WABUNGE WAPONGEZA UJENZI WA MUHIMBILI MPYA NA MFUKO WA BIMA YA AFYA

Mwenyekiti wa Bunge Deo Mwanyika, akifungua semina ya wabunge iliyokuwa ikizungumzia ujenzi wa Hospitaliu ya  Taifa ya Muhimbili kando kando mwa majengo ya zamani yaliyodumu kwa muda wa miaka zaidi ya 100 na Mfuko wa Bima ya Afya kuanza kwake. 
Waziri wa Afya Mohamed Mchengelwa, akisoma hotuba  katika semina ya wabunge  iliyofanyika ukumbi wa Msekwa jijini Dodoma.    














Wabunge wakisikiliza wachangiaji






Ramani inayoonyesha majengo yatakavyokuwa baada ya kukamilika ujenzi wake
Mbunge wa Misungwi, Silvery Luboja, akichangia katika semina hiyo akisema ujenzi wa Hospitali hiyo hauepukiki lakini muda umefika sasa wa kujenga Muhimbili zingine katika mikoa ili kuepusha msongamano katika hospitali hiyo, kuhusu Bima ya Afya kunahitajika marekebisho makubwa nianzuri  ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni njema lakini kunaupigaji sana kwa baadhi ya watumishi na wenye hospitali ambao hupokea wagonjwa wa bima ya afya

Mbunge Mariam Kisanji, akiitaka Serikali kuchukua hata majengo ya Sekondari za Jangwani na Azania ili kuwepo eneo kubwa la Hospitali hiyo
Mbunge Abubakary Asenga wa Kilombero, alisema Mfuko wa Bima ya Afya uje na utaratibu mzuri na siyo mwanachi anabima akifika kutibiwa anaambiwa dawa hakuna na anaonyeshwa zilipo kwenda kununu ambapo maduka yametapaka kando kando mwa Hospitali  inadaiwa ni yawatumishi wa Hospitali hizo
Mbunge wa Mlalo, Rashidi Shangazi, alisifu ujenzi huo akawaomba ujenzi huo ufanyike kisasa kwani eneo hilo ni dogo inahitajika ujenzi wa maghorofa kukidhi mahitaji 

Maofisa wa Wizara ya Afya wakiwasikiliza kwa makini wabunge wakati wakichangia



Mbunge wa Tanga Mjini Kassim Omar, akisifia ujenzi huo ila akaomba Muhimbili nyingine ijengwe Tanga kwani maeneo mengi yapo huko kupunguza msongamano wa wagonjwa katika Muhimbili moja ya Dar es Salaam.

Mbunge jimbo la Katavi, Thomas Kampala, alisema wazo la upanuzi wa Hospitali hiyo ulichelewa sana sasa ni kuhalakisha Serikali isisikilize kelele za wapitanjia kwani hiyo ni faida kwa wananchi wa Tanzania 
Mbunge wa Mafinga Mjini, Dickson  Lutevele Villa, akichangia alisema ni vema sasa kuhalakisha ujenzi huo na wao Iringa wanaomba lifunguliwa Tawi la Muhimbili wagonjwa wengine wawe wakitibiwa huko kuepusha msongamano wa kila tiba Dar
Mbunge wa Sengerema, Hamis Tabasamu, akisema Bima ya Afya isianze kufanya kazi kabla ya kutolewa utaratibu wa bei ya dawa  wanannchi wanaibiwa sana na wauguzi wanabambikiwa bei na kusababisha chuki kwa Serikali na wabunge waliokubali mfuko huo.







Mbunge wa Dodoma Mjini, Pascal Chinyele,aliomba Serikali Muhimbili ijemgwe na Dodoma , maeneo yapo mengi  Dar es Salaam imeishiwa na maeneo kuchukua maeneo na kuyavunja kwa ajili ya upanuzi ni kuuwa historia wasigombana na watunzaji wa maeneo ya urithi




 

Comments

Popular posts from this blog

WALIOPITA KURA ZA MAONI CCM HAWA HAPA

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?