Posts

Showing posts from January, 2026

WAZIRI MAKONDA AFIKISHA UJUMBE WA RAIS DKT.SAMIA KWA RAIS WA CAF DKT. MOTSEPE

Image
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mheshimiwa Paul Christian Makonda amekutana na Rais wa Shirikisho la Kandanda Barani Afrika (CAF) Dkt. Patrice Motsepe Jijini Rabat, Morocco na kukabidhi barua kutoka kwa Rais Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan. Pamoja na kukabidhi barua hiyo Mheshimiwa Makonda aliyeongozana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo na Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Gerson Msigwa amemhakikishia Dkt. Motsepe kuwa Rais Samia yupo tayari wakati wote kushirikiana na CAF katika utekelezaji wa mipango mbalimbali ya maendeleo ya kandanda ikiwemo mashindano mbalimbali. Amesema Tanzania imepiga hatua kubwa katika maandalizi ya kuwa wenyeji wa AFCON 2027 sambamba na Kenya na Uganda na kwamba imedhamiria kuonesha tofauti kubwa na mashindano yaliyopita. Aidha, Makonda amemuomba Dkt. Motsepe kuiangalia Tanzania kimkakati ili mipango inayowekwa na Serikali ipate mafanikio makubwa yanayotarajiwa. Kwa upande wake Dkt. Motsepe amemshukuru Rais Sa...

WAZIRI KIKWETE ASEMA MFUKO WA UWEKEZAJI UNAFAIDA KUBWA SASA WAKUA KWA KASI

Image
  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Wawekezaji wa Mfuko wa Uwekezaji wa Faida (Faida Fund) wakati wa Mkutano wa Tatu (3) wa Mwaka uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano uliopo jengo la PSSSF jijini Dar es Salaam Wawekezaji wa Mfuko wa Uwekezaji wa Faida (Faida Fund) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete wakati akizungumza nao kwenye Mkutano wa Tatu (3) wa Mwaka wa Mfuko huo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano uliopo jengo la PSSSF jijini Dar es Salaam. Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Watumishi Housing Investments (WHI), Bw. Sephania Solomon (wa tatu kutoka kulia) akisubiri kumpokea Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) kabla ya Waziri huyo kufungua Mkutano wa Tatu (3) wa Mwaka wa Mfuko wa Uwekezaji wa Faida (Faida Fund) uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano uliopo je...

KIHONGOSI AMTAKA MZEE WARIOBA AACHE KUSEMA SEMA HOVYO.

Image
Katibu wa NEC, Siasa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, Kenan Kihongosi ( pichani)  amemtaka Waziri Mkuu Mstaafu   Jaji Joseph Sinde Warioba, kupumzika   kwa amani na kujiepucha na masuala ya kuzungumza na waandishi wa Habari mara kwa mara, aliayesam hayo jijini Dodoma leo wakati akizungumzia kuanza ziara ya nchi nzima kuangalia Ahadi za chama hicho zilizotolea wa wagombea wake kwenye kipindi cha kampeni za uchaguzi Mkuu uliofanyika mwaka jana. Warioba alikutana na Rais Dkt. Samia baada ya kutoka Ikulu kesho yake anazungumza na Mwanahabari kitu ambacho anafahamu taratibu zake kama alikuwa hajaridhika ageweza kupeleka dukuduku lake sehemu husika na kusikilizwa. Aidha amempongeza Rais na Mwenyekiti wa Chama hicho Dkt. Samia Suluhu Hassan, alipokutana na mabalozi na kuwaelezea hali halisi ya nchi hii kama msemaji wa chama anajiona Fahari kuwa na Rais kama huyo, Amesema kuwa CCM itaendelea kusimamia misingi yake kwa kuhakikisha ukweli wa historia ya taifa na mafanikio y...