Posts

Showing posts from September, 2025

DODOMA PRES CLABU YAWAFUNDA WAANDISHI WAKE KUHUSU UCHAGUZI MKUU 2025

Image
Mgombea ubunge jimbo la Mtumba, Anthony  Mavunde, akifungua kongamano la wanahabri mkoa wa Dodoma lililohusisha mada kuu uchaguzi mkuu na taratibu zake kwa wanahabari ambapo watoa mada walijikita kuwahabarisha wanahari kuhusu nini kinatakiwa kufanya wawapo kwenye mikutano ya kampeni ili wawe salama. Aidha  Mgombea Anthony Mavunde, amewataka waandishi wa habari kuhakikisha wanazingatia maadili na uhalisia katika kuripoti habari za uchaguzi ili kusaidia wananchi kufanya maamuzi sahihi. ‎ ‎ Mavunde aliyasema hayo wakati  akifungua Mafunzo ya waandishi wa Habari kuhusu masuala ya Uchaguzi na Usalama kwa waandishi wa habari mkoani Dodoma yaliyoandaliwa na Klabu ya  Waandishi wa Habari Mkoa wa Dodoma (DPC),  Mavunde amesema kuwa tasnia ya habari ni nguzo muhimu hasa kuelekea kipindi cha uchaguzi. ‎ ‎“Waandishi wa habari ni watu muhimu sana katika jamii. Taarifa isiyo sahihi inaweza kusababisha hata uvunjifu wa amani. Niwaombe tuendelee kuzingatia maadili, tusi...

UCSAF YAKAMILISHA MINARA 734, UJENZI WAFIKIA ASILIMIA 96.83.

Image
Ujenzi wa minara 758 ya mawasiliano unaosimamiwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) umefikia hatua kubwa ya mafanikio, ambapo minara 734 tayari imekamilika na inatoa huduma za mawasiliano kwa wananchi katika maeneo mbalimbali ya vijijini nchini. Hadi sasa utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 96.83, hali inayodhihirisha dhamira ya Serikali kupitia UCSAF kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma bora za mawasiliano, hususan wale wa maeneo ya vijijini na yenye changamoto za kijiografia. Minara iliyosalia ni 24 pekee, na inatarajiwa kukamilika hivi karibuni ili kuhakikisha huduma za mawasiliano zinafika katika maeneo yote yaliyopangwa. Mradi huu ni matokeo ya ushirikiano mzuri kati ya Serikali na kampuni za simu nchini kwa lengo la kufikisha huduma za mawasiliano vijijini, zikiwemo huduma za intaneti na simu ambazo zimekuwa changamoto katika maeneo yaliyokuwa hayana mtandao wa uhakika. Wananchi wa vijiji ambavyo minara imekamilika wameshaanza kunufaika na mawasiliano bora, hali...

MWENYEKITI WA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI YUPO IRINGA AKIKAGUA VIFAA VYA KUPIGIA KURA

Image
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akiangalia moja ya masanduku ya kupigia Kura wakati alipotembnelea ghala la vifaa vya Uchaguzi katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo  Mkoani Iringa jana. Jaji Mwambegele yupo mkoani humo kukagua maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani uliopangwa kufanyika Oktoba 29, 2025. (Picha na IN Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akiangalia taa ambazo hutumika wakati wa kuhesabu kura pindi kituo kikikosa umeme wakati wa Uchaguzi wakati alipotembnelea ghala la vifaa vya Uchaguzi katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Mkoani Iringa jana. Jaji Mwambegele yupo mkoani humo kukagua maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani uliopangwa kufanyika Oktoba 29, 2025. (Picha na INEC).