Posts

KUMBUKUMB YA PICHA ZA EMMELICIANA KUPATA KIPAIMALA KANISA KUU BAGAMOYO

Image
 

JWT MWENYEJI WA MAADHIMISHO YA SITA YA WIKI YA USHIRIKIANO KWA MAJESHI YA EAC

Image
Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Utawala wa Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Brigedia Jenerali Agatha Mary Katua, akizungumza na wanahabari jijini Dodoma leo kuhusu maadhimisho ya sita ya majeshi ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayotalajiwa kuanza Agost 26 2026. Katua alisema kwamba Jwtz ni mwenyeji  wa Maadhisho hayo kwa nchi za Afrika Mashariki (The 6th EAC Amerd Forces Civilian Military Co-operation Week),  maadhimisho hayo yatafanyika sehemu mbalimbali za nchi hii.  Maadhimisho hayo ambayo hufanyika kila mwaka kwa wanachama kwa kupokezana ambapo kwa mara ya mwisho kufanyika hapa nchini ilikuwa mwaka  2022. Aidha, katika kuadhimisha Ushirikiano huo , Majeshi ya nchi  Wanachama hutoa huduma mbalimbali ikiwemo huduma za matibabu ambapo Madaktari Bingwa kutoka Burundi, Somaria, Tanzania, Rwanda, Kenya na Uganda yatatoa huduma hiyo katika hospitali na vituo vya afya. Sambamba na huduma za tiba , kutakuwa na utoaji wa misaada ya kijamii, ukarab...

Wakulima wa Kitomondo Mkuranga wanufaika na huduma ya mawasiliano

  Wakulima katika Kijiji cha Kitomondo wamenufaika na kuimarika kwa huduma za mawasiliano ambayo imeondoa changamoto kubwa ya ugawaji dawa, pembejeo na upatikanaji wa masoko kupitia mfumo wa kidijitali.   Akizungumzia mafanikio hayo, Katibu wa Chama cha Ushirika - Kitomondo (AMCOS) Yusuf Mansouri amesema hapo awali walikuwa wanapata changamoto kubwa kwa wakulima kuchelewa kupata huduma lakini baada ya Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) kuwawezesha mnara wa mawasiliana changamoto hizo zimemalizika. Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) imetekeleza mradi wa ujenzi wa Minara 768 ya kimkakati ya mawasiliano wenye lengo la kuwezesha upatikanaji wa huduma ya mawasiliano kwa wananchi waishio yasiyo maeneo machache ya mjini na vijijini yenye yasiyo na mvuto wa kibiashara kwa watoa huduma.

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE PAC YAWAWEKA KITIMOTO VIONGOZI WA CHUO KIKUU MZUMBE KWA KUTAFUNA MABILIONI YA SHILINGI

Image
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Devotha Minja , akifungua kikao leo  na Uongozi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe kujadili lipoti ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Uongozi wa chuo hicho ulikutwa na hatia ya manunuzi ya yasiyozingatia sheria kiasi cha sh Bilioni 29.77 aidha  walikutwa na kosa la kutumia wazabuni wasiokidhi viwango walipewa sh bilioni 1.5 kosa mengine ni ujenzi wa barabara isiyokidhi viwango iliyotumia Sh Milio ni 500 aidha kamati hiyo haijalidhika na madai ya ziada sh milioni 718. Kamati hiyo inatafakari hatua za kuchukua kwa makosa hayo. TEMBELEA MHAGALE ONLINE TV KUSIKIA ZAIDI Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Aeshi Hilaly (kulia), akiwa na wabunge wenzake wakisikiliza maelezo toka Mzumbe  

WIZARA YA MAJI WAKUTANA NA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE

Image
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira, Jackson Kiswaga (kulia), akimkalibisha  leo kwenye kikao cha kamati yake Waziri wa Maji Jumaa Aweso ili kushiriki katika wasilisho la Wizara hiyo kwa kamati kuhusu maji na maziwa. (Kushoto) ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhandisi Andrew Kundo. Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira Mhe. Jackson Kiswaga, akifungua kikao hicho Wajumbe wa Kamati hiyo wakiwajibika