Posts

Showing posts from August, 2024

Ushuhuda wa Kusikitisha Wafichua Hatari ya Zebaki kwa Wachimbaji Wadogo Kahama

Image
Na Napaul Kayanda, Kahama Mhandisi Teostine Mwasha, Katibu Mtendaji wa Taasisi ya Kuendeleza Uchimbaji Mdogo Tanzania, ameanza kampeni maalum ya kuelimisha jamii kuhusu athari mbaya za zebaki, kemikali inayotumika katika ukamataji wa dhahabu. Taasisi hiyo inalenga kuboresha mazingira ya kazi katika sekta ya uchimbaji mdogo kwa kuhakikisha wachimbaji wadogo wanatumia zebaki kwa njia salama ili kupunguza madhara yake. Kwa sasa, Mhandisi Mwasha na timu yake wanahamasisha matumizi sahihi ya zebaki, kwa kuwa kemikali hii inaweza kusababisha madhara makubwa kwa afya ya binadamu, hususan kwa wale wanaoishi karibu na maeneo ya uchimbaji. Ameeleza kuwa serikali ya Tanzania imelidhia Mkataba wa Minamata unaolenga kupunguza madhara ya zebaki kwa asilimia 30 ifikapo mwaka 2030. Akizungumza kuhusu jitihada zao, Mhandisi Mwasha amesema kwamba wao kama taasisi wanahusika moja kwa moja katika kuielimisha jamii, hususan wachimbaji wadogo na familia zinazozunguka migodi. Amefafanua kuwa zebaki inaweza k

PICHA ZA MATUKIO YA TAMASHA LA MAPISHI JIJINI MBEYA

Image
S Naibu Waziri wa  Nishati Judith Kapiga, akisikiliza maelezo toka kwa mratibu wa Tamasha la Mapishi kwa Mama na Baba lishe lililojulikana kwa jina la TULIA COOKING FESTIVAL 2024. lilifanyikia jijini Mbeya  na washiriki zaidi ya 100 waliweza kushiriki.Mshindi wa kwanza  alikuwa  Zuena Robison. M bunge Sophia Mwakagenda akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Mkuu wa Oryx Gas Benoit Araman, wakati wakikagua mabanda kwenye tamasha hilo Mama na Baba lishe wakisubili majaji kuwakagua Washiriki wa Tamasha hilo wakimpokea mgeni rasmi Vijana watano wa Kitanzania wanaosomeshwa na Dkt. Tulia Ackson nchini Nigeria, wakiwa stejini kwa ajili ya kujitambulisha Mkurugenzi Mkuu wa Oryx Gas Benoit Araman, akihutubia katika Tamasha hilo Washiriki wakicheza baada ya kufungwa Mjumbe wa Halimashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi  (CCM),Ndele Mwaselela, akihutubia Naibu Waziri wa Nishati Wakili Msomi Judith Kapinga, akihutubia washiriki Machif wa mkoa wa Mbeya wakipakuliwa chakula Washindi wakipewa zawadi Spika