Posts

MBUNGE WA MAGU KIDOGO AKWAMISHE BAJETI YA WIZARA YA UCHUKUZI

Mbunge wa Magu, Boniventura Kiswaga, kidogo akwamishe bajeti ya Wizara ya Uchukuzi pale alipoondoa shilingi akidai kutotendewa haki ujenzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza  ambapo umekuwa ukipigwa kalenda kila mwaka. Mbunge huyo aliungwa mkono na wabunge zaidi ya 10 kama kanuni za bunge zinavyotaka ndipo majadiliano yalianza bungeni  na kupelekea Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba kuingilia kati na kusema  Serikali inaendelea kuchukua hatua kuhakikisha Uwanja wa Ndege wa Mwanza unaboreshwa na kujengwa katika hadhi ya kimataifa ili kuendana na hadhi ya jiji la Mwanza kama kitovu muhimu cha shughuli za kiuchumi Kanda ya Ziwa. Amesema hayo bungeni jijini Dodoma wakati akitoa kauli ya Serikali kuhusu hoja ya maendeleo ya Uwanja wa Ndege wa Mwanza iliyowasilishwa na Mbunge wa Magu, Boniventura Kiswaga, katika mjadala wa bajeti ya Wizara ya Uchukuzi kwenye Kikao cha 28 cha Mkutano wa Tatu wa Bunge la 13, leo Mei 13, 2026. Waziri Mkuu amesema Serikali inatambua umuhimu wa Uwanja wa Nd...

TANZANIA MWENYEJI MKUTANO WA WABUNGE WANAWAKE WA MABUNGE UKANDA WA MAZIWA MAKUU

Image
Spika Mussa Azan Zungu , akizungumzia  Mkutano wa jukwaa la Mabunge la Kimataifa kuhusu Eneo la Maziwa Makuu (FP-ICGLR), kwa ushirikiano na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambapo leo limesaini Makubaliano ya Uenyeji kwa ajili ya Mkutano huo  wa kwanza wa Wabunge Wanawake (WPC) 2026 nchini. hafla ya kusaini ilifanyika ofisini kwake jijini Dodoma. Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Baraka Leonard, akizungumza  kuhusu mkutano wa wanawake wa mabunge ya nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu unaotarajiwa kufanyika nchini una lengo la kuwajengea wanawake uwezo katika masuala ya uongozi, maamuzi na maendeleo ya jamii, mazungumzo hayo yalifanyika Ofisi ya Spika jijini Doddoma leo  

WAZIRI WA UCHUKUZI PROFESA MBARAWA AOMBA BAJETI YA SH TRILIONI 2.87 KWA MWAKA 2026 HADI 2027

Image
Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame  Mnyaa Mbarawa , akiwasilisha bakjeti ya Wizara hiyo leo bungeni jijini Dodoma hebu fuatana naye katika hotuba yake hii.   Mheshimiwa Spika, kufuatia taarifa iliyowasilishwa leo hapa Bungeni na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, ambayo imechambua utekelezaji wa Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi kwa mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/27, ninaomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu sasa likubali kupokea, kujadili na kuidhinisha Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi kwa mwaka wa fedha 2026/27. 2. Mheshimiwa Spika, nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutujalia uhai na kutuwezesha kukutana tena siku ya leo kujadili maendeleo ya Sekta ya Uchukuzi. Ninamuomba Mwenyezi Mungu atuongoze vyema katika kujadili Hotuba hii ya Wizara ya Uchukuzi na Bajeti ya Serikali kwa ujumla ili kufikia malengo ya Dira 2050 katika kuwaletea ...