LUKUVI ATAKUMBUKWA KWA MENGI-------WAZIRI MKUU: MWIGULU
WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) na Mbunge wa Isimani, Mheshimiwa William Lukuvi atakumbukwa kwa mengi na Watanzania kutokana na utumishi wake uliotukuka katika nafasi mbalimbali alizohudumu. “Mheshimiwa Lukuvi atakumbukwa kwa mengi na Watanzania kutokana na utumishi wake uliotukuka katika nafasi mbalimbali. Mchango wake kwa Jamii na Watanzania kwa ujumla katika nafasi mbalimbali alizotumikia kuanzia Chama, Jimboni na Serikalini umekuwa chachu katika kuleta maendeleo kwa wananchi,” amesema Waziri Mkuu ambaye ameongoza mazishi hayo kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan. Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumanne, Machi 31, 2026) wakati akizungumza katika ibada ya mazishi ya marehemu iliyofanyika nyumbani kwake kwenye kijiji cha Idodi, wilayani Iringa, mkoani Iringa. “Kwa niaba ya Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan nitumie nafasi hii kuwahah...