Posts

VIONGOZI KASHUWASA WAWEKWA KITI MOTO NA KAMATI YA KUDUMUYA BUNGE PAC.

Image
  Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya   Hesabu za Serikali ( PAC ), Devota   Minja  (kulia), akiwa na kamati yake wakimsikiliza  Mkurugenzi wa Mamlaka ya Kuuza Maji kwa Jumla (Kashuwasa), Mhandisi, Justine Rujomba, alipokuwa akifafanua hoja za kamati yake katika kikao kilichofanyika leo jijini Dodoma. Kashuwasa ni Mamlaka inayosimamia Mamlaka za Maji za mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Simiyu, Mara, Geita, Singida na Tabora   

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE LAAC YATOA MAELEKEZO KWA HALMASHAURI YA WILAYA YA SAME

Image
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya   Hesabu za Serikali za Mitaa ( LAAC ) Ado Shaibu, ameongoza kikao cha kamati yake na viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Same, ambapo walikaa na kupitia hesabu zilizokaguliwa na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.Mwenyekiti huyo akisoma tamko la kamati amewataka viongozi hao kutekeleza maagizo yote ya Mkaguzi na yale yanayotolewa na Kamati yake , aidha amewarudisha kwenda kutekeleza  na watawaita tena kujiridhisha kama maagizo hayo yote yametekelezwa kama kamati hiyo ilivyoagiza. Aidha ametoa onyo kwa Halmashauri zote nchini kutekeleza maagizo yanayotolewa na Mkaguzi Mkuu na Kamati yake,  amefafanua kwamba kamati hiyo inapoziita Halmashauri ifahamike kwamba kamati yake inafanya kazi kwa niaba ya bunge kuidharau kamati hiyo ni kulidhalau bunge kitu ambacho hakubaliki hata kidogo. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Same, Jimson Mhagama (kushoto), akiwaongoza watendaji wake kuingia katika chumba cha mikutano cha Kamat...

PPRA KUWAPA KIBANO WANAOENDA KINYUME NA UNUNUZI WA UMMA

Image
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma -PPRA   Tanzania), Dennis  Simba,  akizungumza na wanahabari katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO, akizungumzia utendaji kazi wa Mamlaka hiyo. Wanahabari wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi huyo