KANUNI ZA KUTAMBUA MAENEO LINDWA ZANUKIA

Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt.
Selemani Jafo akiwasilisha taarifa ya uratibu wa usimamizi wa masuala ya
mazingira kwa wizara za kisekta, mafanikio, changamoto na utatuzi
pamoja na taarifa ya hali ya usimamizi wa utekelezaji wa mipango ya
ulinzi wa mazingira katika maeneo lindwa na nyeti kwa Kamati ya Kudumu
ya Bunge ya Maji na Mazingira jijini Dodoma leo Januari 24, 2024. 
Katibu
Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Maganga akifafafanua jambo wakati
wa kikao cha kupokea taarifa ya uratibu wa usimamizi wa masuala ya
mazingira kwa wizara za kisekta, mafanikio, changamoto na utatuzi pamoja
na taarifa ya hali ya usimamizi wa utekelezaji wa mipango ya ulinzi wa
mazingira katika maeneo lindwa na nyeti kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Maji na Mazingira jijini Dodoma leo Januari 24, 2024.
Mwenyekiti
wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira Mhe. Jackson Kiswaga
akiongoza kikao cha kupokea taarifa ya ya uratibu wa usimamizi wa
masuala ya mazingira kwa wizara za kisekta, mafanikio, changamoto na
utatuzi pamoja na taarifa ya hali ya usimamizi wa utekelezaji wa mipango
ya ulinzi wa mazingira katika maeneo lindwa na nyeti kwa Kamati ya
Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira jijini Dodoma leo Januari 24, 2024.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira pamoja na Wajumbe wa Menejimenti ya Ofisi ya Makamu wa Rais wakiwa katika kikao cha kupokea taarifa ya uratibu wa usimamizi wa masuala ya mazingira kwa wizara za kisekta, mafanikio, changamoto na utatuzi pamoja na taarifa ya hali ya usimamizi wa utekelezaji wa mipango ya ulinzi wa mazingira katika maeneo lindwa na nyeti kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira jijini Dodoma leo Januari 24, 2024.
@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@
Serikali imesema imeanza kuandaa Kanuni za kutangaza na kusimamia maeneo 77 Nyeti na Lindwa yaliyoainishwa na kutarajiwa kukamilika kabla ya Juni, 2024.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo kwenye Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira jijini Dodoma leo Januari 24, 2024.
Amesema tayari Serikali imeyapa kipaumbele maeneo 12 kwa ajili ya kufanyiwa tathmini zaidi kwa kuzingatia umuhimu wake kiikolojia kutokana na uharibifu wa mazingira.
Akiwasilisha taarifa ya Hali ya Usimamizi wa Utekelezaji wa Mipango ya Ulinzi wa Mazingira katika maeneo Lindwa na Nyeti amesema maeneo yaliyo kwenye mpango huo ni yaliyoko kwenye madakio ya mito, maziwa, shoroba, milima na ardhi oevu
Aidha, Dkt. Jafo ameyataja maeneo hayo kuwa ni Dakio la Mto Kihansi, Ziwa Challa lililoko Wilayani Rombo Mkoa wa Kilimanjaro, Mlima Livingstone na safu ya milima ya Mbeya katika mikoa ya Mbeya, Njombe na Ruvuma na safu ya Milima ya Makonde (Makonde Plateau Mountain Ranges).
Maeneo mengine ni maeneo nyeti na lindwa pendekezwa ambayo ni Mlima Mukendo uliopo mjini Musoma mkoani Mara, Ziwa Singidani, Ziwa Kindai na Ziwa Munang yaliyoko mkoani Singida na Ziwa Burunge, mifumo ikolojia ya hifadhi ya Tarangire na Ziwa Manyara yaliyoko mkoani Manyara.
Waziri Jafo ametaja faida za kuwa na maneo lindwa na nyeti ni kuimarisha uhifadhi wa mifumo ikolojia yenye misitu, vyanzo vya maji na wanyamapori iliyopo nje ya maeneo yanayosimamiwa na sheria nyingine.
Amesema hatua hiyo itasaidia pia Faida nyingine kulinda mazalia, makazi, malisho na makuzio ya viumbe na madhara yatokanayo na majanga ya asili yanayoweza kutokea katika maeneo husika kama vile maporomoko ya ardhi, mafuriko na uvamizi wa wanyamapori.
“Tupo katika hatua ya kupunguza mgongano wa matumizi ya rasilimali kati ya wanyamapori na wananchi, kupunguza mgongano wa matumizi ya rasilimali kati ya wanyamapori, uharibifu wa misitu unaotokana na shughuli za kibinadamu kama vile ukataji miti kwa ajili ya mkaa na kuni na uchimbaji holela wa madini,” amesisitiza Dkt. Jafo.
Hivyo, amesema Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeendelea na juhudi mbalimbali za kuainisha maeneo mengine, kufanya tathmini na ufuatiliaji na kupendekeza njia bora za uhifadhi katika maeneo mengine yenye sifa za kuwa maeneo lindwa au nyeti
Akiwasilisha
taarifa ya Uratibu wa Usimamizi wa Masuala ya Mazingira kwa Wizara za
kisekta, mafanikio, changamoto na utatuzi, amesema Ofisi ya Makamu wa
Rais itaendelea kuhimiza uanzishaji na kuboresha vitengo vya mazingira
katika eneo hilo.
Dkt. Jafo amebainisha kuwa uwepo wa vitengo hivyo umeongeza
ushiriki wa wizara hizo katika maandalizi ya mipango, programu na
mikakati ya kitaifa inayohusu hifadhi ya mazingira na mabadiliko ya
tabianchi.
Baadhi ya nyenzo na mikakati mbalimbali ya kitaifa iliyoandaliwa
ni pamoja na Mpango Kabambe wa Taifa wa Hifadhi na Usimamizi wa
Mazingira, Mkakati wa Taifa wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi,
Mchango wa Nchi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi na Taarifa za
Hali ya Mazingira Nchini.
Comments
Post a Comment