Posts

MEJA JENERALI MABELE AHITIMISHA MAFUNZO YA JKT KANEMBWA

Image
    Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele, akikagua Paredi ikiwa ni ishara ya kuhitimisha mafunzo ya JKT kwa vijana wa Kundi la Mujibu wa Sheria, Operesheni Linda Amani, na Kundi la Kujitolea, Operesheni Nishati Safi. @@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@ Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Meja Jenerali Rajabu Mabele amesema somo la Uzalendo na Uzalendo wa Kidijitali kwenye silabasi za mafunzo ya JKT litaendelea kuboreshwa zaidi ili kuelimisha vijana umuhimu wa kutumia vema mitandao ya kijamii. Meja Jenerali Mabele ameyasema hayo leo Septemba 18, 2026 wakati akifunga ukurasa wa zoezi la uhitimishaji wa mafunzo ya awali ya kijeshi kwa vijana wa Mujibu wa Sheria Operesheni Linda Amani na Kujitolea Operesheni Nishati Safi katika Kikosi cha Kanembwa JKT kilichopo mkoani Kigoma. Katika hatua nyingine, Meja Jenerali Mabele ameishukuru Serikali kwa kuendelea kuliwezesha Jeshi la Kujenga Taifa katika kuboresha miundo mbinu ya Vikosi vyake ili liweze k...

WAANDISHI WATAKIWA KUWAELIMISHA WANACHAMA WA PSSSF KUHAKIKI MICHANGO NA MAFAO KIDIJITALI

Image
  Afisa Mkuu wa Uhusiano wa Mfuko wa PSSSF, Abdul Njaidi  , akizungumza katika semina hiyo  ya wanahabari  @@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@ MFUKO wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umewataka waandishi wa habari kutumia taaluma yao kuwaelimisha na kuwahamasisha wanachama kuhakiki taarifa za michango na mafao yao kupitia mifumo ya kidijitali. Hatua hiyo imeelezwa kulenga kuhakikisha taarifa zao zinakuwa sahihi na kupunguza changamoto zinazoweza kujitokeza wakati wa kudai mafao. Wito huo umetolewa leo, Septemba 18, 2026, mjini Shinyanga wakati wa semina ya PSSSF kwa waandishi wa habari kutoka Mtandao wa Wanablogu Tanzania (Tanzania Bloggers Network – TBN)  na Klabu za Waandishi wa Habari za  mikoa ya Shinyanga na Simiyu. Katika semina hiyo, Msimamizi PSSSF Mkoa wa  Simiyu Salum Miraji ameeleza kuwa matumizi ya mifumo ya kidijitali yamekuwa sehemu ya maboresho ya huduma za mfuko, yakilenga kumwezesha mwanachama kupata na kuhakiki taari...

MWANAHABARI MWANDAMIZI PATRICIA KIMELEMETA AKIWA NA MAPACHA WAKE BAADA YA KUHITIMU JKT MAKUTUPOLA LEO

Image
Wahitimu wakipita mbele ya mgeni rasmi kuhitimisha mafunzo yao Wahitimu wakishangilia baada ya mafunzo yao kufungwa Mwakilishi wa Mkuu wa JKT, Brigedia Jenerali Shija, akitoa salam za jeshi hilo htt Mkuu wa Wilaya ya Bahi Thobias Nyingo, akihitimisha Mafunzo hayo Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Thobias Nyingo,  Akikagua Gwaride la wahitimu Mwandishi Patricia Kimelemeta (kulia), akibadilishana mawazo na watoto wake mapacha Kulwa na Doto baada ya kuhitimu mafunzo ya awali ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) 834 Makutupola Opereshen Linda Amani  kwa upande wa mujibu wa sheria na Operesheni Nishati safi kwa upande wa kujitolea.Sherehe hizo zimejumuisha maonyesho mbalimbali na uonyeshaji wa morali na uzalendo wa vijana hao waliohitimu mafunzo yao katika kikosi hicho kilichopo mkoani Dodoma. Mambo ya keki kwa wahitimu