MATUKIO MBALIMBALI LEO




Mwandishi wa Kituo cha ITV mkoani Arusha,Khalfan Lihundi,akizungumza jana na waandishi wa habari nje ya Kituo cha Polisi cha Usariver,wilayani Arumeru mkoa wa Arusha baada ya kuachiwa kwa dhamana ambapo alishikiliwa kwa zaidi ya saa 24 kituoni hapo akidaiwa kuandika habari za migogoro ikiwemo ya ardhi na maji katika wilaya hiyo PICHA NA JANETH MUSHI

 


Akitoka mahabusi akiwa ameogozana na wanahabari wenzake
WAZIRI MKUU APOKEA  FEDHA ZA MAAFA




Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Askofu Mkuu wa kanisa la EAGT,  Dkt. Brown Mwakipesile kabla ya kupokea msada wa shilingi milioni 10 uliotolewa na kanisa hilo kwa waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera. Makabidhiano hayo yalifanyika  kwenye makazi ya Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Desemba 22, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Askofu Mkuu wa Kanisa la EAGT, Dkt.  Brown Mwakipesile kabla ya kupokea msaada wa Shilingi milioni 10 ukiwa ni mchango wa kanisa hilo kwa waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera. Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye makazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay jijini Dar es salaam

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Askofu Mkuu wa Kanisa la EAGT, Dkt.  Brown Mwakipesile kabla ya kupokea msaada wa Shilingi milioni 10 ukiwa ni mchango wa kanisa hilo kwa waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera. Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye makazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay jijini Dar es salaam

 KAMANDA MPYA WA POLISI SINGIDA AANZA KAZI


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) DEBORA MAGILIGIMBA akikagua gwaride la Askari wa kikosi cha kutuliza ghasia mkoa wa Singida mara baada ya kuteuliwa kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa huo. Kamanda Debora anachukua nafasi ya marehemu SACP PETER KAKAMBA aliyefariki hivi karibuni kwa maradhi ya tumbo. (Picha na Shabani Marissa, Mwandishi wa Habari wa Jeshi la Polisi Singida)

 



Comments

Popular posts from this blog

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

KADA MGEJA AHUDHURIA MAZIKO YA MAMA MZAZI WA MWANDISHI MWANDAMIZI WA HABARI KAHAMA