TANZANIA YA TATU KWA UBORA WA MBEGU AFRIKA

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) ndugu Nyasebwa Chimagu, akizungumza na wanahabari katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO jijini Dodoma leo ,kuhusu huduma za mbegu zinazotolewa na Taasisi yake, Kwa Twakimu za Kimataifa Mkurugenzi huyo alisema  Tanzania ni ya tatu kwa ubora wa mbegu barani Afrika ikitanguliwa na Afrika Kusini na Nigeria na Kidunia ni ya 15,  Mkurugenzi huyo aliendelea kusema kwamba Mbegu ni bidhaa inayosimamiwa na Serikali (regulated product) duniani kote kutokana na umuhimu wake kwa usalama wa chakula na lishe, na ni mojawapo ya pembejeo muhimu katika kuleta mageuzi ya kilimo (Agricultural Transformation) kwa kuongeza tija au technical efficiency, mapato na ubora wa mazao. Aidha, biashara ya mbegu hufanyika pia kimataifa kwa kuzingatia viwango vya ubora vya kimataifa. Mathani, hadi mwaka 2026, thamani ya biashara ya mbegu duniani ilifikia Dola za Kimarekani Bilioni 67.2. Kutokana na umuhimu huo, nchi nyingi duniani zina taasisi mahiri kwa ajili ya kusimamia tasnia ya mbegu hususan kuanzia hatua ya utafiti, uzalishaji, usambazaji, uuzaji na matumizi ya mbegu bora. Hapa Tanzania Taasisi yenye jukumu hilo ni Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) iliyo chini ya Wizara ya Kilimo iliyoanzishwa kwa Sheria ya Mbegu Sura ya 308 (Toleo la Urekebu 2023) au inaweza kurejewa kama Sheria ya Mbegu Na.18 ya mwaka 2003. 1 Umuhimu wa mbegu bora:  Chanzo cha usalama wa chakula na ustawi wa mazao  Kuongezeka kwa tija  Kinga dhidi ya visumbufu vya mazao na mabadiliko ya tabianchi  Ajira katika mashamba ya mbegu, viwanda vya kuchakata mbegu, maduka ya kuuza mbegu na usafirishaji  Kuaminika kimataifa katika biashara ya mbegu ikiwa ni sehemu ya kuingiza fedha za kigeni 2. BAJETI YA WIZARA YA KILIMO Ndugu Waandishi wa Habari, tunapokutana leo hapa kueleza mafanikio katika tasnia ya mbegu, hatuwezi kuacha kusema kwa ujasiri namna Serikali ya Awamu ya Sita ilivyoamua kuipa kipaumbele sekta ya kilimo ikiwa ni sekta ya uzalishaji inayoajiri watanzania wengi ikijumuisha tasnia ya mbegu. Kuwa na kipaumbele ni suala moja muhimu lakini kutoa rasilimali za uwekezaji na kusimamia utekelezaji ni suala muhimu zaidi. Katika kipindi cha miaka mitano sasa uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (Mhula wa Kwanza na Mhula wa Pili unaoendelea), Serikali imeendelea kuongeza Bajeti ya Wizara ya Kilimo kwa ajili ya uwekezaji unaowezesha sekta ya kilimo kutoa mchango unaostahili katika uchumi kwa kuimarisha usalama wa chakula, kuongeza ajira, upatikanaji wa malighafi za viwanda na kukidhi mahitaji ya masoko ya ndani na kimataifa. i. Bajeti ya kilimo imeongezeka kutoka Shilingi Bilioni 294 mwaka 2021/2022 hadi Shilingi Bilioni 751 mwaka 2022/2023 sawa na ongezeko la asilimia 155; 2 ii. Kadhalika, Bajeti imeongezeka kutoka Shilingi Bilioni 751 mwaka 2022/2023 hadi Shilingi Bilioni 970 mwaka 2023/2024 sawa na ongezeko la asilimia 29.2; iii. Vilevile, kutoka Shilingi Bilioni 970 mwaka 2023/2024 hadi Trilioni 1.248 mwaka 2024/2025; ambayo imeendelea kwa kiwango hicho hadi mwaka 2026/2027. Maeneo ya kipaumbele katika uwekezaji huo ni ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji, ghala, kuimarisha utafiti, uzalishaji wa mbegu bora na huduma za ugani. Ndugu Waandishi wa Habari, kati ya maeneo hayo ya kipaumbele kwenye sekta ya Kilimo ambayo Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameyapa kipaumbele na kuwapa dhamana viongozi wakuu wa Wizara ya Kilimo Mheshimiwa Daniel Godfrey Chongolo (Mb), Waziri wa Kilimo na Bw. Gerald G. Mweli, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Leo hii kupitia ninyi wandishi wa Habari kwa niaba ya Serikali ninapenda kuwahabarisha Watanzania kuhusu mafanikio katika tasnia ya mbegu kwa mwaka 2025/2026 na mwelekeo kwa mwaka 2026/2027 chini ya Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) ninayoiongoza kama Mkurugenzi Mkuu. 3. MAFANIKIO KATIKA TASNIA YA MBEGU i. Bajeti katika Tasnia ya Mbegu Ndugu Wandishi wa Habari, Serikali ya Awamu ya Sita imeongeza bajeti katika tasnia ya mbegu inayojumuisha utafiti, uboreshaji wa miundombinu ya uzalishaji na uthibiti wa ubora kutoka Shilingi Blioni 16.79 mwaka 2021/2022 hadi Shilingi Bilioni 85.15 sawa na ongezeko la asilimia 307; 3 ii. Uzalishaji wa mbegu zilizothibitishwa ubora na TOSCI Ndugu Wandishi wa Habari, katika mpango wa kijitegemea kwa mbegu, uzalishaji wa mbegu bora za mazao ya kilimo umeongezeka kutoka tani 50,750 mwaka 2021/2022 hadi tani 78,842 mwaka 2025/2026 sawa na ongezeko la asilimia 55.35. Kati ya hizo, tani 45,101 za mbegu bora sawa na asilimia 57.2 zimezalishwa hapa nchini kupitia Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA) na Makampuni binafsi, na tani 33,741 (42.8%) zimeagizwa kutoka nje ya nchi. iii. Ruzuku ya mbegu za mahindi Kwa upande wa ruzuku ya mbegu bora za mahindi zilizothibitishwa na TOSCI, jumla ya tani 42,850.19 zenye thamani ya Shilingi Bilioni 333.28 zimeuzwa kwa wakulima katika mikoa yote nchini. Kati ya fedha hizo, Shilingi Bilioni 68.75 ni ruzuku ya Serikali na Shilingi Bilioni 264.54 ni mchango wa wakulima.  Uzalishaji huu wa mbegu uchangia kuifaya Tanzania kuendelea kujitegemea kwa chakula kwa utoshelevu wa asilimia 130 kwa kuzalisha tani 23,783,128 za chakula kwa msimu wa 2024/2025 na kuwa na ziada ya tani 5,504,074. Kwa zao la mahindi, nchi yetu ilizalisha tani 10,925,025 na kuwa ya tatu barani Afrika kwa uzalishaji wa mbegu za mahindi baada ya Afrika Kusini na Nigeria.  Aidha, kwa mujibu wa takwimu za USDA, kwa msimu wa 2025/2026 Tanzania ilishika nafasi ya 10 kwa kuwa na eneo la kilimo cha mahindi la Hekta Milioni 4 ikitanguliwa na China (Hekta Milioni 45), Marekani Hekta Milioni 36.9 na Brazili Hekta Milioni 22.8).  Tumeendela kuuza mazao ya kilimo nje ya nchi kama vile mahindi, mchele, mazao ya jamii ya mikunde na horticulture kutokana na kuzingatia kilimo biashara ikiwemo matumizi ya mbegu bora. 4 iv. Ujenzi wa Maabara za Mbegu na Vifaa vya Maabara Ndugu Waandishi wa habari, maabara ni mojawapo ya miundombinu muhimu katika uthibiti wa ubora wa mbegu kwa kupima viwango vya ubora kama vile uhalisia (purity), uotaji (germination), upimaji wa unyevu, afya ya mbegu (seed health), na vipimo vingine vya bayokemia (protin, mafuta, sukari, madini), vipimo vya viinilishe (vutamin, Zinc, Chuma, Calcium), GMO, mabaki ya kemikali, aina ya nasaba za ubora wa mbegu. Katika mwaka 2025/2026 Serikali itoa fedha kuimarisha uwezo wa TOSCI katika uthibiti ubora wa mbegu kwa viwango vya kimataifa ikizingatiwa kuwa TOSCI ina maabara ya taifa ya mbegu yenye ithibati ya kimataifa ya ISTA. Utekelezaji ni ifuatavyo:- MAHALI JINA Na. MRADI LA MRADI UNAKOTEKELEZWA THAMANI YA FEDHA (SHILINGI) HATUA ILIYOFIKIWA YA UTEKELEZAJI 1 Ukarabati wa Maabara ya Kisasa ya Taifa ya Mbegu 1,838,956,142 Ujenzi wa Maabara ya Taifa ya Mbegu Morogoro Ujenzi wa Maabara ya Kisasa 2 na Ofisi Kanda ya Kusini – Mtwara: Mtwara 1,220,173,378 Morogoro asilimia 99. Mradi umefikia ulisainiwa tarehe 22 Mei, 2026, ujenzi umeanza mwezi Juni, 2026 na kutarajiwa kukamilika Februari 2027 Ujenzi 3 wa Maabara ya Kisasa na Ofisi Kanda Mradi 1,203,032,639 Nzega, Tabora umeanza mwezi Juni, 2026 na ulisainiwa tarehe 22 Mei, 2026, ujenzi 5 MAHALI LA Na. JINA MRADI THAMANI YA FEDHA (SHILINGI) MRADI UNAKOTEKELEZWA HATUA ILIYOFIKIWA YA UTEKELEZAJI ya Magharibi Tabora Ujenzi kutarajiwa kukamilika Februari 2027 Mradi wa Maabara ya Kisasa 4 na Ofisi Kanda ya Ziwa – Mwanza ulisainiwa tarehe 22 Mei, 2026, ujenzi 1,208,999,116 Mwanza 5 Uboreshaji wa huduma za maabara kwa vitendea kazi 1,762,597,000 umeanza mwezi Juni, 2026 na kutarajiwa kukamilika Februari 2027 Vifaa vya ya kipima sifa mahsusindani na nje ya mbegu. Jumla ndogo ya Fedha kwa Miradi Yote ya Ujenzi 2025/2026 –TZS 7,233,758,275 Makao Makuu na Mbaara za Kanda v. Usajili wa aina mpya za mbegu kisasa vimenunuliwa ikiwemo germination chambers kwa ajili ya majaribio ya uotaji, fume hoods kwa ajili ya kijikinga na kemikali hatarishi, seed analyser kwa ajili Ndugu waandishi wa Habari, ili mbegu iweze kuzalishwa na kuuzwa hapa nchini au nje ya nchi, Sheria inataka ni lazima iwe imekidhi vigezo 6 muhimu ikiwemo kusajiliwa baada ya majaribio ya kufaa kwa uzalishaji kwa mazingira ya Tanzania na pia iwe ni teknolojia mpya. Katika mwaka 2025/2026 Wizara ya Kilimo kupitia TOSCI ilisajili aina mya za mbegu 113 za mazao mbalimbali baada ya kukamilika kwa utafiti na kukidhi viwango. Mchanganuo wa aina mpya zilizosajiliwa kwa mwaka 2025/2026 ni zifuatazo:- a) Mahindi aina 6; b) Mtama aina 2; c) Mharage ya soya aina 1; d) Muhogo aina 2; e) Tumbaku aina 3; f) Ndizi aina 12; g) Alizeti aina 2; h) Parachichi aina 5 (HASS, PINKERTON, FUERTE, X-IKULU na BOOTH 7); i) Mazao ya bustati (horticulture) aina 85 Usajili huo unafanya jumla aina mpya za mbegu 1318 zilizosajiliwa hapa nchini zikiwemo za mahindi aina 229, ngano aina 31, mtama aina 25, mpunga aina 27, maharage aina 58, soya aina 12, alizeti aina 19, ufuta aina 5, pamba aina 8, MALISHO 9, na korosho aina 64. Tunaendelea kusisitiza watafiti kugundua aina mpya za mbegu zinazokabiliana na changamoto za mabadiliko ya nchi, changamoto za uzalishaji, mahitaji ya wakulima na soko. Mathani kweye korosho tuna aina 64 za mbegu za korosho zinazoweza kuzalishwa katika mikoa mbalimbali zaidi ya mikoa iliyozoeleka ya Mtwara na Lindi. Leo hii 7 Korosho inazalishwa Dodoma, Singida, Morogoro, Tanga, Mbeya na mikoa mingine hali inayoifanya Tanzania kuongeza uzalishaji na kuwa katika ramani ya Dunia. Uzalishaji wa korosho umeongezeka kutoka tani 210,786.80 mwaka 2020/2021 hadi tani 618,497.41 mwaka 2025/2026 na kuifanya Tanzania kuwa mzalishaji wa 4 duniani baada ya Ivory Coast (Tani 1,5000,000), Cambodia (tani 1,020,000), na India tani 750,000. vi. Udhibiti wa matukio ya mbegu zisizokidhi viwango vya ubora (mbegu feki) Ndugu Waandishi wa Habari, Wizara ya Kilimo kupitia TOSCI imeendelea kudhibiti matukio ya mbegu zisizokidhi viwango vya ubora kwa kuimarisha ukaguzi wa maduka ya mbegu, ghala na viwanda vya kuchakata mbegu kwa kushirikiana na Uongozi wa Ofisi za Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama. Kutokana na hatua hizo katika mwaka 2025/2026 wahusika wa matukio ya ukiukwaji wa Sheria ya Mbegu wapatao 22 wamechukuliwa hatua mbalimbali za kisheria ikiwemo kufikishwa mahakamani, kulipa faini na fidia kwa wakulima. 4. MAENEO MENGINE YA MAFANIKIO KATIKA TASNIA YA MBEGU i. Viashiria vya Ufanisi katika Tasnia ya Mbegu Ndugu Waandishi wa Habari, Tanzania inashika nafasi ya 3 kati ya nchi 55 za Umoja wa Afrika (AU) ikiwa na wastani wa alama 7.25 kati ya 10 kwa ubora wa Sekta ya Mbegu baada ya Afrika Kusini (8.62) na Zambia 7.89 (The African Seed Access Index – TASAI, 2023) Maeneo yaliyofanya vizuri: ubora wa vifungashio vya mbegu (9.89), Sheria na Sera za Mbegu (9.00), Mifumo ya Mbegu inayosimamiwa na Wakulima (9.00), Kuoanisha Sheria na Sera za Mbegu na Miongozo ya 8 Kikanda (8.00), Mfumo wa uidhinishaji aina mpya za mbegu (8.00), taratibu za kuuza mbegu nje na kuingiza mbegu ndani ya nchi (8.00), uwepo wa kutosha wa mawakala wa mbegu (8.00), na udhibiti wa mbegu ambazo hazikidhi viwango (8.00) ii. iii. Ithibati ya International Seed Testing Association (ISTA) Ndugu Waandishi wa Habari, kwa mwaka 2025/2026 Tanzania imeendelea kudumisha uanachama wake kwa ISTA. Aidha, Tanzania ni miongoni mwa nchi 14 za Afrika na 80 duniani zenye maabara zilizo na Ithibati ya kimataifa ISTA. Faida ya ithibati ya ISTA ni Tanzania kutambuliwa kimataifa katika umahiri wa kitaalamu wa upimaji wa ubora wa Mbegu, kutoa vyeti vya (ISTA Orange International Certificate -OIC) kwa Mbegu zinazosafirishwa nje ya nchi; na kuvutia wawekezaji wapya wa biashara ya mbegu kimataifa. Tunazo kampuni za kimataifa (multinational companies) takriban 29 zinazohusika katika uzalishaji na biashara ya mbegu hapa nchini. Uanachama wa Skimu za Mbegu za OECD Ndugu Waandishi wa Habari, Tanzania ni miongoni mwa nchi 10 za Afrika zinazoshiriki katika skimu za mbegu za kimataifa za Shirika la OECD na kwa mwaka 2025/2026 tumeendelea kudumisha uanachama. Umuhimu wa Tanzania kuendelea kulinda uanachama wake kwa kuimarisha maeneo yote muhimu ikiwemo kuwa na maabara bora utachangia katika kukuza ushirikiano wa Kimataifa na bidhaa za mbegu kuuzwa bila vikwazo vya kimasoko. Mathani, katika Mwaka wa Fedha 2025/2026, jumla ya vibali 392 vimetolewa kwa ajili ya kuuza nje ya nchi tani 993.21 za mbegu. Kati ya hizo, tani 55.44 zilikuwa mbegu za mazao ya bustani, tani 9 204.07 za nafaka, tani 722.2 za mikunde na tani 11.5 za mazao ya mafuta. 5. MWELEKEO KWA MWAKA 2026/2027 Ndugu Waandishi wa Habari, sote tunatambua kuwa tarehe 17 Julai, 2025 jijini Dodoma Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, alizindua Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ikiwa ni Ramani ya Tanzania tuitakayo ifikapo mwaka 2050. Katika uzinduzi huo, pamoja na mambo mengine, Mhe. Rais alielekeza “Kila taasisi ya Serikali italazimika kuwa na vigezo vya kupima utendaji (Key Performance Indicators – KPIs) vinavyoendana na malengo na shabaha ya Dira,”. Aidha, tarehe 03 Agosti, 2026 Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alizundua nyenzo za utekelezaji wa Dira jijini Dar es Salaam. Hivyo basi, kwa kuzingatia maelekezo hayo ya Mheshimiwa Rais, Shabaha za Dira 20250 sambamba na Mpango Kabambe wa Mageuzi katika Kilimo kwa Mwaka 2026/2026 Wizara ya Kilimo kupitia TOSCI inaendelea na utekelezaji wa malengo na Shabaha za Dira kwa kutekeleza yafuatayo:- i. Kuwezesha uwekezaji na biashara ya mbegu kwa kuimarisha uratibu wa wadau na uthibiti ubora kwa mazao ya kipaumbele ambayo ni pamoja na mazao ya mboga mboga, matunda na viungo; pamba, korosho, mkonge, kahawa, mahindi, ufuta, alizeti, mpunga, ngano, mtama, maharage ya soya, mazao ya jamii yamikundi, na malisho ili kufungamanisha sekta ya kilimo mazao na ufugaji. Hatua hizi zinafanywa kwa kuzingatia kuwa mojawapo ya shabaha za Dira ni kuifanya Tanzanua kuwa mzalishaji mkubwa wa Chakula barani Afrika na miongoni mwa nchi 10 duniani ifikapo mwaka 20250;  Tutaimarisha mafunzo kwa wadau ili waweze kuzalisha mbegu za mazao ya kipaumbele kwa viwango vinavyokubalika  Tushirikiana na sekta binafsi na sekta ya umma kuvutia mitaji ya kuwekeza katika sekta ya mbegu kupitia 10 majadiliano kwa manufaa ya wote na kutengeneza sera za utoaji wa mitaji katika tasnia ya mbegu  Kutumia miundombinu iliyopo kutoa mafunzo kwa wanafunzi na wahitimu kwenye vyuo vya elimu ya juu kama sehemu ya Elimu Amali kuwapatia ujuzi katika tasnia ya mbegu ili waweze kujiajiri hususan vijana na wanawake  Kushirikiana na Uongozi wa Mikoa na Wilaya katika kutenga na kulinda ardhi kwa ajili ya mashamba ya mbegu ili kuondoa utegemezi wa kuagiza kutoka nje. ii. iii. iv. v. vi. Kuendelea kusimamia kamilishaji wa miradi ya maendeleo ya maabara mpya katika mikoa ya Mwanza, Tanora na Mtwara; na Arusha. Kuundelea kununua na kusimika vifaa vya kisasa vya maabara za mbegu. Kuhakikisha upatikanaji wa mbegu bora tani 105,000 zilizothibitishwa ubora kwa wakulima kulingana na Kalenda ya kilimo sambamba na kudhibiti mbegu feki kwa watu wenye nia ovu. Uimarishaji wa matumizi ya TEHAMA katika utoaji wa huduma za uthibiti wa ubora wa mbegu. Hivi karibuni tutakamilisha maboresho ya Mfumo wa TEHAMA wa TOAS. Kuendelea kuimarisha mashirikiano ya kikanda na kimataifa ili kubadilishana maarifa, uzoefu, teknolojia na kuoainisha viwango vya ubora. 6. HITIMISHO Ndugu Waandishi wa Habari, Mbegu bora itaendelea kuwa nguzo muhimu ya kuleta mageuzi ya kilimo kama walivyofanikiwa mataifa mengine kwa kuwa mbegu ni uhai, mbegu ni biashara na mbegu bora inalipa. Ndugu Waandishi wa Habari, nihitimishe kwa kuwashukuru nyote kwa kufika katika mkutano huu ili kuwahabarisha watanzania. Aidha, 11 niwashukuru wote ambao wamefuatia mkutano huu kwa njia mbalimbali ya vyombo vya habari. Aidha, nishukuru Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kuandaa na kuratibu Mkutano huu. Nichukue nafasi hii kuwashukuru Mheshimiwa Daniel Godfrey Chongolo (Mb), Waziri wa Kilimo na Bw. Gerald G. Mweli, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo kwa kuendelea kusimamia vipaumbele vya Taifa vya kuendeleza sekta ya kilimo hususan eneo la tasnia ya mbegu ambayo TOSCI imepewa dhamana ya kuisamia kwa mujibu wa Sheria ya Mbegu Sura ya 308 (Toleo la Urekebu 2023). Kipekee nimshukuru Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye kama nilivyoeleza awali amekuwa kinara wa kuleta mageuzi katika kilimo na kuamusha fikra za kilimo biashara kwa makundi mbalimbali ya watanzania kutoka na uwekezaji anaoufanya kwenye kilimo ikiwemo fedha za utafiti, uzalishaji na uthibiti wa ubora wa Mbegu sambamba na kufungua masoko. Hatua hizo zimedhihirisha Tanzania itafikia malengo yake ya kuilisha dunia ikiwa ni moja ya Shabaha za Dira ya 20250.



Wanahabari wakiwajibika 





 

Comments

Popular posts from this blog

AJIRA MPYA 41,500 SERIKALINI ZATANGAZWA KATIBU MKUU UTUMISHI JUMA MKOMI

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

WALIOPITA KURA ZA MAONI CCM HAWA HAPA