Posts

MRADI WA KUFUA UMEME WA JULIUS NYERERE WAKAMILIKA RASMI - DKT. BITEKO

Image
📌 Asema ni ndoto ya watanzania kupata umeme wa uhakika   📌 Asisitiza kazi iliyobaki ni kuimarisha miundombinu ya kuwafikishia wananchi umeme   📌 Rais Samia na Rais wa Misri kuzindua rasmi Mradi wa Julius Nyerere   Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewataka Watanzania kutegemea kupata umeme wa uhakika baada ya Mradi wa kufua umeme kutoka Bwawa la Julius Nyerere uliokuwa ukisubiriwa kwa shauku kubwa na Watanzania  kukamilika  rasmi.   Dkt. Biteko ameyasema hayo April 5, 2025 baada ya kutembelea Mradi huo akiwa ameambatana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na uwekezaji, Mhe. Profesa Kitila Mkumbo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mhe. Hamadi Masauni pamoja na Viongozi wengine mbalimbali.   Amesema hivi sasa mitambo yote tisa imekamilika na inafanya kazi tayari, amefafanua kuwa kukamilika kwa Mradi huo kumechangiwa na maono ya Rais wa Awamu ya Sita, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye aliu...

RAIS DKT. SAMIA AFUNGUA MAKAO MAKUU YA MAHAKAMA YA TANZANIA JIJINI DODOMA

Image
  . Rais  Dkt. Samia Suluhu Hassan akipanda mti wa kumbukumbu pembezoni mwa Jengo la Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania Jijini Dodoma tarehe 05 Aprili, 2025 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua Jengo la Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania, Tume ya Utumishi wa Mahakama pamoja na Nyumba za Makazi ya Majaji Mkoani Dodoma, tarehe 05 Aprili, 2025. Taswira ya Jengo la Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania, Tume ya Utumishi wa Mahakama pamoja na Makazi ya Majaji ambayo yamezinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, tarehe 05 Aprili, 2025 Jijini Dodoma. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Hamis Juma mfano wa ufunguo mara baada ya uzinduzi wa Jengo la Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania, Tume ya Utumishi wa Mahakama pamoja na Makazi ya Majaji tarehe 05 Aprili, 2025, Jijini Dodoma.

MAKAMU MWENYEKITI WA CCM, WASIRA APOKEA TAARIFA UTEKELEZAJI ILANI YA CHAMA HICHO JIMBO LA ILALA

Image
Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara. Stephen Wasira akizungumza na Viongozi na Wajumbe wa Mkutano Mkuu  leo April 05, 2025 katika uwasilishaji wa taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM Jimbo la Ilala Jijini Dar Es  Salaam  Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Ndg. Stephen Wasira akizungumza na Mwenyekiti wa CCM Moka wa Dar eś Salaam Ndg. Abasi Mtemvu  leo April 05, 2025 katika uwasilishaji wa taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM Jimbo la Ilala Jijini Dar Es  Salaam. Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila akizungumza na Viongozi  wa CCM leo April 05, 2025 katika uwasilishaji wa taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM Jimbo la Ilala Jijini Dar Es  Salaam Mbunge wa Jimbo la Ilala  Naibu Spika wa Bunge, Mussa Zungu   akizungumza na Viongozi  wa CCM leo April 05, 2025 akiwasilisha  taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM Jimbo la Ilala Jijini Dar Es  Salaam Viongozi na wajumbe wa mkutano Mkuu jimbo ...

MWENGE WA UHURU UPO RUFIJI MKOANI PWANI

Image
KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ismail Ali Ussi, amesisitiza umuhimu wa kuitunza na kuenzi amani, utulivu na upendo miongoni mwa Watanzania kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu. Akizindua bweni la wasichana katika Shule ya Sekondari Ikwiriri, Jimbo la Rufiji, Mkoani Pwani, lililogharimu kiasi cha Shilingi milioni 185.4, alitoa rai kwa wanafunzi waliofikisha miaka 18 na kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura, pamoja na vijana, kuhakikisha wanatunza amani katika maeneo yao. Vilevile, Ussi aliwataka Watanzania na wale wa Zanzibar waliojiandikisha kuhifadhi shahada zao za kupiga kura, ili ifikapo uchaguzi, kila mmoja aweze kutimiza haki yake ya msingi ya kupiga kura na kumchagua kiongozi atakayewafaa. Kwa mujibu wa Ussi, Mwenge wa Uhuru ni tunu ya Taifa inayolenga kukagua thamani na maendeleo ya miradi inayotekelezwa. “Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea ku...

DKT. NCHEMBA ATETA NA CEO WA BENKI YA ASOCIATE GENERALE JIJINI PARIS

Image
  Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akiwa na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa  Benki ya Kimataifa ya Societe Generale, Bw. Pierre Palmieri, iliyoshiriki kugharamia  mradi wa SGR kipande cha 2 na ununuzi wa mabehewa na vichwa vya treni vya SGR, Makuu ya benki hiyo, Jijini Paris, nchini Ufaransa. Na Benny Mwaipaja, Paris   Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), amesema kuwa mradi wa treni ya kisasa, SGR, utainufaisha nchi ya Tanzania na nchi nyingine zinazotumia Bandari ya Dar es Salaam kiuchumi na kijamii kwa kukuza biashara na uchumi katika Ukanda wa Maziwa Makuu na Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC).   Dkt. Nchemba amesema hayo Jijini Paris nchini Ufaransa, alipokutana na kufanya mazungumzo na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Kimataifa ya Societe Generale, Bw. Pierre Palmieri, iliyoshiriki kugharamia  mradi wa SGR kipande cha 2 na ununuzi wa mab...

Mkutano wa Kimataifa wa Akili Unde Barani Afrika unaofanyika Kigali nchini Rwanda

Image
  Matukio mbalimbali katika picha wakati wa siku ya pili ya Mkutano wa Kimataifa wa Akili Unde Barani Afrika unaoendelea katika Kituo cha Mikutano cha Kigali (KCC, jijini Kigali, nchini Rwanda, Aprili 4, 2025.