Posts

RAIS DKT. SAMIA AONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA KUMBUKUMBU YA MASHUJAA JIJINI DODOMA

Image
       Matukio mbalimbali katika Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa, zilizofanyika kitaifa katika Uwanja wa Mashujaa, uliopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma, tarehe 25 Julai, 2026.                 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameongoza Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa, zilizofanyika kitaifa katika Uwanja wa Mashujaa, uliopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma, tarehe 25 Julai, 2026.

MBUNGE JIMBO LA CHALINZE AFANYA VIKAO JIMBONI KWAKE

Image
Mbunge wa jimbo la Chalinze Akbaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, amekutana na kufanya mkutano na Madiwani na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze wakiwemo Watendaji Kata, Maafisa Tarafa, Wakuu wa Idara za Halmashauri ya Chalinze na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Ndg. Ramadhani Possy. Mbunge huyo alisema Kikao hicho kimewapa nafasi ya kujadili kwa pamoja majukumu na mipango ya utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050 ambayo itawezesha Halmashauri ya Chalinze kutoa mchango wake mkubwa katika ustawi wa Taifa  kwa kuzingatia vipaumbele vilivyowekwa.  Ridhiwani aiwahakikishia watendaji kwamba atajitahidi kulitumikia jimbo hilo kwa nguvu zake zote  alizomjalia mwenyezi mungu hadi hapo atakapompumzisha aunatakapoona panafaa kupumzika. "Tuchape kazi kwa pamoja tuwaletee maendeleo wananchi wanayotaka kuyaona, mimi nimechaguliwa na wananchi, kuwatumikia ninyi mmeajiliwa kuwatumikia tukiunganisha maalifa yetu na tukimtanguliz...

WAZIRI WA KILIMO CHONGOLO AFANYA ZIARA WILAYA YA ARUMERU.

Image
  WAZIRI wa Kilimo na mlezi wa Mkoa wa Arusha, Daniel Godfrey Chongolo (Mb) akisalimiana na Mkuu wa wilaya ya Arumeru Mwinyi.Ahmed Mwinyi alipofanya ziara yake wilayani humo leo .   @@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@ WAZIRI wa Kilimo na mlezi wa Mkoa wa Arusha  Mhe. Daniel Godfrey Chongolo (Mb) amewataka  wananchi wa wilaya ya Arumeru kuendelea kulinda tunu ya amani ya Taifa, inayopelekea utulivu wa kufanya kazi za uzalishaji kwa maendeleo ya Taifa la Tanzania. Waziri Chongolo ameyasema hayo leo wilayani Arumeru wakati akiwa.katika.ziara yake ya siku.moja ya kukagua miradi mbalimbali. Aidha Waziri Chongolo  amewasili wilayani Arumeru na kupokelewa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Mwinyi Ahmed Mwinyi pamoja na viongozi wa chama na Serikali. Katika ziara yake Waziri  Chongolo ameweza kukagua shughuli za utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya mradi wa ujenzi wa barabara ya KIA- Usa River,pamoja na  kutembelea mradi wa ujenzi wa skimu ya umwagiliaji Kipande- Nkoavere Kata...

RAIS DKT. SAMIA AKISHIRIKI MKUTANO MAALUM WA WAKUU WA NCHI ACCRA GHANA By fullshangwe July 22, 2026 | 12:51 pm

Image
    ‌ Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza katika Mkutano Maalum wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) kuhusu Afya, katika hoteli ya Elisa, jijini Accra, Ghana, tarehe 22 Julai, 2026. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Rais wa Jamhuri ya Ghana, Mhe. John Dramani Mahama, Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) na Rais wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Evariste Ndayishimiye, kwenye picha na viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla ya ufunguzi wa Mkutano Maalum wa Umoja wa Afrika kuhusu Afya, jijini Accra, Ghana, tarehe 22 Julai, 2026.

MSIGWA ATEMBELEA MACHINGA NA BENJAMINI MKAPA HOSPITALI DODOMA

Image
  Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na  mseamji Mkuu wa Serikali,Gerson Msigwa , akisani kitabu cha wageni baadanyan kuingia ofisi ya Meneja wa soko la Machinga jijini Dodoma kuanza kulitembelea na kuzunguza na baadhi ya wafanyabiashara, ambapo aliwaambia Serikali  imewekeza   zaidi ya Sh Bilioni 9.5 katika kujenga soko hilo  sasa linahudumia zaidi ya wafanyabishara 2800 hao walipo ndani achilia mbali wanaopanga bidhaa zao jioni nje ya soko ambao nao wanazidi 200 huku likiwa na huduma mbalimbali kama CCTV, kituo cha Polsi, zimamoto na vituo vya kifedha nia ya Serikali ni kuwekeza masoko kama hayo mikoa yote na badae katika wilaya.  ziara hiyo ilihitimishwa katika  Hospitali ya Benjamini Mkapa, ambapo  alizungumza na wanahabari na kusema  Serikali imewekeza  jumla ya sh bilioni 283 katika kipindi cha miaka 10 ili kuifanya hospitali hiyo kuwa kituo cha kisasa  cha utalii wa matibabu , vifaa mbalimbali vya ma...

WAZIRI MKUU DKT . MWIGULU AKUTANA NA MZEE JOSEPH BUTIKU

Image
  Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Mzee Joseph Butiku, akizungumza na Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, wakati wa mazungumzo yaliyofanyika katika Ofisi Ndogo ya Waziri Mkuu, Oysterbay, jijini Dar es Salaam, Julai 20, 2026. Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, akipokea nyaraka kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Mzee Joseph Butiku, baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika katika Ofisi Ndogo ya Waziri Mkuu, Oysterbay, jijini Dar es Salaam, Julai 20, 2026. Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Mzee Joseph Butiku, na ujumbe wake baada ya mazungumzo yaliyofanyika katika Ofisi Ndogo ya Waziri Mkuu, Oysterbay, jijini Dar es Salaam, Julai 20, 2026. @@@@@@@@@@@@@@@@@@ WAZIRI MKUU AKUTANA NA MZEE JOSEPH BUTIKU WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema maendeleo ya kweli ya Taifa yanategemea kujenga wananchi wenye maadili, uzalendo, uwajibi...

RAIS SAMIA: KIGOMA KUWA KITOVU CHA FURSA ZA BIASHARA BAADA YA UJENZI WA SGR TABORA–KIGOMA

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisikiliza maelezo ya ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Sita kutoka Tabora hadi Kigoma, baada ya kuwasili Katosho mkoani Kigoma, tarehe 20 Julai, 2026.  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Sita kutoka Tabora hadi Kigoma kwenye hafla iliyofanyika Katosho mkoani Kigoma tarehe 20 Julai, 2026.   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwahutubia wananchi wa Kigoma baada ya kuzindua meli 4 za mizigo na kuweka jiwe la Msingi la Ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Sita kutoka Tabora hadi Kigoma kwenye hafla iliyofanyika Katosho Mkoani Kigoma tarehe 20 Julai, 2026. Matukio mbalimbali katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Sita kutoka Tabora hadi Kigoma kwenye hafla iliyofanyika ...