NAIBU WAZIRI MKUU BITEKO AWAKOSHA WANAMASUMBWE

Wakazi wa Masumbwe mkoani Geita, wakimkalibisha Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko, alipokuwa akipita katika eneo lao na kusimama kwa muda kisha kuzungumza nao pamoja na Mbunge wao Nicodemus Maganga.  Doto alipita eneo hilo akitokea jimboni kwake  huku akiwahi kupanda ndege  uwanja wa ndege wa Kahama kwa ajili ya kuwaha jijiji Dar es salaam alikosema kunafanyika kikao leo hii

Mkuu wa Mkoa wa Geita,  Martine Shigela, akimkalibisha Biteko kuzungumza na wanamasumbwe


Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Nishati Dkt, Doto Biteko, akiwasilimia wanambogwe baada ya kuwasili akitokea jimboni kwake leo mchana,  akizungumza huku akishangiliwa na umati wa watu waliojitokeza eneo hilo aliwaambia ombi la Mbunge wao linafanyiwa kazi siku si nyingi watapatiwa zahanati mpya kama alivyoomba mbunge wao, aidha kuhusu barabara ya lami aliwaambia ombi lao linafanyiwa kazi  siku si nyingi barabara za wilaya hiyo zitapatiwa lami hiyo ni ahadi ya lazima itekelezwe. AIdha kuhusu Umeme aliwahakikishia wanamasumbwe hakuna umeme kukatika katika kwani hilo lilikuwa agizo la Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, alipompeleka katika wizara hiyo alimwagiza kwenda kutatua tatizo hilo la umeme hivi sasa mabo shwali.Amewaomba wajitokeze kwa wingi katika uchaguzi wa Serikali za mitaa unaotalajiwa kufanyika hivi karibuni na wajiandae kumpa kura nyingi Rais Samia.

Aidha Mbunge wa jimbo hilo Maganga, alimwambia Biteko kura za Rais Samia katika jimbo hilo ni nyingi  kwani amewakosha wanamasumbwe kwa kuwatatulia kero zao watakuwa watovu wa nidhamu kwa mema yote aliyowafanyika kuanzia kwenye madini wafanyabishara wadogowadogo wamepatiwa leseni tofauti na tawala zilizopita, maji, umeme  na barabara. Hakika mama ameupiga mwingi na hawatamwangusha. Nae  Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita Nicolaus Kasendamila akizungumza hapo alisema  Wanamasumbwe  mbunge wao amewafanyia mambo mengi mazuri wanahaki ya kumpongeza ,amewataka wanaotaka kugombea jimbo hilo wajipange wasiwe na makando kando yeye na kamati yake hawanamuda wa kumsafisha mgombea  wajitokeze waliowasafi na wasioanza kampeni mapema kwani watakwama mapema.


Mbunge Maganga, akizungumza

Wananchi wakimshangilia Biteko



















































 

Comments

Popular posts from this blog

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.

KADA MGEJA AHUDHURIA MAZIKO YA MAMA MZAZI WA MWANDISHI MWANDAMIZI WA HABARI KAHAMA