TANZANIA YAPENDEKEZA MKAKATI WA PAMOJA KUPAMBANA NA UGAIDI, MAJANGA AU
Na Mwandishi wetu, Malabo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imezishauri nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) kuwa na mpango mkakati wa pamoja katika kupambana na masuala ya ugaidi na majanga ya kibinadamu. Akitoa pendekezo la Tanzania katika Mkutano wa 16 wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika uliomalizika jana usiku Malabo, Equatorial Guinea, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) ambaye alimwakilishwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema Tanzania inapendekeza Umoja wa Afrika uwe na mpango mkakati utakaosaidia kuhakikisha kuwa nchi wanachama wanakwenda pamoja lakini pia kusaidiwa kujengewa uwezo wa kupambana na vitendo vya kigaidi. “Hakuna nchi hata moja inaweza kusema iko salama kwani vikundi vya kigaidi viko sehemu mbalimbali hivyo kwa kutumia mpango mkakati wa umoja na mshikamano ni rahisi kukabiliana na ugadi…..kwa hiyo ujumbe wetu Tanzania kwa (AU) ni kwamb...