DKT. KINGWANGALLA ATUMBUA MAJIPU NA MTOKO WA DIAMOND
MAPEMA ASUBUHI YA LEO DKT. KINGWANGALLA ATUMBUA MAJIPU YA WATUMISHI WACHELEWAJI WA WIZARA YA AFYA
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt.
Hamisi Kingwangalla akiwaamrisha askari wa getini wizarani hapo kuweka
kufuli na kutoruhusu mtumishi yoyote wa ofisi hiyo kuingia ndani ya
ofisi za wizara ilipotimu saa 1:32 asubuhi mapema leo.(Picha zote na
Zainul Mzige wa Modewjiblog).
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt.
Hamisi Kingwangalla akisimamia zoezi la ufungwaji wa geti hilo, Kulia ni
askari wa SUMA JKT akiweka kufuli katika lango kuu la kuingia katika
ofisi za Wizara ya Afya.
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt.
Hamisi Kingwangalla akiwauliza askari wa getini kuhusu daftari la
mahudhurio ya watumishi wa wizara baada ya kufungwa geti hilo, na kupewa
maelezo kuwa watumishi huonyesha vitambulisho pekee na husaini katika
vitengo vyao.
Mmoja
wa wafanyakazi wa Wizara ya Afya akiwasili ofisini huku muda wa kuingia
kazini ukiwa umepitiliza. Kushoto ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kingwangalla akizungumza na
mmoja watumishi wa wizara hiyo na kuagiza kuletewa vitabu vya
mahudhurio kwa vitengo vyote vilivyopo wizarani hapo.
Mkurugenzi
wa Utawala na Rasilimali Watu katika Wizara ya Afya, Michael John
akitoa maelezo kuhusu mahudhurio ya watumishi kwa Naibu Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kingwangalla.
Magari
ya watumishi wa Wizara ya Afya yakiendelea kuwasili ofisini bila ya
kutambua kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri, Dkt. Kigwangalla ametoa agizo la
kuizuia watumishi wachelewaji.
Askari
wa getini wakimpa maelezo mmoja wa watumishi wa wizara hiyo kuwa Mh.
Naibu Waziri ameagiza watumishi wote waliochelewa kuzuiliwa kuingia
ndani.
Mmoja
wa wasaidi wa idara ya rasilimali watu akimkabidhi vitabu vya
mahudhurio Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto, Dkt. Hamisi Kingwangalla.
Kichupa cha 'Utanipenda' cha Diamond nyuma ya pazia
Nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ akiwa kasimama mbele ya magari aliyoyatumia katika video yake mpya ya Utanipenda.
Diamond akiangalia vipande vya video hivyo kabla ya kuendelea kushuti.
Sasa
hivi kwenye ulimwengu wa muziki, gumzo ni ngoma aliyoitoa Mwanamuziki
Nasibu Abdul ‘Diamond’ inayokwenda kwa jina la Utanipenda.
Ni
ngoma kali ambayo itatambulishwa kwa mara ya kwanza ndani ya Ukumbi wa
Kimataifa wa Burudani wa Dar Live uliopo Mbagala jijini Dar.
Mbali na utambulisho wa ngoma hii ambayo itapigwa live kwa kutumia
vyombo, nyimbo nyingine ambazo Diamond atazipiga siku hiyo ni pamoja na
Mdogomdogo, Nasema Nawe, Nana na nyinginezo zinazobamba huku akiwa na
madansa wake kutoka Wasafi Classic Baby (WCB).
Itakuwa
ni siku ya Krismasi (Ijumaaa ijayo) ambayo msanii huyo ameahidi kufanya
mambo makubwa akisindikizwa na mkali wa nyimbo za Singeli, Msaga Sumu
pamoja na wacheza dansi hatari Afrika Mashariki, Wakali Dancers na
wasanii wengine kibao.
Burudani yote hiyo ambayo imedhaminiwa na huduma kutoka kampuni ya simu
Tanzania, Airtel Money utaipata kwa kiingilio cha shilingi 15,000 tu
getini na wale watakaohitaji huduma ya VIP watalipia shilingi 30,000.
Katika kuelekea kwenye shoo hiyo, Showbiz ilifanikiwa kunasa baadhi ya
picha za nyuma ya pazia ‘behind the scene’ wakati kichupa cha wimbo huo
kikiandaliwa.
Video hiyo ni mkono wa yuleyule mkali wa vichupa kutoa Sauzi anayekwenda
kwa jina la God Father.
Hajakosea! Amefanya bonge la kazi na hata mashabiki ni mashahidi kwamba wimbo ni mkali na kideo chenyewe ni ‘kitamu’.
Maneno mengi siyo ishu, kwenye hili picha zinaongea zaidi hivyo pitisha macho kwenye baadhi ya picha hizo ili upate uhondo!
Kwani kuna mtu kaibiwa?
Imeandaliwa na Andrew Carlos/GPL
Comments
Post a Comment