Posts

Showing posts from December, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Same Aeleza Jitihada za Kuendeleza Utalii na Uhifadhi

Image
  NA ASHRACK MIRAJI Mkuu wa Wilaya ya Same, Kasilda J. Mgeni, amefungua milango ya maendeleo ya utalii kwa kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Nkoba Mabula, leo Septemba 25, 2024. Katika mkutano huo, Mgeni alisisitiza kwamba utalii si tu fursa ya kiuchumi, bali pia njia ya kuboresha maisha ya wananchi na kuhifadhi mazingira, huku akielezea jitihada za kutangaza vivutio vya wilaya ili kuvutia wawekezaji na kuimarisha uchumi wa eneo hilo. ā€œHapa Same tumezungukwa na hifadhi mbalimbali na kutambua umuhimu wa uhifadhi, mwaka huu tulifanya tamasha kubwa la Same Utalii Festival. Tamasha hili liliwakutanisha wadau mbalimbali, na wananchi wameweza kuona umuhimu wa kuhifadhi mazingira na wanyamapori,ā€ alisema Mgeni. Aliongeza kuwa tamasha hilo lilikuwa jukwaa muhimu la kuhamasisha jamii kuhusu faida za uhifadhi na jinsi unavyoweza kuchangia katika ustawi wa kiuchumi. Mgeni alitoa shukrani kwa Rais kwa kuendelea kutekeleza sera za maendeleo ya utalii, akieleza kuw...

MKUU WA MAJESHI JENERALI JACOB MKUNDA AVISHA NISHANI

Image
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania Jenerali Jacob John Mkunda kwa niaba ya Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt Samia Suluhu Hassan amewavisha nishani mbalimbali Majenerali, Maafisa na Askari wa JWTZ Mkoani Tabora  tarehe 21 Disemba 2024. Nishani alizovisha  ni pamoja na Nishani ya Kumbukumbu ya Muungano Daraja  la Nne, Nishani ya  Utumishi Uliotukuka, Nishani ya Utumishi Mrefu, Nishani ya Utumishi Mrefu na Tabia Njema, na Nishani ya Miaka 60 ya JWTZ. Aidha,Jenerali Mkunda amewavisha nishani ya Jumuiya ya SADC Askari walioshiriki Ulinzi wa Amani nchini Msumbiji chini ya mwavuli wa Jumuiya hiyo. Akizungumza na Wanajeshi Kanda ya Magharibi Jenerali Mkunda amemshukuru Mheshimiwa Rais kwa kuwatunuku Nishani hizo. Aidha, amewatakia Heri ya Christmas na Mwaka mpya Wanajeshi wote Nchini huku akiwataka Kuviishi Viapo Vyao walivyoapa, kufanya kazi kwa Nguvu zote kwa Uhodari, Uaminifu, Utii na Nidhamu ili kuweza kuilinda Nchi, kuli...

WAZEE NI TUNU YA TAIFA ASEMA MAVUNDE

Image
Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Mkoa wa Dodoma , na Mstahiki Meya wa zamani wa mji huo ambaye pia ni MC wa Taifa kama anavyojulikana  Peter Mavunde , akizungumza na wanahabari jijini Dodoma leo, pamoja na mambo mengine  aliwaomba wananchi hususan vijana nchini  kuwatunza wazee wao  ili wawaletee baraka kwa mwenyezi mungu. Hakuishia hapo mwenyekiti huyo ambae amesema anawanachama zaidi ya 100 katika Baraza lake, amempongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwajali wazee pamoja na machif nchini na kuwapa hadhi ya kualikwa kila shughuli zinapofanyika za kitaifa na mikoa pamoja na wilaya, amewataka watanzania kuheshi,u mila na desturi za makabila yetu aidha mshikamano uendelee katika uchaguzi mkuu unaotalajiwa kufanyika mwakani nchi hii ni kioo cha amani Afrika  baadhi ya nchi zinakuja kujifunza hapa amani na mambo mengine. Baraza lake  linatalajiwa kuanza kupanda miti ili kuhifadhi mazingira nchini  

RPC KATABAZI ATEMA CHECHE DODOMA KUELEKEA SIKUKUU ZA KRISMAS NA MWAKA MPYA

Image
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma   Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) George Katabazi, akiwaonyesha wanahabari mapanga ambayo yamekamatwa katika msako wa kuelekea sikukuu  za Krismas na Mwaka mpya , ametoa onyo kwa wale wote wanaotaka kufanya uhalifu katika mkoa wa Dodoma,  chamoto watakiona na watajuta kuzaliwa  bora wakaachana na  tabia hiyo. Kamanda aliwaomyesha wanahabari zaidi ya pikipiki 30 zilizokamatwa na askari wake katika misako hiyo  Bastora moja  na lisasi zake iliyoibiwa  kwa mkazi wa Dodoma kisha kutelekezwa, gari moja na dawa za kulevya aina ya bangi zingine zikiwa zimefungwa kwenye paketi tayari kwa kuuzwa kwa watumiaji. Aidha amewapa onyo waendesha pikipiki ataanza kuwakamata wanaofanya bishara hiyo huku wakiwa hawavai kofia pamoja na abilia wao na wengine kuzifanya pikipiki ziwe  zinatoa mlio mkubwa kama wa gari wakati wakiwa wanaendesha. Katabazi akionyesha silaha iliyokamatwa Akionyesha  chombo cha kukatia...

MWAMPOSA, NSSF NA LEOPARD TOUR WAKABIDHI PIKIPIKI 60 KWA MAKONDA NAE AWAKABIDHI POLISI ARUSHA

Image
  Mtume Boniface Mwamposa wa Kanisa la Arise and Shine (Inuka Uangaze),Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii NSSF pamoja na Mfanyabiashara na Mmiliki wa Kampuni ya Utalii ya Leopard Tour wametoa Pikipiki 60 kwa Jeshi la Polisi mkoani Arusha ili kuendeleza jitihada za Kuimarisha Ulinzi na usalama na kuchochea ukuaji wa Utalii Mkoani Arusha. Aidha kati ya pikipiki hizo ,Pikipiki 20 ni kutoka kwa Mtume Mwamposa, 20 kutoka NSSF na 20 kutoka kwa Leopard Tour ambapo  zimetolewa na kukabidhiwa leo kwa Mkuu wa Mkoa  Paul Christian Makonda. Aidha  Mtume Boniface Mwamposa ameahidi kuendelea kujitoa kwa Wananchi wa mkoa wa Arusha kama sehemu ya kuchangia kwenye maendeleo ya Mkoa huo wa Kaskazini mwa Tanzania ulio kitovu cha Utalii wa Tanzania. Kwa Upande wake Mkuu wa Mkoa wa Arusha na Kamanda wa Polisi mkoani Arusha Justine Masejo wameshukuru kwa msaada huo, Huku RPC Masejo akiahidi kuzitumia kikamilifu pikipiki hizo katika kuhakikisha ulinzi na usalama wa Mkoa wa Arusha unaimarik...

WAZIRI BASHE AWAPASHA WADAU WA TASINIA YA MBEGU

Image
Waziri wa Kilimo Hussein Bashe, akizungumza katika mkutano wa wadau wa Tasnia ya Mbegu nchini katika mkutano uliofanyika jijini Dodoma leo Waziri wa kilimo Husein Bashe, amewataka wazalishaji wa mbegu za kilimo nchin kukusanya taarifa zao za uzalishaji ndani ya masaa 24 na kuzipeleka katika Taasisi ya kudhibiti ubora wa  mbegu nchini watakaopuuza agizo hilo watafutwa katika orodha ya wazalishaji nchini Agizo hilo amelitoa baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wanunuzi wa mbegu nchini katika mkutano wa wadau wa Tasinia ya mbegu katika mkutano wa kusikiliza kelo na adha wanazopata katika biashara hiyo Akiongea kwa ukali Waziri Bashe aliwataka wazalishaji hao kuwa makini na uzalishaji  kwani hataki tena kusikia wakulima wakilima  wanapotegemea kupata mavuno bora wanaambulia kupata hasara kwa kuuziwa mbegu feki. Tasinia ya kilimo siyo kificho cha makanjanja wa kuuza mbegu feki, amewambia hakuna majadiliano atakaepuuza atapoteza kazi kama mfanyakazi wa wizara hiyo. Aliwambia ...