Posts

Showing posts from November, 2025

Kwagilwa awataka watumishi wa umma kuheshimu na kuzingatia muda wa kazi

Image
    Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu, Mhe. Reuben Kwagilwa, amewataka watumishi wote walio chini ya Ofisi hiyo kuripoti kazini saa 1:30 asubuhi na kutekeleza majukumu yao hadi saa 9:30 alasiri kama ilivyoanishwa katika Kanuni F.1 ya Kanuni za Kudumu za Utumishi wa Umma za mwaka 2009. Kwagilwa am etoa maelekezo hayo leo tarehe 24 Novemba, 2025 baada ya kufanya ziara ya kikazi ya kushtukiza katika Shule ya Msingi Kisasa jijini Dodoma majira ya saa 1:30 asubuhi na kubaini idadi kubwa ya walimu wa shule hiyo hawajaripoti kazini kwa wakati ili kutekeleza wajibu wao kama ilivyokusudiwa na Serikali. “Wakati nimefika hapa nimekagua kitabu cha maudhurio ya walimu na kubaini walimu 16 tu kati ya walimu zaidi ya 55 ndio waliowahi kazini, hivyo kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI Mhe. Profesa Riziki Shemdoe ninaelekeza kuwa, watumishi wote walio chini ya OWM- TAMISEMI wakazingatie muda wa ...

KASIMAMIENI UBORA WA ELIMU KWA WACHINI YENU UTENDAJI UWE MZURI---PROFESA SHEMDOE

Image
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI),  Profesa. Riziki Shemdoe, amewataka wakuu wa shule za msingi nchini  kufanya kazi kwa upendo huku wakiwasimamia walimu waliochini yao kufanya kazi kwa amani na mshikamano ili kuhakikisha huduma ya elimu na ubora wake unaacha  tabasamu  kwa wanafunzi nchini. Waziri huyo ameyasema hayo leo wakati akifungua mkutano wa siku tatu wa  UMOJA wa Walimu Wakuu wa Shule za Msingi Tanzania Bara (TAPSHA),   unaofanyika jijini Dodoma. TAMISEMI ni kuwatumikia watanzania hivyo kila aliyebahatika kupata nafasi ya uongozi ahakikishe anawatumikia watanzania kwa ufanisi na uzalendo. “Sisi watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI tunao wajibu wa kipekee wa kuleta tabasamu kwa wananchi, tukitimiza kikamilifu jukumu la kutoa huduma bora,” amesema Profesa. Shemdoe. Naye, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI anayeshughulikia Elimu. Atupele Mwambene amesema, Walimu Wakuu walioudh...

WAZIRI MAVUNDE AAGIZA LESENI 73 ZA UTAFITI WA MADINI NCHINI ZIFUTWE

Image
Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, ameiagiza Tume ya Madini kufuta jumla ya leseni 73 za utafutaji na uchimbaji wa kati wa madini, kutokana na maeneo husika kutokuendelezwa kama sheria inavyotaka. Akizungumza na wanahabri Leo Jumanne jijini Dodoma huku akiwa ameambatana na Naibu waziri wa wizara hiyo Dkt Steven Kiruswa, Waziri Mavunde amesema hatua hiyo imechukuliwa baada ya baadhi ya wamiliki wa leseni kushindwa kurekebisha makosa yaliyobainishwa na Tume ya Madini, licha ya kupewa muda wa kufanya hivyo na wasifanye . Amesema kuwa wamiliki wa leseni 44 za utafutaji wa madini pamoja na wamiliki wa leseni 29 za uchimbaji wa kati wameshindwa kutekeleza masharti ya leseni zao na hivyo kukiuka sheria ya madini nchini . Waziri Mavunde amewataka wamiliki wote wa leseni za madini kuhakikisha wanazingatia matakwa ya sheria na masharti ya leseni wanazomiliki, akisisitiza kuwa Serikali haitavumilia tabia ya watu kuchukua leseni na kisha kushindwa kuyaendeleza maeneo husika na baadae inapotokea ku...

TANZANIA ,JAPAN KUIMARISHA USHIRIKIANO SEKTA YA UJENZI .WAZIRI SANGU

Image
  @@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@ Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu, amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka Japan kuhusu kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Japan katika maendeleo ya rasilimali watu hususan kwenye sekta ya ujenzi. Katika mazungumzo hayo, pande zote mbili zimejadili fursa za kuboresha ujuzi wa wataalam wa sekta ya ujenzi kupitia mafunzo, kubadilishana uzoefu na programu maalumu za kukuza uwezo.  Aidha, Ujumbe wa Japan umeonesha utayari wa kuendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuhakikisha nguvu kazi ya Kitanzania inakuwa na weledi unaokidhi mahitaji ya soko la kimataifa. Mazungumzo hayo yamefanyika Novemba 24, 2025 Jijini Dar es salaam ambapo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mohmoud Thabit na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Bi. Zuhura Yunus wamehudhuria mazungumzo hayo.

RAIS DKT. SAMIA KUTUNUKU KAMISHENI MAAFISA WANAFUNZI (JWTZ) MONDULI

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na viongozi mbalimbali mara baada ya kuwasili katika Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi (TMA) Monduli mkoani Arusha kwa ajili ya kutunuku Kamisheni Maafisa Wanafunzi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kundi la 06/22 Shahada ya Sayansi ya Kijeshi, kundi la 72/24-Regular pamoja na mahafali ya sita ya Shahada ya kwanza ya Sayansi ya Kijeshi kundi la 06/22 katika sherehe zilizofanyika chuoni hapo, tarehe 22 Novemba, 2025.       Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimama wakati Wimbo wa Taifa ukiimbwa mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi (TMA) Monduli mkoani Arusha, tarehe 22 Novemba, 2025.         Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride rasmi la kumaliza Mafunzo la Maafisa Wanafunzi w...