KILANGO ATEMBELEA CHUO CHA UFUNDI STAD CHAN'OMBE DAR

 Mkufunzi wa Chuo cha VETA cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)-Kipawa, Bw. Abdul Mollel (kulia) akimuonesha na kumuelezea Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mh Anna Kilango Malecela, nyenzo na mifumo mbalimbali inayotumika kufundishia wanafunzi katika chuo hicho. Naibu Waziri Anna Kilango Malecela alitembelea Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) ikiwa ni pamoja na Vyuo vya vinavyomilikiwa na VETA vilivyopo jijini Dar es Salaam siku ya Jumanne, 21 Aprili, 2015.





Rhoda Mbwanji Mwanafunzi wa Kozi ya Wasaidizi wa Maabara inayotolewa na Chuo cha Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi na Huduma Dar es Salaam-Chang’ombe, 
 (kushoto), akimuonesha Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Anna Kilango Malecela (wa pili kushoto) namna ya kuchanganya kemikali kwa ajili ya mahitaji mbalimbali wakati Naibu Waziri alipotembelea Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) Jumanne, 21 Aprili, 2015. Wengine kutoka kushoto ni Mratibu wa Mafunzo, VETA kanda ya Dar es Salaam, Bi. Florence Kapinga, Kaimu Mkurugenzi wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Thomas Katebalirwe, Mkufunzi wa Chuo cha VETA Dar es Salaam Henry Maseko na Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Mhandisi Zebadiah Moshi.

Comments

Popular posts from this blog

UNAMKUMBUKA AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIAA.

Je, wajua kwamba Australia ni bara, nchi na kisiwa?

KADA MGEJA AHUDHURIA MAZIKO YA MAMA MZAZI WA MWANDISHI MWANDAMIZI WA HABARI KAHAMA