Posts

WAKULIMA WANUFAIKA NA HUDUMA ZA STAKABADHI GHALA WRRB

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) Asangye BangU, akizunhumza na wanahabari leo katika ukumbi wa Idara ya Habari MAERLEZI Mtumba jijini Dodoma, akizungumzia huduma mbalimbali wanazozitoa kwa wakulima nchini na hivi sasa wanafaidika na huduma zao, mkurugenzi huyo aliwabainishia wanahabari haya yafuatayo  Mwaka huu ni mwaka wa kihistoria kwa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala na Taifa kwa ujumla. Tarehe 19 Mei 2026 , Mfumo wa Stakabadhi za Ghala uliadhimisha miaka 20 tangu kuanzishwa kwake mwaka 2006 . Katika kipindi hiki, Mfumo umebadilisha kabisa namna biashara ya mazao inavyofanyika nchini kwa kuweka msingi wa biashara yenye uwazi, ushindani na usalama wa masoko ya wakulima. Mafanikio haya yasingewezekana bila uongozi madhubuti wa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , ambaye ameendelea kusimamia sera zinazoweka mazingira bora ya biashara, uwekezaji, matumizi ya...