Posts

Showing posts from September, 2026

MOI SASA MATIBABU YA KISASA TUPU BALOZI DKT. MPOKI

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya amesema kuwa utoaji wa tiba bora, uwepo wa wataalamu wabobezi pamoja na matumizi   kupitia QR Code, unaolenga kupunguza msongamano wa wagonjwa katika hospitali. Amesema hayo leo wakati akizungumza na wanahabari katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO jijini Dodoma leo. Aidha, amesema Kuwa baada ya mgonjwa kuweka miadi, mfumo wa MOI utaonyesha taarifa za mgonjwa, daktari anayetarajiwa kumuona pamoja na kliniki na muda wa huduma, hivyo kupunguza muda wa kusubiri hospitalini. Aidha akibainisha Kuwa mfumo huo umeanzishwa kutokana na changamoto ya msongamano, ambapo historia wagonjwa walikuwa wakifika hospitalini saa 10 za alfajiri na kusubiri hadi saa 8 mchana ili kuonana na daktari. Pia, ameseme kuwa mfumo huo utawawezesha wagonjwa kufika katika muda waliopangiwa na kuendelea na shughuli nyingine, badala ya kutumia muda mrefu kusubiri huduma hospitalini. Mkurugenzi huyo amesema katika mwaka wa fedha 2025/26 MOI imehudumia juml...

MBUNGE ACHACHAMAA KUHUSU SOKO LA HISA DAR ES SALAAM

Image
Mbunge Hawa Mwaifunga, akichangia maoni yake katika semina iliyowahusisha viongozi wa Soko la Hisa Dar es Salaam (DSE) na baadhi ya makampuni yaliyomo kwenye soko hilo na kutaka fedha zake alizowekeza miaka kumi iliyopita arejeshewe kwani haoni faida ya kuwekeza kwenye baadhi ya makampuni.       Akichangia huku akishangiliwa na wabunge alisema miaka kumi iliyopita aliwekeza zaidi ya Sh milioni 10 Kampuni ya Vodacom Tanzania  lakini chakushangaza alikuja kulipwa sh. lakini mbili (200,000) baada siku nyingi kupita tofauti na matarajio yake.  "Bora ningeenda kuwapatia wapigakura wangu kuliko kuwekeza huku sioni faida yake kama mtakuwa mkifanya hivi mtakuwa hampati wa kuwekeza fedha zao nakuomba mwenyekiti nije kuchukuwa fedha zangu kwako sasa hivi ,"alisema hayo huku   akimuomba mwenyekiti wa kikao hicho ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti ya Bunge Mashimba Mashauri Ndaki aende kuchukuwa fedha zake alizowekeza kwenye soko hilo. Hata hivyo M...