Posts

MBUNGE LUFUNGIJA ALILIA MAENDELEA JIMBONI KWAKE SERIKALI YAAHIDI KUMPELEKEA

Image
Mbunge wa jimbo la Ulyangulu CCM,  Masanja Lufungija (pichani) leo akichangia bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani, ameitaka Serikali kukamilisha ujenzi wa vituo vya Polisi vilivyojengwa na wananchi kwa kujitolea imebaki umaliziaji tuu wa kuezeka mabati na sakafu. Akijibu maswal ya wabuge  waliochangia  bajeti hiyo Waziri wa wizara hiyo Protas Katambi amemhakikishia mbunge huyo kwamba bajeti ya mwaka huu watahakikisha maboma hayo yanamaliziwa ili kuwe na vituo hivyo . Kabla ya hapo katika maswali ya asubuhi alimuuliza Waziri wa ujenzi ni lini Barabara ya  Kahama Ulyangulu Kaliua Mpanda itajengwa kwani tangu mwaka 2015 aliahidi mgombea urais pia na Mgombea Mwenza  kwamba ingejengwa hadi leo haijajengwa.  

WAZIRI KAPINGA ASOMA BAJETI YA WIZARA YAKE LEO. WABUNGE WAMSIFIA KWA UTENDAJI KAZI

Image
Waziri wa Viwanda na Biashara , Judith Kapinga, akiwasilisha Hotuba ya  Makadilio ya Bajeti ya Wizara yake kwa mwaka  2026 na 2027 bungeni Dodoma  leo. Soma hotuba yake yote hapa 1. Mheshimiwa Spika; kutokana na taarifa iliyowasilishwa leo hapa Bungeni na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo ambayo imechambua Bajeti ya Wizara ya Viwanda na Biashara tarehe 24 na 26 Machi, 2026, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu likubali kupokea na kujadili Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Mwaka 2025/2026. Aidha, ninaliomba Bunge lako likubali kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda na Biashara kwa Mwaka 2026/2027. 2. Mheshimiwa Spika; nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema, kwa afya njema na kuwepo hapa siku hii muhimu ya leo. 3. Mheshimiwa Spika; kwa unyenyekevu na moyo wa shukrani, nitumie nafasi hii kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, R...