Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Utawala wa Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Brigedia Jenerali Agatha Mary Katua, akizungumza na wanahabari jijini Dodoma leo kuhusu maadhimisho ya sita ya majeshi ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayotalajiwa kuanza Agost 26 2026. Katua alisema kwamba Jwtz ni mwenyeji wa Maadhisho hayo kwa nchi za Afrika Mashariki (The 6th EAC Amerd Forces Civilian Military Co-operation Week), maadhimisho hayo yatafanyika sehemu mbalimbali za nchi hii. Maadhimisho hayo ambayo hufanyika kila mwaka kwa wanachama kwa kupokezana ambapo kwa mara ya mwisho kufanyika hapa nchini ilikuwa mwaka 2022. Aidha, katika kuadhimisha Ushirikiano huo , Majeshi ya nchi Wanachama hutoa huduma mbalimbali ikiwemo huduma za matibabu ambapo Madaktari Bingwa kutoka Burundi, Somaria, Tanzania, Rwanda, Kenya na Uganda yatatoa huduma hiyo katika hospitali na vituo vya afya. Sambamba na huduma za tiba , kutakuwa na utoaji wa misaada ya kijamii, ukarab...