MWENYEKITI UWT, CHATANDA AMPA KONGORE MBUNGE SOPHIA MWAKAGENDA

Mwenyekiti  wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi (UWT) Mary  Chatanda (kushoto), akimkabidhi kanga  mbunge   wa viti maalum Chadema,Sophia Mwakagenda baada ya kumnunulia kwa kufurahishwa kwake kwa kuweza kuandaa Kongamano la Wanawake  wauza mbogo mboga na Matunda  jiji la Dodoma  ambapo yeye alikuwa mgeni rasmi, zaidi ya  wanawake 3000 walihudhulia . Lilifanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete.
Chatanda,akimuonyesha kanga kabla ya kumkabidhi

Wauza mboga mboga na matunda, wakijipatia chai kabla ya kuingia katika mkutano


Wajasiriamali wakijiburudisha na  muziki kabla ya kuanza mkutano

Rais samia oyeee ndivyo wanavyosema  Wajasiriamali hao

      


Mkurugenzi wa  Kampuni ya SHIM Media Company Limited, Sophia Mwakagenda, akizungumza katika kongamano hilo ambalo aliliandaa yeye  chini ya udhamini wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS)
Mkurugemzi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dkt. Albina Chuwa, akiwapungia mikono wajasiliamali baada ya kutambulishwa na Mwakagenda katika kongamano hilo
Wabunge wakisikiliza hotuba
Wabunge wakicheza muziki
Mwenyekiti Chatanda, akikabidhiwa kapu la mazagazaga mboga na matunda na wajasiliamali hao
Mwakagenda nae akikabidhiwa
Dkt. Chua na Sophia,wakibadilishana mawazo

Chatanda amezitaka Halmashauri   nchini kuhakikisha mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri hizo  iwafikie walengwa hususani wafanyabiashara wanawake wadogo wadogo ili waweze kujiinua kiuchumi, ametoa agizo hilo , Jumamosi Mei 04.2024 wakati akizungumza na wanawake hao baada ya kusikiliza hotuba ya Mwenyekiti wa wanawake wauza mboga na matunda jijini Dodoma, Anna Chacha, wakati hotuba yake katika kongamano hilo akidai changamoto ya wafanyabiashara hao kukosa mikopo wakiambiwa na taasisi za kifedha hawana vigezo vya kupatiwa mikopo ,  alibainisha kuwa mikopo  mingi ikiwemo ya kausha damu ambayo imekuwa mwiba kwa wanawake wauza mboga mboga kujiendeleza kiuchumi na kuwa kikwazo kufikia malengo yao."Kulikuwa na changamoto ya mikopo ya Halmashauri kutowafikia walengwa husika, naelekeza Halmashauri zote nchini zitoe  mikopo kwa wanawake wote walengwa wanapata mikopo hiyo bila kupindisha pindisha" -Chatanda "Natoa rai kwa serikali kuidhibiti au kusitisha kabisa  mikopo ya kausha damu, ujinga hauishi, kwani inawaumiza wanawake wengi sana nchini" , alisema mwenyekiti huyo Aidha amempomgeza Mbunge Sophia Mwakagenda  kwa kutekeleza irani ya chama cha Mapinduzi kwa kuwezesha wananchi hao wote kuhudhulia  warsha hiyo.

Mwenyekiti Chatanda  Amewaomba wabunge wote kuiga alichokifanya mbunge huyo ili wanawake wote nchini wanufaike na alichokifanya Mwakagenda. Maendeleo hayana chama  na kausha damu haichagui chama wapewe elimu akina mamam hao ili wasiendelee kuibiwa.

Naye Mkazi wa Makole Mwajuma Ahthuman alimsifia Mbunge Sophia Mwakagenda kwa kuwa mfano wa wabunge bora wanawake anawakusanya hajali cha chama anachojuwa yeye ni kuwasaidia , alisema hakika ni mbunge wa kuigwa, amewaomba wabunge wa chamachake kuiga

Anasema Makongamano kama hayo anayasakia kwenye redio na TV wakikusanyana viongozi na kugawiana posho lakini Sophia amewafuata wauza mchicha na mbogambogo kwenye masoko karibu saba ya jiji la Dodoma ", Tangu nizaliwe sijawahi kuhudhulia kongamano kama hili lililoitishwa na chama  au mbunge wa chama changu huwa nayasikia tu hakika mbunge huyu mtu wa watu.", alisema Mwajuma. 




Chatanda, akimkabidhi Menyekiti  Chacha Sh Milioni 1 kwa wauza mbogamboga na matunda
Chatanda oyee na CCM oyeeeeeee pia Mwakagenda adumuu, akisema mwenyekiti huyo baada ya kupokea  fedha hizo
Tedson NNgwale, akitoa mada ya  ujasiriamali katika kongamano hilo





Dkt. Albna Chuwa, akinunua kanga baada ya kutoka katika kongamano hilo
 

Comments

Popular posts from this blog

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

AMANI YETU TUILINDE NAIBU WAZIRI CHANDE AZUNGUMZA KATIKA IJITIMAI JIJINI DODOMA

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.