Msemaji Mkuu wa Serikali azungumza siku ya Kimataifa ya Upatikanaji Habari kwa wote
Viongozi Toeni Taarifa kuhusu Mafanikio ya Serikali-Msigwa Na Grace Semfuko, MAELEZO Septemba 28, 2022 Msemaji Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO Bw. Gerson Msigwa amewataka Viongozi wa Taasisi za Serikali Nchini, kutoa taarifa za mafanikio ya utendaji kazi wa taasisi hizo kwa Vyombo vya Habari, ili kuwaonesha Wananchi maendeleo yanayofanywa na Serikali yao. Amesema yapo mambo mengi yanayofanywa na serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan na hivyo ni muhimu kuyaweka wazi ili wananchi wayaone. Ameyasema hayo leo Septemba 28, 2022 Jijini Dar es Salaam aliposhiriki mahojiano katika kipindi cha Baragumu kinachorushwa na Televisheni ya Channel Ten ikiwa ni Siku ya Kimataifa ya Upatikanaji wa Habari kwa Wote, na kubainisha kuwa wapo baadhi ya watendaji wanaokwepa kutoa taarifa za mafanikio ya taasisi zao kwa wananchi na kuwataka kuzitoa taarifa hizo. “Wapo baadhi ya viongozi ni wakwep...