Posts

PROF. SHEMDOE: SERIKALI IMEWEKEZA BILIONI 2.8 KUBORESHA AFYA, BARABARA, ELIMU YA AMALI GAIRO

Image
  Na. OWM–TAMISEMI, Gairo Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imewekeza Shilingi bilioni 2.8 katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya Kituo cha Afya Chanjale, Barabara ya Confort Pub–Magoweko na Shule ya Amali Kwipipa, hatua iliyoboresha upatikanaji wa huduma za afya, kurahisisha usafiri na usafirishaji pamoja na kupanua fursa za elimu ya amali kwa wananchi wa wilaya ya Gairo. Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, Julai 17, 2026 katika kijiji cha Kwipipa, kata ya Rubeho, wilaya ya Gairo, baada ya kukagua na kuweka mawe ya msingi katika miradi hiyo ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma. Prof. Shemdoe amesema miradi hiyo inaonesha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora karibu na maeneo wanayoishi kupitia uwekezaji unaogusa m...

RAIS WA MISRI APOKELEWA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM NA RAIS DKT.SAMIA

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Mhe. Abdel Fattah El-Sisi baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam kwa Ziara ya Kitaifa, tarehe 18 Julai Juni, 2026       Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimama na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Mhe. Abdel Fattah El-Sisi wakati wakupokea heshima ya wimbo wa Taifa wa Tanzania na ule wa Misri baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 18 Julai Juni, 2026 .           Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Mhe. Abdel Fattah El-Sisi akikagua Gwaride rasmi la Mapokezi lililoandaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 18 Julai Juni, 2026.   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amemkaribisha Ikulu jijini Dar ...

TANZANIA YAELEZA MAFANIKIO YA MIAKA 10 YA UTEKELEZAJI WA AJENDA MPYA YA MIJI

Image
Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa-New York Mhe. Balozi Togalani Mavura (kushoto), Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga (Katikati) na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Makazi Wizara ya Ardhi Bw. Deogratius Kalimenze wakiwa katika mkutano wa ngazi ya juu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Makazi (UN Habitat) kuhusu mapitio ya utekelezaji wa ajenda mpya ya miji kwa kipindi cha miaka 10 tarehe 16 Julai 2026. Na   Munir Shemweta, New York  Tanzania imeeleza mafanikio makubwa yaliyopatikana katika utekelezaji wa Ajenda Mpya ya Miji (New Urban Agenda) katika kipindi cha miaka 10, ikiwemo kupungua kwa umaskini wa upatikanaji wa huduma za msingi, kuongezeka kwa umiliki wa ardhi kwa wanawake na kurasimishwa kwa zaidi ya milki milioni 1.1 za ardhi. Mafanikio hayo yamewasilishwa katika tamko la Tanzania kwenye Mkutano wa Ngazi ya Juu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Makazi (UN-Habitat) kuhusu mapi...

JWTZ LAWAAGA MAJENERALI 17 JIJINI DODOMA

Image
Magari maalumu  yaliyobeba  maafisa jenerali  17 wastaafu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), yakisukumwa katika hafla ya kuwaaga iliyoongozwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob Mkunda katika Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa Kikombo jijini Dodoma Julai 10, 2026. Askari wakiwa wamejipanga tayari kupita katikati magari maalumu yaliyowabeba maafisa Jrnrrali wastaafu Jenerali Mkunda akiagana na Meja Jenerali Mstaafu Suleiman Mungiya Mzee. Aidha Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob Mkunda amewaasa maafisa jenerali  17 Wastaafu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), kuacha kuhangaika na mambo ya siasa na mengineyo, bali watulie waishi vizuri na familia zao. Pamoja na mambo mengine Jenerali Mkunda ameyasema hayo wakati wa hafla ya kuwaaga maafisa Jenerali hao  katika Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa Kikombo jijini Dodoma Julai 10, 2026. Jenerali Mkunda (aliyekaa mbele katikati pamoja na viongozi wengine)  wakiwa katika picha ya kumbukumbu na  maaf...

WAZIRI MKUU MWIGULU ALIFUNGA BUNGE NA KUWATAKA WATANZANIA WATUNZE AMANI

Image
HOTUBA YA MHESHIMIWA DKT. MWIGULU LAMECK NCHEMBA (MB.), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUAHIRISHA MKUTANO WA TATU (3) WA BUNGE LA 13 LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAREHE 26 JUNI, 2026 JIJINI DODOMA   1.             Mheshimiwa Spika, awali ya yote ninamshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa fadhili zake zilizotuwezesha sote kuiona siku hii muhimu katika historia ya Bunge la 13. Kama mnavyofahamu, tumekutana leo kwa ajili ya kuhitimisha mkutano wa Tatu ambao ulikuwa mahsusi kwa ajili ya kupokea na kujadili bajeti ya serikali.   2.             Mheshimiwa Spika, nimesema leo ni siku muhimu na ya kihistoria kwa sababu, hii ni Bajeti ya kwanza ya Serikali kupitishwa na Bunge la 13 baada ya uchaguzi mkuu wa 2025. Hongereni sana waheshimiwa Wabunge!   3.             Mheshimiwa Spik...