Kigogo Escrow aruhusiwa kwenda kutibiwa
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, imeamuru Mmiliki wa Kampuni ya Kufua Umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), Harbinder Singh Seth, aende kutibiwa kutokana na matatizo ya kiafya yanayomsumbua. Amri hiyo imekuja baada ya Seth kusimama mbele ya mahakama hiyo jana wakati shauri lake likiendelea na kudai kuwa ana matatizo ya kiafya na kuomba apewe kibali ili aweze kutibiwa. Kutokana na hali hiyo, Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shahidi, aliitaka Serikali kumpeleka hospitali ili aweze kupatiwa matibabu kutokana na maradhi hayo. Hakimu Shahidi aliahirisha shauri hilo hadi Agosti 3, mwaka huu, kwa ajili ya kutajwa tena. Julai 14, mwaka huu, upande wa utetezi, ukiongozwa na Wakili Alex Balomi, uliieleza mahakama hiyo kuwa mteja wao anahitaji kupewa mtaalamu wa afya kwa sababu ana uvimbe tumboni kama puto, pia anakosa usingizi. Awali, washtakiwa hao walipandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka sita, yakiwamo kula njama, uhujumu uchumi, kujihusisha n...