Posts

TIA KIOO CHA WAHASIBU TANZANIA

Image
Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Profesa William Pallangyo , akizungumza na wanahabari leo katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO,akizungumzia miaka  mitano yautendaaji kazi wa chuo hicho  Wanahabari wakimsikiliza kwa makini mtendaji huyo alipokuwa akizungumza  

SGR TOKA DODOMA HADI MWANZA KUKAMILIKA 2030 WAZIRI MKUU DKT MWIGULU

Image
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba  akisoma hotuba ya  kufunga Bunge la 13, Mkutano wa Nne, jijini Dodoma.  limeahirishwa rasmi hadi  Oktoba 27, 2026. Wakati akisoma hotuba yake  ameiagiza Wizara ya Fedha na Wizara ya Uchukuzi, kwa kushirikiana na Shirika la Reli Tanzania (TRC), wakandarasi na taasisi zinazohusika na uhamasishaji wa fedha, kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi ya Reli ya Kisasa (SGR), akilenga kuona ifikapo mwaka 2030 wajumbe kutoka Mwanza na mikoa ya Kanda ya Ziwa wakisafiri kwa treni kutoka Mwanza hadi Dodoma. Ameagiza agizo hilo leo  wakati akitoa hoja ya kuahirisha Bunge la 13, Mkutano wa Nne, jijini Dodoma. “Naziagiza Wizara ya Fedha na Wizara ya Uchukuzi, zikishirikiana na Shirika la Reli, wakandarasi waliopewa kazi ya kujenga vipande hivi pamoja na wale waliopewa jukumu la kuhamasisha fedha za miradi hiyo, kupambana usiku na mchana,” amesema. Amesema Serikali inalenga kuhakikisha vipande vya Mwanza–Isaka, Isaka–Tabora, Tabora–Kigoma...

MABINGWA WA MASHINDANO YA KAFITI MWANZA WATINGA BUNGE NA KOMBE LAO

Image
Wachezaji wa na Viongozi wa Timu ya Kawekamo  ya jijini Mwanza wakiwasili ukumbi wa Msekwa kwa ajili ya kujifunza mambo mbali mbali ya bunge tangu kuanzishwa kwake, timu hiyo ilinyakuwa kombe lililokuwa likishindaniwa katika mashindano yaliyoanzishwa na Mbunge wa Ilemela Kafiti W. Kafiti, yalishilikisha timu 24. Hakika wachazeji na viongoz wake na mbunge wa jimbo hilo waliweza kujumuika na wabunge pamoja na mawaziri katika mapokezi ya mabingwa hao. Waliweza kuvitawala viunga vya bunge tangu kuwasili kwao .  

MOI SASA MATIBABU YA KISASA TUPU BALOZI DKT. MPOKI

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya amesema kuwa utoaji wa tiba bora, uwepo wa wataalamu wabobezi pamoja na matumizi   kupitia QR Code, unaolenga kupunguza msongamano wa wagonjwa katika hospitali. Amesema hayo leo wakati akizungumza na wanahabari katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO jijini Dodoma leo. Aidha, amesema Kuwa baada ya mgonjwa kuweka miadi, mfumo wa MOI utaonyesha taarifa za mgonjwa, daktari anayetarajiwa kumuona pamoja na kliniki na muda wa huduma, hivyo kupunguza muda wa kusubiri hospitalini. Aidha akibainisha Kuwa mfumo huo umeanzishwa kutokana na changamoto ya msongamano, ambapo historia wagonjwa walikuwa wakifika hospitalini saa 10 za alfajiri na kusubiri hadi saa 8 mchana ili kuonana na daktari. Pia, ameseme kuwa mfumo huo utawawezesha wagonjwa kufika katika muda waliopangiwa na kuendelea na shughuli nyingine, badala ya kutumia muda mrefu kusubiri huduma hospitalini. Mkurugenzi huyo amesema katika mwaka wa fedha 2025/26 MOI imehudumia juml...