TAARIFA YA KATIBU MKUU WA WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO NA MSEMAJI MKUU WA SERIKALI NDUGU GERSON MSIGWA KUHUSU MASUALA MBALIMBALI YALIYOTEKELEZWA NA SERIKALI WAKATI WA MKUTANO NA WAANDISHI WA HABARI TAREHE 11 JUNI, 2025


Mkutano huu ni mwendelezo wa mikutano yangu ambayo nimeifanya katika maeneo mbalimbali nchini nikiwa nimeambatana na waandishi wa habari kuelezea utekelezaji wa shughuli za Serikali. Kama ambavyo nimekuwa nikieleza wakati wote, niliamua kuwa nafanya mikutano hii

katika maeneo inakotekelezwa miradi nikiwa nimeambatana na waandishi wa habari ili mpate fursa ya kufika na kuona uhalisia wa utekelezaji wa miradi Serikali.

Ndugu wanahabari, katika kuhakikisha wananchi wanaendelea kupata taarifa kuhusu utekelezaji wa shughuli za Serikali, Idara ya Habari, MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, tulianza kufanya mikutano ya Wakuu wa Taasisi na waandishi wa habari, ikafuata mikutano ya Mawaziri na sasa tunaandaa mikutano ya Wakuu wa Mikoa wote na Waandishi wa Habari itakayofanyika Jijini Dodoma kuanzia kuanzia mwezi huu ili kutoa fursa kwa Watanzania kuona utekelezaji wa miradi mbalimbali katika ngazi ya Mikoa. Mkutano wa leo tumeamua kuufanyia katika Mji wa Serikali Mtumba ili Watanzania kupitia vyombo vya habari waweze kuona maendeleo makubwa ya mradi wa ujenzi wa majengo ya Ofisi za Serikali ambao umeweka alama ya kudumu katika nchi yetu pia kuonesha kazi kubwa iliyofanywa na inayoendelea kufanywa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
5.
Ndugu wanahabari, Kipekee naomba nitumie fursa hii kwanza kumshukuru na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
3
Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa uongozi wake makini, mahiri na uliobeba maono na dhamira ya dhati ya kuwahudumia wananchi. Sote ni mashuhuda wa miradi mikubwa inayotekelezwa na inayoendelea kutekelezwa na Serikali kwa lengo la kuboresha huduma na kuwaletea maendeleo Watanzania. Aidha, naomba nitumie fursa hii pia kuwashukuru sana ninyi waandishi wa Habari kwa kuendelea kuunga mkono na kushiriki katika mikutano inayoandaliwa na Idara ya Habari, MAELEZO na Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali ambayo imekuwa ikifanyika katika maeneo mbalimbali nchini pia ile inayofanyika hapa Jijini Dodoma.
6.
Baada ya utangulizi huu, naomba nieleze kuwa katika mkutano wetu wa leo nitazungumzia masuala mbalimbali ya maendeleo yaliyotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita katika maeneo yafuatayo;-
i.
⁠Maendeleo ya ujenzi wa awamu ya pili ya mji wa Serikali, Mtumba – Dodoma,
ii.
Ujenzi wa barabara ya Igawa - Tunduma, barabara ya Songea - Makambako, mradi wa barabara za mzunguko Dodoma na miradi mingine mikubwa ya barabara Mikoa ya kusini.
iii.
Maendeleo na ufanisi wa Bandari ya Dar es salaam kutokana na uwekezaji wa kampuni ya DP World.
iv.
Uboreshaji wa miundombinu ya viwanja vya ndege Songwe, Iringa, Njombe, Mtwara, Msalato na Songea.
v.
Miradi ya kuimarisha na kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji katika jiji la Dodoma
4
vi.
Mradi wa kuunganisha mfumo wa Gridi ya Taifa ya Umeme yaTanzania na nchi za Kenya na Zambia.
SEKTA YA UJENZI
UJENZI WA MJI WA SERIKALI MTUMBA
7.
Ndugu wanahabari, Katika kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi na kuboresha mazingira ya kufanyia kazi kwa watumishi wa umma, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, inaendelea na Awamu ya Pili ya ujenzi wa majengo ya ofisi za Wizara na Taasisi katika Mji wa Serikali, Mtumba ambapo hadi sasa wastani wa ukamilishaji wa majengo umefikia asilimia 91 Aidha, kati ya majengo 34, majengo matano (5) ya Wizara na majengo matatu (3) ya taasisi yamekamilika yamekamilika.
Aidha, gharama zilizoidhinishwa kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya awamu ya pili ni shilingi bilioni 738.95 ambapo hadi kufikia sasa jumla ya shilingi bilioni 562.7 sawa na asilimia 74.8 zimetolewa kwa wakandarasi na washauri waelekezi.
HATUA ILIYOFIKIWA KATIKA UJENZI WA MAJENGO
a)
Wastani wa jumla wa ukamilishaji wa majengo ya awamu ya pili umefikia asilimia 91.0. Aidha, kati ya majengo 34, majengo
5
matano ya wizara na majengo matatu ya taasisi yamekamilika kwa asilimia 100.
b)
Majengo yaliyokamilika kwa upande wa wizara ni: Ofisi ya Rais - UTUMISHI, Wizara ya Maliasili na Utalii, Wizara ya Maji, Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
c)
Majengo yaliyokamilika kwa upande wa taasisi ni: Kituo cha Polisi, Ofisi ya Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini na Hoteli ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma.
d)
Majengo 16 ujenzi wake umefikia zaidi ya asilimia 90.
e)
Wizara na taasisi 22 zimekamilisha taratibu na kutoa zabuni kwa wakandarasi wa ndani ya nchi zenye jumla ya Shilingi Bilioni 66.7 na wizara 14 zimeanza kupokea samani.
f)
Jengo la Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (NGOME) litakalotumiwa na Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ujenzi wake umekamilika.
6
UJENZI WA JENGO LA OFISI YA SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR
Kwa upande wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imekabidhiwa kiwanja chenye ukubwa wa ekari 33 sawa na mita za mraba 121,698 kwa ajili ya ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Aidha, Wakala wa Majengo Zanzibar (ZBA) umekamilisha rasimu ya michoro ya jengo hilo lenye ukubwa wa ghorofa nne (4) na michoro imewasilishwa kwenye Mamlaka husika kwa ajili ya idhini.
ENEO KWA AJILI YA UJENZI WA BALOZI
Serikali imetenga jumla ya viwanja 75 kwa ajili ya Balozi na Mashirika ya Kimataifa katika Mji wa Serikali; Kati ya Viwanja hivyo, 71 ni kwa ajili ya Ofisi za Balozi na vinne (4) ni Mashirika ya Kimataifa; Aidha, Ofisi za Ubalozi wa Uganda, Ubalozi wa Burundi na Ubalozi wa Ethiopia zimeanza maandalizi ya ujenzi.
UJENZI WA MIUNDOMBINU
Serikali imekamilisha ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya kudumu katika Mji wa Serikali ikiwemo;-
1.
Ujenzi wa barabara za lami zenye urefu wa Kilomita 59.1 na kukamilisha upembuzi yakinifu wa barabara inayounganisha Mji wa Serikali na Ikulu yenye urefu wa kilometa 9.9,
7
2.
Kuendelea na ujenzi wa miundombinu ya kudumu ya umeme inayopita chini ya ardhi yenye urefu wa Kilomita 42 ya msongo wa kilovoti 33 ambao umefikia asilimia 59,
3.
Kukamilika kwa usambazaji na usimikaji wa miundombinu ya mtandao wa mawasiliano,
4.
Kwa upande wa huduma za maji mkandarasi amekabidhiwa kazi na ameanza ujenzi wa miundombinu ya maji taka na ujenzi wa mfumo nab wawa la kutibu majitaka katika eneo la Buigiri,
5.
Kuendelea na ufungaji wa mifumo ya kamera za usalama (CCTV) ambayo imefikia asilimia 55,
UJENZI WA UWANJA WA MASHUJAA
Awamu ya kwanza ya ujenzi wa Uwanja wa Mashujaa kwa ajili ya maadhimisho ya Siku ya Mashujaa imekamilika. Awamu hii ilihusisha ujenzi wa uwanja wa gwaride. Maandalizi ya ujenzi wa awamu ya pili utakaojumuisha majukwaa matatu (3) yenye uwezo wa kuchukua jumla ya watu 5000, jengo la mapokezi na eneo la maegesho ya magari yanaendelea.
8
UJENZI WA BARABARA YA IGAWA – SONGWE – TUNDUMA (TANZAM), BARABARA YA SONGEA - MAKAMBAKO, NA MIRADI MINGINE MIKUBWA YA BARABARA KUSINI.
8. Ndugu wanahabari, nchi yetu inaendelea kushuhudia mageuzi makubwa katika ujenzi wa miundombinu ya barabara. Chini ya uongozi mahiri wa Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, tumeshuhudia ujenzi wa barabara mpya, madaraja yanayounganisha Vijiji, Miji na Majiji. Sekta ya ujenzi imeendelea kuwa na umuhimu wa kipekee katika ukuaji wa uchumi wa nchi kutokana na kujenga na kukarabati miundombinu ya usafiri na usafirishaji ambayo imewezesha usafiri na usafirishaji wa haraka wa bidhaa mbalimbali kutoka na kuelekea maeneo ya uzalishaji.
9. Katika kipindi cha uongozi wa Awamu ya Sita tumeshuhudia kuongezeka kwa mtandao wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka kilometa 38,086.95 mwaka 2020 hadi kilometa 40,902.434 mwaka 2025 na mtandao wa barabara za changarawe kutoka kilometa 24,493 mwaka 2020 hadi kilometa 44,372.21 mwaka 2025. Aidha, katika sekta hii, Serikali inaendelea kujenga miradi mikubwa ya barabara katika maeneo mbalimbali nchini kama ifuatavyo; -
a)
UJENZI WA BARABARA YA IGAWA – SONGWE – TUNDUMA (MRADI WA TANZAM)
Barabara ya Igawa – Songwe - Tunduma yenye urefu wa kilometa 218.0 ni Barabara kuu inayounganisha Mikoa ya Njombe, Mbeya na Songwe pamoja na nchi jirani za Zambia, Malawi na Jamhuri ya
9
Kidemokrasia ya Kongo. Barabara hii ni muhimu katika shughuli za kiuchumi na kijamii kwa mikoa ya nyanda za juu kusini na ni kiungo muhimu cha Nchi zilizopo ukanda wa kusini mwa Afrika (SADC).
Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya njia nne (sehemu ya Tatu) kuanzia Nsalaga – Ifisi kwa kiwango cha lami yenye urefu wa kilometa 29.0 ni moja ya mikakati ya Serikali ya kuharakisha maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika jiji la Mbeya na maeneo jirani kwa kuboresha mtandao wa barabara ili kuongeza ufanisi katika sekta ya usafiri na usafirishaji.
Ujenzi wa Barabara hii unafadhiliwa kwa asilimia 100% na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Ujenzi chini ya Wakala ya barabara Tanzania (TANROADS).
Mkataba unatelekezwa na Mkandarasi China Henan International Cooperation Group Company Limited (CHICO) kwa gharama ya Shilingi Bilioni 138.7 (Shilingi 138,726,824,662.20 Bila VAT) na Msimamizi wa mradi huu ni kitengo cha usimamizi wa miradi cha TANROADS (TECU – Mbeya)
UTEKELEZAJI WA MRADI
Usanifu wa Barabara ya Igawa – Songwe – Tunduma; kipande cha tatu, Nsalaga – Ifisi (km 29.0) kwa kiwango cha lami, ulifanywa na kampuni ya M/s STUDI International ya kutoka nchini Tunisia ikishirikiana na
10
kampuni ya M/s G-PES Engineers ya hapa Tanzania ambapo mkataba wake ulisainiwa tarehe 18 Disemba 2018 kwa gharama ya Shilingi Bilioni 4.12. Kazi hiyo ya Usanifu ilikamilika mwezi Septemba, 2021.
Aidha, mkataba wa Ujenzi wa Barabara hii ulitiwa saini kati ya Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) kwa niaba ya Serikali na Mkandarasi M/s China Henan International Cooperation Group Co. Ltd (CHICO) kutoka China tarehe 14 Februari, 2023 na unatekelezwa kwa gharama ya shilingi Bilioni 138.7 kwa muda wa miezi 24.
KAZI ZINAZOENDELEA KWENYE MRADI NI; -
i.
Ujenzi wa mataba ya udongo ambayo ni G3, G7 na G15
ii.
Ujenzi wa makalvati madogo na Makalvati Makubwa (Box Culvert).
iii.
Ujenzi wa Daraja la Nzovwe
iv.
Uondoaji wa miundombinu mbalimbali (Umeme, Maji na Mawasiliano)
Kwa upande wa ajira mradi huu umefanikiwa kutoa jumla ya ajira 301 ambapo kati ya hizo, ajira 281, sawa na asilimia 93.4 zimetolewa kwa Watanzania kati ya hao, 36 ni wanawake sawa na asilimia 11.9.
b)
UJENZI WA BARABARA YA SONGEA KWA KIWANGO CHA LAMI
Mradi huu unahusisha ujenzi wa Kilomita 116 ambapo utahusisha kipande cha Songea – Lutukira Kilomita 100 pamoja na kipande cha
11
Songea bypass Kilomita 16. Upembuzi yakinifu, na Usanifu wa Kina wa awali ulifanywa na Mhandisi Mshauri BEOMAN Engineering and Architect Co. Ltd na kukamilika mwaka 2014.
Serikali imefanikiwa kupata ufadhili wa benki ya dunia kwa ajili ya kutekeleza ujenzi wa mradi huu. Hali kadhalika Serikali ilitangaza zabuni ya kutafuta mkandarasi tarehe 30 Novemba, 2023 na kufunguliwa 28 Februari, 2024. Hivi sasa hatua za kupitia zabuni zinaendelea. Mkandarasi anatarajiwa kuanza kazi muda wowote baada ya taratibu za manunuzi kukamilika.
Kwa upande wa fidia, Serikali kupitia Wizara ya Fedha imetoa fidia kwa wananchi kupisha mradi kiasi cha shilingi Milioni 646.9.
C). MRADI WA UJENZI WA BARABARA YA IRINGA (SAMORA –
MSEMBE KILOMETA 104 KWA KIWANGO CHA LAMI
Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Iringa – Msembe (km 104) ni moja ya Barabara za Mkoa inayotoka Samora Mkoani Iringa na Kuishia Hifadhi ya Taifa ya Ruaha (Msembe). Mkataba wa ujenzi wa barabara hii ulisainiwa Septemba 25, 2024 na kazi ya ujenzi ilianza Februari 21, 2025 Chini ya Mjenzi – CHINA HENAN INTERNATIONAL COOPERATION GROUP Co. Ltd kutoka China
Mradi huu ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuendeleza mtandao wa barabara na kusaidia maendeleo ya kiuchumi na kijamii kupitia matumizi ya barabara hii. Barabara hii itachochea shughuli za kiuchumi
12
Kama vile usafirishaji wa mazao ya chakula na biashara na shughuli za kijamii kwa ujumla.
Aidha barabara hii pia ni kiungo muhimu kwa shughuli za utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha.
Ujenzi wa barabara hii utafanyika kwa kutumia fedha za Mkopo kutoka Benki ya Dunia kupitia programu ya Tanzania Transport Integration Project (TanTIP) ambapo thamani ya awali ya mkataba wa ujenzi shilingi Bilioni 132.5 (Shilingi 132,506,398,404.84).
UTEKELEZAJI WA MRADI; Utekelezaji wa mradi huu unaendelea katika maeneo yafuatayo;-
a)
Kusafisha na kutoa udongo wa juu
b)
Uchimbaji wa kawaida (Common Excavation)
c)
Uchimbaji wa miamba (Rock Excavation)
d)
Kujaza tabaka la udongo lenye ubora wa G3
e)
Kuweka tabaka la udongo ulioboreshwa G7 / G15
f)
Tabaka la chini lililobadilishwa daraja C1
g)
Tabaka la msingi lililochanganywa na mawe ya kusagwa CRR
h)
Kumwaga lami nyepesi MC 70
i)
Kujenga Tabaka la lami na kokoto (DSD)
j)
Kujenga njia kwa ajili ya watembea kwa miguu na baiskeli (Walk ways)
k)
Kujaza Mawe/ miamba (Rock Fill)
13
l)
Kujenga Madaraja makubwa eneo la Kalenga, Nyamahana, na Tungamalenga, makalavati makubwa 49 na Makalavati madogo (pipe culvderts) 242 yenye vipenyo mbalimbali.
m)
Kujenga Mitaro ya Maji (side drains)
n)
Kufunga Taa za Barabarani Eneo la Mjini na katika vijiji vyote.
D). MRADI WA UJENZI WA BARABARA YA IRINGA (IPOGOLO) –
KILOLO KWA KIWANGO CHA LAMI KILOMETA 33.61.
Mradi huu wa barabara ya Iringa (Ipogolo) - Kilolo (33.61 km) ni sehemu ya barabara ya Mkoa inayotoka Ipogolo (Mzunguko wa barabara ya TANZAM) mkoani Iringa na kuishia mji wa Kilolo. Mradi huu ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuendeleza mtandao wa barabara na kusaidia maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Shughuli kuu za kiuchumi katika eneo hili ni kilimo, madini, utalii na uwindaji.
MAENDELEO YA UTEKELEZAJI WA MRADI
Mradi huu ulianza kutekelezwa na Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi kupitia (TANROADS) tarehe 21/02/2025 huku muda wa utekelezaji wa awali ukiwa miezi 24 ikijumuisha miezi 3 ya maandalizi ya kuanza kazi. Thamani ya awali ya mkataba wa ujenzi huu unaofanywa na mjenzi – CHINA HENAN INTERNATIONAL COOPERATION GROUP Co. Ltd kutoka China ni shilingi Bilioni 132.5.
Utekelezaji wa mradi hadi kufikia mwezi Mei ni asilimia 52.18 ambapo muda uliokwisha kutumika hadi sasa ni miezi 15 ambao ni sawa na
14
asilimia 62.50% ya utekelezaji wa mradi ikijumuisha pia muda maandalizi/mobilization. Muda uliobaki hadi sasa ni miezi 09 sawa na asilimia 37.50%
Aidha, utekelezaji wa mradi huu umezalisha jumla ya ajira 393, ambapo ajira 373 zimetolewa kwa wazawa sawa na asilimia 95% na ajira 20 pekee zilitolewa kwa wageni sawa na asilimia 5%
E). UJENZI WA BARABARAYA MNIVATA – NEWALA – MASASI KILOMETA 160 NA UJENZI WA DARAJA LA MWITI.
Barabara hii ni sehemu ya ushoroba wa Mtwara unaoanzia Mtwara kupitia Masasi, Tunduru, Songea mpaka Mbamba bay wenye urefu wa kilometa 845 inayounganisha bandari ya Mtwara na ile ya Mbamba bay na pia inaunganisha Tanzania na Malawi.
Kukamilika kwa ujenzi wa barabara hii ambayo pia hujulikana kama barabara ya Uchumi kutokana na kupita maeneo yenye uzalishaji mkubwa wa korosho kutachochea zaidi ukuaji wa uchumi ikiwa ni pamoja na kupunguza gharama na muda wa usafiri, urahisishaji wa kufanya biashara na kuwezesha wananchi kuchangamana kwa urahisi, kuwa kiungo kizuri kati ya Bandari za Dar es Salaam na Mbamba bay.
Mradi unafadhiliwa kwa pamoja kati ya Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo Benki ya Maendekleo ya Afrika imetoa mkopo wa Dola za Marekani Milioni 116.34 sawa na shilingi za Tanzania Bilioni 267.42 na Serikali
15
ya Tanzania inachangia jumla ya Dola za Marekani Millioni 1.52 sawa na shilingi za Tanzania Bilioni 3.49.
ZIFUATAZO NI KAZI ZITAKAZOFANYIKA KATIKA MRADI HUU
i.
Ujenzi wa Barabaraya Mnivata –Masasi (km 160) kwa kiwango Cha lami yenye teknolojia mpya ya Superpave SP 12.5
ii.
Ujenzi wa Daraja la Mwiti (mita 84)
iii.
Ujenzi wa Mizani ya kisasa Kudhibiti Uzito wa Magari eneo la Ng’ongolo (Tandahimba) na Mpeta (Masasi)
iv.
Maboresho ya miteremko na kona kali za Nanyamba na Namaleche
v.
Uwekaji wa taa za usalama barabarani 4,587
vi.
Ujenzi wa Maegesho ya Magari Makubwa Tandahimba.
vii.
Ujenzi wa Miradi Jumuishi katika Halmashauri zote zinazopitiwa na mradi
F). UKARABATI WA BARABARAYA MTWARA - MINGOYO –
MASASI - KILOMETA 201.
Barabara ya Mtwara – Mingoyo – Masasi yenye urefu wa kilomita 201 inapita katika mikoa ya Mtwara na Lindi. Kati ya kilomita hizo, takribani kilomita 110.51 ziko ndani ya Mkoa wa Mtwara na kilomita 90 ziko katika Mkoa wa Lindi.
Barabara hii ni ya kimkakati na kiuchumi, kwani inapita katika maeneo yenye uzalishaji mkubwa wa mazao ya biashara hususan korosho na ufuta katika Mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma. Vilevile, barabara hii ni njia kuu ya kusafirishia makaa ya mawe kutoka Songea hadi Bandari ya Mtwara, hivyo kuchochea shughuli za kiuchumi na biashara ndani na nje ya nchi.
16
Barabara hii zaidi ya kuwa kiungo cha usafirishaji wa bidhaa, barabara hii ni sehemu ya Ukanda wa Maendeleo wa Mtwara (Mtwara Development Corridor) unaounganisha Bandari ya Mtwara na Bandari ya Mbamba Bay katika Ziwa Nyasa, Mkoa wa Ruvuma. Barabara hii inarahisisha usafirishaji wa mizigo, kukuza uchumi wa kanda, na kuimarisha uhusiano wa kibiashara kati ya Tanzania, Jamhuri ya Malawi na nchi nyingine jirani
G). UJENZI WA BARABARA YA MZUNGUKO WA NJE KATIKA JIJI LA
DODOMA
Serikali inaendelea na ujenzi wa Barabara ya Mzunguko wa Nje (Outer Ring Road) katika jiji la Dodoma kwa kiwango cha lami yenye urefu wa kilometa 112 ambapo Sehemu ya Kwanza ya Nala – Veyula – Mtumba – Ihumwa Bandari Kavu (km 52.3) ujenzi wake umefikia asilimia 86, na Sehemu ya Pili ya Ihumwa Bandari Kavu – Matumbulu – Nala (km 60) ujenzi wake umefikia asilimia 85.
SEKTA YA UCHUKUZI
UTENDAJI WA BANDARI YA DAR ES SALAAM
8.
Ndugu wanahabari, Kama mnavyohamu Oktoba 22, 2023, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirkiana na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) ilisaini mikataba mitatu ya uwekezaji na Kampuni ya DP World MEA FZE ya Falme ya Dubai
17
(Mkataba wa Nchi Mwenyeji, Mkataba wa Upangishaji na Mkataba wa Uendeshaji) ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuifanya bandari ya Dar es salaam kuendelea kuwa shindani kikanda na kimataifa pia kuiwezesha bandari ya Dar es Salaam kutoa huduma kwa ufanisi wa hali ya juu.
FAIDA ZA UWEKEZAJI WA KAMPUNI YA DP WORLD KATIKA BANDARI YA DAR ES SALAAM
1.
Katika kipindi kinachoanzia mwezi Januari hadi Desemba 2024, Kampuni ya DP World imefanya uwekezaji wa awali katika maeneo mbalimbali ya uendeshaji ili kuboresha na kuongeza ufanisi wa huduma za bandari suala kiasi cha shilingi Bilioni 214.42.
2.
Usimikaji wa Mitambo Nane (8) aina ya “Rubber Tyred Gantry Crane” Mitambo hiyo iligharimu kiasi cha Shilingi za Tanzania Bilioni 96. Mitambo hiyo ni mahsusi kwa ajili ya kuhudumia shehena ya makasha kwa ufanisi na kasi kubwa zaidi. Kabla ya uwekezaji huu TPA ilikua na mitambo miwili (2) tu wakati ambapo mahitaji yalikuwa ni mitambo isiyopungua 10.
3.
Ununuzi wa Mitambo Miwili (2) aina ya “Ship to Shore Gantry Cranes”, Mitambo hii mipya kwa ajili ya kutumika katika Kitengo Na. 1 cha Makasha cha Bandari ya Dar es Salaam ina thamani ya shilingi za Bilioni 115.
18
4.
Ununuzi wa “Terminal Tractors”, “Trailers” na “Generators” Kampuni ya DP World imefanya uwekezaji kununua mitambo mingine mbalimbali ikiwemo “terminal tractors” ishirini (20) ambazo hutumika katika kuhamisha na kusafirisha shehena kutoka eneo moja la bandari kwenda eneo jingine na “trailers” thelathini na moja (31) ambazo hutumika katika kubeba shehena za aina mbalimbali. Sambamba na uwekezaji huo, jumla ya “Generators” kubwa saba (7). Uwekezaji huu kwa pamoja umegharimu kiasi cha jumla ya Shilingi za Tanzania Bilioni 13.32.
5.
Usanifu wa Mifumo ya TEHAMA, Kampuni ya DP World inaendelea na kazi ya kusanifu mfumo wa kisasa wa TEHAMA wa kuhudumia shehena. Mfumo huu ni mahsusi kwa kutoa huduma za uendeshaji wa Page 9 of 21 bandari. Sehemu ya kwanza ya kazi ya usanifu wa mfumo huu imekamilika na kwa sasa umeanza kutumiwa na wateja pamoja wadau wanaopatiwa huduma na DP World. Aidha, Jumla ya Shilingi za Tanzania Bilioni 3.6 zinatarajiwa kutumika kama gharama za uwekezaji katika eneo hili.
6.
Ununuzi wa Mitambo Zaidi ya Kisasa na Uendelezaji wa Miundombinu, Katika cha mwaka 2025, Kampuni ya DP World imeanza utekelezaji wa awamu ya pili ya mpango wa uwekezaji utakaogharimu zaidi ya Shilingi za Tanzania Bilioni 104. Mpango huo unahusisha manunuzi ya mitambo mingine
19
miwili mitambo miwili (2) aina ya “Ship to Shore Gantry Cranes-SSG”, ujenzi wa milango mipya bandari inayotumika kuingiza na kuondosha shehena mbalimbali bandarini na maboresho ya maeneo ya kuhifadhi na kuhudumia shehena bandarini.
7.
Kuongezeka kwa shehena ya Jumla (mchanganyiko) katika Bandari ya Dar es Salaam, Katika kipindi cha miezi kumi na moja kwa mwaka 2024/2025 shehena/mizigo imeongezeka kwa asilimia 11, ambapo Bandari ya Dar es Salaam imehudumia mizigo tani milioni 23.9 kulinganisha na tani milioni 21.5 za miezi 11 ya mwaka 2023/2024.
8.
Kuongezeka kwa Shehena ya Makasha (TEUs) Idadi ya makasha iliyohudumiwa na waendeshaji binafsi katika kipindi cha mwaka 2024/25 imefikia makasha ya futi ishirini (TEUs) 1,159,387 sawa na ongezeko la asilimia 28 ikilinganishwa na makasha (TEUs) 904,424 yaliyohudumiwa katika kipindi kama hiki mwaka uliopita (2023/24)
9.
Mapato kwa ujumla yameongezeka kutoka shilingi trilioni 1.1 mpaka trilioni 1.5. Aidha, faida imeongezeka kutoka shilingi bilioni 49 sawa na asilimia 4 hadi shilingi bilioni 329 ambazo ni sawa na ongezeko la asilimia 36.
20
10.
Kuongezeka kwa mapato ya kodi yanayokusanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kazi za Bandari kutoka shilingi trilioni 7 hadi shilingi trilioni 8 na matumizi yameshuka kwa asilimia 46 kutoka trilioni 1.1 hadi Bilioni 597.
11.
Kupungua kwa Muda wa Meli Kusubiri Nangani;- Muda wa meli kuhudumiwa bandarini unaojumuisha muda wa kusubiri nangani umepungua katika Bandari ya Dar es Salaam kutoka wastani wa siku 30 mwaka 2023/24 hadi kufikia wastani wa siku 6 mwaka 2024/25 kwa meli za makasha. Kwa sasa, meli za makasha zinazohudumiwa na DP World hazisubiri nangani na uhudumiwa moja kwa moja gatini pindi zinapowasili kwa muda wa wastani wa siku 4.
12.
Ajira kwa Watanzania, Hadi kufikia mwezi Machi 2025, jumla ya wafanyakazi 764 wamepata ajira za moja kwa moja katika Kampuni ya DP World na TEAGTL katika fani mbalimbali wakiwemo maafisa wa idara mbalimbali, makarani wa shughuli za uendeshaji, waendesha mitambo mikubwa na midogo pamoja na askari. Sambamba na ajira hizo za moja kwa moja, Kampuni ya DP World na TEAGTL zimetengeneza pia ajira nyingine zisizo za moja kwa moja kufuatia ongezeko la shehena mchanganyiko. Ajira hizi zinajumuisha wafanyakazi wa kutwa, madereva wa malori, mawakala wa forodha n.k
21
13.
Baadhi ya makampuni ya meli yameanza kupunguza gharama za usafirishaji wa shehena kwa njia ya maji, hii kufuatia kuondoshwa kwa muda wa kusubiri nangani kwa meli za makasha. Kwa mfano, Kampuni ya Mediterranean Shipping Company-MSC imeondoa kiasi cha Dola za Marekani (USD) 1000 kwa kasha ambacho kilikuwa kikitozwa kama tozo ya ziada kwa mteja kwa sababu ya ucheleweshaji wa uhudumiaji wa makasha katika Bandari ya Dar es Salaam. Kuondolewa kwa tozo hii kumetoa nafuu kwa watumiaji wa bandari katika usafirishaji wa shehena kupitia bandari.
UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA VIWANJA VYA NDEGE
9.
Ndugu wanahabari, Sekta ya uchukuzi imeendelea kuwa kiungo muhimu katika kuchangia ukuaji wa uchumi wa nchi kutokana na uendelezaji wa miradi ya kimkakati na uboreshaji wa miundombinu na huduma za uchukuzi. Utekelezaji wa miradi mbalimbali katika sekta hii umerahisisha usafirishaji wa watu na mizigo na hivyo kusaidia kupunguza gharama za uzalishaji na kuongeza fursa za ajira. Mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na: -
a)
UKARABATI NA UJENZI WA KIWANJA CHA NDEGE SONGEA
Ukarabati wa kiwanja hiki cha ndege ulianza 29 Aprili 2019 ukitekelezwa na mkandarasi China Henan International Cooperation Group Co. Ltd (CHICO). Shughuli za ukarabati wa uwanja huu zilihusisha;-
22
I.
Kuongeza upana wa uwanja kutoka mita 23 hadi mita 30
II.
Kujenga upya matabaka ya barabara ya kurukia ndege kiwango cha zege ya lami unene wa 100mm.
III.
Kuongeza urefu wa barabara ya ndege kutoa mita 1,625 hadi mita 2,840.
IV.
Kujenga eneo jipya la maegesho ya ndege (Apron) lenye upana wa mita 126 na urefu wa mita 139 linaloweza kutosha kuengesha ndege 5.
V.
Kujenga barabara ya kuunganisha uwanja wa ndege nae neo la maegesho la ndege (taxiway) lenye urefu wa mita 75 na upana wa mita 25
VI.
Kujenga na kuimarisha maeneo ya usalama kiwanjani (runway strips) zenye upana wa mita 60 kila upande.
VII.
Kujenga eneo la maegesho ya dharura
VIII.
Kujenga mnara, kuweka taa na kupaka rangi za kuongozea ndege na vifaa vyake vya mawasiliano
IX.
Pamoja na kazi zingine kama vile mifereji, mifumo ya umeme, gari la zima moto, uzio na
Mradi huu umekamilika kwa gharama ya shilingi Bilioni 38.139 Mhandisi mshauri wa mradi alikuwa ni kampuni ya Atkins Tanzania Ltd kwa kushirikiana na Howard Humphreys na Advanced Engineering Solutions Limited. Mradi umekamilika tarehe 30 Machi 2023 kwa gharama ya shilingi Bilioni 40.87.
23
b). UKARABATI NA UPANUZI WA UWANJA WA NDEGE WA IRINGA
Uwanja wa ndege wa Iringa ni moja kati ya viwanja 16 vilivyoainishwa katika mpango wa maendeleo wa kitaifa wa miaka 15 ambao ulizinduliwa mwaka 2011 na ukaratibiwa kuanza kutekelezwa kupitia programu ya pili ya uboreshaji wa sekta ya usafirishaji. Uwanja huu unaunganisha Mkoa wa Iringa na Mikoa mingine nchini hivyo kurahisisha shughuli za kiuchumi na kibiashara. Kutokana na Usanifu uliofanyika kazi zilizopangwa kufanyika ni : -
i.
Ukarabati na Upanuzi wa Barabara ya kutua na kurukia ndege (Runway) yenye urefu wa mita 2100 na upana wa mita 30 kwa kiwango cha lami,
ii.
Ujenzi wa Barabara ya kiungio (Taxiway) yenye urefu wa mita 155 na upana wa mita 23 kwa kiwango cha lami,
iii.
Ujenzi wa eneo la Maegesho ya Ndege (Apron) yenye urefu wa mita 180 na upana wa mita 126 kwa kiwango cha lami,
iv.
Ujenzi wa Kituo cha Huduma za Zimamoto pamoja na Ununuzi wa Gari la Zimamoto,
v.
Ununuzi na usimikaji wa mifumo ya kuongozea ndege,
vi.
Ujenzi wa kituo cha umeme na ununuzi wa jenereta 400kVA,
vii.
Ujenzi wa Uzio wa Usalama wenye urefu wa kilomita 10,
viii.
Ujenzi wa Maeneo ya usalama kwenye barabara ya kutua na kurukia ndege,
ix.
Ujenzi wa Mifereji ya kuondoa maji ya mvua uwanjani
24
x.
Ujenzi wa Jengo la waongoza ndege pamoja na mitambo ya kuongozea Ndege,
xi.
Uwekaji wa alama za usalama uwanjani
xii.
Ujenzi wa Jengo la abria muda
MAENDELEO YA UJENZI
Hadi sasa sasa mradi huu umefikia asilimia 93%. Aidha, tarehe 31/08/2024, Wakala ya Barabara (TANROADS), Mkoa wa Iringa ilikabidhi rasmi mradi huu kwa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kwa ajili ya matumizi baada ya kukamilika kwake. Kwa sasa Mradi upo kwenye kipindi cha maangalizi.
KAZI ZINAZOFANYIKA SASA NA MAENDELEO YAKE:
i.
Ujenzi wa barabara ya kutua na kurukia ndege, asilimia 100.
ii.
Ujenzi wa barabara ya kiungio – asilimia 100.
iii.
Ujenzi wa eneo la maegesho ya ndege- asilimia 100.
iv.
Ujenzi wa Kituo cha huduma za zimamoto na Gari la zimamoto - asilimia 97.
v.
Mifumo ya kuongozea ndege kama - asilimia 30.
vi.
Ujenzi wa kituo cha umeme - asilimia 97.
vii.
Ununuzi wa jenereta 400kVA – asilimia 100.
viii.
Ujenzi wa Uzio wa usalama - asilimia 100.
ix.
Ujenzi wa maeneo ya usalama kwenye barabara ya kutua na kuruka ndege – asilimia 100.
25
x.
Kuweka taa za ardhini kwenye njia za kutua na kuruka ndege – asilimia 100
xi.
Ujenzi wa mifereji ya kuondoa maji ya mvua kiwanjani- asilimia 100
xii.
Uwekaji wa Alama za Usalama Kiwanjani - asilimia 100
xiii.
Ujenzi wa jengo la abria muda - asilimia 100
1.
UJENZI WA JENGO LA ABIRIA LA UWANJA WA NGEGE IRINGA
Mradi huu unafadhiliwa na Benki ya Dunia chini ya Programu ya TanTIP. Kazi hii inahusisha ujenzi wa jengo la abiria la kiwanja cha ndege cha Iringa lenye ukubwa wa ghorofa moja ambalo linauwezo wa kuhudumia abiria 250,000 kwa mwaka na abiria 150 kwa wakati mmoja. Aidha, Serikali iliingia Mkataba wa ujenzi wa jengo la abiria wenye gharama ya shilingi Bilioni 41 na Mkandarasi China Harbour Engineering Company Ltd tarehe 23/12/2024.
Mradi huu unatarajiwa kukamilika katika kipindi cha miezi 18. Pia jengo hili la abiria litakuwa na sehemu ya Mnara wa kuongozea ndege na barabara za ndani (Access roads)
c)
UJENZI WA UWANJA WA NDEGE WA MTWARA
Ujenzi na ukarabati wa uwanja wa Mtwara umeshakamilika na kupokelewa tarehe 14 April, 2023. Mkandarasi aliyetekeleza kazi hii ni M/S Beijing Construction Engineering Group Company Ltd ya China kwa gharama ya Bilioni 56.7 (Shilingi 56,710,778,701.59).
26
d). UJENZI WA UWANJA WA NDEGE KIMATAIFA MSALATO,
DODOMA
Kuendelea na ujenzi wa Kiwanja cha Kimataifa cha Ndege cha Msalato – Dodoma ambapo utekelezaji wake umefikia asilimia 87 ukiwa umegawanyika katika sehemu mbili. Sehemu ya kwanza inayohusisha ujenzi wa barabara ya kuruka na kutua Ndege (runway), Barabara za maungio (Taxiways), Maegesho ya Ndege (Aprons), Uzio wa usalama, Barabara ya kuingia na kutoka Kiwanjani, Maegesho ya Magari na Usimikaji wa Taa za kuongozea Ndege ambapo utekelezaji.
Awamu ya pili inayohusisha Jengo la Abiria, mnara wa kuongozea Ndege na majengo mengine ujenzi wake umefikia asilimia 53.2.
SEKTA YA MAJI
MIRADI YA KUIMARISHA UPATIKANAJI WA MAJI NA KUONDOA CHANGAMOTO YA MAJI KATIKA JIJI LA DODOMA
10.
Ndugu wanahabari, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kusimamia rasilimali za maji kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa kutekeleza mikakati na programu mbalimbali ambapo kwa upande wa Jiji la Dodoma,
27
Serikali kupitia Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) imeendelea kutekeleza mikakati ya muda mfupi, wa kati na muda mrefu kuhakikisha inaboresha huduma ya majisafi na usafi wa mazingira katika maeneo yote ya kihuduma ndani ya Jiji la Dodoma na Miji ya Bahi, Chamwino, Kongwa na mji mdogo wa Kibaigwa.
HALI YA SASA YA MAHITAJI NA UZALISHAJI WA MAJISAFI
KATIKA JIJI LA DODOMA.
1.
JIJI LA DODOMA - Mahitaji ni lita milioni 149 kwa siku wakati uzalishaji kwa sasa ni lita milioni 88.7 kwa siku.
2.
BAHI - mahitaji ni milioni 1.02 kwa siku wakati uzalishaji ni lita 990,000 kwa siku
3.
CHAMWINO - mahitaji ni lita milioni 7.5 wakati uzalishaji ni lita milioni 4.6 kwa siku.
4.
KONGWA – mahitaji ni lita milioni 2.9 wakati uazilishaji ni milioni 2.4 kwa siku.
5.
KIBAIGWA - mahitaji ni lita milioni 3.0 wakati uzalishaji ni lita milioni 2.7 kwa siku.
MIRADI YA MAJI INAYOHUDUMIA WANANCHI KATIKA JIJI LA DODOMA.
Serikali imekuwa ikitekeleza ujenzi wa miradi mbalimbali ya maji na kukamilisha ile iliyo katika hatua za ujenzi katika Jiji la Dodoma ili
28
kutoa huduma kwa wananchi. Katika eneo hili, Serikali imekamilisha ujenzi wa miradi 14 ya maji kwa asilimia 100 na tayari imeishaanza kutoa huduma kwa wananchi. Miradi hii ina Jumla ya thamani ya shilingi Bilioni 13. Utekelezaji wa miradi hii umeongeza uzalishaji kutoka lita milioni 68 hadi 81 kwa siku ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 20. Orodha ya miradi hii ni kama ifuatavyo; -
1.
Mradi wa Maji wa Ihumwa – Njedengwa – Mradi huu umekamilika kwa asilimia 100 kwa gharama ya shilingi Bilioni 2.95 ukiwanufaisha wananchi 22,954 wa maeneo ya Iyumbu, Njedengwa, Mwangaza na Nyumba 300 Jijini Dodoma.
2.
Mradi wa Kuchimba Visima Vikubwa Mzakwe, Mradi huu umekamilika kwa asilimia 100 ukiwanufaisha wakazi takribani Laki Tano (5) Ujenzi umehusisha uchimbaji wa visima vitatu (3), Kusimika pampu na kufunga mifumo ya umeme. Gharama za mradi ni shilingi Milioni 957)
3.
Mradi wa Kuboresha huduma ya maji kwa kusogeza mtandao eneo la St. Gemma. Mradi huu umekamilika kwa asilimia 100 ukihudumia wananchi 3,371. Gharama za mradi ni shilingi milioni 79.
4.
Mradi wa maji safi wa Ndachi Mnadani. Mradi huu unawanufaisha wananchi 11,320 wa maeneo ya Ndachi na Mtaa
29
wa Mnadani. Mradi huu umekamilika kwa asilimia 100 kwa gharama ya shilingi Milioni 235.7.
5.
Mradi wa majisafi Nala - ITRACOM; Mradi huu pia umekamilika kwa gharama ya shilingi milioni 509.6 ikiwa ni gharama za Kuchimba Visima viwili (2), kulaza bomba urefu wa kilomita 7 na kujenga DPs 3.
6.
Mradi wa kuchimba Kisima kirefu (300m) Nzuguni, Mradi huu unagharimu kiasi cha shilingi milioni 570.4 na umekamilika kwa asilimia 95 ukihudumia wananchi 25,000 wa Dodoma Mjini.
7.
Mradi wa Ujenzi na Uboreshaji wa Mtandao wa Majisafi Nzuguni- Awamu I; Mradi huu una thamani ya shilingi Bilioni 4.39. Mradi huu umekamilika kwa asilimia 98 na utawanufaisha wananchi 75,968 wa eneo la Nzuguni na baadhi ya maeneo jirani ya Ilazo.
8.
Mradi wa majisafi Njedengwa-NHC-UDOM, Mradi huu umekamilika kwa asilimia 100 kwa gharama ya shilingi Milioni 291 ambapo utahudumia wakazi 20,000 ambao ni Wanafunzi wa Chuo Kikuu Dodoma (UDOM) na wakazi wa NHC Iyumbu.
9.
Mradi wa Maji Nala, Mradi huu umegharimu kiasi cha shilingi Bilioni 1.38. Aidha, ujenzi wake umekamilika kwa asilimia 85 na
30
utahudumia wananchi 14,731 wa maeneo ya Nala Centre, Segu Juu, Chihoni na kiwanda cha Mbolea cha INTRACOM.
10.
Mradi wa Maji wa Kisima cha Mahungu, Mradi huu umekamilika kwa asilimia 100 kwa gharama ya shilingi Milioni 115 na unawanufaisha wananchi wa Mahungu block B E, F, G, H.
11.
Mradi wa Maji wa Kisima cha Makulu Ostabay; Mradi huu umekamilika kwa asilimia 100 kwa gharama ya shilingi milioni 56.9. Mradi huu unahudumia Mtaa wa Mkalulu Ostabay.
12.
Mradi wa Maji Kisima cha Kisasa-Nyumba 300, Mradi huu wa maji umegharimu kiasi cha shilingi Milioni 42.4 unahudumia wakazi wa Kisasa, Nyumba 300 na Mwangaza
13.
Mradi wa Maji wa Kisima cha Mkonze – Muungano;- Mradi huu umegaharimu shilingi Milioni 150. Maeneo yanayonufaika na mradi huu ni Mkonze na eneo lote la Kata ya Muungano.
14.
Miradi ya maji yenye lengo la kupambana na UVIKO -19.
Mradi huu umekamilika kwa asilimia 100 kwa gharama ya shilingi Bilioni 1.25 ukiwanufaisha wananchi 40,759 maeneo ya Ntyuka mtaa wa Chimalaa na sehemu ya mtaa wa Nyerere, Bahi sokoni na Vijiji 12 (Hombolo Makulu, Nala, Mpunguzi A,
31
Mpunguzi B,Chololo, Ihumwa, Chihikwi, Kitelela, Matumbulu, Ipala, Zepisa na Ntyuka).
MIRADI INAYOENDELEA KUJENGWA KUPUNGUZA CHANGAMOTO YA MAJI KATIKA JIJI LA DODOMA.
Serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuendelea kupunguza changamoto ya Maji katika Jiji la Dodoma ambapo kukamilika kwake kutaongeza uzalishaji wa maji kutoka lita Mil. 81 hadi 121 kwa siku. Miradi hii ina Jumla ya thamani ya shilingi Bilioni 62.84. Miradi hii ni kama ifuatavyo; -
1.
Mradi wa uchimbaji Visima Nzuguni Awamu ya Pili – Mradi huu utahudumia wananchi 100,000 upo asilimia 80 na unajengwa kwa gharama ya shilingi Milioni 220.
2.
Mradi wa kusogeza na kuboresha huduma Dodoma Mjini na Chamwino;- Mradi huu umefikia asilimia 60 na unajengwa kwa gharama ya shilingi Bilioni 4.18.
3.
Mradi wa majisafi wa DTC at Nala – Mradi huu utahudumia wananchi 15,000. Ujenzi wake umefikia asilimia 20 na unajengwa kwa gharama ya shilingi milioni 425.
4.
Mradi wa Ujenzi na Uboreshaji wa Mtandao wa Majisafi Nzuguni- Awamu II – Mradi huu una thamani ya shilingi
32
Bilioni 4.77 ukihudumia wakazi 123,095 wa maeneo ya Nzunguni, Ilazo, Swawa, Ipagala, Kisasa.
5.
Mradi wa Majisafi Zuzu-Nala – Ujenzi wa mradi huu umefikia asilimia 10, unajengwa kwa gaharama ya shilingi Bilioni 13.64. Matarajio ni kuhudumia wananchi 38,096 wa Kata za Nala, Zuzu, na eneo la Viwanda, Mkonze, Michese, Miganga.
6.
Ujenzi wa Mtandao wa majisafi Mji wa Serikali –Mtumba; -
Mradi huu umefikia asilimia 5 unajengwa kwa gharama ya
shilingi 35.6. Utakapokamilika utahudumia Mji wa Kiserikali na maeneo Jirani.
7.
Utafiti na Uchimbaji wa visima katika maeneo mbalimbali ya Dodoma Mkonze, Mzakwe, Zuzu, Nkuhungu, Miganga, Nzuguni, Ihumwa, Michese, Mahomanyika, Kisasa, Mahungu;- Mradi huu una thamani ya shilingi Bilioni 3, utekelezaji wake umefikia asilimia 5. Mradi huu utawanufaisha wananchi wa Jiji la Dodoma 184,642.
MIRADI YA MAJITAKA INAYOTEKELEZWA JIJI LA DODOMA
Serikali inaendelea kukabiliana na changamoto ya Majitaka katika Jiji la Dodoma kwa kutekeleza miradi mbalimbali yenye thamani ya shilingi Bilioni 248.7. Kukamilika kwa miradi hii
33
kutaongeza huduma ya majitaka kutoka 20% hadi 40%. Miradi hiyo ni kama ifuatavyo; -
1.
Mradi wa ukarabati wa mtandao wa majitaka katika maeneo ya Area C na Area D awamu ya kwanza
2.
Ujenzi wa bomba kubwa la majitaka Swaswa kata ya Ipagala
3.
Ujenzi wa Mtandao wa Majitaka (Sub-trunk Sewer and Reticulation Sewerage) katika Mji wa Magufuli-LOT 1
4.
Ujenzi wa Mabwawa ya kuhifadhi na Kutibu Majitaka (Trunk Sewer and Waste Stabilization Ponds) katika eneo la Buigiri Chamwino-kwa ajili ya mji wa Magufuli-LOT 2
5.
Ujenzi na Ukarabati wa mfumo wa majitaka katika Jiji la Dodoma kwenye kata 21.
HATUA ZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA FARKWA NA ZIWA
VICTORIA
Miradi hii ni mikakati ya muda wa kati na mrefu ya kutatua changamoto ya upungufu wa majisafi katika jiji la Dodoma. Hatua zake za utekelezaji ni kama ifuatavyo: -
1.
MRADI WA BWAWA LA FARKWA – Mradi huu unajengwa kwa gharama ya shilingi Bilioni 309.46 ukitarajia kuhudumia wananchi Milioni mbili (2) wa Wilaya za Dodoma Mjini, Chemba, Bahi na Chamwino. Mradi huu
34
katika awamu ya kwanza upo katika hatua za Manunuzi ya Mkandarasi wa Ujenzi wa Bwawa na Usanifu wa Mtandao wa Kusafirisha Maji kutoka Bwawani kwenda Dodoma mjini, Bahi na Chamwino na unategemewa kukamilika mwaka 2028.
Awamu ya pili ya mradi huu itahusisha ujenzi wa Mtadao wa Bomba kuu kutoka Bwawani kwenda Dodoma Mjini, Bahi na Chamwino ipo katika hatua za mwisho za upatikanaji wa fedha kutoka Benki ya Maendeleo Afrika na Awamu ya Tatu itahusisha Ujenzi wa Mtandao wa Majisafi na Usafi wa Mazingira itatekelezwa baadae baada ya upatikaji wa fedha.
2.
MRADI WA ZIWA VICTORIA - Mradi huu upo katika hatua za usanifu na ambapo gharama za mradi zitajulikana na baada kukamilika kwa kazi ya usanifu ambayo kwa sasa imefikia asilimia 60. Usanifu wa mradi huu unategemewa kukamilika ndani ya mwaka huu 2025. Mradi huu utakapokamilika utawahudumia wananchi wa Mikoa ya Dodoma na Singida.
35
SEKTA YA NISHATI
MRADI WA KUUNGANISHA MFUMO WS GRIDI YA TAIFA YA UMEME YA TANZAANIA NA NCHI JIRANI ZA KENYA NA ZAMBIA
11.
Ndugu wanahabari , Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) imekuwa ikitekeleza miradi mikubwa ya kimkakati ya nishati ili kuhakikisha kuwa nchi inakuwa na mfumo wa kisasa, wa uhakika na wa kuaminika wa usambazaji wa umeme. Katika jitihada hizo, Serikali imeanzisha miradi ya kuunganisha Gridi ya Taifa na gridi za nchi jirani kama vile Kenya na Zambia. Lengo kuu la miradi hii ni kuongeza uwezo wa biashara ya umeme baina ya nchi wanachama wa mashirika ya kikanda ya nishati, yaani Eastern Africa Power Pool (EAPP) na Southern Africa Power Pool (SAPP), sambamba na kuongeza usalama wa nishati kwa taifa na kikanda.
Mradi wa Kenya - Tanzania Power Interconnection Project (KTPIP)
Mradi wa KTPIP ni mojawapo ya miradi ya kimkakati inayolenga kuunganisha mfumo wa Gridi ya umeme wa Tanzania na ule wa Kenya, ambapo Kenya tayari imeunganishwa na Ethiopia. Kupitia mradi huu, Tanzania ina nafasi ya kupokea au kuuza umeme wa bei nafuu kwa nchi jirani kwa njia ya gridi ya pamoja ya kikanda. Hii ni hatua muhimu kuelekea kufanikisha biashara ya nishati kati ya mataifa ya Afrika Mashariki na baadaye Afrika Kusini kupitia SAPP.
36
Mradi huu ulianza kutekelezwa mwaka 2017 na umekamilika mwaka 2024 kwa asilimia 100. Ujenzi wake ulijumuisha njia ya umeme yenye urefu wa kilomita 414 kutoka Singida hadi Namanga yenye uwezo wa msongo wa kilovoti 400, pamoja na kituo cha kupoza na kukuza umeme cha Lemugur kilichopo Arusha chenye uwezo kilovoti 400.
MAFANIKIO YA UTEKELEZAJI WA MRADI HUU

Kuanza kwa usafirishaji wa umeme kutoka Tanzania kwenda Kenya na kupokea umeme kutoka Ethiopia. Mikataba ya kuuziana umeme kati ya nchi hizi iko katika hatua za mwisho za kusainiwa. Mradi umefadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Japan (JICA), Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), na Serikali ya Tanzania kwa gharama ya jumla ya Dola za Marekani milioni 258.2.

Mradi huu umeimarisha mfumo wa usafirishaji wa umeme katika Kanda ya Kaskazini-mashariki mwa nchi, na pia umeiwezesha Tanzania kuwa sehemu ya mfumo wa umeme wa Afrika Mashariki (EAPP), na kujiandaa kujiunga na mfumo wa SAPP pindi gridi ya umeme ya Zambia itakapounganishwa.
6. Mradi wa Tanzania - Zambia Transmission Interconnector Project (TAZA)
Mradi wa TAZA ni sehemu ya utekelezaji wa makubaliano ya ushirikiano kati ya Serikali za Tanzania, Zambia na Kenya yaliotiwa saini tarehe 15 Desemba 2014 (Inter-Governmental Memorandum of Understanding - IG-MoU). Mradi huu ni muendelezo wa juhudi za Serikali ya Tanzania
37
katika kuhakikisha kuwa nchi inakuwa na mifumo ya kisasa ya usambazaji wa umeme na kuimarisha biashara ya nishati na nchi wanachama wa SADC kupitia SAPP.
Mradi unahusisha ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovolti 400 yenye urefu wa kilomita 620 kutoka Iringa, kupitia Kisada (Mafinga), Iganjo (Mbeya), Nkangamo (Tunduma), hadi Malangali (Sumbawanga), pamoja na kipande cha kilomita 4 kinachoenda mpaka wa Tanzania na Zambia (Nakonde). Ujenzi huu unaenda sambamba na ujenzi wa vituo vya kupoza umeme katika maeneo ya Tagamenda, Kisada, Iganjo, Nkangamo, na Malangali.
Mradi wa TAZA umefadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia International Development Association (IDA) kwa Dola za Marekani milioni 605, Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) kwa Euro milioni 100, Umoja wa Ulaya kwa Euro milioni 26, pamoja na Serikali ya Tanzania ambayo imetoa Dola milioni 10 kwa ajili ya fidia kwa wananchi waliopisha mradi. Jumla ya gharama ya ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme na vituo ni takribani Dola za Marekani milioni 583.5 ambayo ni sawa na Shilingi trilioni 1.57.
Utekelezaji wa mradi huu umefikia asilimia 42, ambapo asilimia 55 ya kazi ni ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme na asilimia 23 ni ujenzi wa vituo vya kupoza umeme. Mradi unatarajiwa kukamilika tarehe 21 Mei 2026.
38
Mradi wa TAZA utaiwezesha Tanzania kujiunga rasmi na masoko ya nishati ya ukanda wa Kusini mwa Afrika kupitia SAPP na kuongeza uhakika wa upatikanaji wa umeme kwa mikoa ya nyanda za juu kusini, sambamba na kukuza uchumi wa wananchi.
Hitimisho
Kupitia miradi hii, Tanzania inaendelea kujijengea nafasi ya kuwa kitovu cha biashara ya nishati ya umeme katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini na hivyo kuchangia kikamilifu katika maendeleo ya kiuchumi ya nchi na ustawi wa wananchi wake.
ASANTENI KWA KUNISIKILIZA


Wanahabari wakimsikiliza kwa makini Msemaji


Jengo la Wizara lilivyo  sasa limekamilika kwa asilimia 90.1





TAARIFA FUPI KUHUSU MAENDELEO YA USAJILI WA WAAN DISHI WA HABARI KATIKA MFUMO WA TAI-HABARI

Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeshaanza kutoa vitambulisho kwa Waandishi wa Habari waliokidhi vigezo vilivyoainishwa kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229 katika Mfumo wa TAI-Habari. Kazi hii ya kutoa Vitambulisho imeanza tangu tarehe 19 Mei, 2025 na kazi hii itaendelea mpaka tarehe 21 Juni, 2025 ambapo Bodi ilitangaza kuwa ndiyo mwisho wa kuwasilisha maombi ya usajili kwa waandishi wa Habari wote ambao wana nia ya kuendelea na kazi ya uandishi wa Habari. Baada ya tarehe ya mwisho wa Maombi Waandishi wote wa Habari ambao Hawajajisajili hawataruhusiwa kufanya kazi za Habari mpaka pale watakapojisajili.

Hatua hii inalenga kuboresha huduma, kuimarisha usimamizi wa taaluma ya Uandishi wa Habari na kurahisisha upatikanaji wa vitambulisho kwa waandishi waliokidhi vigezo kwa mujibu wa Sheria.

Aidha, mpaka tarehe ya leo waandishi wa Habari 370 wameshajisajili katika mfumo wa TAI HABARI. Tunatoa wito kwa waandishi wote wa Habari ambao bado hawajajisajili, kujisajili katika mfumo huo kabla ya tarehe ya mwisho iliyotangazwa. Ikiwa mwandishi yeyote atapata changamoto ya kujisajili awasiliane na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari kwa namba ya simu 0754053725 au 0762879342.

Mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa kuomba usajili katika mfumo wa TAI-HABARI ni pamoja na kuwa na:

  • Namba ya simu na barua pepe vinavyofanya kazi,
  • Picha ndogo (passport size) iliyoskaniwa,
  • Vyeti vya elimu vilivyoskaniwa,
  • Barua ya utambulisho kutoka taasisi anayotoka au anakopeleka kazi zake ikiwa ni mwandishi wa kujitegemea (Freelancer),
  • Nakala ya Kitambulisho cha Taifa (NIDA), na
  • Ada ya Ithibati shilingi Elfu Hamsini (50,000).

Mahitaji haya ni muhimu ili kukamilisha mchakato wa maombi kwa mafanikio.

MWANDISHI ATAJISAJILI WAPI?

Waandishi wanapaswa kuingia kwenye kiunganishi cha  https://taihabari.jab.go.tz na kufuata maelekezo ya kiujisajili.

Baada ya kujaza taarifa kwa usahihi, mwombaji atapokea msimbo (code) kupitia SMS na kiungo kwenye barua pepe ili kuendelea na hatua za kujaza;

a)    Wasifu,

b)    Kufanya maombi,

c)     Kupata ankara ya malipo,

d)    Kulipia na

e)    Kuwasilisha maombi ya kupata Kitambulisho (Press Card).

 

Aidha, waombaji wote wanasisitizwa kuhakikisha wanakuwa na:

·       Vyeti halali na vilivyohakikiwa na mamlaka husika;

·       Taarifa sahihi kuepusha usumbufu; na

·       Picha ya (Passport size) ya hivi karibuni;

 

NI NANI ANAWEZA KUJISAJILI NA KUPEWA ITHIBATI?

Kwa mujibu wa Kanuni ya 17 (a) ya Kanuni za Sheria ya Huduma za Habari Watu wanaopaswa kujisajili ili kuthibitishwa na kupatiwa vitambulisho ni;

  • Waaandishi
  • Wahariri
  • Waandishi wa kujitegemea (Freelancers na Correspondents)
  • Watangazaji wa Radio na Televisheni
  • Wapiga picha wa Televisheni na Magazeti
  • Waandaaji wa vipindi vya habari (Producers) na
  • Wanafunzi wa Vyuo vya Uandishi wa habari (wanaokwenda mafunzo kwa vitendo).



Msemaji akipiga ngoma pamoja na kikundi cha burudani cha NYOTA chenye makazi yake Dodoma  katika hafla hiyo

Picha pamoja na viongozi wa wizara

Msemaji akipiga picha na wanahabari


 

Comments

Popular posts from this blog

WALIOPITA KURA ZA MAONI CCM HAWA HAPA

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.