Posts

KISWAGA AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YAKE YA KUDUMU YA BUNGE, MAJI NA MAZINGIRA

Image
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge, Maji na Mazingira ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Karenga Jackson Kiswaga   akiongoza kikao na  kupokea na kujadili taarifa za Wizara ya Maji na Taasisi zake jijini Dodoma leo Wajumbe wa Kamati hiyo wakiwajibika Wakuu wa Taasisi za Wizara hiyo na Wakurugenzi wa Idara wakiwa kikao hapo Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira Mhe. Jackson Kiswaga   , Kulia kwake ni Naibu Wizara ya Maji  Mhandisi Andrew Kundo na Katibu wa Wizara hiyo Mhandisi, Mwajuma Waziri  

KYOMBO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YAKE LEO JIJINI DODOMA

Image
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya   Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ( TAMISEMI ), Florent   Kyombo , akiongoza kikao cha   kamati  ... Wajumbe wa Kamati hiyo wakiwa kikaoni  

Mahakama ya Rufaa yaipa ushindi IPTL, PAP katika USD 168m Mgogoro Dhidi ya Standard Chartered

Image
kiwanda cha kufua Umeme cha IPTL kilichopo Salasala  jijini  Dar es Salaam Na Mwandishi Wetu Mahakama ya Rufani ya Tanzania imezipa gharama za kisheria Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited - IPTL na Pan Africa Power Solutions (T) Limited ya Dola za Kimarekani 8,000,000 kufuatia kufanikiwa kupinga rufaa iliyokatwa na Benki ya Standard Chartered kuhusu mgogoro wa kibiashara wa muda mrefu wa dola za Marekani 168,000,000. Uamuzi huo ulitolewa Agosti 5, 2026 na Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani , J.E. Fovo, katika kesi ya Kodi namba 65 ya 2026, iliyotokana na Rufaa ya Madai namba 386 ya 2022. Waombaji hao waliwakilishwa na Wakili Musa Mhagama akiwakilishwa na Wakili Teeshatia. Uamuzi huu wa hivi punde unafunga sura nyingine katika kesi ambayo imeendelea kwa zaidi ya muongo mmoja na imehusisha mahakama nchini Tanzania, Uingereza na Malaysia. Kiini cha mzozo huo kinahusiana na mikataba ya uzalishaji umeme iliyotiwa saini mwishoni mwa miaka ya 1990 na mwanzoni mwa miaka ya ...

TANZANIA NA CHINA KUIMARISHA MAHUSIANO KUPITIA VIJANA WAKE------BALOZI CHEN

Image
Balozi  wa China nchini Tanzania Chen   Na Prosper Makene  Dar es Salaam, 12 Agosti 2026 Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Tanzania, Mhe. CHEN Mingjian, amesema vijana ndio msingi wa mustakabali wa uhusiano kati ya China na Tanzania.  Balozi Chen alisema hayo jijini Dar es Salaam leo wakati wa "Mjadala wa China-Tanzania kuhusu Maendeleo na Ubadilishanaji wa Vijana". Mjadala huo umehudhuriwa na wawakilishi zaidi ya 100 kutoka serikali za China na Tanzania, vyuo vikuu, makampuni ya ujenzi, vyombo vya habari na wanafunzi. Unafanyika katika mwaka maalumu ambapo 2026 inatimiza miaka 70 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya China na Afrika. Pia umetangazwa kuwa "Mwaka wa Ubadilishanaji wa Watu kwa Watu kati ya China na Afrika". Akifungua mjadala huo, Balozi Chen amesema katika kipindi cha miaka 70 iliyopita, China na Tanzania zimeandika historia nzuri ya udugu na ushirikiano. "Urafiki wetu umepitia vipimo vya muda na umethibitika kwa vitendo. Kuanzia ujenzi wa ...

TUTAWAPIGANIA VIJANA WOTE WA CHADEMA NA TUTAWASOMESHA POPOTE NDANI YA NCHI AU NJE YA NCHI---HECHE

Image
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Heche, amewataka vijana wa chama hicho kupitia Baraza lao la BAVICHA kukipigiania chama hicho kwa lolote popote na wasiwe na woga, wao kama viongozi watawatetea popote watakapokutwa na madhira yoyote na hawatawatelekeza. Heche aliyasema hayo wakati akifungua Kongamano la  Maadhimisho ya Vijana Duniani kwa vijana wa chama hicho lililofanyika jijini Dodoma, amebainisha kwamba vijana wa chama hicho waliokamatwa huko Geita wakisingiziwa kesi za Ugaidi watawatetea na wale wanafunzi pindi kesi zao zikiisha watawalejesha shuleni na watasoma popote pale Duniani.  Mwenyekiti wa Bavicha Taifa, Deogratius Mahinyila, akizungumza katika mkutano huo Kabla ya kumruhusu Heche kuzungumza Lema, akitema cheche katika kongamano hilo Mwenyekiti wa Chama cha Wanasheria nchini (TLS), Mwambukusi, akihutubia kongamano hilo na kuwataka vijana wa chama hicho kutochoka kudai haki  na katiba bora Wakisikiliza kwa makini Mwanaharak...