MRADI WA KUFUA UMEME WA JULIUS NYERERE WAKAMILIKA RASMI - DKT. BITEKO

📌 Asema ni ndoto ya watanzania kupata umeme wa uhakika 📌 Asisitiza kazi iliyobaki ni kuimarisha miundombinu ya kuwafikishia wananchi umeme 📌 Rais Samia na Rais wa Misri kuzindua rasmi Mradi wa Julius Nyerere Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewataka Watanzania kutegemea kupata umeme wa uhakika baada ya Mradi wa kufua umeme kutoka Bwawa la Julius Nyerere uliokuwa ukisubiriwa kwa shauku kubwa na Watanzania kukamilika rasmi. Dkt. Biteko ameyasema hayo April 5, 2025 baada ya kutembelea Mradi huo akiwa ameambatana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na uwekezaji, Mhe. Profesa Kitila Mkumbo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mhe. Hamadi Masauni pamoja na Viongozi wengine mbalimbali. Amesema hivi sasa mitambo yote tisa imekamilika na inafanya kazi tayari, amefafanua kuwa kukamilika kwa Mradi huo kumechangiwa na maono ya Rais wa Awamu ya Sita, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye aliu...