Posts

WANANCHI KARIBUNI BANDA LA JKT KATIKA MAONESHO YA 88 HATA KAMA YAKIFIKIA KILELE SISI TUPO---MEJA JENERALI MABELE

Image
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele, akisalimiana na Mkuu wa Dawati la Habari wa Jeshi hilo  Meja Janeth Charles Mkamba, baada ya kuwasili katika eneo la jeshi hilo lililopo katika maonesho ya Nane nane jijini Dodoma. Mabele alitembelea na kujionea uzalishaji unaofanywa na askari wake kama , ufugaji wa ng'ombe, samaki, Kuku wa mayayi, bata bukini, kilimo cha mazao mbalimbali, utegenezaji wa fenicha, ushaonaji wa nguo  na viatu. Mkuu huyo baada ya kutembelea aliongea na wanahabari ambapo aliwaeleza kwamba Jeshi hilo ni la wananchi, wananchi wasiogope kutembelea eneo hilo ili kujifunza elimu mbalimbali inayotolewa na Askari hao kwa ajili ya manufaa yao, alibainisha kwamba pamoja na kufungwa maonesho hayo wao huishi katika eneo hilo wakihudumia wananchi wapo katika maeneo ,nbalimbnali ya maonesho hayo nchini wkitoa huduma hizo.", wananchi karibuni Nanenane mjionee uzalishaji unaofanywa na vijana wa jeshi lenu huku wakitoa elimu kwa ajili ya kujenga T...

CHUO KIKUU CHA MZUMBE CHATENGA BILIONI 4.5 KWA AJILI YA MAENDELEO YA NDAKI ZAKE

Image
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Prof.   William Mwegoha, akizungumza leo na wanahabari katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO Mtumba jijini Dodom, kuhusu utendaji kazi wake jinsi kinavyotekeleza dira ya maendeleo ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Proesa Mwegoha amebainisha kwamba malengo yake kiwe kitovu cha ubunifu ,maarifa na maendeleo, huku kikiandaa wahitimu wenye uwezo wa kushindana katika soko la ajira na kuchangia maendeleo ya ujenzi wa Taifa.   Msikilize zaidi  mhagale online TV Wanahabari wakimsikiliza kwa makini Makamu huyo alipokuwa akizungumza nao.  

MAKAMU WA RAIS DKT. NCHIMBI ATEMBELEA MAONESHO YA KIMATAIFA YA NANE NANE - DODOMA

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ameitaka Tume ya Maendeleo ya Ushirika kuendelea kufanya usimamizi wa vyama vya ushirika na kutoa miongozo ya kitaalamu kwa vyama vyote nchini.   Makamu wa Rais ametoa wito huo, wakati wa Siku Maalum ya Ushirika katika Maonesho ya Kimataifa ya Nane Nane kwa mwaka 2026, yanayofanyika katika Viwanja vya John Malecela, Nzuguni mkoani Dodoma. Amesisitiza Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO) kuhakikisha linaendelea kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwa vyama vya ushirika kwa lengo la kuhakikisha nidhamu ya matumizi ya fedha, kuzuia ubadhirifu na kuongeza uwazi katika uendeshaji wa vyama hivyo.   Makamu wa Rais, amesema Ushirika wenye uadilifu ni muhimu sana katika kujenga imani kwa wanachama na kuvutia uwekezaji zaidi. Amesema kuimarika kwa ushirika kunategemea uwajibikaji, uaminifu na uadilifu wa wanachama, viongozi na watendaji wa vyama vya ushirika.   Makamu wa Rais ...