MOI SASA MATIBABU YA KISASA TUPU BALOZI DKT. MPOKI
Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya amesema kuwa utoaji wa tiba bora, uwepo wa wataalamu wabobezi pamoja na matumizi kupitia QR Code, unaolenga kupunguza msongamano wa wagonjwa katika hospitali. Amesema hayo leo wakati akizungumza na wanahabari katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO jijini Dodoma leo. Aidha, amesema Kuwa baada ya mgonjwa kuweka miadi, mfumo wa MOI utaonyesha taarifa za mgonjwa, daktari anayetarajiwa kumuona pamoja na kliniki na muda wa huduma, hivyo kupunguza muda wa kusubiri hospitalini. Aidha akibainisha Kuwa mfumo huo umeanzishwa kutokana na changamoto ya msongamano, ambapo historia wagonjwa walikuwa wakifika hospitalini saa 10 za alfajiri na kusubiri hadi saa 8 mchana ili kuonana na daktari. Pia, ameseme kuwa mfumo huo utawawezesha wagonjwa kufika katika muda waliopangiwa na kuendelea na shughuli nyingine, badala ya kutumia muda mrefu kusubiri huduma hospitalini. Mkurugenzi huyo amesema katika mwaka wa fedha 2025/26 MOI imehudumia juml...