Posts

MKUU WA WILAYA YA SAME AWATAKA WANAFUNZI KUJIEPUSHA NA VITENDO VYA MMOMONYOKO WA MAADILI.

Image
  NA Ashrack Miraji-----SAME Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni, amewataka wanafunzi wa shule za sekondari wilayani humo kujiepusha na vitendo vinavyoashiria mmomonyoko wa maadili ikiwemo ushoga, usagaji, mapenzi kabla ya umri pamoja na utoro, akisisitiza kuwa mienendo hiyo inaweza kuhatarisha mustakabali wao na kupelekea kukatisha ndoto zao za kielimu. Akizungumza na wanafunzi wa baadhi ya shule akiwa kwenye ziara ya kufuatilia hali ya mahudhurio ya wanafunzi kwa mwaka 2025, Mhe. Kasilda alisema vitendo vya mmomonyoko wa maadili vinakwamisha juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuboresha elimu nchini. “Mimi, kama Mkuu wa Wilaya, nataka ninyi mtimize ndoto zenu. Ni marufuku kujihusisha na vitendo vyovyote vya mmomonyoko wa maadili vikiwemo kujihusisha na mapenzi, usagaji, ushoga pia utoro kwa kuwa vitendo hivyo vinarudisha nyuma jitihada za serikali katika kuinua sekta ya elimu,” alisisitiza Mhe. Kasilda. Aidha, aliwasihi wanafun...

CCM MKOA WA DODOMA WAMPOKEA WASIRA SHUHUDIA PICHA ZA MATUKIO

Image
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Tanzania Bara, Stephine Masatu Wasira, akipokelewa na Naibu katibu Mkuu wa Chama hicho tanzania bara John Mongera baada ya kuwasili makao makuu ya chama hicho jijini Dodoma leo, hafla ya mapokezi hiyo iliandaliwa na mkoa wa Dodoma. Katika mapokezi hayo Wasira aliwaambia waliofika kumpokea kwamba CCM itaendelea kutawala na wapinzani wataendelea kuchezea ndevu na kuota kwenda Ikulu. Gari la Waziri likiingia Makao Makuu Msafara wa mapikipiki kwenda Makao Makuu Akivalishwa skafu na Chipukizi wa Chama Akisalimiana na Dennis Joe Msacky amabaye ni  Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel John Nchimbi Makamu Wasiri akisalimiana na Aboubakary Liongo ambayue ni  Mkuu wa Mawasiliano katika Idara ya Uenezi, Itikadi na Mafunzo ya CCM. Wanaccm katika mapokezi hayo  

NAIBU WAZIRI MKUU DKT. BITEKO ATAKA MITAALA VYUONI IENDANE NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA

Image
  *Asisitiza matumizi ya teknolojia za kisasa, zinazojibu changamoto za jamii *Taasisi za elimu ya juu zatakiwa kuweka mkazo mafunzo ya ujasiriamali Vyuo na taasisi zinazotoa elimu ngazi ya Kati ikiwemo Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), zimetakiwa kuboresha mitaala yake ya masomo ili iendane na mahitaji ya sasa ya soko la ajira kimataifa sambamba na mahitaji ya kijamii na kiuchumi.  Hayo yamebainishwa leo Januari 21, 2025 na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko katika Maadhimisho ya miaka 60 ya chuo hicho kilichoanzishwa Januari 21, 1965. “Serikali inasisitiza matumizi ya teknolojia za kisasa na mbinu za kujifunza zinazojibu changamoto za kimataifa, ” Amesema Dkt. Biteko. Amesema kuwa Serikali inazitaka taasisi za elimu ya kati kikiwemo Chuo cha CBE kuweka mkazo kwenye mafunzo ya ujasiriamali, ili wahitimu wake waweze kuchangia kikamilifu katika uchumi wa taifa kupitia biashara bunifu na ajira binafsi. Aidha, taasisi za elimu, zikiwemo vyuo kama CBE, a...

WAZIRI MHAGAMA AZINDUA BODI YA WAKURUGENZI YA MFUKO WA NHIF JIJINI DODOMA

Image
Waziri wa Afya Jenista Mhagam, akizindua bodi ya Wakurugenzi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, uzinduzi huo ulifayika jijini Dodoma leo, akizungumza katika uzinduzi huo aliitaka bodi hiyo iliyojaa wajuzi kusimamia vyema marekebisho ya mfuko huo , aidha wawe wabunifu wa kuufanya mfuko huo unakuwa na huduma bora zaidi na upendwe na kila Mtanzania. "sina wasiwasi na wajumbe wa bodi hii kuanzia kwa Mwenyekiti wake ni zamu yenu sasa kuwaonyesha Watanzania kwamba mpo katika mfuko huo siyo kwa bahatai mbaya bara kwa uchapa kazi wenu uliotukuka ndiyo umewafanya muwe hapo", alisema Waziri huyo Mwenyekiti wa Kamati ya   Kudumu   ya Bunge ya Afya   na Masuala   ya   UKIMWI, Dkt. Elibariki   Kingu, akizungumza katika hafla hiyo Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko huo, Dkt. Irene Isaka, akizungumza katika uzinduzi huo amesema Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ( NHIF), umepanua wigo wa kuwahudumia wateja kwa kuwa na zaidi ya vituo 10,000 nchini kwa ajili ya kuhudumia wananchi, Dkt. I...