MAADHIMISHO YA MIAKA 62 YAFANA JIJINI DODOMA
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati akimpatia kioaza sauti Rais wa Chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania na Naibu Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile, afafanue jambo Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati *Rais Samia atunukiwa Tuzo ya Ubinadamu; *Ombi la ruzuku kwa Chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania lafanyiwa kazi; Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa Serikali inatambua mchango mkubwa unaotolewa na Chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania (Tanzania Redcross Society) katika utoaji huduma mbalimbali za kibinadamu hususan nyakati za dharura. Dkt. Biteko amesema hayo leo (Mei 11, 2024) Jijini Dodoma alipomwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa mgemi rasmi katika maadhimisho ya miaka 62 ya Chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania ambapo amesema huduma zinazotolewa na chama hicho zinazingatia sheria na kanuni na taratibu za kuanzishwa kwa chama hicho ikiwa ni pamoja na kutoa huduma bila upendeleo