RAIS DKT. SAMIA AKISHIRIKI MKUTANO MAALUM WA WAKUU WA NCHI ACCRA GHANA By fullshangwe July 22, 2026 | 12:51 pm
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza katika Mkutano Maalum wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) kuhusu Afya, katika hoteli ya Elisa, jijini Accra, Ghana, tarehe 22 Julai, 2026. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Rais wa Jamhuri ya Ghana, Mhe. John Dramani Mahama, Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) na Rais wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Evariste Ndayishimiye, kwenye picha na viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla ya ufunguzi wa Mkutano Maalum wa Umoja wa Afrika kuhusu Afya, jijini Accra, Ghana, tarehe 22 Julai, 2026.