WAZIRI BASHE AWAPASHA WADAU WA TASINIA YA MBEGU
Waziri wa Kilimo Hussein Bashe, akizungumza katika mkutano wa wadau wa Tasnia ya Mbegu nchini katika mkutano uliofanyika jijini Dodoma leo
Waziri wa kilimo Husein Bashe, amewataka wazalishaji wa mbegu za kilimo nchin kukusanya taarifa zao za uzalishaji ndani ya masaa 24 na kuzipeleka katika Taasisi ya kudhibiti ubora wa mbegu nchini watakaopuuza agizo hilo watafutwa katika orodha ya wazalishaji nchini
Agizo hilo amelitoa baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wanunuzi wa mbegu nchini katika mkutano wa wadau wa Tasinia ya mbegu katika mkutano wa kusikiliza kelo na adha wanazopata katika biashara hiyo
Akiongea kwa ukali Waziri Bashe aliwataka wazalishaji hao kuwa makini na uzalishaji kwani hataki tena kusikia wakulima wakilima wanapotegemea kupata mavuno bora wanaambulia kupata hasara kwa kuuziwa mbegu feki.
Tasinia ya kilimo siyo kificho cha makanjanja wa kuuza mbegu feki, amewambia hakuna majadiliano atakaepuuza atapoteza kazi kama mfanyakazi wa wizara hiyo.
Aliwambia kulikuwa na tatizo la mbolea feki hivi sasa limeisha kwa kuwa na mfumo mzuri wa kuuza mbolea hizo kila mkoa na kodi namba yake.
Wapo katika mpango wa kubadilisha sheria kuanzia mwakani haitaruhusiwa kuuza duka la dawa za kilimo kama muuzaji hajasomea uuzaji huo kwa shughuli za kilimo lazima awe na kisomo cha kuanzia awe na elimu ya Diploma ,shahada na kuendelea.
Haiwezekani dhana za kilimo kuuzwa na mtu asiyekuwa na elimu ya kilimo na dawa zake ."Hatutaki makanjanja kwenye kuuza bidhaa za kilimo, kila mtu anayefdeli katika maisha anakimbilia kuja kwenye kuwapiga wakulima kwa kuwauzia bidhaa fiki, stakubali kama mimi nitaendelea kuwa waziri katika wizara hii, labda mwakani wananchi wa nzega waninyime kura na Waziri asiniteua kuwa Waziri",Alisema Waziri Bashe.
Aidha naye Mkurugenzi wa Taasisi ya udhibiti wa ubora mbegu Patrick Bodiagi, alisema bado wanakabiliwa na changamoto za wazalishaji kutokuwa na elimu ya kutosha kukabiliana na utengenezaji wa mbegu bora.
Akwilini Makata wa Karanosi Amcos, akizungumza katika mkutano huo alimuomba Waziri bashe kuwasaidia wao kama wauzaji wa dawa za kilimo na pembejeo zake wamekuwa wakipata wakati mgumu kutokana na baadhi ya wafanyabiashara wa maduka ya kuuza vyakula vya binadamu wanauza bidhaa wanazouza wao na hawakamatwi.
Matuyani Loipotoki Laizel, ambaye ni msambazaji wa bidhaa za kilimo, alimpongeza Waziri Bashe kwa kuwa mkali kwa wale ambao wanacheza na zana za kilimo ambapo kilimo ni uti wa mgongo katika nchi hii.
Wadau wa mbegu za pembeje wakiwa katika mkutano huo
Akwilini Makata wa Karanosi Amcos, akizungumza katika mkutano huo alimuomba Waziri bashe kuwasaidia wao kama wauzaji wa dawa za kilimo na pembejeo zake wamekuwa wakipata wakati mgumu kutokana na baadhi ya wafanyabiashara wa maduka ya kuuza vyakula vya binadamu wanauza bidhaa wanazouza wao na hawakamatwi.
Washiriki wa mkutano huo wakimsikiliza Waziri Bashe kwa makaini
Mfanyabishara Laizel, akibadilishana mawazo na Waziri Bashe
Waziri akitoka mkutanoni
Waziri wa kilimo Husein Bashe, amewataka wazalishaji wa mbegu za kilimo nchin kukusanya taarifa zao za uzalishaji ndani ya masaa 24 na kuzipeleka katika Taasisi ya kudhibiti ubora wa mbegu nchini watakaopuuza agizo hilo watafutwa katika orodha ya wazalishaji nchini
Agizo hilo amelitoa baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wanunuzi wa mbegu nchini katika mkutano wa wadau wa Tasinia ya mbegu katika mkutano wa kusikiliza kelo na adha wanazopata katika biashara hiyo
Akiongea kwa ukali Waziri Bashe aliwataka wazalishaji hao kuwa makini na uzalishaji kwani hataki tena kusikia wakulima wakilima wanapotegemea kupata mavuno bora wanaambulia kupata hasara kwa kuuziwa mbegu feki.
Tasinia ya kilimo siyo kificho cha makanjanja wa kuuza mbegu feki, amewambia hakuna majadiliano atakaepuuza atapoteza kazi kama mfanyakazi wa wizara hiyo.
Aliwambia kulikuwa na tatizo la mbolea feki hivi sasa limeisha kwa kuwa na mfumo mzuri wa kuuza mbolea hizo kila mkoa na kodi namba yake.
Wapo katika mpango wa kubadilisha sheria kuanzia mwakani haitaruhusiwa kuuza duka la dawa za kilimo kama muuzaji hajasomea uuzaji huo kwa shughuli za kilimo lazima awe na kisomo cha kuanzia awe na elimu ya Diploma ,shahada na kuendelea.
Haiwezekani dhana za kilimo kuuzwa na mtu asiyekuwa na elimu ya kilimo na dawa zake ."Hatutaki makanjanja kwenye kuuza bidhaa za kilimo, kila mtu anayefdeli katika maisha anakimbilia kuja kwenye kuwapiga wakulima kwa kuwauzia bidhaa fiki, stakubali kama mimi nitaendelea kuwa waziri katika wizara hii, labda mwakani wananchi wa nzega waninyime kura na Waziri asiniteua kuwa Waziri",Alisema Waziri Bashe.
Aidha naye Mkurugenzi wa Taasisi ya udhibiti wa ubora mbegu Patrick Bodiagi, alisema bado wanakabiliwa na changamoto za wazalishaji kutokuwa na elimu ya kutosha kukabiliana na utengenezaji wa mbegu bora.
Akwilini Makata wa Karanosi Amcos, akizungumza katika mkutano huo alimuomba Waziri bashe kuwasaidia wao kama wauzaji wa dawa za kilimo na pembejeo zake wamekuwa wakipata wakati mgumu kutokana na baadhi ya wafanyabiashara wa maduka ya kuuza vyakula vya binadamu wanauza bidhaa wanazouza wao na hawakamatwi.
Matuyani Loipotoki Laizel, ambaye ni msambazaji wa bidhaa za kilimo, alimpongeza Waziri Bashe kwa kuwa mkali kwa wale ambao wanacheza na zana za kilimo ambapo kilimo ni uti wa mgongo katika nchi hii.
Wadau wa mbegu za pembeje wakiwa katika mkutano huo
Akwilini Makata wa Karanosi Amcos, akizungumza katika mkutano huo alimuomba Waziri bashe kuwasaidia wao kama wauzaji wa dawa za kilimo na pembejeo zake wamekuwa wakipata wakati mgumu kutokana na baadhi ya wafanyabiashara wa maduka ya kuuza vyakula vya binadamu wanauza bidhaa wanazouza wao na hawakamatwi.
Washiriki wa mkutano huo wakimsikiliza Waziri Bashe kwa makaini
Mfanyabishara Laizel, akibadilishana mawazo na Waziri Bashe
Waziri akitoka mkutanoni
Comments
Post a Comment