Posts

WAKULIMA TANZANIA CHANGAMKIENI MIKOPO KWENYE BENKI YAKE---NYABUNDEGE

Image
  Mkurugenzi Mwendeshaji, Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) Frank Nyabundege, akizungumza na wanahabri leo asubuhi katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO Mtumba jijini Dodoma, Mkurugenzi  huyo, amewaomba wakulima wa tanzania kuchangamkia mikopo inayotolewa na benki hiyo ambayo liba yake ni kidogo, akawataka wajiepushe na mikopo ya kausha damu ambayo imekuwa ikiwafanya wananchi kudaiwa na wengine kupata presha na kupelekea vifo. Aidha alianza kuwaeleza wanahabri kwamba   TADB ni benki ya Serikali iliyoanzishwa kuwezesha wakulima, wafugaji na wavuvi kupata huduma za kifedha. •    Adhima kuu ya TADB ni kuchangia kuimarisha usalama wa chakula na kupunguza umaskini kupitia mageuzi ya sekta ya kilimo. •    TADB inatekeleza dhamira hiyo kwa kutoa suluhisho bunifu za kifedha zinazojenga minyororo ya thamani ya kilimo iliyo endelevu na jumuishi. •    Benki imeanzishwa pia kuhakikisha kilimo kinabadilika kutoka kilimo cha kujikimu kwenda k...

PROFESA MKENDA AZUNGUMZA NA WANAHABARI LEO JIJINI DODOMA KUHUSU WANAFUNZI 150

Image
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia. Profesa Aldof Mkenda, akiingia katika ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo kwa ajili ya kuzungumza na waandishi wa Habari kuhusu wanafunzi 150 waliochanguliwa katika mpango wa masomo wa Samia Scholarship kwa mwaka wa masomo 2026 na 2027.Mazungumzo hayo yamefanyika jijini Dodoma leo . Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, akizungumza na waandishi wa Habari leo jijini Dodoma ofisini kwake  kuhusu wanafunzi 150 waliofanya vizuri zaidi katika mtihani wa Kidato cha Sita mwaka 2026 ambao watanufaika na mpango wa Samia Scholarship kwa mwaka wa masomo 2026/2027, ukiwahusisha wanafunzi waliofanya vizuri katika masomo ya sayansi, hisabati na tiba.Vigezo na Sifa za Wanufaika Ufaulu wa Juu: Wanafunzi waliochaguliwa ni wahitimu waliopata alama za juu (marks) katika mitihani yao ya Kidato cha Sita kwenye tahasusi za sayansi kama vile PCM, PCB, CBG, PMG, CBA na PMC.Fani za Kipaumbele: Wanufaika wametakiwa kujiunga na shahada zin...