Posts

Papa Francis aanguka akisoma misa CZESTOSHOWA: Poland

Image
Papa Francis aanguka akisoma misa CZESTOSHOWA: Poland Wasaidizi wake wakimwinua KIONGOZI wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis (79) jana alianguka wakati wa ibada,     kwenye madhabahu ya Jasna Gora, mjini Czestoshowa, Poland. Tukio hilo lilitokea   baada ya Papa Francis kujiikwaa akiwa madhabahuni hali iliyowalazimu mapadre waliokuwa karibu naye kumsaidia kuinuka. Taarifa zinasema Papa alianguka chini karibu na ngazi za madhabahuni na aliinuliwa na mapadri waliokuwa kwenye misa hiyo.  Kwa mujibu wa taarifa za utabibu, Papa Francis amekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa sciatica unaosababishwa na   maumivu chini ya mgongo. Papa Francis , ambaye ni mzaliwa wa   Argentina alionekana akitembea huku akitafakari   hali iliyomfanya asigundue kuwa kulikuwa na ngazi mbele yake.     B aad ya kuinuka, Papa Francis , aliendelea na taratibu za ibada kama ilivyopangwa. Alihubiri kwa muda mrefu kwenye ...

KIKWETE AMKABIDHI KIJITI MAGUFULI

Image
Mwenyekiti wa CCM Mstaafu na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete(kushoto) akimkabidhi   Mwenyekiti mpya   Rais Dk. John Magufuli,ripoti ya chama ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka jana baada ya kumtangaza kwenye mkutano Mkuu Maalum wa chama hicho mjini Dodoma  Wakikumbatiana kwa mara ya mwisho kama mwenyekiti   Mwenyekiti mstaafu wa CCM,Jakaya Kikwetena Mwenyekiti mpya Rais Dk. John Magufuli (kulia), wakiwapungia wanachama wa chama hicho baada ya kumtangaza kwenye Mkutano Mkuu Maalum Dodoma Wakikumbatiana na rais wa zanzibar Magufuli ni wa kuogopwa *Asema walioimba wana imani na Lowassa kwake yeye wangepotea ndani ya nusu saa *Asema hana uvumilivu, atangaza kuifumua CCM, awawashia taa nyekundu wasaliti *Sasa kuihamishia Serikali yake Dodoma ndani ya miaka minne UNAWEZA kumwelezea Rais John Magufuli kama rais anayetisha, anayepaswa kuogopwa au pengine kuhofiwa kutokana na kauli anazozitoa hadharani kila anapopata fursa ya kuhutubia. Hali hiyo ili...