JAJI MKUU TANZANIA AWATAKA MAWAKILI KUTENDA HAKI
Jaji Mkuu wa Tanzania Jaji George M. Masaju amewataka Mawakili wapya waliopokelewa na kukubaliwa kufanya kazi kwa kuzingatia uadilifu kwa kufuata Katiba na Sheria za Tanzania ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi mkubwa “Mnapokwenda kutekeleza majukumu yenu ni muhimu mkafanye kazi kwa uadilifu mkubwa na kuzingatia miongozo mbalimbali ikiwemo Katiba, Sheria na Kanuni mbalimbali.” Amesema Jaji Mkuu. Sambamba na hilo, Jaji Mkuu wa Tanzania amewaeleza Mawakili hao kuhakikisha wanatenda haki kwa wananchi, kwa kusimamia misingi ya sheria , kanuni na taratibu, huku wakiwa sehemu ya kuendelea kulinda amani ya Taifa. “Niwaombe Mawakili mliokubaliwa na kupokelewa leo mkatende haki kwa wananchi, mkazingatie utawala wa sheria unafuatwa, pia ninyi ni sehemu ya kuilinda na kuitetea Amani ya Taifa hili.” Amesema Jaji Mkuu. Sherehe hizo za 73 za kuwapokea na kuwakubaki Mawakili wapya Kujitegemea zimehusisha jumla ya wahitimu 774. Jaji Masajim amewakumbusha mawakili Mahakamani...