiri wa kutoa taarifa, na kubainisha kuwa Serikali imeisikiliza sauti ya wanafunzi na itac...