KUPANDA KWA MAFUTA NI DUNIA NZIMA WANANCHI WAJIHADHARI NA WAPOTOSHAJI

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Kenan Kihongosi, amezungumza na wanahabari leo jijini Dodoma na kuwahakikishia  wananchi kwamba Serikali imeanzisha mfuko maalum kwa ajili ya kukabiliana na uhaba wa mafuta. Aidha Chama cha Mapinduzi kimeitaka Serikali kuhakikisha  inalitumia shirika la TPDC  kuwa muagizaji mafuta mkuu ili kuwauzia wananchi kwa bei ya soko kwani baadhi ya wafanyabishara huwa na mambo yao kwa kujali faida zaidi. Kihongosi amebainisha kwamba hakuna nchi ambayo haijaguswa na kupanda kwa mafuta hata kule ulaya mafuta yamepanda kuliko  Tanzania hata majirani wa Tanzania mfano hapo Kenya na Uganda bei ipo juu sana kuliko hapa nchini "Mafuta yamepanda kwenye soko la Dunia kutokana na vita vya mashariki ya kati  kati ya Marekani, Israel na Irani tuombee vita viishe ili hali ilejee kama kawaida", alisema Kihongosi.

Aidha mewataka wanasiasa kuaacha kutumia uhaba wa mafuta kujitafutia umaarufu 










 

Comments

Popular posts from this blog

WALIOPITA KURA ZA MAONI CCM HAWA HAPA

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?