DODOMA WASEMA AMANI KWANZA

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rose-Mary Senyamule, akiongoza Matembezi ya Kuhamasisha Amani na kuliombea Taifa, matembezi hayo yalianza leo asubuhi  Lango la Bunge Mkabala na  Shule ya Sekondari Dodoma  hadi viwanja vya Nyerere Square. Matembezi hayo pia  yaliambatana na uchunguzi wa matibabu ya magonjwa ya Moyo, Macho, Figo, Saratani na Selimundo. Uchunguzi huo uliendeshwa na madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Benjamini Mkapa wakiongozwa na Mkurugenzi wake Profesa Abel Makubi..Makundi yote ya jumuiya ya Wanadodoma  yakiongozwa na viongozi wake au wawakilishi wao kila aliyesimama alikuwa akiomba uchaguzi Mkuu  uwe wa amani, bila amani hakitafanyika kitu. Akihitimisha Mkuu wa Mkoa alisema Serikali ipo makini wananchi mtoe taarifa  kama kuna mtu au kikundi cha watu watakachokibaini kwamba kinataka kuhatarisha amani ili washugulike naye serikali imejipanga  ipo makini na wasithumubu chamoto watakiona watakaothubutu, alibainisha Senyamule.


























 

Comments

Popular posts from this blog

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

KADA MGEJA AHUDHURIA MAZIKO YA MAMA MZAZI WA MWANDISHI MWANDAMIZI WA HABARI KAHAMA