WAZIRI SILAA ASIMAMISHA MATUMIZI YA KITUO CHA MAFUTA CHA BARREL DAR ES SALAAM
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry Silaa akiozungumza na wananchi wa Mikocheni wakati akisimamisha matumizi ya Kituo cha Mafuta cha Barrel Petrol Energy cha Mikocheni Desemba 23, 2023 jijini Dar es salaam. . Mwakilishi wa Kituo cha Mafuta cha Barrel Petrol Energy cha Mikocheni Mhandisi Stanley Kitundu akizungumza na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry Silaa (hayupo pichani) kwa niaba ya mmiliki wa kituo hicho ambacho kimesimamishwa kutoa huduma 23, 2023 jijini Dar es salaam Na Eleuteri Mangi, WANMM Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry Silaa amesimamisha matumizi ya Kituo cha Mafuta cha Barrel Petrol Energy cha Mikocheni jijini Dar es salaam na kupiga marufuku ujenzi holela wa vituo vya mafuta nchi nzima vinavyojengwa kwenye makazi ya watu hatua inayohatarisha usalama wa watu na mali zao. Waziri Silaa ametoa agizo hilo Desemba 23, 2023 alipoenda kukagua eneo kilipojengwa kituo hicho na ...