Posts

BAJETI YA WIZARA YA MAKONDA YAPITISHWA KWA SHANGWE BUNGENI

Image
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,  Paul Makonda (pichani)  amewasilisha bajeti ya Wizara yake kwa mwaka wa fedha 2026/27 Bungeni jijini Dodoma ambapo paamoja na  mambo mengine, aliweza kuwa na wageni wengi mmoja wapo ni Mwanasoka maarufu barani Afrika , Drogba. Aidha wasanii mbalimbali nchini pamoja na walimbwende waliunakisisha ukumbi wa bunge, hakika waziri huyp kijana amekuja na ubunifu mkubwa katika usomaji wa bajeti yake na ndiyo maana bajeti yake imeweza kujadiliwa na wabunge na kueleweka na kupitishwa kwa idadi kubwa ya wabunge  huku akimwagiwa sifa kemukemu kwa uchapa kazi wake pamoja na watendaji wake.   Uwasilishaji huo ulifanyika leo, Mei 4, 2026, ambapo pamoja na mambo mengine, amezungumzia mikakati mbalimbali ya wizara ikiwa  pamoja na masuala ya klabu za Simba na Yanga ambapo sasa muda umefika wa kuwa na viwanja vyao kutokana na ukongwe wao na jinsi wanavyoiletea sifa nchi hii. Walimbwende wakiongozwa na kiongozi wao Mu...