KASIMAMIENI UBORA WA ELIMU KWA WACHINI YENU UTENDAJI UWE MZURI---PROFESA SHEMDOE
TAMISEMI ni kuwatumikia watanzania hivyo kila aliyebahatika kupata nafasi ya uongozi ahakikishe anawatumikia watanzania kwa ufanisi na uzalendo.
“Sisi watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI tunao wajibu wa kipekee wa kuleta tabasamu kwa wananchi, tukitimiza kikamilifu jukumu la kutoa huduma bora,” amesema Profesa. Shemdoe.
Naye, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI anayeshughulikia Elimu. Atupele Mwambene amesema, Walimu Wakuu walioudhuria mkutano huo ndio wenye jukumu la kupeleka tabasamu kupitia malezi watakayoyatoa kwa walimu wanaowasimamia na hatimaye wanafunzi watapata uelewa na ufaulu mzuri.
Akizungumza kwa niaba ya washiriki wa mkutano huo, Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Wakuu wa Shule za Msingi, Didas Bambaza amemuahidi Profesa. Shemdoe kuwa, Walimu Wakuu watakwenda kutekeleza kwa vitendo maelekezo yote aliyoyatoa ili huduma zitakazotolewa katika shule zote zilete tabasamu kwa wanafunzi na wananchi.
Kaulimbiu ya Mkutano Mkuu huo wa Saba wa Mwaka wa Chama cha Walimu Wakuu wa Shule za Msingi (TAPSHA) ni Mtaala Ulioboreshwa kwa Elimu Bora; Ujuzi na Ubunifu kwa Maendeleo endelevu ya Taifa.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu, Reuben Kwagilwa, akisisitiza jambo katika mkutano huoMwenyekiti wa UMOJA wa Walimu Wakuu wa Shule za Msingi Tanzania Bara (TAPSHA),Rehema Ramole akizungumza katika mkutano huo
Waziri na naibu wake wakiteta
Comments
Post a Comment