JESHI LA KUJENGA TAIFA (JKT) LAWAITA KIDATO CHA SITA KUANZA MAFUNZO KWA MUJIBU WA SHERIA ZA NCHI

MKUU wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele amewataka wahitimu wa kidato cha sita Tanzania Bara na Visiwani waliochaguliwa kujiunga na mafunzo ya Jeshi hilo kwa mujibu wa sheria kuripoti katika makambi waliyopangiwa  ili waweze kuanza mafunzo ya  uzalendo,ukakamavu ,kufundishwa nidhamu,Umoja wa Kitaifa,Stadi za kazi na utayari wa kulijenga na kulitumikia Taifa pasipo kulinyongonyesha.

Akizungumza na Wanahabari kwa niaba yake leo katika ofisi za Makai Mkuu ya Jeshi hilo jijini Dodoma   Mkuu wa Tawi la Utawala JKT Brigedia Jenerali Hassan Mabena, amesema majina ya waliochaguliwa yanapatikana kwenye tovuti ya JKT ambayo ni  www.jkt.mil.tz. Hii hapa ni taarifa nzima ya Mkuu huyo. TAARIFA KWA UMMA

WITO WA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA JKT

KUNDI LA LAZIMA (MUJIBU WA SHERIA)

MWAKA 2026

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Meja Jenerali Rajabu Nduku

Mabele, anatoa wito kwa Vijana waliohitimu elimu y a

sekondari kidato cha sita mwaka 2026, kutoka shule zote

za Tanzania Bara na Visiwani kuhudhuria Mafunzo ya JKT

Kundi la Lazima (Mujibu wa Sheria) kwa mwaka 2026.

Sanjari na wito huo, JKT limewapangia Makambi watakayo

kwenda kupatiwa Mafunzo na wanatakiwa kuripoti

makambini kuanzia tarehe 0 1 Juni hadi tarehe 0 7 Juni

2026.

1

Vijana hao wamepangwa katika Kambi za JKT zifuatazo;

Rwamkoma JKT-Mara, Msange JKT-Tabora, Ruvu JKT na

Kibiti JKT-Pwani, Mpwapwa JKT na Makutupora JKT-

Dodoma, Mafinga JKT-Iringa, Mlale JKT-Ruvuma, Mgambo

JKT na Maramba JKT-Tanga, Makuyuni JKT n a Oljoro JKT-

Arusha, Bulombora JKT,Kanembwa JKT n a Mtabila JKT-

Kigoma, Itaka JKT-Songwe, Luwa JKT n a Milundikwa JKT-

Rukwa, Nachingwea JKT- Lindi na Chuo cha Uongozi JKT

(CUJKT) Kimbiji- Dar es Salaam.

Wahitimu wenye ulemavu wa kuonekana kwa macho

(Physical disabilities) waripoti katika Kambi ya Ruvu iliyopo

Mlandizi Mkoani Pwani ambayo ina miundombinu ya

kuwahudumia watu hao.

Aidha, JKT linawataka vijana hao kuripoti wakiwa na vifaa

vifuatavyo:

1. Bukta ya rangi ya 'Dark Blue' yenye mpira

kiunoni (lastic) iliyo na mfuko mmoja

nyuma, urefu inayoishia magotini, isiyo na

zipu.

2. T-shirt ya rangi ya kijani.

3. Raba za michezo zenye rangi y a kijani au

blue.

4. Shuka mbili za kulalia zenye rangi ya blue

bahari.

2

5. Soksi ndefu za rangi nyeusi.

6. Nguo za kuzuia baridi kwa waliopangiwa

Mikoa yenye baridi.

7. Track suit ya rangi ya kijani au blue.

8. Nyaraka zote zinazohitajika katika udahili

wa kujiunga n a Elimu ya juu, zikiwemo vyeti

vya kuzaliwa, Vyeti vya kuhitimu kidato cha

nne n.k

9. Nauli ya kwenda kuripoti makambini na

kurudi nyumbani.

Orodha kamili ya majina ya vijana hao, Makambi ya JKT

waliyopangiwa, maeneo Makambi hayo yalipo na vifaa

wanavyotakiwa kwenda navyo, inapatikana katika tovuti ya

JKT ambayo ni www.jkt.mil.tz

Aidha, ili kufahamu kambi kijana aliyopangiwa, atatakiwa

kuingiza jina la shule au namba ya shule aliyohitimu elimu

ya kidato cha sita, mbele ya jina la shule yake ataona neno

lililoandikwa waliochaguliwa, akichagua neno hilo ataona

majina ya waliochaguliwa kujiunga na Mafunzo ya JKT kwa

Mujibu wa Sheria kwa mwaka 2026, ikionesha kambi

aliyopangiwa, Wilaya na Mkoa ilipo kambi hiyo.

Ili kuona majina yote ya Vijana na kambi walizopangiwa,

mtumiaji atapakua JKT PDF 2026 iliyopo juu kulia katika

ukurasa huo.

3

Mkuu wa JKT Meja Jenerali Rajabu Nduku Mabele,

anawakaribisha vijana wote waliohitimu kidato cha sita

nwaka 2026 ili waweze kujiunga n a vijana wenzao katika

kujengewa Uzalendo, kufundishwa Nidhamu, Ukakamavu,

Umoja wa kitaifa, Stadi za Kazi, Stadi za Maisha na utayari

wa kulijenga na kulitumikia Taifa.

Suncol Imetolewa na:

Kurugenzi ya Habari n a Uhusiano,

Makao Makuu ya JKT,






Baadhi ya Makamanda wa Jeshi hilo wakifatilia hafla hiyo





Wanahabari wakiwa katika hafla hiyo


 

Comments

Popular posts from this blog

WALIOPITA KURA ZA MAONI CCM HAWA HAPA

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

WAZIRI MKUU MAJALIWA ASHIRIKI IBADA YA KUSIMIKWA ASKOFU