Posts

Kampuni ya CRCEG inatekeleza kwa ubora na kasi ujenzi uwanja wa AFCON Arusha-Serikali

Image
Na Prosper Makene, Arusha  NAIBU Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Hamis Mwinjuma ameipongeza Kampuni ya CRCEG ya kutoka nchini China ambayo inajenga uwanja wa mpira wa miguu jijini Arusha utakaotumika kwa michuano ya AFCON 2027 kwa kuweza kujenga uwanja huo kwa kasi na viwango vya hali ya juu. Akizungunza mwishoni mwa wiki wakati wa halfa ya kumalizika kwa awamu ya kwanza ya ujenzi wa zege na kuanza ramsi kufunga paa la uwanja huo, Naibu Waziri amesema kuwa ni mara ya kwanza nchini kuona mkandarasi anamaliza kazi aliyopewa kabla ya muda kwani amemaliza awamu ya kwanza siku 20 kabla ya  muda uliopangwa kwenye mkataba. Mwinjuma alimaalufu kama Mwana Fa amesema: "Mkataba huu wa ujenzi wa uwanja mkubwa wa michezi jijini Arusha, ulitiwa saini tarehe 19, mwezi wa 3, mwaka jana (2024), lakini natambua kazi rasmi zilianza tarehe 25, mwezi wa 7, mwaka huo huo, baada ya utaratibu wa kukabidhiana site pamoja na shughuli zingine za awali kukamilika. Mkandarasi amepewa jukumu la kufa...

MKOA WA ARUSHA MAFANIKIO YA SERIKALI YA AWAMU YA SITA KATIKA MKOA WA ARUSHA

Image
Awali ya yote nichukue nafasi hii kumshuru sana Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehema, kwa kutujalia kukutana   hapa siku ya leo tukiwa wazima na afya njema, huku tukijivunia mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka minne (2021 hadi 2025) ya Serikali ya Awamu ya Sita , chini ya jemedari makini sana Mheshimiwa Dkt Sami Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Niliyepo mbele yenu kuzungumzia mafanikio ya Mkoa wa Arusha ni Kenani Laban Kihongosi , niliyepewa heshima na dhamana na Mhe Rais ya kusimamia shughuli mbalimbali za Serikali katika Mkoa wa Arusha. Ndugu Waandishi wa Habari; Mkoa wa Arusha ni miongoni mwa Mikoa 31 nchini, wenye Wilaya sita , Halmashauri saba , Tarafa 23 , Kata 158 , Vijiji 394 , Mitaa 154 , na Vitongoji 1,505 wenye jumla ya wakazi 2,356,255, kulingana na Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022. Kati ya watu hao wanaume ni 1,125,616 na wanawake ni 1,230,639, kukiwa na wastani wa ongezeko watu kwa asilimia 3.4% kwa mwaka. Ndugu ...