PROFESA MKENDA AZUNGUMZA NA WANAHABARI LEO JIJINI DODOMA KUHUSU WANAFUNZI 150
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia. Profesa Aldof Mkenda, akiingia katika ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo kwa ajili ya kuzungumza na waandishi wa Habari kuhusu wanafunzi 150 waliochanguliwa katika mpango wa masomo wa Samia Scholarship kwa mwaka wa masomo 2026 na 2027.Mazungumzo hayo yamefanyika jijini Dodoma leo . Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, akizungumza na waandishi wa Habari leo jijini Dodoma ofisini kwake kuhusu wanafunzi 150 waliofanya vizuri zaidi katika mtihani wa Kidato cha Sita mwaka 2026 ambao watanufaika na mpango wa Samia Scholarship kwa mwaka wa masomo 2026/2027, ukiwahusisha wanafunzi waliofanya vizuri katika masomo ya sayansi, hisabati na tiba.Vigezo na Sifa za Wanufaika Ufaulu wa Juu: Wanafunzi waliochaguliwa ni wahitimu waliopata alama za juu (marks) katika mitihani yao ya Kidato cha Sita kwenye tahasusi za sayansi kama vile PCM, PCB, CBG, PMG, CBA na PMC.Fani za Kipaumbele: Wanufaika wametakiwa kujiunga na shahada zin...