Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ridhiwani Kikwete, akizungumza na wanahabari kuhusu siku 100 za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan tangu kushika madaraka . Mkutano huo ulifanyika Ofisi za Idara ya habari (MAELEZO) zilizopo Mtumba jijini Dodoma Akizungumza na waandishi wa habari Januari 30, 2026 jijini Dodoma, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwan Kikwete, amesema kuwa Serikali imeajili watumishi 12,000 kibari cha ajira kilitolewa baada ya kuapishwa tarehe 3 Novemba 2025. Amebainisha kuwa kwa mujibu wa kifungu cha 7, kifungu kidogo cha 7 cha Sheria ya Utumishi wa Umma, Sura ya 298, jukumu la kuendesha mchakato wa ajira katika Utumishi wa Umma linafanywa na Sekretarieti ya Ajira iliyo chini ya Ofisi ya Rais. Amesema kuwa baada ya tangazo la ajira kutolewa na maombi kupokelewa, Sekretarieti ya Ajira ya Utumishi wa Umma iliratibu usaili uliofanyika katika mik...