Posts

Showing posts from July, 2024

SEKTA YA NISHATI MANENO KIDOGO VITENDO ZAIDI - DKT. BITEKO

Image
📌 Ashiriki Bonanza la Nishati Dodoma 📌 Ataka Watumishi kupendana na kushirikiana   📌 Atunukiwa Nishani ya Uasisi Bonanza la Nishati 📌 EWURA yaibuka mshindi wa Jumla; Mkurugenzi Mkuu amshukuru Dkt.Biteko kuthamini Watumishi Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe, Dkt. Doto Biteko amewakumbusha Watumishi wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake kuiishi  Kauli Mbiu ya Sekta ya Nishati ambayo ni Maneno Kidogo  Vitendo zaidi ili kuweza kutoa huduma iliyobora kwa wananchi. Amesema hayo leo tarehe 27 Julai 2024, wakati Watumishi wa Wizara ya Nishati na Taasisi zilizo chini yake waliposhiriki kwenye  Bonanza la Nishati ambalo limefanyika Jijini Dodoma likibebwa na Kaulimbiu Shiriki Michezo Imarisha Afya. “Sekta ya Nishati ni muhimu kwenye ujenzi wa uchumi wa nchi yetu na tufahamu kwamba Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anatutegemea sisi ili kuweza kutoa huduma hii muhimu kwa wananchi, hivyo watumishi tupendane, tushirikiane na kufanya kazi kwa bidi zaidi ili kusukuma mbele gurudumu la N

KIKWETE ASHIRIKI KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI CHALINZE

Image
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete,  akizungumza katika kikao cha Baraza la Madiwani Cha Chama Cha Mapinduzi kuchagua diwani atakayegombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze kilichofanyika Chalinze leo hii.  

MEJA JENERALI NKUNDA ATEMBELEA MELI YA MATIBABU YA KICHINA ILIYOTIA NANGA DAR

Image
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.  

NAIBU WAZIRI MKUU BITEKO AWAKOSHA WANAMASUMBWE

Image
Wakazi wa Masumbwe mkoani Geita, wakimkalibisha Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko, alipokuwa akipita katika eneo lao na kusimama kwa muda kisha kuzungumza nao pamoja na Mbunge wao Nicodemus Maganga.  Doto alipita eneo hilo akitokea jimboni kwake  huku akiwahi kupanda ndege  uwanja wa ndege wa Kahama kwa ajili ya kuwaha jijiji Dar es salaam alikosema kunafanyika kikao leo hii Mkuu wa Mkoa wa Geita,  Martine Shigela, akimkalibisha Biteko kuzungumza na wanamasumbwe Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Nishati Dkt, Doto Biteko, akiwasilimia wanambogwe baada ya kuwasili akitokea jimboni kwake leo mchana,  akizungumza huku akishangiliwa na umati wa watu waliojitokeza eneo hilo aliwaambia ombi la Mbunge wao linafanyiwa kazi siku si nyingi watapatiwa zahanati mpya kama alivyoomba mbunge wao, aidha kuhusu barabara ya lami aliwaambia ombi lao linafanyiwa kazi  siku si nyingi barabara za wilaya hiyo zitapatiwa lami hiyo ni ahadi ya lazima itekelezwe. AIdha kuhusu Umem