SGR TOKA DODOMA HADI MWANZA NI KUKAMILIKA 2030 WAZIRI MKUU DKT MWIGULU
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akisoma hotuba ya kufunga Bunge la 13, Mkutano wa Nne, jijini Dodoma. limeahirishwa rasmi hadi Oktoba 27, 2026. Wakati akisoma hotuba yake ameiagiza Wizara ya Fedha na Wizara ya Uchukuzi, kwa kushirikiana na Shirika la Reli Tanzania (TRC), wakandarasi na taasisi zinazohusika na uhamasishaji wa fedha, kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi ya Reli ya Kisasa (SGR), akilenga kuona ifikapo mwaka 2030 wajumbe kutoka Mwanza na mikoa ya Kanda ya Ziwa wakisafiri kwa treni kutoka Mwanza hadi Dodoma. Ameagiza agizo hilo leo wakati akitoa hoja ya kuahirisha Bunge la 13, Mkutano wa Nne, jijini Dodoma. “Naziagiza Wizara ya Fedha na Wizara ya Uchukuzi, zikishirikiana na Shirika la Reli, wakandarasi waliopewa kazi ya kujenga vipande hivi pamoja na wale waliopewa jukumu la kuhamasisha fedha za miradi hiyo, kupambana usiku na mchana,” amesema. Amesema Serikali inalenga kuhakikisha vipande vya Mwanza–Isaka, Isaka–Tabora, Tabora–Kigoma...