Posts

JAJI MKUU TANZANIA AWATAKA MAWAKILI KUTENDA HAKI

Image
Jaji Mkuu wa Tanzania  Jaji George M. Masaju amewataka Mawakili wapya waliopokelewa na kukubaliwa kufanya kazi kwa kuzingatia uadilifu kwa kufuata Katiba na Sheria za Tanzania ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi mkubwa “Mnapokwenda kutekeleza majukumu yenu ni muhimu mkafanye kazi kwa uadilifu mkubwa na kuzingatia miongozo mbalimbali ikiwemo Katiba, Sheria na Kanuni mbalimbali.” Amesema Jaji Mkuu. Sambamba na hilo, Jaji Mkuu wa Tanzania amewaeleza Mawakili hao kuhakikisha wanatenda haki kwa wananchi, kwa kusimamia misingi ya sheria , kanuni na taratibu, huku wakiwa sehemu ya kuendelea kulinda amani ya Taifa. “Niwaombe Mawakili mliokubaliwa na kupokelewa leo mkatende haki kwa wananchi, mkazingatie utawala wa sheria unafuatwa, pia ninyi ni sehemu ya kuilinda na kuitetea Amani ya Taifa hili.” Amesema Jaji Mkuu. Sherehe hizo za 73 za kuwapokea na kuwakubaki Mawakili wapya Kujitegemea zimehusisha jumla ya wahitimu 774. Jaji Masajim amewakumbusha mawakili Mahakamani...

JMAT YAOMBA KUFANYIKA MAOMBI YA AMANI KITAIFA

Image
Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT), imeomba yafanyike maombi ya kitaifa nchi nzima yatakayotanguliwa na mfungo wa siku tatu, maombi hayo yawe ya kina kwa watu wa Imani na madhehebu mbalimbali .  Hayo yote nikumuomba mungu msamaha na toba ya kweli na kumuomba mungu roho ya kutoa msaamaha tulipokosewaa na wenzetu. Hayo yamejili leo wakati Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Sheikh  Alhadi Mussa Salum, alipokuwa akizungumza na wanahabari jijini Dodoma Pamoja na viongozi wa dini mbalimbali . Mwenyekiti huyo amebainisha kwamba Taifa limepitia katika kipindi kigumusana kutokana na kadhia ya Tarehe 29.10.2025 wakati wa Uchaguzi  Mkuu nchini Tanzania, kadhia hiyo ilisababisha hasara ya roho za watu Pamoja na uharifu wa miundombinu na mali za Serikali na watu binafsi. Mwenyekiti huyo amesema baada ya kufuatilia Kamati yake imebaini kwamba mambo hayo yaliyotokea siku hizo yamesababisha  na kuleta chuki na Athari kubwa ya kisaikolojia katika akili na mioyo ya watu. Hivyo Tai...

KUNAVIONGOZI HAWAMWAMBII UKWELI RAIS DKT. SAMIA--------BUTIKU

Image
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), Joseph Butiku, akisisiti jambo katika kongamano la Wazee lililoandaliwa na Taasisi hiyo lililofanyika jijini Dodoma leo, huku likizungumzia Haki na Amani ya Tanzania kuelekea 9 Desemba 2025. Kongamano hilo lililoshirikisha wazee , Butiku aliuliza kwa mshangao chanzo cha ghasia ya 29-11-2025 moja wapo lilikuwa watu kupotea , viongozi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama  kwanini walishindwa kumwambia ukweli  Rais ukweli kwanini watu wanapote, mtu anashushwa kwenye gari na kwenda kuuliwa hapo kunatatitizo, Butiku alisema Rais hawezi kufanya kila kitu anamambo mengi ya kufanya amewakaimisha watu kufanya kazi kwa niaba yake , watu wanapotea mhusika upo tu haiwezekani hata kidogo.  

Kwagilwa awataka watumishi wa umma kuheshimu na kuzingatia muda wa kazi

Image
    Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu, Mhe. Reuben Kwagilwa, amewataka watumishi wote walio chini ya Ofisi hiyo kuripoti kazini saa 1:30 asubuhi na kutekeleza majukumu yao hadi saa 9:30 alasiri kama ilivyoanishwa katika Kanuni F.1 ya Kanuni za Kudumu za Utumishi wa Umma za mwaka 2009. Kwagilwa am etoa maelekezo hayo leo tarehe 24 Novemba, 2025 baada ya kufanya ziara ya kikazi ya kushtukiza katika Shule ya Msingi Kisasa jijini Dodoma majira ya saa 1:30 asubuhi na kubaini idadi kubwa ya walimu wa shule hiyo hawajaripoti kazini kwa wakati ili kutekeleza wajibu wao kama ilivyokusudiwa na Serikali. “Wakati nimefika hapa nimekagua kitabu cha maudhurio ya walimu na kubaini walimu 16 tu kati ya walimu zaidi ya 55 ndio waliowahi kazini, hivyo kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI Mhe. Profesa Riziki Shemdoe ninaelekeza kuwa, watumishi wote walio chini ya OWM- TAMISEMI wakazingatie muda wa ...