Posts

DKT. BITEKO AMWAKILISHA RAIS SAMIA UWEKAJI WAKFU ASKOFU MPYA JIMBO KATOLIKI BUKOBA

Image
📌 Asema Nchi inajivunia Haki, Uhuru, Umoja na Amani Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko, leo amemwakilisha Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Sherehe za kuwekwa Wakfu na Kusimikwa kwa Askofu Mpya wa Jimbo Katoliki Bukoba, Mhashamu Jovitus Mwijage ikiwa ni tukio la kihistoria kutokana na kupita takriban miaka 50 kutoka kufanyika sherehe kama hiyo ya uwekaji wa wakfu. Sherehe hizo zimefanyika katika uwanja wa Kaitaba wilayani Bukoba Mkoa wa Kagera, na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Fatma Mwasa na Mbunge wa Bukoba Mjini ambaye pia ni Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato. Akitoa Salam za Dkt. Samia kwa waumini na wananchi waliohudhuria sherehe hizo, Dkt. Biteko ameeleza kuwa, Rais  ataendelea kutoa ushirikiano kwa Kanisa Katoliki na madhehebu mengine ili kwa pamoja walete maendeleo nchini. Amesema, Rais anatambua kuwa bado kuna changamoto mbalimbali nch...

CHAMA CHA WALIMU TANZANIA ( CWT) CHAMTAKIA HERI YA KUZALIWA RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

Image
 

RAIS SAMIA AADHIMISHA SIKU YAKE YA KUZALIWA KWA KUPANDA MITI 4720 NA 120 YA MATUNDA

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ameungana na wananchi wa makundi mbalimbali kupanda miti 4720 inayotarajiwa ikiwemo miti 120 ya matunda. Miti hiyo imepandwa katika eneo la Donge Muwanda jimbo la Tumbatu lenye ukubwa wa ekari 35.7 ikiwa ni maadhimisho ya kumbukumbu ya siku yake ya kuzaliwa.  Aidha, Rais Samia amesema siku hii inaadhimishwa kwa kupanda miti kwasababu ya kuwepo kwa uharibifu mkubwa wa mazingira nchini hasa visiwani Zanzibar. Rais Samia amesema upandaji wa miti kwa wingi pamoja na mikoko kutasaidia kurudisha hali asilia ya bahari na kupunguza kasi ya mmomonyoko wa ardhi.  Rais Samia ametoa wito kwa wananchi wa eneo hilo kuitunza miti hiyo ili imee na kuwa na manufaa kwa vizazi vijavyo.  Rais Samia ameitaka Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar kuzuia uchimbaji wa mchanga kiholela pamoja na kusitisha shughuli za kukata matofali ya miamba na kutoa vibali vya uchimbaji kwa wananchi w...

WABUNGE WA YANGA WAENDELEA KUWANYANYASA SIMBA WA BUNGENI

Image
Timu za watani wabunge wa Yanga na Simba zikiingia uwanjani kwa ajili ya mpombano wa Azania Bunge Bonanza uliofanyika leo katika uwanja wa CCM  Jamhuri jijini Dodoma  ambapo Timu ya wabunge wa wapenzi na wanachama wa yanga waliendeleza kuwakung'uta watani zao simba bao 5-4 hivyo hivyo katika mchezo wa kuvuta kamba waliwaburuta mara mbili na kujinyakulia ushindi. Wabunge wa Yanga na baadhi ya wafanyakazi wa bunge  wakitoa salamu ya Taifa ya 5G wakiongozwa na Waziri wa Fedha  Dkt. Mwigulu Nchemba wasita toka kulia waliosimama. Wabunge wa Simba na Wafanyakazi wa Bunge wakiwa katika picha ya pamoja kbla ya kuanza mpambano huo Timu zote zikipiga picha ya pamoja ya ukumbusho Timu ya yanga walioanza mpambano Viongozi wa Yanga  Rais na Makamu wake walitoka Dar kwa ajili ya Bonanza hilo Mchezaji wa Yanga Dkt. Mwigulu Nchemba, akionyesha kwamba na leo ni 5G kabla ya kuanza mpambano huo Kipa wa simba akipisha na bao Kipa wa Yangaa Michael Kadebe, akipangua penati  na ...

KANUNI ZA KUTAMBUA MAENEO LINDWA ZANUKIA

Image
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akiwasilisha taarifa ya uratibu wa usimamizi wa masuala ya mazingira kwa wizara za kisekta, mafanikio, changamoto na utatuzi pamoja na taarifa ya hali ya usimamizi wa utekelezaji wa mipango ya ulinzi wa mazingira katika maeneo lindwa na nyeti kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira jijini Dodoma leo Januari 24, 2024. Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Maganga akifafafanua jambo wakati wa kikao cha kupokea taarifa ya uratibu wa usimamizi wa masuala ya mazingira kwa wizara za kisekta, mafanikio, changamoto na utatuzi pamoja na taarifa ya hali ya usimamizi wa utekelezaji wa mipango ya ulinzi wa mazingira katika maeneo lindwa na nyeti kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira jijini Dodoma leo Januari 24, 2024. Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira Mhe. Jackson Kiswaga akiongoza kikao cha kupokea taarifa ya ya uratibu w...

KAMATI YA KUDUIMU YA BUNGE PAC YAPOKEA UTEKELEZAJI WA PROGRAMU YA KUKUZA UJUZI KWA VIJANA

Image
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Mhe. Naghenjwa Kaboyoko akichangia hoja baada ya wasilisho la taarifa ya programu ya kukuza ujuzi wa nguvu kazi nchini inayotekelezwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu wakati wa kikao cha kamati hiyo kilichofanyika leo Januari 24, 2024 Bungeni jijini Dodoma. @@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@ Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imepokea taarifa ya Programu ya kukuza Ujuzi wa Nguvu Kazi nchini inayotekelezwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu. Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Naghenjwa Kaboyoka akizungumza leo Januari 24, 2024 baada ya kupitia na kuchambua wasilisho la Ofisi hiyo Fungu 65 kuhusu programu hiyo, amesema wasilisho hilo litasaidia kamati kutoa ushauri utakaoongeza ufanisi kwenye utekelezaji wake wa kukabiliana na tatizo la ukosefu wa ajira. Akijibu hoja za wajumbe wa kamati hiyo, Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, M...